Ukiwa shabiki wa Arsenal unaweza kufa wakati wowote

mpimamstaafu

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2018
Posts
4,445
Reaction score
4,707
Hakika nawaonea huruma sana mashabiki wa Klabu ya Arsenal.Klabu isiyo na uhakika wa kushinda mechi,iwe inacheza ugenini au uwanja wa nyumbani,wakishinda sana ni Draw match.Nadhani wamiliki wa Klabu ya Arsenal sio watu wa Mpira wapo pale kibiashara tu,timu inavurunda timu inauza wachezaji muhimu ,timu inasajili wachezaji wenye uwezo mdogo,ni vema Arsenal ikawekeza kwa vijana wadogo na kuwapa mechi kama ifanyavyo Chelsea na Bayern ili mwisho wa siku iepukane na Usajili ambao Arsenal haina uwezo wa kusajili wachezaji wenye uwezo mkubwa.Kwa mwenendo huu Mashabiki wa Arsenal mjiandae Kufa ghafla kwa hayo matokeo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuweni wavumilivu, hata Liverpool nayo miaka michache iliyopita ilikuwa inasuasua tu. Ila kwa sasa wanatabasamu muda wote! maana Klopp anawafikisha tu kileleni.
 
Kufa ghafla siwezi aiseee Mana me mwenyewe Arsenal damu,,,Pale Arsenal hatupangi kushindwa Ila tunashindwa kupanga. Ila dah mechi 20 pointi 24 πŸ™„πŸ™„πŸ™„
 
Arseno ilifariki na kuzikwa miaka mingi limebaki jina tu na mzimu ndio unaowasumbua,hamieni kWa kina Rashid hamtojutia!!!
 
Watu hatushabikii arsenal sababu ya makombe au big 4..
Mfano mimi toka naanza shabikia arsenal mwaka 2007 sijawahi kuchukua EPL... nimechukua FA na ngao ya hisani tu NA BADO SINA MPANGO WA KUHAMA TIMU..

watu wangekuwa wanashabikia mpira kisa makombe nadhani watu woote walioshabikia mpira kuanzia 2008 wangekuwa madrid na barca maana kule wanapata kila kitu kuanzia soka safi hadi makombe..

Arsenal.tunaishabikia hata ilishuka daraja tutashuka nayo na tutapanda nayo.. mambo ya kupoteza mechi 6 ndio soka lenyewe na ndio inafanya soka liwe exciting
 
Mkuu ingekuwa hamshabikii kwa ajili ya makombe isingeingia kwenye mashindano yoyote

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…