Ukitumia internet vizuri kufanya utafiti wako binafsi utagundua Uchawi haupo. Hakuna mganga wala nabii atakayekutapeli. Wajinga ndio waliwao

Mkuu kama umeishi Tz maisha hayo hauwezi yaita ya upweke maisha ya upweke ni kukosa maji na umeme wa uhakika.
Umeme nimeukosa 2006-7 ile intensely,siku hizi hakuna shida ya umeme,mi mtu wa tabora,shida ya maji huko nyuma,Leo maji ya Viktoria
 
Mtoa mada nina uhakika huujui UCHAWI. Kwanza kabisa uchawi upo na ni uhalisia kabisa usio kuwa na shaka ndani yake.

Uchawi umegwanyika sehemu kuu mbili, wa kufarakanisha watu yaani wanandoa na ule u ao dhuru, kwa maana ya kuuwa na mfano wake.
 
Sasa hichi ulichokiweka hapa ni mazingaombwe, sasa kuna uchawi wenyewe.
 
Mfano wa magonjwa gani hayo ?

Kansa, heart attack, figo kufeli, kuganda kwa damu, homa ya ini etc etc .

Watu wa zamani enzi za middle age walikuwa hawana teknolojia ya vipimo na wala elimu ya kuyajua na kuyatibu hayo magonjwa

Hivyo mtu alikuwa akiugua ama akifariki kwa hayo magonjwa wanajua amerogwa na wachawi.

Ila baada ya sayansi kuyatolea majibu. Ndipo wakajua imani za uchawi zilikuwa zinawadanganya
 
Ni wapumbavu tu wanaokataa uchawi haupo,kutokuwa na experience na kitu hakukifanyi kitu hicho kutokuwepo
 
Bado hujawa mtu mzima,usiongee hayo maneno uwapo kwenye mikoa baadhi,be humble
 
Afrika watu wengi wanaishi dunia ya miaka 500 iliyopita.
hapo hapo marekani unapoishi kuna taasisi ya tiba asili na mimea na serikali ya marekani inaithamini kama dhahabu, je wajua kuwa mama wa tiba asili na uganga anatokea hapo hapo marekani?
 
hapo hapo marekani unapoishi kuna taasisi ya tiba asili na mimea na serikali ya marekani inaithamini kama dhahabu, je wajua kuwa mama wa tiba asili na uganga anatokea hapo hapo marekani?
Tiba ya asili ya mimea si uchawi.

Hiyo inaelezeka kwa chemistry, kwa biology. Hiyo ni science.

Dawa karibu zote zinatokana na mimea.

Hata huko nyumbani mimi sipingi waganga wa kienyeji wanaotumia dawa za mimea, huo si uchawi, huo ni uganga wa jadi.

Uchawi ni habari za kunuiza abracadabra na kupaa kwa ungo na ujinga kama huo, hizo si tiba za asili za mimea.

Umeelewa tofauti hapo?
 
Human psychology ndio inafanya uone wewe yamekukuta , mimi hayajanikuta
unaelewa nini kuhusu human physiology na human psychology? Je unajua kuwa physiology chimbuko lake liko kwenye uganga wa kienyeji?
 
Hakuna uchawi wewe.

Nyie wote mnaouamini uchawi hamuwezi kunifanya chochote.

🖕
Point yangu ni kuamini uchawi upo hayo ya kusema hatukufanyi kitu ni yako kwani mimi nimekuahidi naweza kukufanya kitu.Wachawi wa uliko ndio watadili na wewe na bila shaka wameshakuchezea vya kutosha
 
Kuhusu Salem mbona ya semekana mpaka Leo ukiienda waweza ongea na mzimu wa Tituba sindio uchawi wenyewe
 
Kuhusu Salem mbona ya semekana mpaka Leo ukiienda waweza ongea na mzimu wa Tituba sindio uchawi wenyewe
Hizo habari za uchawi ni udanganyifu mkubwa kuwahi kutokea anza leo chunguza kwa makini sana hizi story zinakuzwa na watu duni ,chunguza tu hata kwenye jamii unayoishi.
 
Hizo habari za uchawi ni udanganyifu mkubwa kuwahi kutokea anza leo chunguza kwa makini sana hizi story zinakuzwa na watu duni ,chunguza tu hata kwenye jamii unayoishi.
Sawa nime kuelewa vipi kuhusu sauti ya Tituba ni ya nani kule salem
 
Ushirikina ni story za kusadikika zinazotamalaki kwenye jamii za watu wajinga na maskini. Ni rahisi mtu wa Nanguruku kuamini kalogwa akiumwa malaria kuliko mtu wa Masaki.
 
mzee ramadhan ni mtaalam wa nyota biashara mali bira kafara mausiano cheo nk 0678663769
 
Human psychology ndio inafanya uone sijapata matatizo , nenda kasome kuhusu Human psychology utajua mengi kuhusu akili za binadamu na tunavyoamini vitu
wewe unaelewa nini kuhusu akili ya binadamu? Unaweza kutuelezea kidogo ktk mhtizamo yote? Tuanzie hapa kwanza
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…