Ukosefu wa maji: Watumia mkojo wa ng'ombe kujisafisha wakiwa hedhini

Ukosefu wa maji: Watumia mkojo wa ng'ombe kujisafisha wakiwa hedhini

Inside10

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2011
Posts
29,909
Reaction score
32,414
Changamoto ya upatikanaji wa maji katika Kijiji cha Oltepes kilichopo Kata ya Orbomba, wilayani Longido huwalazimu wasichana na wanawake wa eneo hilo kutumia siagi ya ng’ombe ili kudhibiti damu ya hedhi na mkojo wa ng’ombe kujisafisha.

Wanawake hao hulazimika kutumia siagi hiyo (mafuta ya ng’ombe) kujipaka maeneo ya sirini, sambamba na vipande vya nguo za zamani ili kuifanya damu hiyo isishike katika nguo zao.

Eneo hilo lenye wakazi wapatao 4,000, hutembea umbali wa kilomita tano kutafuta maji, lakini nyakati za kiangazi wanapolazimika kutumia mkojo wa ng’ombe hutembea mpaka kilomita 10 kutafuta tu maji ya kunywa na kupikia kwenye mabwawa.

Hiyo ni sehemu ya adha wanayoipata wakazi wa maeneo kadhaa wilayani humo, licha ya sera ya maji kuelekeza majisafi na salama yapatikane umbali usiozidi mita 400 kutoka makazi ya watu yalipo.

Elizabeth Olodo (40) ni miongoni mwa wanawake wanaopitia changamoto hiyo kijijini hapo. Katika maisha yake yote, amekuwa akitegemea nguo za zamani na siagi ya ng’ombe ili kudhibiti hedhi yake.

Ingawa ni njia isiyo salama na kawaida, hii imekuwa ni chaguo lake pekee katika eneo ambalo taulo za hedhi ni anasa.

Elizabeth hujipaka siagi hii sehemu za siri ili kuepuka madoa kwenye nguo zake. Wakati wa kiangazi, ambapo maji ni haba, anakutana na changamoto kubwa zaidi kukusanya mkojo wa ng'ombe na kuuweka kwenye ndoo.

1731407897214.png
 
Changamoto ya upatikanaji wa maji katika Kijiji cha Oltepes kilichopo Kata ya Orbomba, wilayani Longido huwalazimu wasichana na wanawake wa eneo hilo kutumia siagi ya ng’ombe ili kudhibiti damu ya hedhi na mkojo wa ng’ombe kujisafisha.

Wanawake hao hulazimika kutumia siagi hiyo (mafuta ya ng’ombe) kujipaka maeneo ya sirini, sambamba na vipande vya nguo za zamani ili kuifanya damu hiyo isishike katika nguo zao.

Eneo hilo lenye wakazi wapatao 4,000, hutembea umbali wa kilomita tano kutafuta maji, lakini nyakati za kiangazi wanapolazimika kutumia mkojo wa ng’ombe hutembea mpaka kilomita 10 kutafuta tu maji ya kunywa na kupikia kwenye mabwawa.

Hiyo ni sehemu ya adha wanayoipata wakazi wa maeneo kadhaa wilayani humo, licha ya sera ya maji kuelekeza majisafi na salama yapatikane umbali usiozidi mita 400 kutoka makazi ya watu yalipo.

Elizabeth Olodo (40) ni miongoni mwa wanawake wanaopitia changamoto hiyo kijijini hapo. Katika maisha yake yote, amekuwa akitegemea nguo za zamani na siagi ya ng’ombe ili kudhibiti hedhi yake.

Ingawa ni njia isiyo salama na kawaida, hii imekuwa ni chaguo lake pekee katika eneo ambalo taulo za hedhi ni anasa.

Elizabeth hujipaka siagi hii sehemu za siri ili kuepuka madoa kwenye nguo zake. Wakati wa kiangazi, ambapo maji ni haba, anakutana na changamoto kubwa zaidi kukusanya mkojo wa ng'ombe na kuuweka kwenye ndoo.

Mimi nilifikiri Rais akiwa mwanamke haya hayatatokea!!!
 
Serikal ya Ccm ni wao ndo wameichagua
Mbunge,diwan, mwenyekiti wa mtaa wao ndo wamewachagua na kuwaweka madarakan hayo malalamiko wawapelekee viongozi wao wa CCm
 
Serikal ya Ccm ni wao ndo wameichagua
Mbunge,diwan, mwenyekiti wa mtaa wao ndo wamewachagua na kuwaweka madarakan hayo malalamiko wawapelekee viongozi wao wa CCm
Halfu wanasema kutumia tambara za nguo kujistiri si salama wakati mimi naona hayo mapedi yana kemikali kibao,, tamba zikitumika ambazo ni safi mimi naona ni salama zaidi,, au wenzangu ninyi mnaonaje
 
Back
Top Bottom