Ukoo wa Kivuruga wapewa barabara Tabora

Ukoo wa Kivuruga wapewa barabara Tabora

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
UKOO WA KIVURUGA UMEPEWA BARABARA TABORA

Katika moja ya koo maarufu Tabora ni ukoo wa Kivuruga.

Ndugu wawili Maulidi na Abdallah Kivuruga ni watu waliokuwa mashuhuri Tabora mjini katika siasa na harakati za kupeleka mbele Uislam.

Wananchi wa Tabora katika mradi wa Anuani na Makazi wametumia fursa hii kwa kuenzi ukoo wa Kivuruga kwa yale waliyofanya katika kuunda African Association na TANU kupigania uhuru wa Tanganyika.

PICHA: Kulia ni Abdallah Kivuruga na kushoto ni Maulidi Kivuruga.

Screenshot_20221018-164126_Photos.jpg
1666110225705.png
 
Mzee napenda sana kukufuatilia. Natamani vitabu yvako na machapisho yako yangetumika mashuleni kwenye HISTORIA NA URAIA.
MUNGU AKUWEKE
 
Napenda sana post zako za historia hasa za waislamu wa sehemu mbali mbali.

Binafsi najiuliza. Uislamu ulitangulia kufika Tanganyika na zanzibar kwa miaka zaidi ya 800. Inasemekana mwaka 1000 uislamu tayari umeshakuja africa mashariki.. huku ukristo umekuja miaka ya 1800s

Najiuliza kwa nini uislamu ulienea kwa watu wachache zaidi huku ulikuwa na advantage ya kutangulia kufika..

Kwa nini leo katika nchi zote za africa mashariki ikiwemo Tanzania yetu idadi ya waislamu ni ndogo kuliko wakristo. Huku ukristo umechelewa sana kuja..
 
Napenda sana post zako za historia hasa za waislamu wa sehemu mbali mbali.

Binafsi najiuliza. Uislamu ulitangulia kufika Tanganyika na zanzibar kwa miaka zaidi ya 800. Inasemekana mwaka 1000 uislamu tayari umeshakuja africa mashariki.. huku ukristo umekuja miaka ya 1800s

Najiuliza kwa nini uislamu ulienea kwa watu wachache zaidi huku ulikuwa na advantage ya kutangulia kufika..

Kwa nini leo katika nchi zote za africa mashariki ikiwemo Tanzania yetu idadi ya waislamu ni ndogo kuliko wakristo. Huku ukristo umechelewa sana kuja..
Freshman...
Ukisema hivyo utaleta ubishi mkubwa sana kwani utatakiwa utoe takwimu na Tanzania haijachukua takwimu za dini toka mwaka wa 1970.

Utaulizwa umejuaje kuwa Waislam wachache au Wakristo wachache?
Zogo litakuwa kubwa sana kwani umegusa mahali nyeti sana.
 
Napenda sana post zako za historia hasa za waislamu wa sehemu mbali mbali.

Binafsi najiuliza. Uislamu ulitangulia kufika Tanganyika na zanzibar kwa miaka zaidi ya 800. Inasemekana mwaka 1000 uislamu tayari umeshakuja africa mashariki.. huku ukristo umekuja miaka ya 1800s

Najiuliza kwa nini uislamu ulienea kwa watu wachache zaidi huku ulikuwa na advantage ya kutangulia kufika..

Kwa nini leo katika nchi zote za africa mashariki ikiwemo Tanzania yetu idadi ya waislamu ni ndogo kuliko wakristo. Huku ukristo umechelewa sana kuja..

1. Uislamu ulipoingia ilibidi upambane na dini za asili.

2. Huenda walioeneza Uislamu walikuja Afrika Mashariki kwa malengo mengine kama biashara na si lengo mahsusi la kueneza dini.

3. Uislamu unafundishwa kwa Kiarabu na hicho kinaweza kuwa kikwazo ktk kueneza imani hiyo.

4. Walioeneza Uislamu hawakuwa na support au ufadhili wa serikali au dola za nchi walikotoka, hivyo uwezo wao kifedha ulikuwa mdogo.

5. Ukristo ulienezwa Afrika Mashariki na Wamisionari. Hawa walikuja kwa lengo mahsusi la kueneza dini.

6. Wamisionari walikuwa na msaada na ufadhili wa serikali na dola za nchi walikotokea. Kwa msingi huo walikuwa na ukwasi wa kiwango fulani.

7. Wamisionari walijifunza lugha za wenyeji wa eneo walilolenga kueneza Ukristo. Kwa hiyo Ukristo ulifundishwa na kuenezwa hata kwa lugha za wenyeji.

8. Juhudi kubwa zilifanyika kutafsiri Biblia, vitabu vya sala, na nyimbo za wakati wa ibada, kwa lugha za wenyeji. Zipo Biblia na vitabu vya sala za Kisukuma, Kichaga, etc.

9. Ukristo ulikuwa ndio dini ya MTAWALA hapa Afrika Mashariki hivyo kurahisisha kusambaa kwake.

Cc Mohamed Said
 
1. Uislamu ulipoingia ilibidi upambane na dini za asili.

2. Huenda walioeneza Uislamu walikuja Afrika Mashariki kwa malengo mengine kama biashara na si lengo mahsusi la kueneza dini.

3. Uislamu unafundishwa kwa Kiarabu na hicho kinaweza kuwa kikwazo ktk kueneza imani hiyo.

4. Walioeneza Uislamu hawakuwa na support au ufadhili wa serikali au dola za nchi walikotoka, hivyo uwezo wao kifedha ulikuwa mdogo.

5. Ukristo ulienezwa Afrika Mashariki na Wamisionari. Hawa walikuja kwa lengo mahsusi la kueneza dini.

6. Wamisionari walikuwa na msaada na ufadhili wa serikali na dola za nchi walikotokea. Kwa msingi huo walikuwa na ukwasi wa kiwango fulani.

7. Wamisionari walijifunza lugha za wenyeji wa eneo walilolenga kueneza Ukristo. Kwa hiyo Ukristo ulifundishwa na kuenezwa hata kwa lugha za wenyeji.

8. Juhudi kubwa zilifanyika kutafsiri Biblia, vitabu vya sala, na nyimbo za wakati wa ibada, kwa lugha za wenyeji. Zipo Biblia na vitabu vya sala za Kisukuma, Kichaga, etc.

9. Ukristo ulikuwa ndio dini ya MTAWALA hapa Afrika Mashariki hivyo kurahisisha kusambaa kwake.

Cc Mohamed Said
jibu murua kbs
 
1. Uislamu ulipoingia ilibidi upambane na dini za asili.

2. Huenda walioeneza Uislamu walikuja Afrika Mashariki kwa malengo mengine kama biashara na si lengo mahsusi la kueneza dini.

3. Uislamu unafundishwa kwa Kiarabu na hicho kinaweza kuwa kikwazo ktk kueneza imani hiyo.

4. Walioeneza Uislamu hawakuwa na support au ufadhili wa serikali au dola za nchi walikotoka, hivyo uwezo wao kifedha ulikuwa mdogo.

5. Ukristo ulienezwa Afrika Mashariki na Wamisionari. Hawa walikuja kwa lengo mahsusi la kueneza dini.

6. Wamisionari walikuwa na msaada na ufadhili wa serikali na dola za nchi walikotokea. Kwa msingi huo walikuwa na ukwasi wa kiwango fulani.

7. Wamisionari walijifunza lugha za wenyeji wa eneo walilolenga kueneza Ukristo. Kwa hiyo Ukristo ulifundishwa na kuenezwa hata kwa lugha za wenyeji.

8. Juhudi kubwa zilifanyika kutafsiri Biblia, vitabu vya sala, na nyimbo za wakati wa ibada, kwa lugha za wenyeji. Zipo Biblia na vitabu vya sala za Kisukuma, Kichaga, etc.

9. Ukristo ulikuwa ndio dini ya MTAWALA hapa Afrika Mashariki hivyo kurahisisha kusambaa kwake.

Cc Mohamed Said
JK,
Unataka tujadili hili la wingi au uchache wa Waislam na Wakristo Tanganyika.

Lakini tokea mwanzo nimetahadharisha kuwa somo hili litasababisha ubishi mkali.

Uhakika wa kutaka kujua ukweli ni kufanya sensa na kuweka kipengele cha dini.

Kwa zaidi ya miaka 40 kipengele hiki kimeondolewa Tanzania.

Walioondoa wana sababu zao.

Ila nitaeleza suala hili kama nilivyokabiliananalo katika mhadhara niliotoa Chuo Kikuu cha Iowa Marekani mwaka wa 2011.

Katika maswali na majibu niliambiwa na Mmarekani mmoja kuwa Waislam hawana nafasi nyingi katika serikali, vyama vya siasa, nafasi za elimu nk. nk. ukilinganisha na Wakristo kwa kuwa Tanzania Waislam ni "minority," yaani wachache.

Huyu bwana alitoa ushahidi wa takwimu za CIA.

Jibu langu lilikuwa kuwa zipo takwimu za miaka mingi ambazo ni tofauti na takwimu za CIA zinazotoa hesabu tofauti.

Mimi nikasisitiza kuwa tuachane na takwimu zote hizo za CIA na zinginezo tuangalie "political history ya Tanganyika," kama moja ya "variable."

Nikajibu swali kwa kuuliza swali.

Hapa nilikuwa katika mhadhara wa wataalamu wa African History.

Nikawaomba wanipe mfano wa nchi moja duniani iliyokuwa chini ya ukoloni na waumini wa dini iliyokuwa "minority," ndiyo walionyanyua silaha kupambana na mvamizi mkoloni.

Nikawapa mfano wa Vita Vya Maji Maji (1905 - 1907) na majemadari Waislam 67 walionyongwa na Wajerumani na kuzikwa katika kaburi la halaiki Songea.

Nikawauliza iweje baada ya Waafrika kushindwa katika Maji Maji katika "nationalist politics" na madai ya kupigania uhuru wa Tanganyika hao hao "minority," wakaongoza mapambano dhidi ya ukoloni wa Muingereza.

Hawa niliowauliza maswali haya ni maprofesa wa historia katika vyuo mbalimbali Marekani.

Nikawaomba kwa dakika moja waitazame India wakati inapigania uhuru wake na iwe walioongoza mapambano hayo ni Waislam ambao ni wachache wakiongozwa na Mohamed Ali Jinah badala ya Nehru ambae ni Mhindu na ndiyo wengi nchini wakawa katika duru ya nje.

Ukumbi ulikuwa kimya na baridi.
Sikupewa jibu.

Badala yake Mkuu wa Idara ya African History Northwestern University, Evanston Chicago, Jonathon Glassman aliniomba nikafanye mhadhara kama huu chuoni kwake na nilikwenda.

Kiasi muuliza swali alijihisi mdogo.
 
JK,
Unataka tujadili hili la wingi au uchache wa Waislam na Wakristo Tanganyika.

Lakini tokea mwanzo nimetahadharisha kuwa somo hili litasababisha ubishi mkali.

Uhakika wa kutaka kujua ukweli ni kufanya sensa na kuweka kipengele cha dini.

Kwa zaidi ya miaka 40 kipengele hiki kimeondolewa Tanzania.

Walioondoa wana sababu zao.

Ila nitaeleza suala hili kama nilivyokabiliananalo katika mhadhara niliotoa Chuo Kikuu cha Iowa Marekani mwaka wa 2011.

Katika maswali na majibu niliambiwa na Mmarekani mmoja kuwa Waislam hawana nafasi nyingi katika serikali, vyama vya siasa, nafasi za elimu nk. nk. ukilinganisha na Wakristo kwa kuwa Tanzania Waislam ni "minority," yaani wachache.

Huyu bwana alitoa ushahidi wa takwimu za CIA.

Jibu langu lilikuwa kuwa zipo takwimu za miaka mingi ambazo ni tofauti na takwimu za CIA zinazotoa hesabu tofauti.

Mimi nikasisitiza kuwa tuachane na takwimu zote hizo za CIA na zinginezo tuangalie "political history ya Tanganyika," kama moja ya "variable."

Nikajibu swali kwa kuuliza swali.

Hapa nilikuwa katika mhadhara wa wataalamu wa African History.

Nikawaomba wanipe mfano wa nchi moja duniani iliyokuwa chini ya ukoloni na waumini wa dini iliyokuwa "minority," ndiyo walionyanyua silaha kupambana na mvamizi mkoloni.

Nikawapa mfano wa Vita Vya Maji Maji (1905 - 1907) na majemadari Waislam 67 walionyongwa na Wajerumani na kuzikwa katika kaburi la halaiki Songea.

Nikawauliza iweje baada ya Waafrika kushindwa katika Maji Maji katika "nationalist politics" na madai ya kupigania uhuru wa Tanganyika hao hao "minority," wakaongoza mapambano dhidi ya ukoloni wa Muingereza.

Hawa niliowauliza maswali haya ni maprofesa wa historia katika vyuo mbalimbali Marekani.

Nikawaomba kwa dakika moja waitazame India wakati inapigania uhuru wake na iwe walioongoza mapambano hayo ni Waislam ambao ni wachache wakiongozwa na Mohamed Ali Jinah badala ya Nehru ambae ni Mhindu na ndiyo wengi nchini wakawa katika duru ya nje.

Ukumbi ulikuwa kimya na baridi.
Sikupewa jibu.

Badala yake Mkuu wa Idara ya African History Northwestern University, Evanston Chicago, Jonathon Glassman aliniomba nikafanye mhadhara kama huu chuoni kwake na nilikwenda.

Kiasi muuliza swali alijihisi mdogo.

..asante kwa majibu yako.

..muuliza swali aliuliza kuhusu kuenea kwa dini za Kiislamu na Kikristo ktk AFRIKA MASHARIKI.

..jibu langu halikujikita ktk kufanya mlinganisho wa idadi ya waumini baina ya imani hizo mbili.

..nilichojaribu kukielezea ktk hoja yangu ni utofauti wa mazingira ya jinsi Uislamu ulivyoingia Afrika Mashariki vs Ukristo ulivyoingia.

..mada kuhusu idadi ya Waislamu vs Wakristo hapa Tanganyika / Tanzania ni ngumu kama ulivyoeleza ktk majibu yako ya awali, na mimi sikutaka kwenda huko.
 
..asante kwa majibu yako.

..muuliza swali aliuliza kuhusu kuenea kwa dini za Kiislamu na Kikristo ktk AFRIKA MASHARIKI.

..jibu langu halikujikita ktk kufanya mlinganisho wa idadi ya waumini baina ya imani hizo mbili.

..nilichojaribu kukielezea ktk hoja yangu ni utofauti wa mazingira ya jinsi Uislamu ulivyoingia Afrika Mashariki vs Ukristo ulivyoingia.

..mada kuhusu idadi ya Waislamu vs Wakristo hapa Tanganyika / Tanzania ni ngumu kama ulivyoeleza ktk majibu yako ya awali, na mimi sikutaka kwenda huko.
JK,
Labda utazame upya nini chanzo cha wewe kuandika na kunikaribisha.
 
Freshman...
Ukisema hivyo utaleta ubishi mkubwa sana kwani utatakiwa utoe takwimu na Tanzania haijachukua takwimu za dini toka mwaka wa 1970.

Utaulizwa umejuaje kuwa Waislam wachache au Wakristo wachache?
Zogo litakuwa kubwa sana kwani umegusa mahali nyeti sana.
Mzee uache ubishi hata ukitumia general assesment Kimikoa utakubakiana nami kwamba mikoa mingi imetawaliwa na ukristo. Mikoa yenye waislam wengi ni

1. Tanga
2.pwani
3. Zanzibar
4. Lindi
5. Mtwara

Halaf kuna mikoa ambayo watu hudhani ina waislam wengi kumbe assesment yao imefanyika mjini tu ambapo ukiingia wilaya za vijijini huko kuna idadi kubwa ya wakristo. Hii ni

1. Kigoma
i. Kigoma mjini ( waislam)
ii. Uvinza (50/50)
iii. Kasulu ( ukristo)
iv. Kibondo(ukristo)
v. Bugigwa(ukristo)
vi. Kakonko(ukristo

2. Tabora
3. Singida

Lakini mikoa mingine yote iliyobakiwa imetawaliwa na ukristo.
 
Mzee uache ubishi hata ukitumia general assesment Kimikoa utakubakiana nami kwamba mikoa mingi imetawaliwa na ukristo. Mikoa yenye waislam wengi ni

1. Tanga
2.pwani
3. Zanzibar
4. Lindi
5. Mtwara

Halaf kuna mikoa ambayo watu hudhani ina waislam wengi kumbe assesment yao imefanyika mjini tu ambapo ukiingia wilaya za vijijini huko kuna idadi kubwa ya wakristo. Hii ni

1. Kigoma
i. Kigoma mjini ( waislam)
ii. Uvinza (50/50)
iii. Kasulu ( ukristo)
iv. Kibondo(ukristo)
v. Bugigwa(ukristo)
vi. Kakonko(ukristo

2. Tabora
3. Singida

Lakini mikoa mingine yote iliyobakiwa imetawaliwa na ukristo.
Tash...
Sijafanya ubishi.

Nimeeleza kile nikijuacho kama wewe ulivyonipa hizi takwimu zako.
Tunarudi pale tulipoanzia.

Nini chanzo cha takwimu zako ilhali hakuna sensa yenye kipengele cha dini toka mwaka wa 1970?
 
UKOO WA KIVURUGA UMEPEWA BARABARA TABORA

Katika moja ya koo maarufu Tabora ni ukoo wa Kivuruga.

Ndugu wawili Maulidi na Abdallah Kivuruga ni watu waliokuwa mashuhuri Tabora mjini katika siasa na harakati za kupeleka mbele Uislam.

Wananchi wa Tabora katika mradi wa Anuani na Makazi wametumia fursa hii kwa kuenzi ukoo wa Kivuruga kwa yale waliyofanya katika kuunda African Association na TANU kupigania uhuru wa Tanganyika.

PICHA: Kulia ni Abdallah Kivuruga na kushoto ni Maulidi Kivuruga.

View attachment 2391159View attachment 2391254
Mkuu unaona mambo ya udini yana tija sana katika maendeleo ya hili Taifa? kuhimisa sera za udini ni sawa tu na kupanda mbegu ya ukabila kwenye Taifa. Serikali yenye nia njia na umoja wa Taifa haiwezi kupigia chapuo masuala ya dini au kabila kwakuwa hizo ni nyenzo za kuligawa Taifa na watu wake kwa ujumla.
Binafsi nakushauri jikite kwenye mada ambazo zinachochea umoja wa kitaifa katika nyanja mbalimbali hasa kiuchumi ili tuweze kujipatia maendeleo endelevu. Mambo ya dini yabaki jambo la mtu binafsi na Muumba wake na isiwe mjadala wa kitaifa.

Sent from my TECNO KC6 using JamiiForums mobile app
 
Tash...
Sijafanya ubishi.

Nimeeleza kile nikijuacho kama wewe ulivyonipa hizi takwimu zako.
Tunarudi pale tulipoanzia.

Nini chanzo cha takwimu zako ilhali hakuna sensa yenye kipengele cha dini toka mwaka wa 1970?
Nimekwambia general assesment maana wakazi wanaoishi huko dini zao sio siri zinajulikana maana wanenda kanisani na misikitini. Hivi ukiulizwa kati wa waislam na wa buddha hapa Tanzania wepi wengi utahitaji sensa ili kuthibitisha hilo?
 
Mkuu unaona mambo ya udini yana tija sana katika maendeleo ya hili Taifa? kuhimisa sera za udini ni sawa tu na kupanda mbegu ya ukabila kwenye Taifa. Serikali yenye nia njia na umoja wa Taifa haiwezi kupigia chapuo masuala ya dini au kabila kwakuwa hizo ni nyenzo za kuligawa Taifa na watu wake kwa ujumla.
Binafsi nakushauri jikite kwenye mada ambazo zinachochea umoja wa kitaifa katika nyanja mbalimbali hasa kiuchumi ili tuweze kujipatia maendeleo endelevu. Mambo ya dini yabaki jambo la mtu binafsi na Muumba wake na isiwe mjadala wa kitaifa.

Sent from my TECNO KC6 using JamiiForums mobile app
Mini...
Inaelekea huijui historia ya Tanganyika.

Udini umeanza mara tu baada ya uhuru kupatikana 1961.
 
Back
Top Bottom