Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ukiishi Kigamboni Wewe ni Mshamba ( Mbwiga ) tu sawa?Acha fix wewe. Mimi kuna siku nakaa huko Juliana,samaki samaki Hadi saa Saba nane na ninarudi Kigamboni usiku sina mlinzi geti nafungua mwenyewe. Niliishi miaka mitatu bila geti
Njoo uchukue,million 8.avic town kigamboniNdio napotaka kununua kiwanja huko.. Hata iwe maporini kabisa
Vibaka walikua ni beach boys,maeneo ya mikadi,machava na ferry .wengi walishakamatwa,mji mwema,geza ulole,shagwe,uko kwa kishua saivi,kibaka hauwezi muona.Ndugu yangu tulimpoteza kwa kuchomwa kisu tumboni na vibaka saa mbili tu usiku. Kigamboni nehiiiii.
Hiyo ilikua zamani sio sasa,gari zinakwenda kibada ,kongowe saivi nyingi tu ,mpaka za kariakoo kupitia darajaniKigamboni panamfaa kwanza mtu asiye na Mambo mengi uwe saa 1 usiku upo kwako nje ya Hapo uwe na usafiri wako. Gari za abiria zinakata saa mbili tu .
Kwa kina Jose mtamboninoooJaamaaaniiiiiiiiii
Kigamboninoooooooo........🤪
Shida ni ile foleni ya pale kisiwani.......Kwahio tunakaa huku hatuna magari? Natumia average 45minutes kwenda Kijitonyama asubuhi jioni kurudi average one hour via darajani.
Usiku 15-20 minute's kivukoni niutafute nini
Kigamboni (sasa ni wilaya) ni sehemu ya jiji la Dar es Salaam ambayo tofauti na maeneo mengine ilichelewa kuendelezwa kimiundombinu mpaka kufika miaka ya 90 .Watu walichelea kuishi huko kutokana na kupaona ni maporini palipostahili kuishi wanyama.
Hivi leo,mambo ni tofauti sana,mji unakua kwa kasi ya ajabu, barabara zinajengwa kutangulia makazi ya watu,ni sehemu pekee katika jiji la Dar es Salaam ambako ukiingia unasahau kuhusu foleni za barabarani , hali ya hewa ni nzuri kutokana kutokuwepo kwa ujenzi holela wa nyumba, ni karibu sana na city centre na kuna fursa nyingi za kuanzisha biashara.
Binafsi nilifika kwa mara ya kwanza na kuhamia kigamboni mwaka 2015 kutoka Survey maeneo ya karibu na Mlimani city nilipoishi kwa takribani miaka minne,ila mpaka kufikia leo sijawahi kujutia kuishi huku wala kuwaza kuhamia mahali pengine katika mji huu kutokana na sifa nilizozitaja hapo juu na kwa bahati nzuri Mungu amenijaalia kujenga kakibanda huku huku.
Kwa ambao hawajawahi kufika huku hudhani kwamba Kigamboni ni kisiwa na kwamba usafiri pekee wa kufika huku ni wa kuvuka maji kwa pantoni, la hasha! Kigamboni si kisiwa bali imetenganishwa na sehemu nyingine ya jiji kwa sehemu ya bahari iliyoingia nchi kavu (ghuba) ambayo ni bandari ya Dar es Salaam na Kwa sasa ukiachilia usafiri wa wa pantoni kuna daraja na baraba mbili ambazo unaweza kupita bila hata kuiona hiyo bahari.
Karibuni sana Kigamboni.
Probably mara ya mwisho ulitembelea Kigamboni mwaka 2008 .Ukitaka mwisho wako wa Kutembea kutokana na Vibaka na Majambazi kuwa wengi na Kula Kwako Bata ( Kustarehe ) kuwe ni Saa 12 Jioni, basi kaishi Kigamboni.
Hio ni wale askari pale shuleni wanaisababisha. Ukipita shule hamna tena foleni.Shida ni ile foleni ya pale kisiwani.......
Inanikera balaa
Kero ya Kigamboni ni moja tu - kivuko lazima ulipie kama una gari - 2000 kwenda 2000 kurudi - jumla 4,000, kwa wiki 20,000 kwa mwezi 80,000 kwa mwaka 960,000.
Ukiondoa gharama hizi kigamboni ni mji mzuri mno wa kuishi.. Space kubwa, hewa nzuri , wakazi wengi ni wa umri wa 30 - 50 yrs !!
Ni kweli. Mimi ni bonge la mbwiga.Ukiishi Kigamboni Wewe ni Mshamba ( Mbwiga ) tu sawa?
hivyo vikundi ni wakuja kama wewe, wanakuja siku za sikukuu kuwakomesha watu kama nyinyi.True, kule niliendaga kipindi nipo O level Mikadi kuna vikundi vya wizi wanaiba mchana na hawakimbii wala nini.
pole sana mrembo.Ndugu yangu tulimpoteza kwa kuchomwa kisu tumboni na vibaka saa mbili tu usiku. Kigamboni nehiiiii.
Lakini kama unafanya kazi na ofisi zenu zipo Ilala & Kinondoni Temeke ama Posta basi utabana matumizi kama utaishi Kigamboni sababu mafuta ya kufika kazini ni kidogo, hakuna foleni pia utaamka saa 1 kamili ndiyo unaaza safari.Mimi na ka passo kangu 4000 ndio bajeti ya mafuta kila siku... kigamboni sipawezi kama darajani tu panataka 4000 kila siku
Kuna jamaa juzi kapigwa risasi mbezi beach mchana kweupe, mama na familia kauawa Masaki sijui Oysterbay...kwahio na huko hakufai?Ndugu yangu tulimpoteza kwa kuchomwa kisu tumboni na vibaka saa mbili tu usiku. Kigamboni nehiiiii.
Ni kweli. Mimi ni bonge la mbwiga.