Risasi iliingilia juu ya bega la kushoto (upande wa abiria) na kuingia shingoni na kutokea upande wa pili. Nani aliyeifyatua? Ni abiria (Mwalimu Dorothy)? Ni 'polisi jamii' watatu waliokuwa upande huo wa gari? Maana imeripotiwa 'wavamizi' walikuwa watano; wawili walisimama upande wa dereva (Barlow) na watatu upande wa abiria (Dorothy). Mtoto aliyekuja kufungua geti kasema wale waliokuwa upande wa abiria walimpora 'mama' pochi yake, it's unlikely walipora pochi huku wanafyatua risasi. After all mgomvi wao alikuwa dereva, ndiye waliyekuwa wanazozana naye. Na pia sitarajii wafyatue risasi kuelekeza upande waliko wenzao wawili maana ingewadhuru hao wenzao. Nabaki na mwalimu Dorothy. Kuna uwezekano alifyatua yeye risasi kwa tendo la kujihami mambo yakaenda kombo. Mtu mwenye ukaribu kama huo na RPC si ajabu alishawezeshwa kumiliki bastola. Na alitumia mkono wa kulia ambao isingekuwa rahisi kwa wavamizi waliokuwa kushoto kwake kumuona ili kuepuka kunyang'anywa. Baada ya kustushwa na alichokifanya (kumuua RPC) ali-panic, na hii ikarahisisha tendo la wavamizi kumpora bastola yake na kumsachi marehemu.
Kwa kuwa hakuwepo shahidi mwingine, na ili kukwepa hatia ya 'kuua bila kukusudia', Dorothy akatunga maelezo ambayo kila anayeyasikia anashangaa.