Ukiwa muajiriwa wa sekta binafsi punguza majivuno

Ukiwa muajiriwa wa sekta binafsi punguza majivuno

Zero Competition

JF-Expert Member
Joined
Sep 12, 2018
Posts
347
Reaction score
553
Sekta binafsi ndo inaongoza kwa kutoa ajira nchini na hata duniani kote lakini ukiwa muajiriwa wa sekta binafsi amini kwamba kesho asubuhi unaweza amka ukaenda ofisini kisha ukakuta barua yako ya kuachishwa kazi iko mezani inakusubiri

Jambo lingine ni kwamba ukiwa muajiriwa wa sekta binafsi muda wote unakua na wasiwasi na unakosa amani hasa pale ambapo mkataba wako unaelekea kutamatika mana kuna baadhi ya mashirika na makampuni mkataba wako ukiisha unakua huna uhakika wa kuongezewa mwingine.

Kuna rafiki yangu flani yeye anafanya kwenye shirika moja la kimataifa linalojihusisha na masuala ya afya, huyu rafiki yangu aliniambia kwenye shirika lao watu wanakua na presha sana pindi mikataba yao inapoelekea ukingoni mana uhakika wa kuongezewa mingine ni mdogo sana.

Kuna jamaa zetu wanafanya kazi private sector lakini wana maringo utadhani wana mkataba wa maisha, sisi watu kama hao huwa tunawasubiri mtaani mana tushafanya kazi na makampuni mbalimbali na tunajua changamoto za kufanya kazi sekta binafsi.

Kitu ninachotaka kuwashauri wanaofanya kazi sekta binafsi ni kwamba, muda wowote unaweza fukuzwa kazini au kampuni ikafungwa ghafla tu baada ya kujiendesha kwa hasara.Hapa sasa ndo utakumbuka kwamba kuna washkaji mtaani niliwahi kuwaletea nyodo na majivuno sijui nitawaambia nini.

Ukiwa kwenye ajira especially ya private sector jitahidi kuwaheshimu watu wote mana muda wowote unaweza amka huna kazi then ukashindwa kuwaomba watu msaada.
 
Eeh kubwa zima ovyo! Kama ni dongo la mtu unaemfahamu ungemtumia direct🙄
 
Ndio maana watu wa sekta binafsi, ni wachapa kazi, Sana, mkataba ukiisha, ni faster Sana, kutafuta Chaka jingine, wale wa serikalini, ni sawa na kuku wa kizungu, wamezoea kulishwa, wakitimuliwa, presha, kisukari, juu siku mbili, six feet under!
 
Ukiwa kwenye ajira especially ya private sector jitahidi kuwaheshimu watu wote mana muda wowote unaweza amka huna kazi then ukashindwa kuwaomba watu msaada.
Kuheshimu watu ni jambo jema iwe ni kwa wafanyakazi wa private sectors na wale wa serikali. Uhakika/usalama wa ajira husikupe kibri kwa watu.
 
Sekta binafsi ndo inaongoza kwa kutoa ajira nchini na hata duniani kote lakini ukiwa muajiriwa wa sekta binafsi amini kwamba kesho asubuhi unaweza amka ukaenda ofisini kisha ukakuta barua yako ya kuachishwa kazi iko mezani inakusubiri

Jambo lingine ni kwamba ukiwa muajiriwa wa sekta binafsi muda wote unakua na wasiwasi na unakosa amani hasa pale ambapo mkataba wako unaelekea kutamatika mana kuna baadhi ya mashirika na makampuni mkataba wako ukiisha unakua huna uhakika wa kuongezewa mwingine.

Kuna rafiki yangu flani yeye anafanya kwenye shirika moja la kimataifa linalojihusisha na masuala ya afya, huyu rafiki yangu aliniambia kwenye shirika lao watu wanakua na presha sana pindi mikataba yao inapoelekea ukingoni mana uhakika wa kuongezewa mingine ni mdogo sana.

Kuna jamaa zetu wanafanya kazi private sector lakini wana maringo utadhani wana mkataba wa maisha, sisi watu kama hao huwa tunawasubiri mtaani mana tushafanya kazi na makampuni mbalimbali na tunajua changamoto za kufanya kazi sekta binafsi.

Kitu ninachotaka kuwashauri wanaofanya kazi sekta binafsi ni kwamba, muda wowote unaweza fukuzwa kazini au kampuni ikafungwa ghafla tu baada ya kujiendesha kwa hasara.Hapa sasa ndo utakumbuka kwamba kuna washkaji mtaani niliwahi kuwaletea nyodo na majivuno sijui nitawaambia nini.

Ukiwa kwenye ajira especially ya private sector jitahidi kuwaheshimu watu wote mana muda wowote unaweza amka huna kazi then ukashindwa kuwaomba watu msaada.
Truth by 100%

On the scale of 0-10 I gave that assertion over 7. It's clear, relevant and tentative

Niliwah kufanya kazi shirika moja hiv ile ngoma ilikuwa Nagwa. Kila miez miwili unasikia mtu kaachia au kaachishwa ngazi bibi mchuma unaondoka huo.

Bos wangu mm alikaa miez mitatu tu, akatimuliwa nikabakia mimi. Mm nikapewa majukum yake nikadum nayo miez 2 tu nikakataa kile cheo. Miez minane ilitosha kabisa kutafuta kona nyingine. Nimekaa mtaan miez miwili na yule bos wetu (GM) kaachia ngaz nakutana nae linked in anatumikia ofis nyingine.

Private sectoral employment accords should be reformed/revived
 
Back
Top Bottom