Ukweli: Kidunda atapigwa tena na Katompa

Ukweli: Kidunda atapigwa tena na Katompa

Kwa kadri ya kumbukumbu zangu na kwa kadri ya muonekano wa game ya kwanza , huyo bondia mwanajeshi wa Tanzania aitwaye Kidunda hana uwezo wa kumpiga Bondia Mkongo Katompa , hata afanye mazoezi gani .

Mbinu pekee ya ushindi ni ile ile ya siku zote ambayo ni Mbeleko ya Majaji akina Antony Ruta na wengine .

Sent from my SM-J500H using JamiiForums mobile app
Nimeahirisha kukudhararu kwsababu fulani fulani...

Ahsanta
 
Tumheshimu Kidunda kama alivyo tuheshimisha. Kitendo Cha Kidunda kupigana Kwa Staili ya kuingia ndani kabisa ya katompa na kupiga ngumi mchanganyiko ni jambo la hatari na la kishujaa.
Kwa power punch na wepesi wa Katompa inahitaji akili, kujitoa mhanga na uvumilivu wa Hali yajuu.
usifikiri Ngumi za Katompa azikumpata Kidunda!! Ila ni ujasiri uliomuwezesha kuingia na kupiga bila kumwachia Katompa nafasi.

Staili kama ya Kidunda ndiyo iliyo mwezesha Evanda Holyfield kumpiga Mike Tyson. Ni kumsogelea mpinzani na kupiga punch uku ukivumilia punch nzito kutoka Kwa mpinzani wako.
 
Halikuvunjika bali kidunda aliokolewa baada ya kuchanwa

Sent from my SM-J500H using JamiiForums mobile app
Achana na kufuatilia ngumi, jaribu hata kushabikia rede huu mchezo huuelewi. Yaani mtu kafanyiaa faulo mbaya ya kupigwa kichwa cha makusudi hadi damu zikavuja na kushindwa kuendelea, unakuja kusema ameokolewa.

Basi kama ulikuwa hujui kama zingekuwa zimetimia raundi nne angepewa ushindi moja kwa moja kwa faulo ile aliyofanyiwa, napo mngerudi kusema majaji walimbeba na kumpa ushindi.

Hakuna kuokolewa wala nini, mkongo alifanya figisu na kumpiga kichwa makusudi.
 
Eti kapigwa kichwa halafu drooo !!
Sasa kichwa kinaruhusiwa kwenye ngumi? Technical draw ilikuja kwasababu hazikutimia raundi nne, kama zingetimia na kafanyiwa faulo mbaya hadi hawezi kupambana tena angepewa ushindi direct kwa mujibu wa sheria za ngumi.

Huu mchezo kama hamuuelewi msiushabikie
 
Achana na kufuatilia ngumi, jaribu hata kushabikia rede huu mchezo huuelewi. Yaani mtu kafanyiaa faulo mbaya ya kupigwa kichwa cha makusudi hadi damu zikavuja na kushindwa kuendelea, unakuja kusema ameokolewa.

Basi kama ulikuwa hujui kama zingekuwa zimetimia raundi nne angepewa ushindi moja kwa moja kwa faulo ile aliyofanyiwa, napo mngerudi kusema majaji walimbeba na kumpa ushindi.

Hakuna kuokolewa wala nini, mkongo alifanya figisu na kumpiga kichwa makusudi.
[emoji38][emoji38][emoji38]Endeleeni kupanua magoli , halafu mbona ushindi wenyewe hamuushangilii kivile ?
 
Back
Top Bottom