Ukweli kuhusu utajiri wa ndagu

Yupo mganga mmoja jilani yangu magari ya kila aina hayaishi kuja miye namuona anawatapeli maana naye choka mbaya
Mwingine alinifuata kaniambia kama ninataka kupanda cheo nimujulishe anitengenezee dawa
Hii dunia ina mambo mengi Kuna mambo yako nyuma ya pazia hatuyajui
 
Kama unaamini uchawi/ushirikina una exist Karne hii jipige kifuani huku ukisema "mimi ni zwazwa."
 
Na mkuu bora umesema anako enda anatapeliwa sio muda mrefu, kuna jamaa yangu keshapoteza sana pesa kwa kupewa ndumba ambazo hazifanyi kitu chochote kesha zunguka sana hii tanzania kutafta huo utajiri ni zaidi ya miaka 6 mpaka leo kuna kipindi nilimwambia aokoke tu ili anusurike tu kweli Mungu kamnusuru mana alikua kashafirisik kwaajiri ya waganga matapeli.
 
Unataka ukaue familia nzima mkuu?duh tangulia kabla hujawaua ndugu zo!
 
Kuna sehemu unaambiwa hela yako ni lazima uitumie hakuna kuweka akiba.

Sasa wana wanalazimisha watu kulewa, akifika bar analipia bia mnywe tu. Kuhonga ndo usiseme.

Yaani hela inakuweka busy isivyo kawaida.
Hii IPO njombe kuna majamaa ndio zao kuingia bar ananunua vinywaji vyote halafu watu wanakunywa bure. Sema sasa hivi watu wameanza kusanuka wanakataa ofa zao yaani ni tafrani
 
Haya nenda mpka mulusagamba huko,, uliza wenyeji ukiona wapata tabu uliza kwa mzee wa matuta na maji aliemlimisha matuta mtu na wazifa wake akaleta dharau kilichomkuta anakijua yeye sa hivi ni story,,,, halafu uchawi ni gharama za pesa, muda, na mali hakuna cha rahisi kisicho na gharama..... Pia ndagu, uchawi, na dawa zake una code zake kirahisi mtu akufungukie humu jf.... Haya location hiyo nenda
 
Mulusagamba wapi huko
 
Mtu apataye mali isiyo halali ni kama kware akusanyaye makinda ambayo hakuyaangua: Wakati wa kilele cha ujana wake itamchopoka, na mwishoni atakuwa mtu mpumbavu.
Yeremia 17:11 BHND
 
Kama bakhera asipokoment humu basi uchawi wa ndagu hakuna.......
 
Nimemwambia manake nimeshayaona mengi hadi huko makaburini nishaenda. Ngoja niishie hapa.

NB: WAKWELI WAPO. ILA NI UTASOTA SANA. TENA SANA.
 
Waonee huruma watoto wako, maana lazima utaanza kuwatoa kafara Kwa kuwaua ama uwafanye mandondocha Dukani kwako
Doohhh..nime imagine, nikaogopa kabisaa.. watoto wangu hawa hawa ninavyowapenda na kujihangaisha kwa ajili yao leo et niwafamye ndondocha mazezeta kisa nipate pesa, ooohhh no no no!!!! Acha nikomae hiv hiv tu
 
Mshana jr,popote ulipo nje ya Tanganyika au ndani ya Tanganyika njoo unipe muongozo mkuu,umasikini ni laana
 
Doohhh..nime imagine, nikaogopa kabisaa.. watoto wangu hawa hawa ninavyowapenda na kujihangaisha kwa ajili yao leo et niwafamye ndondocha mazezeta kisa nipate pesa, ooohhh no no no!!!! Acha nikomae hiv hiv tu
Wengi hupewa hayo masharti Mkuu
 
Mtoa mada nili Ahidi kukupa connection yahili na pm msg ulinitumia nadhani ila pm yangu inashida kidogo hivo chukua namba hapa nakutumia.
 

Attachments

  • IMG_20240510_093724_377.JPG
    116.9 KB · Views: 29
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…