Ukraine yakubali mazungumzo ya amani na Urusi, leo 28/02/2022

Ukraine yakubali mazungumzo ya amani na Urusi, leo 28/02/2022

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374
Ukraine imekubali kushiriki mazungumzo ya amani na Urusi, ambapo wajumbe wa pande zote mbili wamepanga kukutana katika eneo la mpaka kati ya Belarus na Ukraine.

Taarifa hiyo ni kwa mujibu wa ofisi ya Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelensky, inaelezwa kuwa hakuna masharti yoyote yaliyowekwa katika mazungumzo hayo ya mpakani yanayotarajiwa kufanyika leo Jumatatu Februari 28, 2022.

Awali, Zelensky alikataa kukutana na wajumbe wa Urusi katika eneo lililoainishwa na Serikali ya Urusi kwa madai kwamba taifa hilo kwa sehemu fulani lilipanga uvamizi wake nchini Belarus.

Tangazo hilo limetolewa katika kipindi kifupi baada ya Rais wa Urusi, Vladimir Putin kuamuru kuwekwa katika hali ya tahadhari kwa silaha za kujikinga katika pasipo kuzitaja silaha za nyuklia.

Akitoa tangazo hilo Rais Putin amesema viongozi wa nchi zinazoongoza Umoja wa Kujihami NATO, wanaruhusu kauli za uchochezi dhidi ya taifa lao, kwa hivyo amewaamuru Waziri wa Ulinzi na mkuu wa majeshi kuliweka jeshi katika mfumo maalumu wa tahadhari.

60931987_354.jpg

 
walifikiri Putin anatania, hawakuelewa wanadili na JASUSI LILILOBOBEA
Ondoa upuuzi wako apa aliyetaka mazungumzo zaidi ni Russia baada ya hali ngumu Kiev ambayo hawakutarajia, miji ya kiev ipo under control of Ukraine ndio mana sasa anatishia kutumia nuclear ngoma nzito kwake lakini vikwazo ndio vinamtesa zaidi baada mwezi kutoka sasa russia watahitaji gunia la pesa kununua mkate tu, transaction za benk zote zimekuwa blocked, raia wake kwa maelfu wanaandamana kupinga upumbav wa Putini
 
Ondoa upuuzi wako apa aliyetaka mazungumzo zaidi ni Russia baada ya hali ngumu Kiev ambayo hawakutarajia, miji ya kiev ipo under control of Ukraine ndio mana sasa anatishia kutumia nuclear ngoma nzito kwake lakini vikwazo ndio vinamtesa zaidi baada mwezi kutoka sasa russia watahitaji gunia la pesa kununua mkate tu, transaction za benk zote zimekuwa blocked, raia wake kwa maelfu wanaandamana kupinga upumbav wa Putini
😁😁😁😁Kaka pole Sana hujui kitu Russia sio Zimbabwe...
 
😁😁😁😁Kaka pole Sana hujui kitu Russia sio Zimbabwe...
Meli ya russia juzi imekamatwa ufaransa cape sized imezuiwa watu washagawana ngawira sasa wanadoea nyengine itakayotokeza., ndivyo Putini anavyoenda kuumia alifikiri Ukrain ni vita ya Syria, jana tu Germany kapeleka lethal weapon za kuzuia kombora za russia 1000 na 500 missiles., ndio mana sasa anatishia nuclear
 
masharti ya Urusi kwenye mazungumzo ni yaleyale Ukreine asijiunge na NATO.
Putin ni mtemi aisee,nchi huru unaipangiaje?
 
Meli ya russia juzi imekamatwa ufaransa cape sized imezuiwa watu washagawana ngawira sasa wanadoea nyengine itakayotokeza., ndivyo Putini anavyoenda kuumia alifikiri Ukrain ni vita ya Syria, jana tu Germany kapeleka lethal weapon za kuzuia kombora za russia 1000 na 500 missiles., ndio mana sasa anatishia nuclear
Kaka kwa mawazo haya wazungu watatutawala kwa muda wote mpaka wajichokee wenyewe.
Hiyo ni plopaganda yakijinga mnoo. Ok sawa amini unachoamini kiongozi...
 
Kaka kwa mawazo haya wazungu watatutawala kwa muda wote mpaka wajichokee wenyewe.
Hiyo ni plopaganda yakijinga mnoo. Ok sawa amini unachoamini kiongozi...
Ni kwa sababu Uputini umekushika kichwani kwako, nyinyi ndio wale mulisema Putini ndio baba wa dunia sijuw anatengeneza silaha sijui vipi sijui vile., magharibi wanapigana hii vita kisayansi zaidi ni kama vile babako putini ameingia kichwa kichwa sasa huamini chochote kinachojiri kwa swahiba wako
 
Ni kwa sababu Uputini umekushika kichwani kwako, nyinyi ndio wale mulisema Putini ndio baba wa dunia sijuw anatengeneza silaha sijui vipi sijui vile., magharibi wanapigana hii vita kisayansi zaidi ni kama vile babako putini ameingia kichwa kichwa sasa huamini chochote kinachojiri kwa swahiba wako
Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maharifa..
Jipe fikla huru mawazo huru acha ujinga wako pembeni.amini unachoamini kaka.
 
Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maharifa..
Jipe fikla huru mawazo huru acha ujinga wako pembeni.amini unachoamini kaka.
Jana ametangaza mazungumzo kuomba poo ili akajipange tena lakini ufahamu tu mizigo kama kawaida inaendelea kupokelewa Ukraine germany pekee wamepeleka lethal weapons 1000 na missiles 500
 
Back
Top Bottom