Ukumbi wa Arnautoglo safari ndefu ya Mwalimu Nyerere ilipoanzia

Ukumbi wa Arnautoglo safari ndefu ya Mwalimu Nyerere ilipoanzia

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
UKUMBI WA ARNAUTOGLO SAFARI NDEFU YA MWALIMU NYERERE ILIPOANZIA

1141636


George Arnautoglo alikuwa Mgiriki tajiri na ndiye aliyejenga jumba hilo akalitoa kwa matumizi ya Waafrika wa Tanganyika.

George Arnautoglo alikuwa hawapendi Waingereza kwa kuwa walikuwa wameikalia nchi yake Greece ambako Padri Makarios alikuwa akiongoza mapambano ya kudai uhuru.

Arnautoglo alipata kutoa fedha kwa siri kuwapa TANU zisaidie harakati za kudai uhuru na fedha hizi alimpa Ali Mwinyi Tambwe aliyekuwa mmoja wa viongozi wa juu wa TANU.

Kwenye Ukumbi huu wa Arnautoglo tarehe 17 April 1953 ulifanyika uchaguzi wa mwaka wa TAA kumchagua Rais na viongozi wengine.

Julius Kambarage Nyerere, mwalimu wa shule asiyefahamika sana kutoka Pugu alikuwa anagombea nafasi hiyo dhidi ya kijana maarufu wa Dar es Salaam na Kaimu Rais wa TAA na Katibu wake, mtoto wa mwanasiasa na mfanya biashara maarufu wakati wake, Kleist Sykes, Abdul akiwa Market Master Kariakoo Market.

Nyerere alishinda uchaguzi huu kwa kura chache sana.

Vipi Nyerere aliweza kumshinda Abdul Sykes siku ile ni kisa cha kusisimua katika historia ya Tanganyika na historia ya Mwalimu Nyerere.

Hapa kwenye jengo hili na siku ile ndipo Julius Nyerere alipoanza safari yake ndefu ya siasa na uongozi.

Hapa Nyerere alikuwa siku ile kavuka kiunzi kikubwa katika maisha yake ya siasa.

Meneja wa Ukumbi huu wa Arnautoglo ambae na yeye alishiriki katika kupiga kura ya kunyoosha mikono alikuwa kijana wa Kinyasa kutoka Nyasaland (Malawi) Dennis Pombeah.

Phombeah akiendesha pikipiki yake aina ya BSA alizunguka mji mzima kumfanyia Nyerere kampeni.

Abdul na wenzake katika TAA hawakufanya kampeni yoyote kwani walitaka Nyerere ashinde.

Imenichukua zaidi ya miaka 10 kutafuta picha ya Dennis Phombeah na mwisho nimeipata picha yake.

1141637

Dennis Phombeah
Phombeah kama meneja wa Arnautoglo Hall kafanya mengi katika kuisaidia TAA hadi TANU wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika historia ambayo si wengi wanaifahamu.

Lakini Dennis Pombeah alikuwa rafiki kipenzi wa Oscar Kambona...

1141638

Picha: Ukumbi wa Arnautoglo, Dennis Phomeah Menaja wa Arnautoglo na picha ya tatu kulia Nangwanda Lawi Sijaona, Abdulwahid Kleist Sykes, Julius Kambarage Nyerere na Waziri Dossa Aziz katika Ukumbi wa Arnautoglo kwenye dhifa ya kumuaga Rais wa TANU Julius Nyerere safari ya pili UNO 1957
 
Kituko kingine hichi yani mshindani hakupiga kampeni makusudi ili mtu mwingine ashinde [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
UKUMBI WA ARNAUTOGLO SAFARI NDEFU YA MWALIMU NYERERE ILIPOANZIA

George Arnautoglo alikuwa Mgiriki tajiri na ndiye aliyejenga jumba hilo akalitoa kwa matumizi ya Waafrika wa Tanganyika.

George Arnautoglo alikuwa hawapendi Waingereza kwa kuwa walikuwa wameikalia nchi yake Greece ambako Padri Makarios alikuwa akiongoza mapambano ya kudai uhuru.

Arnautoglo alipata kutoa fedha kwa siri kuwapa TANU zisaidie harakati za kudai uhuru na fedha hizi alimpa Ali Mwinyi Tambwe aliyekuwa mmoja wa viongozi wa juu wa TANU.

Kwenye Ukumbi huu wa Arnautoglo tarehe 17 April 1953 ulifanyika uchaguzi wa mwaka wa TAA kumchagua Rais na viongozi wengine.

Julius Kambarage Nyerere, mwalimu wa shule asiyefahamika sana kutoka Pugu alikuwa anagombea nafasi hiyo dhidi ya kijana maarufu wa Dar es Salaam na Kaimu Rais wa TAA na Katibu wake, mtoto wa mwanasiasa na mfanya biashara maarufu wakati wake, Kleist Sykes, Abdul akiwa Market Master Kariakoo Market.

Nyerere alishinda uchaguzi huu kwa kura chache sana.

Vipi Nyerere aliweza kumshinda Abdul Sykes siku ile ni kisa cha kusisimua katika historia ya Tanganyika na historia ya Mwalimu Nyerere.

Hapa kwenye jengo hili na siku ile ndipo Julius Nyerere alipoanza safari yake ndefu ya siasa na uongozi.

Hapa Nyerere alikuwa siku ile kavuka kiunzi kikubwa katika maisha yake ya siasa.

Meneja wa Ukumbi huu wa Arnautoglo ambae na yeye alishiriki katika kupiga kura ya kunyoosha mikono alikuwa kijana wa Kinyasa kutoka Nyasaland (Malawi) Dennis Pombeah.

Phombeah akiendesha pikipiki yake aina ya BSA alizunguka mji mzima kumfanyia Nyerere kampeni.

Abdul na wenzake katika TAA hawakufanya kampeni yoyote kwani walitaka Nyerere ashinde.

Imenichukua zaidi ya miaka 10 kutafuta picha ya Dennis Phombeah na mwisho nimeipata picha yake.

Phombeah kama meneja wa Arnautoglo Hall kafanya mengi katika kuisaidia TAA hadi TANU wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika historia ambayo si wengi wanaifahamu.

Lakini Dennis Pombeah alikuwa rafiki kipenzi wa Oscar Kambona...
 
matokeo kwa ujumla yalikuwaje? na kwanini abdul hakumpigia kampeni nyerere?
 
Abdul Sykes kwanini hakutaka yeye kushinda na aliingiaa kwenye uchaguzi? ,

Kama hakutaka kushinda kwanini asingejitoa ili iwe kazi rahisi kwa mtu amtakaye aweze kushinda?

Kwanini tusiseme alishindwa ?
Tycho,
Bahati mbaya umelikuta darsa katikati lakini laiti ungelikuwa toka mwanzo
ungejua nini kililipitika.

Abdul mtu aliyemtaka aje TAA wamchague kuwa Rais na kisha waunde
TANU alikuwa Chief Kidaha Makwaia.

Haya yalikuwa kati ya mwaka wa 1950 hadi 1952.

Mpango huu haukufanikiwa ndipo mwaka wa 1952 Abdul akakutana na
Nyerere.

Hamza Mwapachu akijuana na Nyerere kwa miaka mingi.

Hamza aliona mtu anaefaa kuongoza harakati za kudai uhuru ni Julius
Nyerere
na alimgusia hilo Abdul.

Abdul kabla hajaitisha uchaguzi wa TAA wa mwaka wa 1953 alisafiri hadi
Nansio Ukerewe akiongozana na Ali Mwinyi Tambwe kwenda kupata kauli
ya mwisho ya Mwapachu kuhusu Nyerere.

Mwapachu alimfahamisha Abdul kuwa kauli yake ni ile ile kuwa Nyerere
atiwe katika uongozi katika uchaguzi ujao, yaani ule wa 1953 na mwaka
wa 1954 TANU iundwe na Nyerere aongoze harakati za kudai uhuru.

Hii ndiyo sababu Abdul hakufanya kampeni ashinde uchaguzi ule.

Kwa hali ya Dar es Salaam ya miaka ya 1950s Nyerere asingeliweza hata
kidogo kumshinda Abdul.

Siku zile hawa akina Sykes nguvu yao ilikuwa kubwa katika TAA na TANU
ndiyo maana hadi leo nyaraka za vyama hizi pamoja na barua za Nyerere
wanazo wao na hawakuzirejesha TANU.

Kubwa ni kwa kuwa baba yao Kleist ndiye aliyeasisi African Association 1929
akiwa Katibu na mwanae Abdul akaja kukiongoza chama hiki mwaka wa 1950.

Katika mazingira kama haya Abdul angelisema anajitoa katika uchaguzi hili bila
shaka lingezua mzozo ndani ya chama.

Wanachama wangetaka kujua sababu.

Baba yake, Kleist Sykes aliwahi kujiuzulu ukatibu mwaka wa 1933 na nafasi yake
ikashikwa na Erika Fiah.

Chama kilikufa.

Rais wa AA Mzee bin Sudi alimwandika barua ya kumuomba arejee kwenye chama.
Mzee bin Sudi alianza barua hii kwa maneno haya: ''Bismilliah Rahman Rahim...''

Alikubali kurudi kwenye chama na akasema hili jambo letu ni muhimu na hili jambo
tuliloanza hata kama sisi hatutalikamislisha hao wanaokuja watalihitimisha.

Jibu la Kleist ukilisoma litakuacha kinywa kimejaa mate.

Sasa baada ya Nyerere kushinda na kuchukua uongozi wa TAA 1953 chama kilikufa.
 
Askofu Makarios alikuwa anapigania uhuru wa Cyprus na sio Greece. Na ndie alikuja kuwa rais wa kwanza wa Cyprus.
Congo...
Hakika ni Cyprus niwie radhi nimekosea na nitasahihisha.

Kitamaduni Cyprus na Greece wako sawasawa na ni kama
ndugu wawili.
 
Hawa akina Abdul na Kleist inaonekana walikua ni wahuni wa Kariakoo ya enzi hizo na walikua wanalindwa na 'uenyeji wao' tu kwahyo wangewez kushinda chaguzi zozote za AA na TAA kwakua kwanza umedai chama walianzisha wao na chaguzi walikua wanaendesha wao. Ni kama kusema hao ndio haswa waasisi wa ufedhuli wa CCM ya leo, wapanga matokeo. Ila muda wote walijirudi na kumpisha Mwalimu hasa baada ya kujipima uwezo wao wa kiuongozi na kuona hawaenei kwenye viatu vile.
 
Gonga like kama unasubiri part 2 kwa hamu kama mimi[emoji106]
Kingsmann,
Historia ya TANU ni tamu sana na inasisimua.

Namshukuru siku zote Bwana Ally Sykes kwa kunifungulia nyaraka
zake na kunipa mimi fursa ya kuzisoma na pia kumhoji.

Inasikitisha sana kuwa wenye nyaraka hizi wamezuia zisisomwe na
umma.
 
Blac...
Nadhani ushasoma jibu langu kwa Tycho.
hapana hujalijibu ila umeongeza details ngoja nifafanue, abdul alitamani nyerere ashinde lkn aligombea na hakuwaweka wazi wafuasi kuwa msinipigie kura, kura zangu mpeni nyerere(kampeni) naona kama abdul alitamani nyerere ashinde kimoyoni si kwa vitendo so umewezaje kumsemea mtu ya rohoni? hapo huoni kuwa abdul angeshinda coz tayari alikuwa anajulikana zaidi ya nyerere? mkuu said zipo chaguzi nyingi ambazo wagombea walishinda uchaguzi bila kampeni bila shaka unafahamu. Sasa pia nilitaka kufahamu nyerere alipata kura ngapi na abdul alipata ngapi?
 
Hawa akina Abdul na Kleist inaonekana walikua ni wahuni wa Kariakoo ya enzi hizo na walikua wanalindwa na 'uenyeji wao' tu kwahyo wangewez kushinda chaguzi zozote za AA na TAA kwakua kwanza umedai chama walianzisha wao na chaguzi walikua wanaendesha wao. Ni kama kusema hao ndio haswa waasisi wa ufrdhuli wa CCM ya leo, wapanga matokeo. Ila muda wote walijirudi na kumpisha Mwalimu hasa baada ya kujipima uwezo wao wa kiuongozi na kuona hawaenei kwenye viatu vile.
Marashi,
Ungeweza kuliuliza au kutoa fikra zako kiungwana.
Hivi ungenipa nafasi ya mimi kuchangia ninayoyajua.
 
Daudi,
Uliza swali kiungwana mathalan ungeandika kwa nini Abdul hakufanya kampeni?

Uliza kwa adabu nitarejea kukupa kisa cha kusisimua.
Mkuu heshima kwako, sina mpango wa kuuliza hilo kwasababu kama kuna sababu ungeziweka tu kwenye bandiko lako ila fahamu tu nathamini na kuheshimu mchango wako kwenye historia ya nchi yetu.
 
Back
Top Bottom