Ukiwa unaweka mafuta full tank inapunguza ulaji wa mafuta kwenye gari?

Ukiwa unaweka mafuta full tank inapunguza ulaji wa mafuta kwenye gari?

Hizo point zako 1-4 ndio nilizoziita "constant of proportionality" kwenye maelezo yangu. Huwezi kuzifanya zikawa "variables" wakati unataka kufanya ufafiti gari inakula mafuta zaidi ikiwa full tank au half tank. Kwa hiyo tuko palepale.
Nami kwa uzoefu wangu, naona gari linatumia mafuta yale yale, yawe full tank au robo...
Kikubwa tujikite kwenye zile sababu nilizozitoa..
 
Dah...enzi zile za skonga...hii tulikuwa tunaita kuingia Chaka.....hoja ya Uzi ni nyingine na wewe unahitimisha kivingine [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji2960]
Hapana...sijaingia chaka..
Huu uzi naufuatilia tangu ukiwa na zero comments..

Hoja yangu ya msingi kama umenielewa ni kwamba mafuta kuwa full tank au robo tank hayana uhusiano na gari kula mafuta zaidi...
Bali kinachofanya gari kula mafuta zaid ni hizo sababu 4 nilizozieleza...na wengi wameeleza hivyo..

Faida ya kuweka mafuta full tank zipo nyingi ikiwepo kutunza fuel pump na fuel injectors...lakini si kufanya gari litumie mafuta kidogo...

Ikunbukwe magari ya siku hizi yana computer... computer ndiyo inaamua injectors zifunguke namna gani bila kujali tank lina lita ngapi.
 
Habarini wapendwa, Nisiwachoshe niende moja kwa moja kwenye mada, je gari ukiwa unaweka full tank na sio ya mafuta ya buku kumi kumi inapunguza ulaji wa mafuta?

Yaani kuna mtu kanishauri gari yangu niwe naweka full tank siku ikikaribia kuisha najaza tena eti nisiwe naweka ya buku kumikumi inakuwa inakunywa sana, je ni kweli?

Kwa wenye uelewa nielewesheni plz.
Namimi niweke mchango wangu kidogo hapa kwa maelezo rahisi kueleweka hasa kwa matu ambaye hajapita kwenye saiyansi
1. Mafuta kwenye chombo cha moto huhesabiwa kama mzigo hivyo ukiweka full tank maana yake umeweka mziko mkubwa
Hivyo wanapendekeza kama upo mjini uweke wastani wa nusu tank hivi li upate maleage nzuri ila kama upo nje ya mji ambapo vituo vya mafuta viko mbali weka tu full tank kwa kuwa tofauti ni ndogo sana
2. Ukitaka kupata maileage nzuri ( kutumia mafuta kidogo)
a. Usibebe mizigo au kuendesha huku umebeba vitu vizito ndani ya gari
b. Jaza tairi ziwe na upepo stahiki
c. Fanyia gari service kwa wakati
d. Usitumie Aircondition kama sio muhimu sana. ; unaweza kuvaa nguo nyepesi badala yake
e. Wakati unaendesha tumia gia sahihi; kwenda polepole sana mafuta huenda mengi ( mwendo mzuri ni km 60 hivi na 90)
f. mwisho epuka kukimbiza na kutumia tumia break mara kwa mara kwani huongeza ulaji wa mafuta badala yale, achia mafuta gari ipunguze mwendo yenyewe

Kwa kufanya hayo unapatapa matokeo mazuri na ikikupendeza unipe mrejesho
 
We jamaa muongo kweli wewe duuh,uhalisia gari inapokuwa na full tank ulaji unakuwa mzuri unapata km za kutosha tofauti na mafuta ya kidebe.
Kweli kabisa. Na si unajua dunia ni tambalare lakini watu wanasema ni duara kama tufe? Waongo sana. Ingekuwa duara kama tufe tungewezaje kutembea juu ya dunia, si tungekuwa tunaanguka!
 
Ikunbukwe magari ya siku hizi yana computer... computer ndiyo inaamua injectors zifunguke namna gani bila kujali tank lina lita ngapi.
Hebu niambie, hizo computer zinazoamua injectors kufungua zaidi au kidogo, kitu gani kinazifanya computer ziwaambie kina injector fungua zaidi au kidogo?
 
Hebu niambie, hizo computer zinazoamua injectors kufungua zaidi au kidogo, kitu gani kinazifanya computer ziwaambie kina injector fungua zaidi au kidogo?
Kitu kinachofanya kompyuta iungue injectors zaidi ni
1..ukanyagaji wako wa accelerator
2..Mzigo..kama umebeba mizigo gari litahitaji nguvu ya ziada..
3...plugs ambazo hazichomi vizuri..hapa mafuta yataingia mengi kwenye combustion chamber kufidia nguvu iliyopotea.
4...Mfumo mzima wa hewa kuanzia air filter, MAF sensor, throttle body...kama kuna chenye hitilafu, computer itafungua injectors zaidi ili kufidia nguvu inayopetea..

Computer haifungui injectors zaidi kwa sababu tank lina lita chache za mafuta..

Gari kula mafuta zaidi ya yale yaliyokadiriwa kuna factors nyingi sana, ila si suala la tank kuwa full au robo
 
Namimi niweke mchango wangu kidogo hapa kwa maelezo rahisi kueleweka hasa kwa matu ambaye hajapita kwenye saiyansi
1. Mafuta kwenye chombo cha moto huhesabiwa kama mzigo hivyo ukiweka full tank maana yake umeweka mziko mkubwa
Hivyo wanapendekeza kama upo mjini uweke wastani wa nusu tank hivi li upate maleage nzuri ila kama upo nje ya mji ambapo vituo vya mafuta viko mbali weka tu full tank kwa kuwa tofauti ni ndogo sana
2. Ukitaka kupata maileage nzuri ( kutumia mafuta kidogo)
a. Usibebe mizigo au kuendesha huku umebeba vitu vizito ndani ya gari
b. Jaza tairi ziwe na upepo stahiki
c. Fanyia gari service kwa wakati
d. Usitumie Aircondition kama sio muhimu sana. ; unaweza kuvaa nguo nyepesi badala yake
e. Wakati unaendesha tumia gia sahihi; kwenda polepole sana mafuta huenda mengi ( mwendo mzuri ni km 60 hivi na 90)
f. mwisho epuka kukimbiza na kutumia tumia break mara kwa mara kwani huongeza ulaji wa mafuta badala yale, achia mafuta gari ipunguze mwendo yenyewe

Kwa kufanya hayo unapatapa matokeo mazuri na ikikupendeza unipe mrejesho

Dah...hapo kwenye d. Ukiwa unaendesha katikati ya mji ni Sawa...lakini kama unaendesha kwa kasi ya zaidi 60km/saa ukifunga madirisha na kutumia kiyoyozi utaokoa hadi asilimia 17 ya mafuta tofauti na ukifungua madirisha [emoji2960]
 
Kwa experience yangu ya kujaza mafuta full tank nimegundua kwamba ukijaza full tank mafuta hayaendi mengi. Kwa mfano mi nikijaza gari yangu full na nikashindilia kabisa nikiwa natoka dodoma kuja dar natembeaga hadi Morogoro ule mshale wa full ukiwa haujashuka. Hii picha hapa nilikuwa nimetoka Dodoma na hapo nilikuwa chalinze ndo mshale ukawa hivyoView attachment 1811016
🤣🤣🤣 so Dodoma mpaka chalinze zimeshuka bar 2? Tz sihami
 
Gari inakunywa mafuta kulingana na matumizi na sio kulingana na lita ngapi zimebakia kwenye tank.

Process ya kuvuta mafuta na kuyachoma ina correspond relatively with driving and maintenance condition ya gari yako.

Ukiwa unazimua hovyo na kuchochea peda lazima yatalika sana. Factors za kuliwa mafuta zipo nyingi sana.
 
Back
Top Bottom