Ukokotoaji wa bei ya petroli kwa mwezi June baada ya ruzuku ya Sh 100 billion huu hapa: Bei inapaswa kupungua kwa zaidi ya asilimia 60%

Kwa mwezi matumizi ya mafuta nchini ni Lita mil 400
 
bei haitazidi TSh 1,500 kwa lita baada ya ruzuku ya mama yetu.

Hesabu za makaratasi siku zote huwa zipo sawa...

Ila kwa ground mambo huwa ni tofauti sana....

Kaa kwa kutulia usubiri wiki ijayo uone bei za mafuta zitakavopanda.
 
Huu uzi unatia moyo sana. Mungu akubariki Dr Akili. Laiti kama mambo yangeenda hivi hadi 2025, ningeshauri vyama pinzani visiweke mgombea urais, waweke wabunge tu.

Ee Mungu wa mbinguni utusaidie!


JESUS IS SAVIOR!
 
Weka summary in short how much will it be in retail then kwa Dsm na Moro
Kama umenisoma vizuri,retail price haitazidi TSh 1,500 kwa nchi nzima.
Hizi tofauti za bei za mkoa kwa mkoa huwa ni ndogo sana. Kwa mfano kama DSM diesel inauzwa Sh 3,200, kwa Mwanza itauzwa Sh 3,360. Tofauti hizi EWURA wangaliweza kuziondoa kwa kutafuta wastani wa bei kwa sehemu zote za nchi kama yanavyofanya makampuni ya bia na ya soda. Bei ya bia DSM na Morogoro ni ile ile.

Pia reli ingalitumika kusafirisha bidhaa hii muhimu badala ya malori ya tankers. Usafirishaji wa kutumia malori kwa bidhaa hii ni wa hatari sana, EWURA inapaswa kuupiga marufuku. Hii kwanza itaimarisha shirika letu la reli kiuchumi. Tatizo malori haya mengine ni ya vigogo serikalini, mama anapaswa kusimama imara. Usafirishaji kwa njia ya reli ni rahisi mara dufu ukilinganisha na wa barabara na SGR itakapokamilika, ni usafiri wa haraka zaidi kuliko wa barabara. SGR ya kutoka DSM hadi Morogoro itakapokamilika hivi punde. Hatutarajii hata kidogo kuona bidhaa hii ikisafirishwa kwa barabara kwenda Morogoro kutoka DSM baada ya hapo.
 
Hesabu za makaratasi siku zote huwa zipo sawa...

Ila kwa ground mambo huwa ni tofauti sana....

Kaa kwa kutulia usubiri wiki ijayo uone bei za mafuta zitakavopanda.
Ndiyo maana nimewatadharisha ili zitakapopanda sana kupita hiyo bei ya Sh 1,500 kwa lita tupige kelele. Wakipandisha hadi Sh 2,000 kwa lita tunaweza kumezea!
 
Sio sahii..

kwa mujibu wa taarifa kutoka (Nishati | News)

Wastani wa matumizi ni lita 10,900,000 kwa siku sawa na lita 327,000,000 kwa siku 30.

Hivyo chukulia tu bei ya sasa ya soko ndio ya mwezi june, ina maana ahueni itakuwa 100bn÷327mn (matumizi ya mwezi kama ilivyo taarifa ya nishati) = 305.8 maana yake punguzo linatakiwe liwe hilo na bei iwe shs 2,842 kwa dsm. Hii itakuwa hivyo tu kama matumizi ya mwezi ni sahihi na bei ya soko la dunia haitabadilika kupanda.

Ila ulichosema sio sahihi hata kidogo hivyo punguzo halitazidi sh 400 kwa lita kutoka bei ya sasa.
 
Hayo matumizi ya lita 10,900,000 kwa siku umeipata wapi kwani hata kwenye hizo takwimu za Makamba ulizozinukuu hazimo!

Makamba anazungumzia lita za mafuta zinazoshushwa bandarini na kuhifadhiwa kwenye maghala. Tunajua kuwa baadhi ya mafuta hayo yataelekea nchi zingine jirani (yako transit). Hatupi mchanganuo wake ili kutuchanganya.

Kuna mahali anasema tuna lita 118,594,024 zitakazotusheleza kwa mwezi mmoja. Ukikokotoa hii unapata lita 3,933,000 kwa siku. Wewe unasema lita 10,900,000 kwa siku.

Kuna mahala pengine anasema kutakuwa na lita 202,742,704 ambazo zitatosha siku 33. Ukikokotoa hii maana yake ni lita 6,143,718 kwa siku. Sasa hii tofauti kubwa inatoka wapi? Yaani mwezi uliopita matumizi kwa siku yalikuwa lita 3,933,300 lakini mwezi ujao yatakuwa lita 6,143,718 kwa siku. Haya ndiyo mahesabu ya Makamba uliyotuletea hapa. Halafu na wewe ukayaongeza hadi kuwa lita 10,900,000 kwa siku.

Takwimu zilizoko Google ni sahihi kwamba matumizi yetu kwa siku ni barrels 15,000 (= lita 2,285,000) hadi barrels 20,000 (= lita 3,180,000). Wastani ni barrels 18,000 kwa siku sawa na lita 2,862,000 nilizozitumia kufanya ukokotoaji. Hata ukitumia hiyo ya Makamba ya lita 3,933,300 kwa siku bei ya lita moja haitazidi Sh 1,600 kwenye retailers.
 
You must be joking
 
Pricing Decisions depends upon Msoga gang approval!
 
Acha kupotosha, ukweli nafuu haizid 400 labda bei ya dunia ishuke. Kama unajua hesabu hiyo 6.1m na 3.9m ulizoweka tu zinatosha kukuonyesha kiasi kinachotumika, unachopaswa kujua hizo ni aina za mafuta kwa maana ya dizeli, petroli na mafuta ya taa, jumla unajumlisha.
Sio busara kubisha vitu vilivyo wazi.

Hata hivyo hatujuani humu nisitumie nguvu kubwa, pengine uelewa ni wa tofauti sana.
 
Boss,Hizi hesabu mnazopiga zote zinachukulia kuwa hiyo ruzuku ya 100bn ni kwa mwezi June tuu.Kama hivyo ni sahihi maana yake kuanzia July tutarudi kwenye bei za kawaida bila ruzuku!?
Ndo hivyo?
 
Mleta mada amekosea. Hiyo bilioni 100 siyo ya juni pekee, bali ni ya mwezi juni + mwaka mzima wa fedha 2022/2023.

Bei itapungua kwa sh 29.30.
Utata unaanzia hapa. Kama bei ya sasa = 3000 na kwa bei ya soko la dunia inatakiwa ipande kwa amount X mfano tuchukulie 200 kwa kila lita.

Kama hiyo bilioni 100 itapunguza bei kwa Sh. 29.30 huku bei ya soko imepanda zaidi kwa mfano Sh. 200 maana yake si mafuta yatapanda kwa Sh. 200 - Sh. 39 = Sh. 161 ?
 
Mleta mada amekosea. Hiyo bilioni 100 siyo ya juni pekee, bali ni ya mwezi juni + mwaka mzima wa fedha 2022/2023.

Bei itapungua kwa sh 29.30.
Kasikilize vizuri maamuzi ya rais yaliyosomwa bungeni na waziri wa nishati. Hiyo billion moja ni kwa mwezi June pekee. Zimetolewa kwenye OC mbalimbali za mwaka huu wa fedha unaoishia tarehe 30 June.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…