Ukiwa na wananchi kwa upande wa nchi na Kikwete kwa upande wa chama, basi umemaliza. Nape na Makamba kwisha habari yao

Yaani hao wajinga wawili ndio wawe maadui wa kitaifa .?

Kipara aliiba mtihani wa kidato cha 4 na kufutiwa matokeo.

Nepi alipiga vibendera "F"vya kutosha akajipatia daraja la 4 lenye point 29 huku akipata hadi kibendera cha somo la uraia.

Japo Tanzania ina wajinga wengi hawa wawili hawawezi kuwa maadui wa taifa bali ni mfumo mbovu tu ndio umewabeba kufika hapo.

Hao wamefikia hapo kupitia technical who !

Adui wa kitaifa ni CCM na mtaji wa CCM ni wingi wa wajinga Tanzania.
 
Kutumbuliwa kwa hao jamaa sio mtaji kwa mama, bali watu wamefurahi maana hao jamaa walikuwa na nyodo. Bado wizi wa kura ndio silaha ya ccm ya ukweli.
 
Unaelewa maana ya adui wa taifa mkuu au umekurupuka tu kuandika?

Mtu yeyote akiwaharibia wananchi na nchi, basi huyo tayari ni adui wa taifa.
 
Kutumbuliwa kwa hao jamaa sio mtaji kwa mama, bali watu wamefurahi maana hao jamaa walikuwa na nyodo. Bado wizi wa kura ndio silaha ya ccm ya ukweli.
Mkuu hebu punguza mihemko ya siasa, soma kwanza kwa makini kilichoandikwa ili uelewa maana ya uzi.
 
Unaelewa maana ya adui wa taifa mkuu au umekurupuka tu kuandika?
Adui wa kwanza wa taifa ni UJINGA

Ambao ndio mtaji wa CCM..
Mtu yeyote akiwaharibia wananchi na nchi, basi huyo tayari ni adui wa taifa.
Hao wameharibu ila ni sehemu tu ya mfumo , mfumo ndio umewabeba hawa vilaza kuwafikisha hapo!

Mfumo mzima umeoza na ndio unakumbatia crooks.
 
Maana ya huu uzi ni tofauti na ulichoandika, au ulikuwa na maana tofauti, ila ukashindwa kukieleza kwa ufasaha, lakina unataka majibu yatakayoendana na hisia zako?
Mimi nafikiri wew ndo umeelewa tofauti na kile kilichoandikwa.

Kuna watu waliandika kuwa wale vijana wawili waliotenguliwa sasa hivi wanapanga njia za kumkwamisha aliewatengua ili asifanikiwe kupita aidha ktk kinyang'anyiro cha kumpitisha mgombea wa chama chao kugombea uraisi, au wakishindwa hapo basi wamkwamishe katika kinyang'anyiro cha uraisi wa JMT.

Sasa mimi ndo nimekuja kupinga hilo, kwa sababu katika chama chao mwenyekiti ana nguvu mno kuliko mtu yoyote ndani ya chama. Hivyo kupanga kumzuia huko ni sawa sawa na kujaribu kuudaka upepo kwa mkono kitu ambacho hakiwezekani na ukizingatia yeye ndio anaetaka kugombea.

Vilevile kumkwamisha katika uchaguzi mkuu ndo kabisa haiwezekani kutokana yeye ndio mgombea wa nafasi ya uraisi, yeye ndo anaeteua tume inayohesabu kura za uraisi na yeye ndio anaemteua mtu anaetangaza hayo matokea ya uraisi.

Hivyo kumkwamisha katika nafasi zote kwa upande wa chama na uchaguzi mkuu haiwezekani. Hilo ndio lengo la uzi. Na ndio maana nikatolea mfano yule alietambaa kwa magoti kutoka kwao hadi ikulu kuomba msamaha kwa mtu walietaka kujaribu kumkwamisha na matokeo yake wakajikuta wamekwama wao.
 
Mmmh!
Mimi sio mfuasi wa hao wapigaji wawili, lakini ni mapema mnoo kudhani huo ndio mwisho wao. Mimi naona huo ndio mwanzo wao, ni vijana wajanja janja mnoo kwenye siasa za kishenzi za CCM.
Walimtengenezea Magufuli urais wa kimchongo, wakamchimba mkwara akawararua lakini mwisho wa siku wakamlaza kaburini!
 
Nasema hivi, yote yaliwezekana kupitia baba yao msoga. Ila kama katika hili msoga hayupo upande wao basi watakufa kifo cha mende mgongo chini tumbo juu. Huyo Lowasa na umaarufu wake pamoja na fedha zake lakini Msoga alipoamua kumfanyia umafia jamaa alisafa akazurura kutoka chama kimoja kwenda kingine, mpaka mwishoni akaomba poo na kurudi kule kule kwa msoga akiwa mwenye adabu na utii hadi kifo chake, itakuwa hao vijana wa juzi wanywa mnazi.

Soma comment namb 11 utaelewa tu mkuu.
 
Kichwa chako cha habari inaonyesha ukiwa upande wa wananchi, lakini maelezo yako hapa unaonyesha anachotambia rais ni nguvu ya dola na tume isiyo huru ya uchaguzi na sio wananchi, ndio maana nikasema uzi wako una maana tofauti? Hata hivyo mimi nashangaa wanaosema hao unaowaita vijana wawili, kwanza sio vijana, na wala hawana uwezo wowote nje ya mbeleko ya vyombo vya dola inayopatikana kupitia madaraka ya urais.

Hakuna mwanaccm yoyote anaweza kufanya hujuma dhidi ya mwenyekiti wa ccm ambaye mara nyingi ni rais, labda siku ccm itatoka madarakani, maana karibia wote ni watu wa kujipendekeza, na hutegemea hisani ya rais kuendesha maisha yao.
 
Na huo ndio ukweli wenyewe. πŸ™ŒπŸ‘
 
Hawana lolote wakiwa nje ya system !
Ila inawezekana kabisa wakawa wametolewa hapo walipokuwa kimkakati zaidi kutoka upande wa Maza au kutoka upande wa ndumila kuwili ili Maza atengenezewe barricade 2025 !

Najaribu kuunganisha dots
Yale matamshi ya Nape kule Kagera yalitoka kwa bahati mbaya au kwa makusudi ? ?!
Was it a set up ?
Kafanye hivi kisha sisi tutafanya hivi ili ionekane hivi πŸ™„πŸ˜…πŸ˜…
Am just thinking aloud πŸ˜³πŸ€ πŸ™

Time will tell πŸ™ŒπŸ‘
 
Hakuna cha kutengenezewa maneno wala nini. Wakati mungine wanasiasa mzuka ukizidi jukwaani hujikuta wanaropoka na kuongea hata yale ambayo hawakupanga kuyaongea.

Unafikiri Lisu alipokuwa anakishambulia chama chake, na viongozi wenzake kuwa katika uchaguzi wao mkuu wa chama kuna viongozi wenzake wa chama walipokea hela kutoka kwa mama Abdul, ili wapitishe viongozi watakaoendana na matakwa yake mama Abdul, nayo hiyo utasema kuwa Lisu alikuwa amepangwa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…