Uchaguzi 2020 Ukosefu wa hela ya kupiga kampeni wageuka neema kwa vyama vikubwa nchini

Uchaguzi 2020 Ukosefu wa hela ya kupiga kampeni wageuka neema kwa vyama vikubwa nchini

Kule kwetu kuna watu wanalala kwenye nyumba zisizo na milango, hivyo huweka miti, michi/mitwangio na mipini ya majembe mlangoni kuzuia watu kuingia ndani wakati watu wamelala usiku. Sasa wana msemo wao unaosema kujifungia sana kwa kutumia miti hiyo malangoni ni kulala nje, wakiwa na maana kwamba kama ukiiweka miti mingi mno na mizito mlangoni inaweza kuelemeana yenyewe kwa yenyewe na kusababisha ianguke chini na kuondoa kizingiti kilichokusudiwa cha watu kuingia ndani.

Kuna watu walibuni vizingiti vingi sana kwa wapinzani kushinda uchaguzi vikiwemo vile vya kuzuia vyama kuungana na kushirikiana, kuzuia harakati za kisiasa kwa miaka 5, kuzuia vyama kupata pesa za kuendeshea uchaguzi, wabunge na wapinzani kuhama vyama, nk.

Matokeo yake leo hii inaonekana kuwa kuna vyama viwili tu vinavyoshiriki uchaguzi huu wa 2020. Hii imesababishwa na vikwazo vingi mno kwa vyama na kuwafanya wapiga kura wote wagawanyike kwenye vyama viwili tu vilivyohimili vikwazo vyote vilivyowekwa na wadau. Kwa maana nyingine vikwazo viiingi kwa vyama vimewarahisishia kazi wapiga kura kubaki na mzigo wa vyama 2 tu vya kupigia kura.

Mizengwe imevimaliza NCCR Mageuzi, CUF, UMD, TLP, NLD,... kwenye mbio za urais. Hata baba wa taifa aliwahi kutamani vibaki vyama 2 tu vikubwa vya siasa Tanzania. Unabii wake karibu utatokea kwa mapenzi ya Mungu.
 
Zito kala hela za Membe halafu anamchinjia baharini mchana kweupe! mwanasiasa yeyote sio wa kuamini.
Zitto Mungu anakuona.
Acha ramli porojo Zitto keshasema kwamba Membe yuko bize kuliandaa baraza la Mawaziri
 
Njia pekee ya kukabiliana na gharama za uchaguzi ingekuwa kutoa ruzuku na misaada kwa vyama vya siasa nchini. Kukosekana kwa hela ya kumudu gharama za kupiga kampeni imesababisha vyama vidogo kuviunga mkono vyama vikubwa kwenye mbio za uchaguzi.

Kama kungekuwa na ruzuku ya kupigia kampeni TLP na UDP wasingekubali kuunga mkono juhuhi za CCM kwenye uchaguzi. Hivyo hivyo na ATC-Wazalendo wasingefikiria kuunga mkono juhudi za CHADEMA kwenye uchaguzi wa rais.

Aliyebuni wazo la kuvinyima ruzuku na vyanzo vingine vya kupata hela hakujuwa kile ambacho kingejitokeza kwa CCM na Chadema.

Leo hii Chadema bila kutarajia imejikuta ikiungwa mkono na ACT from no where. Hii ina maana kuwa chadema sasa ina nguvu nyingi kuliko ilivyokuwa ikitegemewa.

Hawa washauri wetu lazima watimzamwe upya.
Kabla hujatoa ujinga wako angalia kwaumakini pima unachotaka kukisema act sio kukosa pesa za kampeni balinimkakati wakuitoa ccm njiani act wamesapoti bara chadema wamesapoti visiwani hilondio unaitakukosa pesa zakampeni
 
Kabla hujatoa ujinga wako angalia kwaumakini pima unachotaka kukisema act sio kukosa pesa za kampeni balinimkakati wakuitoa ccm njiani act wamesapoti bara chadema wamesapoti visiwani hilondio unaitakukosa pesa zakampeni
Ndugu yangu Ni ukweli kabisa vyama vyote vya upinzani havina fedha ya kutosha kuendeshea uchaguzi huu. Serikali imehakikisha kuwa hata misaada kutoka kwa marafiki wa nje haiwafikii. Ndio maana hata Chadema inakinga kofia ili kuchangiwa na wananchi hela ya kunywa maji. Unaposema act iko liquid sikatai lakini kauli ya vyama ni hiyo. Ila kusudi langu kwenye huu Uzi Ni kuonyesha namna kila kwenye changamoto kunaibuka fursa hapopo kupitia changamoto hiyo.
 
Ndugu yangu Ni ukweli kabisa vyama vyote vya upinzani havina fedha ya kutosha kuendeshea uchaguzi huu. Serikali imehakikisha kuwa hata misaada kutoka kwa marafiki wa nje haiwafikii. Ndio maana hata Chadema inakinga kofia ili kuchangiwa na wananchi hela ya kunywa maji. Unaposema act iko liquid sikatai lakini kauli ya vyama ni hiyo. Ila kusudi langu kwenye huu Uzi Ni kuonyesha namna kila kwenye changamoto kunaibuka fursa hapopo kupitia changamoto hiyo.
Haya bana
 
Membe ndiye mwanasiasa mjinga na mpumbavu kuliko wote ambao waliwahi kuwa wana CCM.
Sio mjinga huyu, muda wowote anaweza kumiminiwa pesa na wasiojulikana ili aendelee na kampeni kwa manufaa ya chama Cha mapidozi
 
Sio mjinga huyu, muda wowote anaweza kumiminiwa pesa na wasiojulikana ili aendelee na kampeni kwa manufaa ya chama Cha mapidozi
Very poor argument. By the way, kama unaamini Membe anaweza kutumiwa na CCM, vipi unamwamini Lissu?
 
Unajua anachopenda Mungu kufanya huambatana na changamoto. Kwa mpango wa Mungu, Lisu alipaswa kuwa mgombea urais 2020. Angepenyaje ktk makamanda wote wa CDM?
Plan ya Mungu,
1)Lisu anza harakati za kupinga udkt uchwara
2). Jiwe fanya ushirika na Bashite.
3). Anazisha kitengo cha incognito
4). Incognito mimina magazine kwa Lisu.
5)Lisu nusurika kwa nguvu yake Mola, nenda nje kakutane na dunia.
6) Lowasa/Sumaye pata hofu - rejea mlipotoka
7) Nchi yote saiiii!!!!! Yaani kimyaaa!!!
8) Polepole/Bashiru anazisha kero, kero, kero, vikao, nunua wapinzani, TV zote TUMETEKELEZA KWA KISHINDOOOO!!!!. Hakuna kingine cha kuangalia. Kila ukifungua Tv utasikia Mwanantala na reli au Greyson na Bwawa la umeme au Rioba na dream liner.
9) Ni uhakika sasa upinzani umefariki
10) Mara vuuuup! Usiyempenda kaja!
11) Ohooooo, walala hoi wote Lisu, Lisu, Lisu, Lisu, Rais, Rais,, Rais!!!!!!!
12) Zuia huyo Membe asiingize pesa za kampeni, kamata na msaidizi.
13). Mara paaaab! Bakuli la uchaguzi hadharani. Halina CAG wala udhibiti wa msajili. Hata TCRA hawezi ona muamala, TRA haijui nani kaweka nini kwenye bakuli, sasa nani akamatwe kwa kuchangia mgombea?
14) Kwa wasioweza tembea bakuli wamebaki na njia moja tu! Kuunga mkono mgombea wa Uhuru Haki na Maendeleo au kuunga juhudi ujenzi wa miundombinu!
15) Amani iliyopo sasa ni sababu tu ya Robert & Amsterdam, vinginevyo yale ya Ole Sabayi wa Arumeru yangetamalaki!
16) Huenda hata kuondoka mapema kwa Mzee Mkapa ni Mpango wa Mungu kumnusuru na dhambi ya kunyima wananchi Haki yao katika kutangaza mshindi.
17) Mungu hajamaliza kazi yake, ukiona kuna ugumu wowote, jua Mungu anajiandaa kutoa jibu jepesi.
#Tuendelee kusubiri!!!
Nakupa 100% Mkuu, haya yoote uliyoorodhesha na mwisho hilo la Amsterdam umemaliza kila kitu. Huo ndiyo ukweli wenyewe na bado mengi yapo njiani. Hii ni sehemu ndogo tu.
 
Very poor argument. By the way, kama unaamini Membe anaweza kutumiwa na CCM, vipi unamwamini Lissu?
Daa! hakuna asiyekuwa na Bei, lakini Bei ya Lissu inaweza kuwa kubwa Sana kuliko ya mh membe kurudi CCM.
 
Daa! hakuna asiyekuwa na Bei, lakini Bei ya Lissu inaweza kuwa kubwa Sana kuliko ya mh membe kurudi CCM.
Unawezaje usiamini mbwembwe zote za Lissu tangu ajiunge Chadema, mara makesi kibao na hafungwi, mara eti risasi 16 akapona. Mara Ubeleji, mara kavuliwa ubunge, mara akirudi atakamatwa na hakukamatwa, mara mgombea urais wa Chadema. Unaweza kubisha hajanunuliwa na kuandaliwa bila mambulula yanayomshabikia kujua?
 
Unawezaje usiamini mbwembwe zote za Lissu tangu ajiunge Chadema, mara makesi kibao na hafungwi, mara eti risasi 16 akapona. Mara Ubeleji, mara kavuliwa ubunge, mara akirudi atakamatwa na hakukamatwa, mara mgombea urais wa Chadema. Unaweza kubisha hajanunuliwa na kuandaliwa bila mambulula yanayomshabikia kujua?
Hiyo Kali Sasa, yaani anunuliwe huku akubali kuchechemea kwa risasi
 
Unawezaje usiamini mbwembwe zote za Lissu tangu ajiunge Chadema, mara makesi kibao na hafungwi, mara eti risasi 16 akapona. Mara Ubeleji, mara kavuliwa ubunge, mara akirudi atakamatwa na hakukamatwa, mara mgombea urais wa Chadema. Unaweza kubisha hajanunuliwa na kuandaliwa bila mambulula yanayomshabikia kujua?
Wahi Mirembe!!
 
Unawezaje usiamini mbwembwe zote za Lissu tangu ajiunge Chadema, mara makesi kibao na hafungwi, mara eti risasi 16 akapona. Mara Ubeleji, mara kavuliwa ubunge, mara akirudi atakamatwa na hakukamatwa, mara mgombea urais wa Chadema. Unaweza kubisha hajanunuliwa na kuandaliwa bila mambulula yanayomshabikia kujua?
Humjui vizuri Lissu wewe....
 
Kuna kila muujiza mzuri kwa CHADEMA na mgombea wake Tundu Lissu, hata ikibidi mtu mkubwa "atoweke" ili andiko litimie itakuwa hivyo na dadili zote zipo.
Ameen and so shall be
 
Back
Top Bottom