Ukwaju ni kiboko ya kitambi

nayo unaenda choo etnh??
 

Hapo nakataa mkuu, hiyo ikitokea inasababisha constipation.

Chakula kikizidi mwilini kinaenda kutunzwa kwenye ngozi jambo ambalo ndio sababu kuu ya kitambi.

Hapa umezungumzia jinsi ukwaju unavyosafisha tumbo kwa kufanya upate haja kubwa vizuri ambapo utaruhusu utendaji kazi vizuri wa tumbo.

Kama tumbo liko poa mmeng'enyo wa chakula utakuwa poa na chakula kitaingia mwilini vizuri na kikizidi kinaenda kutunzwa kwenye ngozi.

Kwa mantinki hiyo mimi nataka nijue kivipi ukwaju utafanya chakula kilichotunzwa mwilini(ngozi) kipungue.

Nalifanyia kazi hili jambo nikipata jibu lake sahihi nitakupa mrejesho.
 
Kwenye maduka ya wachina ukwaju wanaufunga kama pipi, mwingine wanaweza pilipili kwa mbali mzuri kwa mimba changa
 
sawa mkuu lakini mimi nachosema ni kwamba haiwezekani chakula kilichobaki bila matumizi kikahifadhiwe kwenye ubongo wakati pahala pake ni tumboni

kwa hvyo hapo tumboni ndyo benki kuu ya viyu vyote....


nachojaribu kumaanisha ni kwamba kitambi asili mia kubwa ni mlundikano wa mavi na uchafu ungine katika utumbo mpana

utumbo unakuwa umegandwa na mauchafu mengi kwenye zile kuta zake hvyo njia inakuwa ndogo sana ya kupitisha hata kinyesi na kufanya kinyesi kingine kikwame humo na kubaki


na kikikwama nacho kinatengeza makazi kidogo kidogo na kuwa hapo kwa mda mrefu hakibaki kama mavi tena lazima kijibadili tu na kuwa kitu kingine lakini asli yake ni kinyesi
 
Poa
 
Njia za kuondoa kitambi ni mbili, upasuaji na mazoezi, haya mengine ni uongo mwingine huu
 
Hivi inaingia akilini?

Fat iliyopo tumboni eti iondoke kisa unakunywa ukwaju? Upo serious?
Mara sijui green tea?

Hivyo vitu vina components gani ambazo zinayeyusha fat yote hapo tumboni?

Hii ingekua kweli ungeona jinsi wazungu wanavyotengeneza version yao na kuinadi kwa nguvu zote. Namibia au Angola kama sijakosea kuna mimea ukila sasa hivi unaweza usisikie njaa mpaka kesho kutwa.

Wazungu wakaitransform ile mimea into pills vya kupunguza unene, ukwaju hawakuuona?
 
Duu! Hiyo sayansi yako ulisomea wapi mwenzetu? Acha kupotosha watu kama hujui bora ungenyamaza maana ulichokiandika ni mawazo yako na wala hakuna ukweli wowote!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…