Ukiwa unaweka mafuta full tank inapunguza ulaji wa mafuta kwenye gari?

Ukiwa unaweka mafuta full tank inapunguza ulaji wa mafuta kwenye gari?

Engine inapoa vizuri kisa mafuta yapo full??? I Hii mpya.... As far as I know, fuel level is not part of the cooling system...

Fuel pump ipo affected na uchafu kwenye mafuta au kuvuta hewa.. Any level above sunction pipe is OK kwa gari.. Hayo ya full tank kuongeza efficiency ya fuel pump ni ramli hiyo

Tusisahau kuna fuel pump
Pump huwa inapata moto. Mafuta yakiwa mengi yanasaidia kwenye cooling ya pump.
 
Hii ndio huwa tunaita over thinking. Enzi zile tuko tuko shule kwenye Math unakuta mtu amekokotoa karatasi nzima halafu kapata 2/10.

Kitaalam haya mawazo uliyotoa tunaweza kusema UMECHOPEKA.

Hebu tukuulize
Kwa mfano IST FULL TANK ni lita ngapi?? Convert hizo lita kwa kg, halafu linganisha na uzito wa mtu mzima mmoja Tuambie kama huo uzito ukiamua kupunguza nusu yake utaokoa mafuta kiasi gani?

Usilinganishe load ya mafuta ya ndege na ya gari. Ndege inaweza kubeba mafuta yenye uzito mkubwa unaweza Kufikia 1/3 ya uwezo wake wa kubeba mzigo. Lakini hakuna gari inayoweza kubeba mafuta yake yenyewe yenye uzito wa 1/3 ya uwezo wa gari.
point. nawashangaa sana wanaofananisha gari na ndege.
 
Mkuu kwa kuuliza kuwa full tank ni lita ngapi inaonyesha wazi kwamba umekuja kubisha bila kujua hata haya mambo ya magari. Unabisha tu kwa kuwa una nafasi ya kufnya hivyo. Full tank capacity za magari zinapishana kwa kila aina ya gari, kwa hiyo kuuliza full tank ni lita ngapi haina lojiki.

Labda tuanzie gari kama Nissan Patrol. Inachukua lita 90 kuwa full tank, ambazo kwa kiasi ni kama Kg 90. Njoo BMW. Lita kama 7o, kilo 70. Halafu hizi IST labda full tank litre 45 sana na karibu kilo 45. Sasa unaniambia huo uzito si hoja?

Halafu, kama umesoma hii thread, umeshapewa hadi reference ya watu walifanya utafiti tasmi juu ya hili, wewe unakuja na point zako yeboyebo hapa.

Ist petrol lita 45 iwe karibu kg 45?

Hii ni hesabu ya wapi?

Nani kakuambia petrol ina density sawa na maji?

Acha hizo bhana.
 
Wewe poyoyo sana! Eti ndege inabeba tani 30 za mafuta na gari kubwa lita ishirini tu. Sasa kama ungekuwa na akili kama unavyodai, ungeelewa kwamba kama ukikubali hii theory ni kweli kwa ndege basi ni kweli kwa magari. Unachotakiwa kufanya ni kuingiza factor ya uzito wa ndege kwa uzito wa gari, na kutumia hiyo ratio katika kuangalia fuel capacity ya ndege kwa fuel capacity ya gari. Yaani scale down the the aircraft weight to fuel capacity ratio to the vehicle weight to fuel capacity ratio and see what you get.

Lakini kwa sababu ulikimbia shule huwezi kuelewa utabisha tu kipoyoyo
Hapa umeandika upupu mwingine. Ndege na gari hazifanani. Narudia tena.
 
Wewe unazungumzia gari ya Diesel mimi nazungumzia gari ya petrol.
Hiyo hiyo ya petrol... embu angalia pump location ya escudo. Ipo juu ta tank...

1624090607553.png
 
Una trivialize hoja. Iwe umesema ndege inabeba mafuta tani 30 au 10 za mafuta au ngapi sio hoja kuu hapo, suala ni kwamba mfano wako ni wa kipoyoyo na uliutoa ili kunionyesha mie sijui na unastahili jibu nililokupa. Shule yangu ni UDSM. Sasa kama uliikimbia na kwenda "equivalents" nadhani hapo ndio tatizo lako lipo.
Jamaa anaandika vizuri.. lakini kiongozi unaandika kikorofi Sana..sio poa
 
Ist petrol lita 45 iwe karibu kg 45?

Hii ni hesabu ya wapi?

Nani kakuambia petrol ina density sawa na maji?

Acha hizo bhana.
Density ya petrol 0.71–0.77 kg/L, density of water karibu 0.91 kg /L

Sasa unajua maana ya kusema litre 45 ambazo ni karibu na Kilo 45?

Na wewe acha kubisha kipoyoyo
 
Kwa maswali yako haya inabidi kwanza nikupeleke VETA, maana umeuliza maswali ambayo kwa kweli uko mbali sana na ufahamu wa magari. Lakini ngoja nijaribu kukujibu;

1. Fuel consumption kwa gari husika huwa inakadiria gari ikiwa na mzigo wote inayopaswa kubeba?
Nimekuelewa. Good question. Sidhani, labda kwa gari za mizigo. Gari ya tani 7, wakisema fuel consumption ni 15l/100km ina make sense kwamba hiyo ndio consumption rate gari ikiwa na mzigo wa tani saba katika normal driving. Kwa gari ndogo za abiria mara nyingi consumption ni ukiwa dereva peke yako bila mzigo, kwa hiyo kwa kiasi fulani watakuwa wanadanganya.

2. Fuel consumption huwa inapigwa kwa kuzingatia hali zote za barabara wakati gari ikiwa na mzigo inayostahili kubeba?
Swali halieleweki
Lakini kama una maana fuel consumption inapimwaje, ni kwamba zile zinazoonyeshwa kwenye gari huwa unapewa wastani kwa driving ambayo hauko kwenye rough road na ya lami (normal driving). Kumbuka, kiwango kizuri cha kujua wastani wa fuel fuel consumption yako ni wakati uko spidi kati ya 80-100km/hr. Ukiendesha mwendo taratibu sana unakuwa unatumia gia kubwa na gari inakula mafuta zaidi. Ukiendesha kwa kasi sana, unapotita spidi ya 110km/hr injini inafanya kazi zaidi kwa hiyo inahitaji mafuta zaidi.


3. Ukiwa na tank la lita 10,000 katika umbali wa mita 3 toka ardhini, ukalijaza full, ukianza kutumia maji kutoka kwenye tank hilo, pressure ya maji wakati tank liko full na wakati liko nusu au robo ya mwisho kuisha inakuwa sawa?
Pressure inakuwa kubwa wakati tenki limejaa. Lakini hapa unaogolea flow ya maji kwa kutumia gravity. Gari hazipeleki mafuta kwenye injini kwa kutumia gravity, zinatumia fuel pump. Kwa hiyo hii theory yako hai-apply kwenye gari

4. Ukiwa na closed circuit tuseme ya maji ambayo iko pressurized kwa 3bar, ukaamua kutoa maji kwa kufungua point moja tu ya kutolea maji, maji yote yatatoka?
Hapa unaongelea juu ya flow effect ya atmospheric pressure na pressure head kwenye container. Ukiweka maji kwenye kopo ukatoboa tundu moja juu moja chini, maji yatatoka ikiwa matundu yote yako wazi. Ukiziba tundu la juu hayatatoka. Pressure head ikiwa sawa na atmospheric pressure kwenye tundu la chini asi maji hayatatoka. Sababu mojawapo ni kwamba unakuwa ume create vaccum juu ya maji ndani ya kopo. Ukiondoa kidole tundu la juu unaua effect ya vacuum, na pressure ya chini ya kopo ni atmospheric pressure + pressure head ya container, na maji yanaanza kutoka tena tundu la chini. Mfumo wa mafuta ya gari umetengenezwa kwa kutoruhusu kutengeneza vacuum mafuta yanapopungua.

5. Ni wakati gani pump ya mafuta ina effect kubwa zaidi kwenye uvutaji wa mafuta, full tank au half or one fourth of tank?
Effect ya pump ya mafuta iko vilevile, uwe na full tak au half tank. Iko calibrated kunyonya kiasi kile kile cha mafuta, na kama ikiathirika na mafuta kuwa nusu au full tank imeharibika, peleka gari gereji
If you know, you know
 
Hakuna jibu la maana ulilopewa hadi sasa. Ukweli ni kwamba ukiweka gari full tank utatumia mafuta zaidi katika kuendesha gari kadiri yafuta yalivyo mengi, kwa sababu mafuta yanakuwa sehemu ya mzigo katika gari kwa hiyo injini inabidi ifanye kazi ya ziada kubeba mzigo wa mafuta.

Kihesabu tunasema fuel consumption is directly proportional to fuel level in the tank; C = kL, where C = fuel consumption rate, k = constant of proportionality, na L ni fuel level in the tank. Hiyo "k" ni assumption kwamba factors nyingine hazibadiliki, mfano idadi ya abiria ndani ya gari. Au kwa njia rahisi ni kwamba, rate ya consumption ya mafuta iko directly proportional na uzito wa gari. Kwa hiyo kadiri unavyojaza tank ndivyo unavyoongeza uzito wa gari na ndivyo gari itakula mafuta zaidi. Ulaji wa mafuta utapungua kadiri mafuta kwenye tank yanavyopungua, au kadiri uzito wa gari (load) unavyopungua.

Hiyo pia ndio sababu ndege haziweki full tank zinaporuka kwenda safari fulani, wanaweka mafuta yatakayotosha kuwafikisha wanapokwenda, na ziada kidogo ya emergency

Ndio maana unashauriwa usiweke vitu usivyohitaji kwenye buti ya gari kwa kuwa inafanya gari itumie mafuta zaidi. Utakuwa umesikia watu wakisema magari ya siku hizi ni karatasi sana tofauti na ya zamani - ni kweli na hilo lilifanyika ili kupunguza uzito wa gari ili lisitumie mafuta kwa wingi.
Kumbe ndio maana tunanyimwa lift kwakuwa tutatumia mengi?
 
Hiyo hiyo ya petrol... embu angalia pump location ya escudo. Ipo juu ta tank...

View attachment 1823432
Mkuu hata kama pump iko juu ya tenk sio tatizo. Angalia hizo pipe mbilitoka kwenye pump zimeenda hadi chini kabisa ya tenk. Moja itakuwa ya kuvuta na nyingine ni return. Kwa hiyo hata mafuta yawe nusu au yamejaa sio tatizo. Na unaona ziko chini sana ndio maana unaambiwa sio vizuri kuendesha gari hadi mafuta yakauke kabisa kwenye tenki na gari izimike
 
Hakuna jibu la maana ulilopewa hadi sasa. Ukweli ni kwamba ukiweka gari full tank utatumia mafuta zaidi katika kuendesha gari kadiri yafuta yalivyo mengi, kwa sababu mafuta yanakuwa sehemu ya mzigo katika gari kwa hiyo injini inabidi ifanye kazi ya ziada kubeba mzigo wa mafuta.

Kihesabu tunasema fuel consumption is directly proportional to fuel level in the tank; C = kL, where C = fuel consumption rate, k = constant of proportionality, na L ni fuel level in the tank. Hiyo "k" ni assumption kwamba factors nyingine hazibadiliki, mfano idadi ya abiria ndani ya gari. Au kwa njia rahisi ni kwamba, rate ya consumption ya mafuta iko directly proportional na uzito wa gari. Kwa hiyo kadiri unavyojaza tank ndivyo unavyoongeza uzito wa gari na ndivyo gari itakula mafuta zaidi. Ulaji wa mafuta utapungua kadiri mafuta kwenye tank yanavyopungua, au kadiri uzito wa gari (load) unavyopungua.

Hiyo pia ndio sababu ndege haziweki full tank zinaporuka kwenda safari fulani, wanaweka mafuta yatakayotosha kuwafikisha wanapokwenda, na ziada kidogo ya emergency

Ndio maana unashauriwa usiweke vitu usivyohitaji kwenye buti ya gari kwa kuwa inafanya gari itumie mafuta zaidi. Utakuwa umesikia watu wakisema magari ya siku hizi ni karatasi sana tofauti na ya zamani - ni kweli na hilo lilifanyika ili kupunguza uzito wa gari ili lisitumie mafuta kwa wingi.
Safi Sana injinia
 
Density ya petrol 0.71–0.77 kg/L, density of water karibu 0.91 kg /L

Sasa unajua maana ya kusema litre 45 ambazo ni karibu na Kilo 45?

Na wewe acha kubisha kipoyoyo
Kwa kukusaidia chukua hiyo hiyo 45 zidisha mara 0.7 halafu ukipata jibu jishike kifuani sema kwa sauti kuu "MIMI NI POYOYO"
 
Jibu nikweli kabisa hata Pikipiki ukijaza full tank mafuta hayaendi kabisa hasa ukiwa nasafari ndefu.
Mkuu, ngoja nikueleweshe wewe na wake wanaodhani ukijaza tenki gari au pikipiki hautumii mafuta kwa kasi. Ni kwamba tenki nyingi za magari na hata pikipiki zina namna ya shepu ambayo juu ni kubwa na chini ni ndogo. Kwa hiyo ukijaza mafuta na geji ikaenda hadi juu kabisa, utaona inachukua muda mrefu sana geji kushuka hadi kufikia nusu. Ni kwa kuwa eneo la tenki la juu ni pana kuliko la chini, kwa hiyo geji inaenda taratibu ikianzia juu kabisa.

Ukishafika nusu tenki, eneo la chini la tenki mara nyingi ni jembamba, hivyo geji itaonekana inaenda kasi kuelekea empty tenki. Ndio maana watu wanadhani ukiweka nusu tenki gari inatumia mafuta mengi na yanaisha haraka na ukiweka full tenki mafuta hayaishi haraka! Shape za tenki za mafuta mara nyingi ziko hivi kama michoro hapo chini, na ushukaji wa geji mafuta yakiwa yamejaa unakuwa wa taratibu, na yakiwa chini ya nusu tenki geji inashuka kwa kasi kwa sababu mara nyinki tenki ni nyembamba chini. Lakini bado ujue pamoja na geji kushuka taratibu ukiwa na full tank, gari inatumia mafuta zaidi kuliko ukiwa na half tank kwa sababu ya factor ya uzito kama nilivyoeleza hapo juu.

1624103343255.png
 
Back
Top Bottom