Ukiwa umeenda kuosha gari zingatia haya

Ukiwa umeenda kuosha gari zingatia haya

Gentlemen_

JF-Expert Member
Joined
Nov 24, 2019
Posts
4,431
Reaction score
13,876
1- Hakikisha vitu vyako ulivyoacha ndani ya gari:

- USB flash, Charger, hela, na vitu vingine vidogovidogo ni vyema ukavitia ktk mfuko maalumu ukashuka navyo. Huwa si rahisi kubaini kama vimeibiwa kwa haraka mpaka utakapotoka eneo la tukio.

-Mtindo wa kubadiri vitu au kuiba kabisa hasa Carpets, jana nimeenda kuosha "Mkweche" wangu, wakati anarudishia Carpets hakuweka zote maana hii gari ina Carpets mbili mbili. Yeye akaweka moja moja zingine akasema hazikuwepo, alikuta hivyo. Na mimi sikubishana nae nikasema sawa nikaondoka.

-wengi wanapewa ORDER na watu kwamba nitafutie kitu fulani ambacho kiuhalisia madukani si rahisi kukipata au ni ghali sana, mfano kuna rubber zinazozuia vumbi matope etc ktk baadhi ya sehemu hasa nyuma ya gari huwa wanazichomoa, fuse mbalimbali etc kuna jamaa yangu aliacha gari kuosha akaenda kunywa pombe, walimbadirishia Control box, kurudi gari haiwaki (Baadae kule garage ndio wakagundua Control Box imechapwa)

Spika ndogo ndogo zinazokaa nyuma ya gari ktk baadhi ya magari huwa wanazibandua, wewe huwezi jua siku hiyo hiyo.

2- Kujifanya madereva wakiona gari kali, nzuri au imekaa mkao wa kipekee:-

Hii imenikuta hivi karibuni, nimeenda kuosha gari, akataka nimuachie funguo ya kuisogeza nikamuuliza unaiweza hii gari? Akaitikia ndio naiweza naendesha malori ije inishinde hii?. Kwa confidence yake mie nikamuachia funguo nikakaa pembeni. Baada ya kuosha nikasikia gari imewasha huku imekanyagiwa mafuta (Full Throttle). Akatia gia gari ikaruka na kuzima, bahati nzuri mbele kulikuwa na Tank ambalo halina maji so lile TANK lilisogezwa kwa umbali tu. Nikaenda kumuuliza imekuwaje? akasema alitak kwenda nyuma, badala aweke Reverse yeye akaweka gia namba 5. (Hii gari ni Manual ya 6 gears, na gearbox yake imegeuka sio ordinary) yeye kwa kukariri kwake akataka aniingize hasara.

Tuwe makini na hawa WAOSHA magari hasa ktk kipengele cha kusogeza gari.

3- Kutumia Pressure ya maji katika sehemu ambayo haina haja:-

Anaweka high pressure ktk sehemu sensitive kama ktk taa hasa upande wa nyuma kwenye waya, kama gari yako rangi yake imevimba kidogo atatia pressure hapo mpk rangi inabanduka. Yaan hawaangalii pakutumia high pressure na low pressure.

4- Kuosha Engine (INJINI) bila uangalifu:-

- Kuna magari ni very sensitive ktk maji, hasa haya ya umeme. Unakuta mtu anaenda kupigilia high pressure ktk engine bila tahadhari mwisho wa siku anakuletea faults zisizo na maana. Ni heri uoshe kwa mvuke au afute tu engine-bay yote.

5- Wanasoma Documents zako:

Nilifanya research fupi tu baada ya kufuta kitambulisho changu na kukificha nyuma ya siti pia nilikiweka katikati ya Documents zingine huku nikiziunganisha ndani ya bahasha, nilifanya maksudi.

Baadae wakati nimerudi home nikacheck zile Documents nikakuta zimewekwa ndivyo sivyo na ile ID imeshikwa shikwa inaonyesha Fingerprints. Nikajisemea hawa kumbe nikiacha vitu vyangu humu wanapekua pekua instead of kufanya wanachotakiwa kufanya.

Ni hayo tu, Je wewe ulikutana na Changamoto gani kwa hawa Waosha Magari?

Rejea:- Muosha Magari apatisha ajali gari lenye thamani zaidi ya Milioni 100. Akutwa anaruka sarakasi
 
Kuna mpuuzi alichukua simu yangu nilisomba kijiwe kizima ikapatikana simu.

Jamaa alinipokea akatoa carpets akasema anaenda kuchukua maji kumbe ameona simu akaibeba akapeleka kwenye saluni ya jirani alivyorudi akampa mshkaji mwingine aendelee kuosha gari.

Yule dogo mwingine bila kujua aliosha akamaliza nami sikuhangaika na simu sababu nilikuwa naosha fasta tu nipunguze tope sababu nilikuwa nafata wageni wangu na Ile siku kulikuwa na mvua.

Ile natoka nacheki simu ili niwapigie nakuta haipo simu hapo hapo nikawauliza wakazingua Mie nikakausha nikaenda straight police nikabeba Askari tukaja kusomba wote.

Baada ya kipigo yule wa Kwanza askari walikomaa nae sababu walishamhisi kulingana na maelezo na mazingira pamoja na muonekano wake pia wenzake wote walimnyooshea yeye sababu alishawahi kulalamikiwa na baadhi ya wateja na jamaa zake kijiweni walishamuonya kulikuwa na ras mmoja akasema tukomae nae.

Alitaja akatupeleka mpaka alipopeleka nikapata simu yangu fasta nikawakabidhi wale watuhumiwa kwa Askari wajichukulie posho yao mie nikasepa.

So kama kijiwe hukijui heri kuwa makini.
 
Zipo sehemu za hovyo japo sio zote kwangu walichomoa kile kiplastic cha sehemu ya kufungulia tank ya mafuta. Niliporudi wakasema hawajaona na ni car wash very smart ila nadhani walipata kijana wa kazi wa hovyo. Since that day sijaenda tena.

Ila pia kama gari chafu sana ni kheri kuosha nje tu kama Car wash hauifahamu vizuri au kuwaamini.

Ila idea ya kuweka vitu kwenye mfuko au kuvipanga vizuri kwa pamoja ni nzuri vijana wanatafuta hela kwa pinde sana
 
Unamkuta muoshaji amekaa miguu juu kawasha zake radio anakula mziki. Kusema kweli waosha magari wengi sio wastaarabu. Wengine ukiwaachia funguo wanazicopy. Kama usafi wa kawaida na kwako kuna maji ya kutosha bora tu kuoshea nyumbani.
 
Fanya Practical ewe mwenye gari:

Nunua Chocolate ama biscuits kidogo zipake pilipili kichaa za kutosha nenda nazo car wash, ziache kwenye gari halafu uone hao TUMBILI wadokozi watakavyolia na kusaga meno..

Hutaua ila utawakomesha!

Baadae waambie zilikua za kutegemea panya nyumbani
 
1- Hakikisha vitu vyako ulivyoacha ndani ya gari:-

- USB flash, Charger, hela, na vitu vingine vidogovidogo ni vyema ukavitia ktk mfuko maalumu ukashuka navyo. Huwa si rahisi kubaini kama vimeibiwa kwa haraka mpaka utakapotoka eneo la tukio.

-Mtindo wa kubadiri vitu au kuiba kabisa hasa Carpets, jana nimeenda kuosha "Mkweche" wangu, wakati anarudishia Carpets hakuweka zote maana hii gari ina Carpets mbili mbili. Yeye akaweka moja moja zingine akasema hazikuwepo, alikuta hivyo. Na mimi sikubishana nae nikasema sawa nikaondoka.

-wengi wanapewa ORDER na watu kwamba nitafutie kitu fulani ambacho kiuhalisia madukani si rahisi kukipata au ni ghali sana, mfano kuna rubber zinazozuia vumbi matope etc ktk baadhi ya sehemu hasa nyuma ya gari huwa wanazichomoa, fuse mbalimbali etc kuna jamaa yangu aliacha gari kuosha akaenda kunywa pombe, walimbadirishia Control box, kurudi gari haiwaki (Baadae kule garage ndio wakagundua Control Box imechapwa)

Spika ndogo ndogo zinazokaa nyuma ya gari ktk baadhi ya magari huwa wanazibandua, wewe huwezi jua siku hiyo hiyo.

2- Kujifanya madereva wakiona gari kali, nzuri au imekaa mkao wa kipekee:-

Hii imenikuta hivi karibuni, nimeenda kuosha gari, akataka nimuachie funguo ya kuisogeza nikamuuliza unaiweza hii gari? Akaitikia ndio naiweza naendesha malori ije inishinde hii?. Kwa confidence yake mie nikamuachia funguo nikakaa pembeni. Baada ya kuosha nikasikia gari imewasha huku imekanyagiwa mafuta (Full Throttle). Akatia gia gari ikaruka na kuzima, bahati nzuri mbele kulikuwa na Tank ambalo halina maji so lile TANK lilisogezwa kwa umbali tu. Nikaenda kumuuliza imekuwaje? akasema alitak kwenda nyuma, badala aweke Reverse yeye akaweka gia namba 5. (Hii gari ni Manual ya 6 gears, na gearbox yake imegeuka sio ordinary) yeye kwa kukariri kwake akataka aniingize hasara.

Tuwe makini na hawa WAOSHA magari hasa ktk kipengele cha kusogeza gari.

3- Kutumia Pressure ya maji katika sehemu ambayo haina haja:-

Anaweka high pressure ktk sehemu sensitive kama ktk taa hasa upande wa nyuma kwenye waya, kama gari yako rangi yake imevimba kidogo atatia pressure hapo mpk rangi inabanduka. Yaan hawaangalii pakutumia high pressure na low pressure.

4- Kuosha Engine (INJINI) bila uangalifu:-

- Kuna magari ni very sensitive ktk maji, hasa haya ya umeme. Unakuta mtu anaenda kupigilia high pressure ktk engine bila tahadhari mwisho wa siku anakuletea faults zisizo na maana. Ni heri uoshe kwa mvuke au afute tu engine-bay yote.

5- Wanasoma Documents zako:-

Nilifanya research fupi tu baada ya kufuta kitambulisho changu na kukificha nyuma ya siti pia nilikiweka katikati ya Documents zingine huku nikiziunganisha ndani ya bahasha, nilifanya maksudi.

Baadae wakati nimerudi home nikacheck zile Documents nikakuta zimewekwa ndivyo sivyo na ile ID imeshikwa shikwa inaonyesha Fingerprints. Nikajisemea hawa kumbe nikiacha vitu vyangu humu wanapekua pekua instead of kufanya wanachotakiwa kufanya.

Ni hayo tu, Je wewe ulikutana na Changamoto gani kwa hawa Waosha Magari?
Namshukuru sana Mungu kwa kunipa upekee!Mimi gari nalioshea nyumbani na fundi wa kutengeneza ni nyumbani,nikisafiri linabaki na tope hadi nirudi nyumbani.
 
Kuna mpuuzi alichukua simu yangu nilisomba kijiwe kizima ikapatikana simu.

Jamaa alinipokea akatoa carpets akasema anaenda kuchukua maji kumbe ameona simu akaibeba akapeleka kwenye saluni ya jirani alivyorudi akampa mshkaji mwingine aendelee kuosha gari.

Yule dogo mwingine bila kujua aliosha akamaliza nami sikuhangaika na simu sababu nilikuwa naosha fasta tu nipunguze tope sababu nilikuwa nafata wageni wangu na Ile siku kulikuwa na mvua.

Ile natoka nacheki simu ili niwapigie nakuta haipo simu hapo hapo nikawauliza wakazingua Mie nikakausha nikaenda straight police nikabeba Askari tukaja kusomba wote.

Baada ya kipigo yule wa Kwanza askari walikomaa nae sababu walishamhisi kulingana na maelezo na mazingira pamoja na muonekano wake pia wenzake wote walimnyooshea yeye sababu alishawahi kulalamikiwa na baadhi ya wateja na jamaa zake kijiweni walishamuonya kulikuwa na ras mmoja akasema tukomae nae.

Alitaja akatupeleka mpaka alipopeleka nikapata simu yangu fasta nikawakabidhi wale watuhumiwa kwa Askari wajichukulie posho yao mie nikasepa.

So kama kijiwe hukijui heri kuwa makini.
Sasa unakuta upo Safarini lazima uoshe sehem mpya au ambayo hujazoea kuosha siku zote. Na wakishajua kuwa wewe ni wa kupita tu mara nyingi lazima wakuchape.
 
Back
Top Bottom