Ukiwa unachagua shule ya msingi kwa ajili ya Mtoto wako unazingatia vitu gani? Ukiachana na performance ya Taaluma?

Ukiwa unachagua shule ya msingi kwa ajili ya Mtoto wako unazingatia vitu gani? Ukiachana na performance ya Taaluma?

Jumanne Mwita

JF-Expert Member
Joined
Nov 18, 2014
Posts
530
Reaction score
1,446
Changamoto inayowakumba wazazi wengi wanaotafuta elimu bora kwa watoto wao licha ya vipato vidogo.

Ndugu wanajamii, mimi ni mzazi naomba msaada wenu kupata shule bora na yenye gharama nafuu kwa mtoto wangu mwenye umri wa miaka 7 anayetarajia kuingia darasa la 4 mwakani lakini ninampango wa kumrudisha darasa la 3.

Maendeleo ya kitaaluma si ya kuridhisha. Nimegundua kwamba mwalimu mara nyingi hawana muda wa kumfundisha mtoto kwenye shule hizi za serikali, na mtoto akiona hivi kwamba ufuatiliaji shuleni si mzuri na wao wanaendekeza michezo sana matokeo yake mtoto anakuwa mjinga mjinga tu. Natamani kumpa mazingira bora ya elimu ili kufungua milango ya maarifa kwake, lakini kipato changu ni cha kawaida sana.

Naomba msaada katika mambo yafuatayo:

1. Shule gani bora na yenye gharama nafuu unayoijua naomba unisaidie kama unaijua kwa ambae uko hapa Katoro.

2. Kwa mtazamo wako, unachagua shule ya msingi kwa mtoto wako kwa kuzingatia mambo gani, zaidi ya performance ya kitaaluma?

3. Kwa hali kama yangu, unashauri nifanye nini ili kumsaidia mtoto wangu kupenda na kuelewa masomo zaidi?

Nimejaribu kuwasiliana na mwalimu wake mara kadhaa, lakini majibu huwa ni kwamba "tunaenda naye taratibu." Hata hivyo, najua mtoto ana uwezo, lakini mazingira anayosomea yanamkwamisha.

Naamini kwa pamoja tunaweza kusaidiana ili kujenga kizazi bora.

Maoni kutoka kwa wazazi wengine waliopitia changamoto kama zangu.
 
Sasa unakinzana na bwana LIKUD ambaye ni pioneer wa shule za serikali.
Tumngoje aje atoe maelekezo
 
Uwingi wa wanafunzi

Umbali

Idadi ya walimu kwa wanafunzi (ratio yake i mean)

Vifaa vya kujifunzia (ni ngumu kujua hadi ufuatilie sana)

Usalama wa mtoto

Ushindani wa kitaaluma na shule nyenzie

Ufuatiliaji wa walimu kwa mwanafunzi na feedback za haraka kwa mzazi
 
Mtoto Yuko na seven years then yupo class four Tena St kayumba! What a joke.... Anyway watoto mnawawaisha kuwaingiza mashulen huku age Bado...umri huo awe class two
 
Shida hapo sio mtoto wala shule anayosoma shida ni wewe mzazi.
You have too much expectation.
Utamtesa sana huyo mtoto.

Nawaza haya.
-Mtoto wa miaka saba na yupo darasa la tatu, Why ulimuahisha hivyo?
-Unataka arudie darasa la tatu, unataka kumdumaza kiakili?
-Unataka kumuhamisha shule kwenda shule usiyoijua, unataka kumchanganya mtoto?

Mimi nakuambilia hili, mtoto ambaye hajavuka miaka 8, kuwepo shuleni ni ili kuzoea mazingira ya shule, kucheza, kuhesabu, kusoma na kuandika. Vingine vyote ni kumpotezea muda tu.
 
Katoro shule za serikali zina idadi kubwa mno ya wanafunzi.

Private nazo ni chache mno na hazijawa na ubora wa kuridhisha bado.
 
Changamoto inayowakumba wazazi wengi wanaotafuta elimu bora kwa watoto wao licha ya vipato vidogo.

Ndugu wanajamii, mimi ni mzazi naomba msaada wenu kupata shule bora na yenye gharama nafuu kwa mtoto wangu mwenye umri wa miaka 7 anayetarajia kuingia darasa la 4 mwakani lakini ninampango wa kumrudisha darasa la 3.

Maendeleo ya kitaaluma si ya kuridhisha. Nimegundua kwamba mwalimu mara nyingi hawana muda wa kumfundisha mtoto kwenye shule hizi za serikali, na mtoto akiona hivi kwamba ufuatiliaji shuleni si mzuri na wao wanaendekeza michezo sana matokeo yake mtoto anakuwa mjinga mjinga tu. Natamani kumpa mazingira bora ya elimu ili kufungua milango ya maarifa kwake, lakini kipato changu ni cha kawaida sana.

Naomba msaada katika mambo yafuatayo:

1. Shule gani bora na yenye gharama nafuu unayoijua naomba unisaidie kama unaijua kwa ambae uko hapa Katoro.

2. Kwa mtazamo wako, unachagua shule ya msingi kwa mtoto wako kwa kuzingatia mambo gani, zaidi ya performance ya kitaaluma?

3. Kwa hali kama yangu, unashauri nifanye nini ili kumsaidia mtoto wangu kupenda na kuelewa masomo zaidi?

Nimejaribu kuwasiliana na mwalimu wake mara kadhaa, lakini majibu huwa ni kwamba "tunaenda naye taratibu." Hata hivyo, najua mtoto ana uwezo, lakini mazingira anayosomea yanamkwamisha.

Naamini kwa pamoja tunaweza kusaidiana ili kujenga kizazi bora.

Maoni kutoka kwa wazazi wengine waliopitia changamoto kama zangu.
Mpeleke shule ulioyosoma wewe
 
Matini yaliyoweka katika kila darasa kwa asilimia kubwa yanaendana na umri wa mtoto.

Ikiwa mtoto wako sio genius basi kutokufanya vizuri kwake pengine ni kutokana na umri wake vs matini anayopewa shuleni.

Sasa kwa mtoto wa miaka 8 kuingia std IV naona kama umemuwahisha shule.

Ukiforce akapenya hapo atakutana na mtiti wa sekondari.

Mrudishe darasa hapohapo anaposoma, mtafute mwalimu muadilifu au mwalinu wake wa darasa kaa naye uzungumze naye namna nzuri ya kumfuatilia mwanao shuleni.

Na wewe akirudi nyumbani ufanye follow up hata mara 3 kwa wiki.
 
Back
Top Bottom