Ukitaka kumuona shetani 'live' funga ndoa

Ukitaka kumuona shetani 'live' funga ndoa

Hamna nakuambia atashindwa kabla yaani knockout kabisa!!

Kwanini muunganiko utakua wa kweli kiasi kwamba mmoja akiugua na mwingine anaugua,mmoja akiumia moyoni wote mnaumia!!sijuinkama utanielewa!!

Kelele za nje mtazishinda na inawezekana wanamme au mke akakosa Tamaa kabisa ya kutoka nje!!

Usidharau purity Bond ni Bond yenye nguvu kuliko Diamond!!
Ushajiuliza kwanini wanaume waliowatoa bikira wanawake wengi huingia mitini?

Na kuwaacha wanawake wakiwa na maumivu, alafu baadae wao wanataka kuoa bikira Tena.
 
Changamoto za kwenye ndoa ni nyingi sana...za kiuchepukaji zipo lkn kuna nyingine mpaka unatamani uzaliwe.... Mtu ulikuwa kiuchumi fresh tu gafla kila kitu kinapuputika huna pa kushika ... Sijui kama unalewa lkn... Usikae kwenye angle moja
Kwani hakuna watu waliobaki 0 wakiwa hawajaoa/hawajaolewa?

Nini kinafanya uone umefilisika sababu umeoa/umeolewa?
 
Kuna watu tabia zao ni mbovu hata kabla hajaoa wala kuolewa, Kwahiyo akiingia ndoani hakuna kitakachobadilika.

Hamjawahi sikia mtu anaambiwa yaani huyu kwa tabia zake sijui ataolewa/atamuoa nani. Sasa anatoka mtu huko hawajuani… hayawi hayawi kaolewa/kaoa. Shida walizokuwa wanazipata ndugu, jamaa, marafiki na majirani anahamishiwa “mwenza” na anatakiwa adeal nazo to the rest of his/her life. We kuweza??

Kuna watu wanatabia ngumu nyie acheni, sisi kuna shoga etu anaitwa M****** huwa tunamwambia M******* we utakuwa mchawi si bure!! Msichana ana tabia mbovuuuuuu! Mchoyo, msengenyaji, mchafu, mbinafsi, ana mdomo, mzururaji, controlling, manipulator, she knows it all , muongo kila kitu kibaya yeye, hanaga jema yule dada.

Sasa mtu kama huyu aolewe kweli jamani huyo shemeji hamna rangi ataacha ona.
Huwa mara nyingi wale wanaodhaniwa wenye Tabia mbovu akiolewa au akioa hujirudi haraka sana na kuwa mtulivu esp. wakijaliwa watoto.
 
Shetani wa ndoa ame-graduate..

Ukiwa single Bado ni rafiki yake Shetani ila ukioa ni rafiki wa Mungu..

Sasa sikiliza ule mtanange wa Shetani akiwa anataka ubaki kuwa wake...

Lazima ukione Cha mtemakuni
Kwa hio shetani wa kabla ya ndoa ni tofauti na shetani wa baada ya ndoa au sababu mnakutanisha mashetani wawili pamoja yanaanzisha varangati?
 
Huwa mara nyingi wale wanaodhaniwa wenye Tabia mbovu akiolewa au akioa hujirudi haraka sana na kuwa mtulivu esp. wakijaliwa watoto.
Jichanganye sasa! Kuna kitu kinaitwa red flags ignore hizo halafu urudi kutuambia hapa kataa ndoa.

Labda kwa kukusaidia wahenga walisema tabia ni kama ngozi ni ngumu kubadili, yamkini wahenga hawakujua scientifically walichokisema kinatokana na nini ila experience ndio imewafanya walete huo msemo which is true.

Scientifically, kuanzia mwaka wa 6-12 wa binadamu ndipo anapodevelop tabia na namna ya kudeal na mazingira yake, ubongo wake ndivyo unavyomuelekeza namna ya kudeal na mambo, sasa usifikiri ukubwani mtu anaweza kuadapt namna mpya ya kudeal na mambo, unless apewe msaada wa kuipanga tabia yake upya, kitu ambacho kinahitaji commitment zisizokuwa za kawaida kukifanikisha.

Sasa kama unajipa moyo mtu mzima anaweza badili tabia kirahisi fikiri tena.
 
Kwa hio shetani wa kabla ya ndoa ni tofauti na shetani wa baada ya ndoa au sababu mnakutanisha mashetani wawili pamoja yanaanzisha varangati?
La hasha. Haiko hivyo. Ndoa ni moja lakini inahusisha watu wawili na kila mmoja wenu kaja na Shetani wake. Kwa mantiki hiyo, Ndoa yenu moja inakabiliwa na Shetani wawili au zaidi na lengo ni Kuisambaratisha kabisa hiyo ndoa yenu itokomee mbali.
 
Back
Top Bottom