Ukiwa na tabia hizi, jiandae kuwa middle class na kuteseka ki uchumi!

Kuna UBAYA gani kuwa MIDDLE CLASS?

Hakuna ubaya lakin kuna mambo mengi ya maendeleo utashindwa kufanya.

Pia middle class ni kundi mojawapo la watu wanaolalamika sana kila siku kuomba huruma ya serikali
 
Kuna UBAYA gani kuwa MIDDLE CLASS?

Mtu anakandya kuwa middle class kwa kubeza home ownership, at least early home ownership.

Wakati hajui kwamba bila middle class huna upper class.

Wakati bila middle class values, as a society, individual huwezi ku transcend middle class.

Tunaambiwa Mengi kaanza biashara kwa kujaza wino mirija ya peni nyumbani kwake, jaribu kufanya hivyo katika nyumba ya Baba Ubaya uone.

Watu wengi wana reduce middle class kuwa ni state ya kiuchumi bila ku address the educational aspect, the cultural aspect, the other facest of the social aspect etc.

Mtu anakuja kutupa ushauri kuhusu kuepuka kuwa middle class (presumably advising how to skyrocket into the upper class) bila ya kutuambia "middle class" na "upper class" katika definition yake ni nini?

Kukimbizana na landlords ni "middle class"? "Upper class"?

Katika nchi isiyo na mfumo wa mafao ya uzeeni ya kueleweka, population explosion inayokuwa projected kuifanya Tanzania kuwa ya tano kwa idadi ya watu by the end of the century (UN/ The Economist) kuacha kujenga nyumba angalau moja sehemu unayotaka early ni "middle class"? "upper class"?

This advisory thread epitomizes the plague of a one size fits all solution from narrow minded approach.

Tuna copy paste maisha ya wenzetu, wenye systems tofauti, sheria tofauti, renters rights tofauti, unit availability tofauti, quality of life tofauti, transportation systems tofauti, financial tools tofauti etc.

Watu wengine, particularly the British stiff lipped upper class, kuongelea hela na investment tu ni "soo middle class".

Who is middle class now?
 
Nafikiri watu wanalinganisha maisha ya Ulaya na huku kwetu. Ulaya public transport ni reliable na pia unaweza kupanga kwenye appartment na maisha yakendelea bila shida.
Huku kwetu ni tofauti kabisa, kwa wale wanaoishi Dsm adha ya usafiri ni kubwa kupita maelezo, ndiyo maana vijana wengi wanaona ni bora kujilipua na gari ili kurahihisha mobility zao. Hata ukiwa na biashara ukiwa na gari inakusaidia sana pia.
Kwenye nyumba pia Ma landlord wa Bongo hawaeleweki, na hakuna sheria inayodhibiti upangishaji wa nyumba, ndiyo maana wenye nyumba wanapanga kodi jinsi wanavyojisikia bila hata kujali ubora wa nyumba zenyewe, mwenye nyumba pia anaweza kukufukuza kwenye nyumba wakati wowote tena bila kosa lolote la maana.Ukiwa mkorofi ndiyo kabisa utakuwa ni mtu wa kutafuta nyumba kila mwezi.
Kwa mazingira hayo ndiyo maana Bongo nyumba ni security kubwa sana. Ukiweza kujenga nyumba na ukawa na usafiri wako then your very free to take risk of investment.
Kwahiyo mimi naona ni bora ukakamilisha kwanza nyumba na gari then ukaanza kutake risk za biashara, you will be very secured.
 

watu hapa wanaongea tuuu based on umaskini wao wanaoupitia huku wakijifariji!!...tafuteni hela nyie..ziwe za wizi au halali...hazina alama...i better cry in a vitz rather than on boda boda..halaaaaaaaaaa
 
Its all depending on someone mentality...also its worthy noting that, investing has different meanings to different people, building a house to some is an investment, while to others its not, so its just depending waht investment actually means to you ...also don't overlook the fact that, we are not always starting from similar positions, thus, may be all people are doing the right things as long as they are working along their dreams and plans. all in all you have shared something useful
 
Mtoa mada anaweza akawa yupo sawa tatizo ni kwamba hajawapoint vizuri wale watu wanaohusika, I mean graduates, ambao wengi wao wanaanza na mshahara wa laki 5,
Hawa watu wengi wao baada ya miaka 2 wanachukua mikopo na kununua magari bila ya kufungua hata kigenge au sehem ya kuchomea chips,
Lakni kwa mtu ambae anauwezo wa kujenga nyumba inamaanisha kipato chake ni kizuri coz huwez jenga nyumba km huna hata uwezo wa kupata milion 2 kwa mwezi nje na bajet yako.
Nyumba ni part ya investments otherwise umejenga sehem ambayo hata hati huwez kupata na ni sehemu isiyo na soko hata benk ukienda utapewa milion 10
 
Ame graduate at 25 akaajiriwa na kupanga nyumba ya 150,000

At 30 ana familia na amejaliwa watoto wa 2 aendelee kupanga nyumba ya 300,000?asijenge!

Unafananisha us/uk kwenye 'nhc' nyingi na zile apartment binafsi hamna manyanyaso

Hautakaa unielewe milele,
 
unataka.wote wawe first.class ndugu? au ukisema middle class unamaanisha nini naweza sema kwa Tanzania asilimia 5% ndo first class...wakiwemo wanasiasa na wafanyabiashara wakubwa sana kama kina mengi na bakhera mfano..na watu wengine wachache ambao wanauwezo wa kuearn mil angalao 10 kwa mwez..
hao middle.class unaowakataa ndo wapo kina sisi wengi kiasi kama 45% na kama 55% ni lower class hii ni kwa mujibu wa world bank (2012).
sasa ndugu mtu kuanza na kununua gari ama kujenga nyumba ama kuspend ni maisha yake..kuna wanaopenda maendelei na wapo wanaopenda pia luxury life na yote haya hufanya kwa mipango yake.mtu anaweza kufikiria kujenga nyumba ni mil 50 na hapo amepanga..bado anapigania daladala..sasa kama mshahara wake unaruhusu kununua vitz ya mil.5 kwanini asinunue wakati hiyo mil 5 haitoshi kujenga ama kuanzisha biashara? kila mtu ana malengo yake hata biashara si kila mtu anaweza kuwa interested na biashara fulani..mfano..nina mpangaji wangu ana mke na watoto 2 amepanga rum 2 self analipa laki 250,000/-.kwa mwezi..na ana harrier anapack hapo nje..sasa mtu kama huyu ana malengo yake ameamua kupanga na kununua gar kwanza kama sehem ya malengo yake aliyojiwekea then ndo ajenge..huwezsema awekeze kwenye kuzalisha kumbe hayuko interested na biashara wala nini..mwingine anaona kero kupanga anaamua kujenga kwanza..so kwa suala kama hili jamani linatofaut miongoni mwa watu kulingana na vipaumbele vyao..tena mtu anaeanza kazi na kujenga namheshim coz kujenga sio mchezo..
ila kusema watu watabaki middle clasa umenishtua ndugu..hongera kwakua upo first class na sijui kama tutafika huko ukizingatia gape linazidi kuwa kubwa baina ya wenye nacho.na wasiokua nacho na wanaokitafuta..
 

ndo hapo ndugu lakini si kila mtu yupo interested na ujasiriamali ndugu..
 

mmnh kuna mahala umechemsha..mhindi gani anaelipa mil 1.5 ya kodi kwa mwezi? wewe unawajua wahindi au unawasikia? unajua wanalipa sh ngapi huko kwenye maghorofa? wengine wanaishi kwa kodi za babu zao na baba zao walizolipa kwa miaka 5mpaka 10 siku za nyuma..hakuna watu wanaotaka cheap life kama wahindi wewe usidanganye..i know them well na nimefanya nao kazi..
anyway una point kwenye mawazo yako ila hujaweka clear ni.watu wa namna gani unawazungumzia..
 
nashangaa huyu anataka kutisha watu. hebu waangalie na kodi wanazolipa wenye nyumba sahv ndio waone kama kujenga nyumba mapema inalipa au lah.
lakini hiyo pesa uliyojengea nyumba,ungeinvest pengine badala ya kujenga nyumba baada ya miaka mitano,ungeweza kununua nyumba na ukabaki na investment zako.
 
lakini hiyo pesa uliyojengea nyumba,ungeinvest pengine badala ya kujenga nyumba baada ya miaka mitano,ungeweza kununua nyumba na ukabaki na investment zako.

Ni investment gani ipo certain kiasi hicho? Yaani in 5 years uwe umerudisha mtaji wako na una ziada ya kununua nyumba! Hembu toa mifano halisi ueleweke vizuri. Tena kwa wale ambao wanaotaka kufanya biashara huku wakiendelea na kazi zao ofisini ndiyo ngumu kabisa kufanikiwa, biashara inahitaji usimamizi. Ukipata hela yako ni bora ujenge nyumba, nunua gari, acha maisha yaendelee.
 

Dada wala usisikitie, mimi nimepost hii mada ili watu wajue wale wenye nacho wengi wao utumia mbinu gani, na haiwezekani dunia nzima ikawa na matajiri, it is the matter of choice where to belong, mimi nilichopost hapo ni kujaribu kuelezea jinsi ya kuzungusha hela yako izalishe, maisha ni kuchagua, mimi nimeshare idea tu
 
ndo hapo ndugu lakini si kila mtu yupo interested na ujasiriamali ndugu..

Najua katika jamii hatuwezi kuwa sawa, kwanza tumelelewa tofauti, mtoto wa mjasiriamali atawekeza kwenye biashara, mtoto wa muajiriwa atazungusha CV maofisini, tatizo ni back ground zetu
 

Inawezekana mkuu mimi nilipoanza biashara mwezi mmoja pesa ya mtaji ilirudi na faida zaidi ya mara 3 juu.

Inategemea na biashara unayofanya
 
Kutokuwa finnacial smart ndyo kunawafanya wengi wenu hpa mtoe majibu rahis.....mtoa nada hajawakataza kununua magari wala kujenga nyumba ishu hapa ni muda gani unatakiwa ujenge nyumba au ununue gari? Cha msingi fanya ivo ikiwa tayar na asset ambazo zinakuingizia hela
 
lakini hiyo pesa uliyojengea nyumba,ungeinvest pengine badala ya kujenga nyumba baada ya miaka mitano,ungeweza kununua nyumba na ukabaki na investment zako.
Vijana mmekuwa too global mpaka mnasahau mnaishi Mabibo na mivinjeni

Wengi wanaanza ujenzi wa msingi wakati hawana hela ya lenta acha bati.ni mdogo mdogo

na mkifanikiwa mnadondosha Makasiri Mbezi beach mnasahau role model wenu Warren Buffet anaishi nyumba ya kizamani aliyoanzia maisha
 
Maisha hayana formula jamani....wako walioanza na biashara hadi leo hawana pa kulala....mi nimeamua nianze kujenga kwangu kwanza..halafu sasa nikiwa nimelala kwangu ndo nitapata amani ya kufikiria biashara vizuri....ILA NIKIWA NIMELALA KWANGU.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…