Ukweli kuhusu bajeti ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania 2021/ 2022

Ukweli kuhusu bajeti ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania 2021/ 2022

hivyo vyama vingine ulivyo vitaja je vina wabunge silimia %ngapi humo buni mpaka waweze kupinga yanayopitishwa na wabunge wachama tawala
 
Kila mwaka , ngojera hizo zimekuwa zikiimbwa sana!!cha ajabu waziri anasema itabidi tufunge mikanda, huku wazee wa kusifu na kuabudu(wabunge wa ccm) wanatwambia sasa hii ni bajeti ya kurudisha pesa kwa mwananchi, vyuma vimepatiwa grisi wakiongozwa na nape!

Sasa hadi hapo kuna nini!!?huo ubabaishaji utaisha vipi wakati pesa nyingi inaliwa na wajanja!!eti mashine za efd za makusanyo zimepotea! unaingiza 50, zinapotea 70 hapo utegemee maendeleo?ndio maana marais wengi wa Africa wameamua kuwatesa wanyonge ili wapate pesa za bure za IMF/WB kwa kisingizio cha COVID 19!
Historia mpya itaandikwa kwa wino wa chuma. Serikali imedhamiria kwa dhati kuleta maendeleo jumuishi kwa wananchi wa Tanzania.
Hatutakiwi kuruhusu matatizo yatawale, tunatakiwa kuyatatua.
 
hivyo vyama vingine ulivyo vitaja je vina wabunge silimia %ngapi humo buni mpaka waweze kupinga yanayopitishwa na wabunge wachama tawala
Suala la Msingi ni kwamba wapo Bungeni na sauti zao zinatakiwa kusikika wakishauri kwa hoja.
Bungeni mambo yanajadiliwa kwa maendeleo ya nchi na sio vyama.
 
Historia mpya itaandikwa kwa wino wa chuma. Serikali imedhamiria kwa dhati kuleta maendeleo jumuishi kwa wananchi wa Tanzania.
Hatutakiwi kuruhusu matatizo yatawale, tunatakiwa kuyatatua.
Usisahau tu In Shaa Allah tarehe kama ya leo mwakani uje utupe tathmini ya utekelezaji wa hii bajeti...imekuwa ni kawaida miaka nenda miaka rudi kutenga mipesa lakini miradi haitekelezeki!...kabla sijasahau katika hizo trilion 36 asilimia ngapi tutategemea misaada kutoka kwa wadau wa maendeleo wa nje ya nchi..zamani kidoogo wakiitwa "mabeberu"
 
Wahenga walisema "Hakuna marefu yasiyokuwa na ncha", baada ya mjadala mrefu juzi Juni 22, 2021 Bunge la Tanzania lilipitisha na kuidhinisha Bajeti Kuu ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania shilingi trilioni 36.68 (36,681,897,765,000) kwa mwaka wa fedha 2021/2022 ambapo wabunge 361 sawa na 94% walipiga kura ya ndiyo, wabunge 23 sawa na 6% walipiga kura isiyo ya maamuzi (hawajakataa wala kukubali) na wabunge 5 hawakuwepo wakati wa zoezi hilo la upigaji kura. Ikumbukwe kwamba bajeti ya mwaka wa fedha 2021/2022 ina ongezeko la 4% ikilinganishwa na bajeti ya mwaka wa fedha wa 2020/2021 iliyokuwa ni shilingi trilioni 34.8.

Nilimsikiliza kwa makini Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) wakati akijibu hoja kwa ajili ya kuhitimisha mjadala wa Bajeti Kuu ya Serikali kabla ya Bunge kuidhinisha Bajeti hiyo Bungeni jijini Dodoma, kwa hakika Serikali inahitaji kupewa pongezi za dhati kwa jinsi ilivyojipambanua namna ambavyo itaenda kuitekeleza bajeti hii na kuhakikisha inaleta maendeleo jumuishi na endelevu.

Kuna baadhi ya hoja (mambo) wengi wetu tulizielewa vibaya kutokana na tafsiri tofauti zilizoenea sambamba na kukosa taarifa sahihi na huu hapa chini ndiyo ukweli kuhusu bajeti hii.​

KODI YA MAJENGO KUPITIA MITA ZA LUKU
Kodi hii haitatozwa kwa kila mwenye umeme na wala kwa matumizi ya umeme bali maeneo ambayo yatatozwa ni yale yaliyoainishwa yenye sifa kisheria, hivyo namba za mita za luku za wananchi ambao hawatakiwi kulipa zitaondolewa katika mfumo (blacklisted). Sambamba na hilo kodi hii italipwa na mmiliki wa nyumba na sio ya mpangaji. Kama ilivyokuwa inakusanywa kwa njia ya kawaida (physical) ukusanyaji uleule unapelekwa katika njia ya kielektroniki kwa sababu teknolojia imekuja ili kurahisisha kazi.

Serikali imeeleza kuwa kodi hii haitatozwa kwa kila mwenye umeme na wala kwa matumizi ya umeme kwa sababu kodi ingetozwa kwa matumizi ya umeme gharama za uzalishaji wa umeme zingeongezeka na hivyo kuleta adha kwa wananchi.

MAKATO YA SIMU KWENYE MUDA WA MAONGEZI
Makato hayatafanyika kila siku bali ni pale tu mtu anapoweka muda wa maongezi. Makato yataanzia shilingi 5 kwa wanaotumia shilingi 1000/= kwenda chini mpaka shilingi 222 kwa wanaotumia 100,000/= na kuendelea.

Mhe. Mwigulu Nchemba alisisitiza kuwa nchi hii (Tanzania) itajengwa na watanzania wenyewe, ni lazima tubebe majukumu hayo (ulipaji wa kodi) kama watanzania kwa sababu majukumu hayo ni yetu na nchi yetu ina matatizo pamoja na jitihada kubwa ambazo zimefanyika. Kila hatua ya maendeleo tunayoifanya inatuletea changamoto zaidi; ndivyo utaratibu wa maendeleo ulivyo.

WIZARA YA UJENZI NA UCHUKUZI
Serikali imetenga nyongeza ya bilioni 322 kwa ajili ya kufungua maeneo ambayo hayapitiki (hayana barabara) katika maeneo ya mijini na vijijini. Kila jimbo la uchaguzi litapata si chini ya bilioni 1 kwa ajili ya barabara hizi.

Barabara za vijijini zimekuwa ni kilio kikubwa kwa muda mrefu. Kutengwa kwa fedha hizi ambazo zitatumika kujenga barabara za vijijini ili zikae muda mrefu kutasaidia usafiri wa uhakika kwa wananchi, usafirishaji wa bidhaa na kuanza kusogeza huduma karibu na wananchi sambamba na kuiwezesha TARURA kifedha na kiutaalamu ili ifanye kazi kwa ufanisi zaidi.​

WIZARA YA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA
Serikali imetenga nyongeza ya bilioni 70 ili kuwapeleka chuo wanafunzi 11,000 waliokosa mkopo mwaka 2020 na wanafunzi 10,000 wanaokadiriwa kuwa wangekosa mkopo mwaka 2021. Kutengwa kwa fedha hizi kutawezesha wanafunzi wote waliodahiliwa katika vyuo vikuu nchini na kuomba mkopo katika Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) kuweza kupata mikopo na kutimiza azma yao ya kupata elimu ya juu na kuongeza wasomi wa kada mbalimbali nchini.

Pia Serikali imetenga nyongeza ya bilioni 125 kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya vyumba vya madarasa (maboma) 10,000 kwa wanafunzi wanaoingia kidato cha kwanza, kila halmashauri itapata maboma yasiyopungua 10. Wanafunzi wengi waliofaulu wamekuwa wanashindwa kwenda kujiunga na kidato cha kwanza katika shule za Serikali kwa sababu hakuna nafasi au miundombinu haitoshi.

Ikumbukwe kuwa mwaka kesho (2022) taifa linaenda kupata toleo la kwanza la wanafunzi wanaoenda kumaliza darasa la saba na kuanza kidato cha kwanza ambao waliandikishwa kupitia elimu bila malipo kwa shule ya msingi. Fedha hizi ni sehemu ya hatua nzuri kukabiliana na uhitaji wa vyumba vya madarasa nchini.​

WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO
Serikali imetenga nyongeza ya bilioni 100 kwa ajili ya zahanati kwenye vijiji na kata (maboma ya afya). Fedha hizi zitahakikisha ujenzi ulioanza na ujenzi mpya unakamilika katika maeneo husika na wananchi hususan maeneo ya vijijini wanapata huduma bora za afya.

Pia Serikali imetenga nyongeza ya bilioni 50 kwa ajili ya vifaa tiba pamoja na dawa. Utekelezaji huu utaenda sambamba na suala la bima kwa wote.

WIZARA YA MAJI
Serikali imetenga nyongeza ya bilioni 207 kwa ajili ya shughuli za maji na utaratibu wa visima na mabwawa. Kwa sasa Serikali inajielekeza katika utaratibu wa kisima kwa kila kijiji kama ilivyo kwa umeme.

Pia fedha hizi zinatarajia kufanya ununuzi wa magari ya kujimba visima na greda za kuchimba mabwawa.

Mbali na hoja hizo hapo juu, Serikali imesisitiza kuwa inazingatia mambo yote yanayoikabili nchi yetu sambamba na miradi ya kimkakati ambayo ni lazima ipate fedha; Serikali imeona vyema ikafanya utaratibu wa kupata fedha kiasi (fedha za ndani) lakini kwa wakati huohuo itafute mikopo yenye masharti nafuu ambayo haitaipa mzigo mkubwa wa deni kwa taifa letu.

Ndugu watanzania wenzangu kazi ya kujenga nchi yetu lazima ifanywe na sisi sote.​

Nawasalimu kwa jina la Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania.


bajeti yoyote ambayo kila mwaka inakuja na mbinu mpya ya kumkamua na kumtoa pesa mwananchi hadi yule wa chini kabisa hiyo ni bajeti mufilisi, bajeti bora ni ile inayompa mwananchi wa kawaida hauweni kwenye kodi...
 
bajeti yoyote ambayo kila mwaka inakuja na mbinu mpya ya kumkamua na kumtoa pesa mwananchi hadi yule wa chini kabisa hiyo ni bajeti mufilisi, bajeti bora ni ile inayompa mwananchi wa kawaida hauweni kwenye kodi...
Wizara ya Fedha na Mipango imeweka mapendekezo mbalimbali yanayolenga kupunguza ugumu wa maisha kwa wananchi kama vile; kuzingatia maslahi ya wafanyakazi kwa kupunguza kodi ya mapato ya ajira kutoka asilimia 9% hadi 8%, kufanya marekebisho ya mfuko wa fidia kwa wafanyakazi kupunguza kiwango cha mchango kutoka asilimia1.0% hadi 0.6%, pamoja na kuzingatia maslahi ya wakulima wa mbogamboga na wengineo.
 
Usisahau tu In Shaa Allah tarehe kama ya leo mwakani uje utupe tathmini ya utekelezaji wa hii bajeti...imekuwa ni kawaida miaka nenda miaka rudi kutenga mipesa lakini miradi haitekelezeki!...kabla sijasahau katika hizo trilion 36 asilimia ngapi tutategemea misaada kutoka kwa wadau wa maendeleo wa nje ya nchi..zamani kidoogo wakiitwa "mabeberu"
Amen, Mwenyezi Mungu atujalie uzima.
Mchanganuo ni huo hapa chini.

Screenshot_20210625-103003_1.jpg
Screenshot_20210625-103003_1.jpg
 
NADHANI SI VYEMA KUDANGANYANA KWENYE HAYA MAMBO KWA SABABU:

1. Kodi ya majengo kulipwa kupitia mita za LUKU;

å Kwa hakika kabisa kila mwenye LUKU atalipa kodi hii bila kujali uko wapi na umefunga LUKU yako kwenye nyumba au juu ya mti...!

å Tumuulize waziri na serikali ni lini wamefanya survey nchi nzima ili wajue huyu mwenye LUKU namba hii anastahili au hastahili kulipa na tuna siku 5 tu bajeti hii ianze kutekelezwa...?

å Je, si kwamba wataitaka tu TANESCO kupeleka orodha ya wateja wote wa LUKU - TANESCO wizara ya fedha/TRA na kuingizwa ktk mfumo wa kodi moja kwa moja...?

å For sure, katika nchi hii kusema/kuzungumza huwa ni jambo moja rahisi sana lakini utekelezaji huwa ni jambo jingine gumu mno kwake ambapo mara nyingi hukinzana na kauli zao...

å Mfano ulio bado mbichi kabisa, ni huu wa ni agizo la kisiasa la kupandisha madaraja watumishi umma. Kulinakishiwa kwa kila kauli nzuri na tamu kama asali toka kwa viongozi....

å Lakini matokeo yake ni almost zero na kuacha vilio vingi vya wanufaika waliostahili wakiwa hawana la kufanya...!

å Vivyo hivyo, kodi hii italipwa na wanyonge na masikini wachache tu na wengi wenye majengo wanaostahili kulipa kodi hii hawatailipa...

2. Kodi ya line za simu kwa kadiri ya matumizi ya mwenye line...

å Kama ilivyo ktk kodi ya majengo vivyo hivyo itakuwa kwenye kodi hii. Kila mwenye line ya simu atalipa kodi hii na usije ukapigwa butwaa ikawa ni FLAT RATE kwa kila mwenye line ya simu...

å Watu tusiwe wasahaulifu kiasi hiki. Hebu tukumbuke ule mpango wa TCRA na kutoa unafuu wa vifurushi kwa watumiaji wa huduma za simu na internet...

å Kauli za viongozi wa serikali zilikuwa tamu kama asali kwenye masikio ya wananchi...

å Wenye kuona mbele wakakosoa sana. Wasio ona mbele wakashabikia. Ulipokuja utekelezaji, kilio nchi nzima. Na tukarudi kulekule tulikokuwa kabla...!

## Haya mawili, tegemeeni kilio kikubwa zaidi maana LUKU/TANESCO na kampuni za mitandao ya simu wao hawajasema upande wao watakuwa na charge rate kiasi gani kama gharama za kuikusanyia serikali mapato yake...

NINI TATIZO NA SULUHISHO LAKE?

1. Ni udhaifu wa mifumo ya utambuzi ya walipa kodi stahili ktk kila eneo la kodi kunakosababishwa na unevenly distribution of the nation's population. Hii imepelekea wananchi kuwa na makazi yasiyo ktk mpangilio maalumu kiasi kufanya kukusanya kodi ya majengo kuwa ngumu....

2. Suluhisho ni kurekebisha hayo ambako kunahitajika investment kubwa na wakati huohuo kuacha na kuepukana kabisa na siasa zetu za kijinga na kipuuzi ambazo zimeathiri kila eneo la maisha ya watu kijamii na kiuchumi...
 
Back
Top Bottom