Ukurasa wa Serikali 'Tanzania Government' uliotumika kutangaza kutafutwa Kigogo2014, wafutwa

Si mara moja jeshi la polisi limetangaza kumtaka juyu msumbufu.
 
Kigogo anajitapa huko rais kawaambia wafute...
 
Ndio ushangae akili za mataga 😆😆
 
Kuna mchezo umefanyika pale ndio maana fasta Facebook wakaifunga hiyo account.
 
kwa uelewa wako Polisi haijawhi kutngaza officially au?
 
Ndio maana Mkapa aliwatukana kwa kuwaita malofa. Watanzania wengi wajinga sana, huyo Kigogo mwenyewe ni mpiga ramli tu sio kila taarifa anayotoa ni ya kweli
 
Hongera usie penda udaku ila una comment kwenye udaku,

Account ya serikali ambayo ni verified na fb, harafu unasema tunapenda udaku, ila Mataga dah bado safari ndefu
Una uhakika ni ya serikali? Ulishaingia kwa hiyo account kabla au baada ya hiyo post??
 
Ile siyo account ya serikali. Kwanza kwa jinsi tangazo lilivyotolewa ingekuwa vichekesho sana serikali ku-post tangazo la kijinga namna hiyo. (japo iliyokuwa ya Magufuli kufanya kitu kama hiyo siyo ajabu sana) Ni mhuni mmoja tu ameamua kufungua account na anaweza asiwe huyo Kigogo. Watanzania wengi hawajui kuangalia na kutofautisha genuine na fake kwenye internet hivyo wengi wanatumia huu udhaifu kuwachezea. Kuna sababu mbili zinafanya watu wawe mbumbumbu hivyo 1. Elimu yetu haiandai wahitimu kutafakari bali kumeza kila kilicho mbele yao + ugeni wa watanzana wengi kwenye mtandao 2. Watanzania wa kada ya chini wasio na elimu eg house girls, bar maids, bodabodas wana access na internet na ilivyo ni kuwa hili kundi uelewa wao wa mambo uko chini.
 
Walishindwa waislaeri wataweza hao waliosomea UDOM [emoji23][emoji23]
Hahahahaha kwahiyo na wewe unaamini kabisa eti waisraeli walilipwa wamtafute kigogo? Hahaha Tanzania tuna safari ndefu sana
 
Sasa wewe umeandika logic gani hapa zaidi ya mahaba ndio yanakuendesha?

Unataka nikupe facts? haya hizi hapa

Angalia email iliyotumika kufungulia hii account, je ni email address ya ikulu? Lakini ikawa verified


Kabla ya kuifunga hii account Facebook waliondoa blue tick, umejiuliza why? jamani punguzeni mahaba au chuki mpaka mnagoma kuupokea ukweli.
 
Mkuu badala ya kutuona sisi watanzania ni mambumbu mimi naoana ungejikita kutupa elimu ya kutofautisha Fake account na Genuine acc kwenye mitandao, Tutashukuru mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…