Ukiwa nyumbani halafu huna kazi

Ukiwa nyumbani halafu huna kazi

Yah, ni changamoto.
Hapo bado hawajaficha remote usiangalie TV[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Iyo ya kufichiwa remote nimewai experience nimeenda kwa mamdgo wangu kumsalimia muda wa week moja wakaficha remote zoote duh nilichoka nkasema apa cludi tena.....
 
Umeme ukiisha wewe ndie unaemaliza
Bill ya maji ikiwa kubwa watumia maji vibaya..khaaa!!
 
nikitaka kutoka chumbani au kama niko nje nasikilizia dingi yuko wapi,sitaki kupishana nae koridoni
 
ila wengine manyanyaso ya mama zenu wa kambo mmeyachomekea humuhumu.
 
ukiwa na raha sana unaonekana una kiburi, hutakiwi kuchangia mada za kifamilia maana huo ni uhaini, hata kama kazi za kufanya zimeisha hutakiwi kuonekana uko idle, ni ishara ya dharau, ukitoka ukachelewa kurudi inabidi urudi ulikotoka au ulale kibarazani
 
Mshua akinunua magazeti akaja nayo nyumbani ukatangulia kusoma kabla yake anayasusa na kukasilika sana
 
Mm niliwahi kuvunja chupa ya chai

Niliapizwa kwa kuambiwa,nikipata kazi tu,mshahara wangu wa kwanza
Lazima nilipe

Dah

Mbaya zaidi
Usilale mpaka saa mbili asubuhi
Ilikuwa Balaa

Naambiwa
Tony Blair,analala masaa manne
George Bush,analala Masaa matatu

Wewe ushuzi kunuka,unalala masaa 10!!!!

Yaani ilikuwa Ngonjera

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Ukiwa Nyumbani Halafu Huna kazi

Hata Mtoto Akilia Tu Inaonekana Wewe Ndo Umemchokoza!
[emoji23][emoji23][emoji23]
Ni pale ambapo na house girl amekimbia.... Asubuhi unategemewa udeki nyumba nzima, Madirisha na milango viwe Safi, kuosha vyombo, vyoo viwe Safi, uwanja uwe Safi, maua yanyeshewe, ukoka ukatwe vizuuuurrrriiii😂🤣😂🤣😂
 
Back
Top Bottom