Ukweli kuhusu waasisi wa TANU na harakati za kupigania uhuru

Ukweli kuhusu waasisi wa TANU na harakati za kupigania uhuru

Status
Not open for further replies.
FM La kwanza ni kukubali kwa serikali kuwa imepitika dhulma. Kisha hapo ndiyo tutashauriana nini cha kufanya. Tusisubiri hadi unga uzidi maji tutakuwa tumechelewa.
 
FM La kwanza ni kukubali kwa serikali kuwa imepitika dhulma. Kisha hapo ndiyo tutashauriana nini cha kufanya. Tusisubiri hadi unga uzidi maji tutakuwa tumechelewa.

Unataka serikali ikubali nini? Kuwa wakatoliki ndiyo wanaozuia waislamu kupata elimu? Kwa nini tusianze na kitu ambacho ni dhahiri na ambacho wote tunakubali nalo ni kuwa waislamu wako nyuma kielimu kulingana na wakristu. Sasa badala ya kusubiri hali iwe mbaya zaidi, ni lazima wale wenye nia njema watoe ushauri wa nini kifanyike kudhibiti hali hiyo. Wewe ndiye unayetaka tusubiri hadi unga umezidi maji! Swali ni; " serikali ifanye nini kudhibiti hiyo tofauti ya kielimu kati ya waislamu na wakristu?"

Amandla.......
 
Mkuu Kiranga,
Unarudia kosa la wengine kufanya kuwa Dar ilikuwa ni kule palipoitwa uswahilini peke yake. Nyerere hakuambiwa asivae kaptula bali alifahamishwa kuwa anapokutana na wazee wa Dar es salaam ( ambao wengi walikuwa waislamu) asivae kaptula maana hawatapendezwa kuona kijana kavaa kaptula. Akiwa na wasomi wenzake Magomeni na kwenye klabu zao, kaptula ruksa. Hii ku-conflate Dar es Salaam na uislamu ndiyo uliotufikisha hapa. Hapa Dar es Salaam walikuwepo wanyasa kibao ( wakina Kambona n.k.) ambao vazi lao lilikuwa kaptula na kuweka "wei", Nyerere na kaptula yake asingeonekana mtu wa ajabu. Tatizo lilikuja pale alipotaka kukutana na watu ambao mila na desturi zao hazikukubali uvaaji huo. Hawa ingawa walikuwa wengi lakini hawakuwa ndiyo reflection ya Dar es salaam nzima ya wakati ule!

Kosa hili ndilo linalompelekea Mohamed kudhani kuwa Tanganyika ilikuwa Dar es Salaam na kidogo Tanga peke yao. Anasahau umati mkubwa wa watu wa bara ambao bila wao hamna kitu ambacho kingefanyika. TANU bila kukubalika kwa hao wengine, ingekosa legitimacy na hapo ndipo Nyerere alipomzidi Sykes., uwezo wa kukubalika nchi nzima na si mkoa wa Pwani peke yake!

Amandla........

Kukataa kwamba Dar ya early 50's ilikuwa mainly uswahilini ni kukataa ukweli tu.
 
Mohamed Said,
Mkuu shukran sana unapotoa data kama hizi na kuniwezesha mimi nisiyekuwa ndani ya kabati kuzisoma na kutanzua baadhi ya mambo.

Sasa nachotaka kuuliza ni rahisi kabisa.. najua fika kwamba EAMWS ilifungwa kutokana na Waislaam wenyewe kina Adam Nassibu, na hapa ktk swla la warsha naona tena maelezo yanayowahusu watu hao hao kuhusiana na kufungwa kwa Warsha. Sasa iweje unamlaumu Nyerere wakati maamuzi ya mwisho walikuwa nayo Waislaam wenzako na una uhakika gani kwamba Nyerere alimpa order Jumbe Muislaam ili awasaliti waislaam wenzake wakati akijua Jumbe ni Muislaam!. Leo huyo Jumbe anaandika kitabu baada ya yeye kuwa mmoja wa watu waliofunga warsha..Huu kama sii Unafiki mkuu wangu utauita kitu gani...

Kwani kama angekataa kipi kikubwa kingempata kipi kama sii kuutetea Uislaam na kuweka ukweli bayana Watanzania wote wakauona..Leo hana kitu kwa kutetea Zanzibar lakini alishindwa kuutetea Uislaam hadi katoka madarakani..
How come kila kitu kinazungumziwa leo baada ya Nyerere kufa ndio tunasikia haya ya Vatican kuhusika hali wewe na mimi sote tumesoma wakati wa Nyerere toka mwanzo wa utawala wake. Iweje hizi ziwe hadithi za kusimuliwa na watu waliosoma wakati wa mkoloni hali toka Uhuru ni miaka 50 tu iliyopita ina maana kati yangu na wewe labda ni miaka mitatu au sita tu iliyotupita ya utoto kutofahamu hali halisi ambayo kwa uhakika mabadiliko makubwa ya elimu nchini yalianza mwaka 1967 tukiwa na akili zetu timamu..

Ebu soma tena kuanzia kipande chako hiki kwenda chini kisha nambie kwa nini lawama usiziweke kwa waislaam hawa kina Jumbe, Kawawa, Adam Nassibu, Mohamed Ally na Sheikh Abbas.. hawa wangeweza kabisa kukataa aliyoagiza Nyerere kwa faida ya Uislaam nchini. Kwa nini walifanya waliyoyafanya kama kweli walikuwa na uchungu na Uislaam kama sii kwa utashi wao wenyewe (Bakwata) kufunga warsha.

Warsha were accused of being anti-government and perpetrating animosity between Muslims and Christians through their writings. Nyerere ordered Aboud Jumbe to close the Muslim seminaries. A meeting between Aboud Jumbe and BAKWATA was held at Jumbe's official residence at Laibon Road. In attendance were Rashid Mfaume Kawawa, Adam Nasibu, Sheikh Mohamed Ali and Sheikh Abbas Makbul a representative of Darul Iftar. The stand of Sheikh Mohamed Ali was that if those Muslim seminaries have to be closed then the decision to take that step should be laid upon the government. This was a difficult step to be taken by the government as such an act would provoke Muslims. The meeting left the decision to close the seminaries upon BAKWATA. BAKWATA took a unilateral decision and reverse the schools back to its original state. Warsha not agreeing to BAKWATA's decision called a meeting of all Muslims to discuss the problem.

Domokaya,
Mkuu nimeipenda sana hii kitu ya Mwapachu imesimama kisomi, na inaeleza vizuri sana matoke ya UDINI nchini kwani binafsi naamini ni baada ya kurudisha shule mikononi mwa makanisa na misikiti ndio taabu ziliporudi. Tulikuwa na matatizo haya wakati wa mkoloni na Nyerere alitaifisha shule zote kwa sababu hii ya UDINI tu lakini sisi tumepuuza na kurudi ktk mfumo wa mkoloni na haya ndio matunda yake...Tunavuna tulichopanda, mtasema weee lakini UDINI unakua kwa nguvu kubwa ajabu sana na wala sii muda itakuwa mtu akitambulishwa kwa dini yake.
 
Kukataa kwamba Dar ya early 50's ilikuwa mainly uswahilini ni kukataa ukweli tu.

Kwa nini tuandikie mate wakati wino upo? Historia ya Dar es Salaam hii hapa: http://eprints.soas.ac.uk/3189/1/Brennan_%26_Burton_chapter.pdf

Kuwa mainly uswahili na kuwa ni uswahilini ni vitu viwili tofauti. Nyinyi mnataka kufanya kama vile Dar ya 1950s iliishia Mission Kota na waliishi hao mnaowaita waswahili kibao. Miaka hiyo ya 1950s serikali ilijenga quarters Magomeni, Temeke na Kinondoni ambako asilimia 52 ya wakazi wake walikuwa wakristu. Tusisahau vile vile sehemu za msasani, Mikoroshoni na Buguruni ( Toroli, Kipawa na Mtoni) ambako zilikuwa sehemu za waafrika ambazo hazikuwa planned. Ingawa wakristu walikuwa asilimia 12 tu ya wakazi lakini waislamu waligawanyika kwa makabila. Mgawanyiko huo ndiyo uliyofanya wazaramo 1938 waanzishe Waramo Union ambayo kwa muda ilikuwa na nguvu kuliko TAA! Waislamu wazaramo na wachomvi walikuwa hawaelewani na wamanyema ambao walionekana wanaelekea kutawala biashara na kumiliki nyumba nyingi hapa mjini!

Ostabei ilijengwa katika miaka ya 50 na maboi wake waliishi maeneo ya Kinondoni na Msasani. Wengi wa maboi walitoka bara (wanyasa n.k.) na sio pwani. Hawa nao walikuwa sehemu kubwa ya population ya Dar.

Katika census ya 1955, asilimia 55 ya wakazi wa Dar es Salaam walikuwa wahamiaji kutoka bara. Sasa mnapodai Dar ilikuwa ya waswahili au uswahilini peke yake inabidi mtupe tafsiri ya huo uswahili! Kama uswahili ulikuwa ni uislamu basi bila shaka sehemu kubwa ya dar ilikuwa waswahili. Lakini kama uswahili ni uzaliwa basi wengi wa wakazi wa Dar ya wakati huo hawakuwa waswahili!

Tukirudi nyuma zaidi, mwaka 1905 asilimia 27 ya wakazi wa mji walikuwa wale walioitwa wanyamwezi. Hawa waliishi Kinondoni na eneo la Msimbazi. Wangoni ( na wanyasa) waliishi Keko na Kijitonyama na wanubi waliishi Gerezani. Sehemu la katikati ya mji waliishi wamanyema hadi walipohamishiwa Bagamoyo Road kwenye mwaka 1906. Wazaramo wakati huo waliishi Buguruni, Tabata na Ubungo. n a washomvi, Kunduchi na Msasani.

Sasa leo mnapodai kuwa Dar es Salaam ilikuwa ya waswahili na sio watu wa kuja, hao waswahili mnaowaenzi walitoka wapi?

Amandla........
 
Mohamed Said,
Nilikuuliza ni sababu zipi zilizowafanya wakina Kleist Sykes waanzishe Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika ukajifanya haukunisikia. Ukweli ni kuwa huo mshikamano unaozungumzia baina ya waislamu haukuwepo bali walivumiliana tu. Waislamu waafrika waliona kuwa wenzao waarabu na wahindi wanawabagua na kuwadharau ndiyo maana wakaanzisha umoja wao. Katika miaka ya 1930 palizuka mgogoro mkubwa katika Jamaitul al-Islamiyya Umumiyya ambapo hao walijiona kuwa ndio wenye mji walipopambana na wale waliowaona wakuja. Hao wakuja walijumuisha wamanyema ambao ndio walikuwa waafrika wa kwanza kujenga msikiti wa maana Dar es Salaam na kuwa na makaburi yao amabyo yalimilikiwa na jamii yao. Tofauti hizi ndizo zilizopelekea kuanzishwa Zaramo Union 1938 ambayo ilikuwepo sambamba na TAA. Tofauti hizi baina ya waislamu zilichangia mno vifo vya taasisi zao kuanzia hiyo AMNUT na EAMWS. Mohamed Said anasahau kuwa mamlaka ya kwanza kunyang'anya shule za EAMWS ilikuwa ni serikali ya mapinduzi Zanzibar ambayo viongozi wake karibu wote walikuwa waislamu. Hii ilikuwa hata kabla haijapigwa marufuku Tanzania bara! Kwa nini basi kama kweli anatafuta haki asiwalaumu wakina Amri Abeid Karume pamoja na mkatoliki Julius Nyerere? Kwangu mimi hizo ni ishara ya msimamo wa kichochezi wenye nia ya kuwagawa watu badala ya kuwaunganisha kwa kusema ukweli!

Amandla.......
 
Mkuu wangu Waislaam wanajiua wao wenyewe kama ilivyo asili ya mtu mweusi kwani leo hii na mabaya yoote ya viongozi wetu iwe CCM, bado wananchi wanaichagua CCM kama ndio dini yao kisha hutafuta wachawi nje haswa Wazungu wawekezaji. Na bila shaka wazungu nao wanataka maendeleo pia yao zaidi, hivyo wanayo kila haki ya kujineemesha kutokana na mipango yao.

Wakristu wananeemeka kutokana na mipango yao, kamwe huwezi kuona Unafiki baina yao na kanisa hata kama iwe kuchagua baina ya Taifa na dini na haiwezi kutokea mgongano huo kwa sababu kila kitu kipo ktk vitabu. Lakini njoo kwa Waislaam, historia yoote aloandika Mohamed Said kwa asilimia kubwa waliochangia ugonvi na mabalaa ni Waislaam wenyewe tena basi hadi leo tuna migogoro ndani ya Bakwata, Bakwata na jumuiya za Kiiislaam, Masheikh na viongozi wengi wa dini ni balaa tupu kwa sababu Uislaam sio taasisi ila ni dini.

Nyerere kisha kufa hayupo tena duniani mbona Waislaam bado wanashindwa kujipanga pamoja na kuweka maamuzi yenye manufaa kwao. Nina hakika hata tarehe ya Idd el Fitr/Hajj itakuwa mvutano wengine wakisema tusifuate Saudia sijui hatujauona mwezi na kadhalika. Ili mradi tu ni kubishana kila mmoja wetu anajua zaidi ya mwingine..

Sasa mnapotaka kuufanya Uislaam kama taasisi inabidi mfuate misingi na taratibu za kuanzisha taasisi kwa kufuata vigezo fulani lakini sio kuumiziana sisi wenyewe kisha tunatafuta mchawi hali wachawi ni sisi wenyewe.
 
FM Ahsante kwa mchango wako. Hilo linawezekana sana. Migonganon katika jamii ni jambo la kawaida. Kubadilishana fikra kama hivi ni jambo jema nami unanisomesha yale ambayo yamenipita au sikuyaona kama ulivyoyaona wewe.
 
Mkandara ahsante kwa mchango wako. Umegusa jambo la kweli kabisa. Hadithi ya shoka na mpini. Ila kitu cha kutia moyo miaka ya sasa ni tabu kuwapata akina Rajab Diwani na Selemani Kitundu (Allah awasamehe). Ndiyo maana leo shule za Kiislam walimu wanasomesha historia ya Tanzania ile ya kweli. Mkubwa mmoja baada ya kusoma kitabu changu alinitafuta na kunambia anashukuru kuwa kaujua ukweli.
 
Ahsante Mkandara kwa mchango wako. Mimi nimezungumza yote hayo Nyerere akiwa hai. Sikupata kumuogopa na yeye hilo alilijua fika. Hakuthubutu kunijibu hadi anaingia kaburini. Hapa unaona jina langu kamili sijajificha nyuma ya pazia kwa kuwa nakiamini ninachosema.

Ama ya Mzee Jumbe, Kawawa, Adam Nasibu na wengineo ningependa kama maswali hayo wangejibu wenyewe. Nyerere namlaumu kwa kuwa mkono wake ulikuwapo katika kuwahujumu Waislam na hili linaonekana katika maandiko yangu yote.
 
FM nimekujibu kwanza serikali ikubali lipo tatizo. Serikali haikubali kuwa kuna ubaguzi na ushahidi ulipotolewa na Prof. Hamza Njozi katika kitabu chake "Mwembecha Killings" ilichofanya serikali ya Benjamin Mkapa ni kupiga marufuku kitabu. Waliyoana mle yamewatisha sana.
 
Ahsante Mkandara kwa mchango wako. Mimi nimezungumza yote hayo Nyerere akiwa hai. Sikupata kumuogopa na yeye hilo alilijua fika. Hakuthubutu kunijibu hadi anaingia kaburini. Hapa unaona jina langu kamili sijajificha nyuma ya pazia kwa kuwa nakiamini ninachosema.

Ama ya Mzee Jumbe, Kawawa, Adam Nasibu na wengineo ningependa kama maswali hayo wangejibu wenyewe. Nyerere namlaumu kwa kuwa mkono wake ulikuwapo katika kuwahujumu Waislam na hili linaonekana katika maandiko yangu yote.
Mkuu hapa sasa unakosea. Huwezi kusema kuna mkono wa Nyerere hjali hujawahi kuzungumza na Jumbe na ukamuuliza yeye kuhusika kwake wala kuandika ubaya wowote unaomhusu Jumbe. Hapa nikiwa na maana kama wewe umeweza kujua Nyerere ndiye alitoa order kwa Jumbe afenye vile kwa nini usianze na Jumbe, Kawawa au na wengine, bila shaka kitabu chako chote kinaepuka kutoa lawama kwa Waislaam.. ndivyo nilivyokuelewa mimi..
 
FM nimekujibu kwanza serikali ikubali lipo tatizo. Serikali haikubali kuwa kuna ubaguzi na ushahidi ulipotolewa na Prof. Hamza Njozi katika kitabu chake "Mwembecha Killings" ilichofanya serikali ya Benjamin Mkapa ni kupiga marufuku kitabu. Waliyoana mle yamewatisha sana.

Hamjatoa ushahidi wowote wa structural disrimination bali statistics zinazoonyesha kuwa waislamu hawafanyi vizuri shuleni kuliko wakristu. Ni ndoto za alinacha kutegemea serikali ikiri kitu ambacho hakipo. Na kukazania kuwa hamko tayari kuishauri serikali namna itakavyoweza kuwasaidia waislamu wenzemu ni kuwa irresponsible kuliko kifani maana wakati mkisubiri hiyo apology wenzenu wanasonga mbele na gap inazidi kuongezeka! Ndio maana nasema hamna nia ya kuwasaidia wenzenu bali kuhakikisha hata kile kidogo walichonacho hawatafaidi! Kama mnakataa kumshauri rais wenu ambaye ni muislamu mwenyenu kweli mtaweza kukaa meza moja na mkristu?

Amandla........
.
 
FM Ahsante kwa mchango wako. Hilo linawezekana sana. Migonganon katika jamii ni jambo la kawaida. Kubadilishana fikra kama hivi ni jambo jema nami unanisomesha yale ambayo yamenipita au sikuyaona kama ulivyoyaona wewe.

Hapana, Mkuu. Shida ni kuwa haukuwa na nia ya kutafuta ukweli bali ulitaka kuwamalaikisha waislamu na kuwaatupia lawama zote wakristu. Maandiko yako yenyewe yanakusuta. Hakuna mahali ambapo hao wazalendo hawakushirikiana wakristu kwa waislamu. Kama unyanyasaji na chuki, Nyerere hakuwaonea waislamu peke yao. Unalalamika kuwa wakina Sykes na wakina Mwapachu hawakuenziwa wakati humo humo unaelezea mchango mkubwa wa wakristu wakina John Rupia, Vedasto Kyaruzi, Mwanjisi na wengine. Unazungumziwa kuwekwa ndani viongozi wa vyama vya wafanyakazi na nyerere lakini humo humo unawataja wakristu walioswekwa ndani! Unakiri kuwa ni Jumbe ndiye aliyeuwa EAMSW lakini haumlaumu bali unamshupalia Julius.

Unasahau wakina waziri wa mambo ya ndani wa wakati huo ambaye aliyeandika na kusaini agizo la kuipiga marufuku EAMWS! Hauzungumzii mkutano uliofanyika 1968 ambapo Karume aliikemea EAMWS kuwa inapingana na sera ya ujamaa na ipo kwa ajili ya wageni! Hii ilikubalika kwa wengi wakati ule kwa sababu kila mtu alijua kuwa ingawa viongozi walikuwa Tewa na Bibi Titi lakini msukumo wa kipesa ulitoka kwa waislamu wa kihindi ambao walikuwa wafanya biashara ambao bila shaka hawakufurahia Azimio la Arusha. Yote haya huyaoni, unakimbilia kwenye hiyo myth ya Catholic Christian Movement.

Unatuambia kuwa ishara ya kuwa Nyerere kauupenda uislamu ni yeye kutofurahishwa ( bila kutuambia kama aliwakataza) kitabu kilichoandikwa na muislamu Sykes na mkristu Kleruu!

Hapana, Mkuu, ukivaa miwani ya udini inakuzuia kuona hata kilicho wazi. Sisi wakristu tunaamini kuwa kabla ya kutoa boriti katika jicho la mwenzako heri uanze na la kwako. Wewe umekazania kuonyesha makengeza ya wakristu wakati mwenyewe macho yako yanapofuka!

Amandla.....
 
Duh! Fundi kumbe wewe mkali hivyo kwenye historia eeeh? Heshima mbele mkuu...

Ila nina kaswali hapa....eti Dar kabla ya kuwa Dar ilikuwa inaitwa Mzizima?
 
Mkuu hapa sasa unakosea. Huwezi kusema kuna mkono wa Nyerere hjali hujawahi kuzungumza na Jumbe na ukamuuliza yeye kuhusika kwake wala kuandika ubaya wowote unaomhusu Jumbe. Hapa nikiwa na maana kama wewe umeweza kujua Nyerere ndiye alitoa order kwa Jumbe afenye vile kwa nini usianze na Jumbe, Kawawa au na wengine, bila shaka kitabu chako chote kinaepuka kutoa lawama kwa Waislaam.. ndivyo nilivyokuelewa mimi..

Mkandara hujasoma kitabu, kakisome kwanza..!!!
 
Hamjatoa ushahidi wowote wa structural disrimination bali statistics zinazoonyesha kuwa waislamu hawafanyi vizuri shuleni kuliko wakristu. Ni ndoto za alinacha kutegemea serikali ikiri kitu ambacho hakipo. Na kukazania kuwa hamko tayari kuishauri serikali namna itakavyoweza kuwasaidia waislamu wenzemu ni kuwa irresponsible kuliko kifani maana wakati mkisubiri hiyo apology wenzenu wanasonga mbele na gap inazidi kuongezeka! Ndio maana nasema hamna nia ya kuwasaidia wenzenu bali kuhakikisha hata kile kidogo walichonacho hawatafaidi! Kama mnakataa kumshauri rais wenu ambaye ni muislamu mwenyenu kweli mtaweza kukaa meza moja na mkristu?

Amandla........
.
Ushahidi gani tena wautaka?...Waislam hawataki Apology, wanataka HAKI itendeke....na hii ndio misconception kubwa mliyonayo mnafikiri waislam wanataka favor..waislam wanataka Haki itendeke.
 
Hapana, Mkuu. Shida ni kuwa haukuwa na nia ya kutafuta ukweli bali ulitaka kuwamalaikisha waislamu na kuwaatupia lawama zote wakristu. Maandiko yako yenyewe yanakusuta. Hakuna mahali ambapo hao wazalendo hawakushirikiana wakristu kwa waislamu. Kama unyanyasaji na chuki, Nyerere hakuwaonea waislamu peke yao. Unalalamika kuwa wakina Sykes na wakina Mwapachu hawakuenziwa wakati humo humo unaelezea mchango mkubwa wa wakristu wakina John Rupia, Vedasto Kyaruzi, Mwanjisi na wengine. Unazungumziwa kuwekwa ndani viongozi wa vyama vya wafanyakazi na nyerere lakini humo humo unawataja wakristu walioswekwa ndani! Unakiri kuwa ni Jumbe ndiye aliyeuwa EAMSW lakini haumlaumu bali unamshupalia Julius.

Unasahau wakina waziri wa mambo ya ndani wa wakati huo ambaye aliyeandika na kusaini agizo la kuipiga marufuku EAMWS! Hauzungumzii mkutano uliofanyika 1968 ambapo Karume aliikemea EAMWS kuwa inapingana na sera ya ujamaa na ipo kwa ajili ya wageni! Hii ilikubalika kwa wengi wakati ule kwa sababu kila mtu alijua kuwa ingawa viongozi walikuwa Tewa na Bibi Titi lakini msukumo wa kipesa ulitoka kwa waislamu wa kihindi ambao walikuwa wafanya biashara ambao bila shaka hawakufurahia Azimio la Arusha. Yote haya huyaoni, unakimbilia kwenye hiyo myth ya Catholic Christian Movement.

Unatuambia kuwa ishara ya kuwa Nyerere kauupenda uislamu ni yeye kutofurahishwa ( bila kutuambia kama aliwakataza) kitabu kilichoandikwa na muislamu Sykes na mkristu Kleruu!

Hapana, Mkuu, ukivaa miwani ya udini inakuzuia kuona hata kilicho wazi. Sisi wakristu tunaamini kuwa kabla ya kutoa boriti katika jicho la mwenzako heri uanze na la kwako. Wewe umekazania kuonyesha makengeza ya wakristu wakati mwenyewe macho yako yanapofuka!

Amandla.....
...Fundi nafikiri unashindwa Kujua situation za wakati wa Mwalim na Hao unaowaita "Waislam"...hao wote unaosema walikuwa hawafuruki kwa Nyerere. Ikiwa Nyerere aliweza mficha Jumbe....hayo mengine madogo angeshindwaje? Hao walikuwa wapokea Order tu....!!!

Mohammed Said kaandika tukio lingine la AGIP, Aziz...Nyerere alitoa order ya Kukamatwa Muft wa Tanganyika Shekh Hassan Bin Ameir...AGIP Aziz alikataa hio order...lkn nini kimefanyika...?Nyerere akafanya lake?

Ukisoma vema kitabu utajua Fitna za Nyerere...ilikuwa ukimpinga order zake anakutengenezea Zengwe...unatiwa ndani au kusahaulika kabisa....so hao unaowataja walikuwa Rubber Stamp.

Mzee Jumbe ameandika Kitabu..kitafute pia ukisome...!!!

Hivi waweza kunieleza kuwa Mahakama ya Kadhi na OIC ktk Utawala wa Jakaya umezuiwa na Jakaya?....!!!
Misamaha ya Kodi ya Makanisa imeruhusiwa kwa Serikali kupenda?.....Na hii ndio Christian Lobby anaiyozungumza Mohammed Said...!!!
 
Almost fifteen years later, on 2 February, 1999 the Member of Parliament for Kigamboni Hon. Kitwana Kondo told the parliament that out of every 100 students who sat for the standard seven examination in Dar es Salaam in the year 1998, 71 were Muslim and 29 Christian. But out of every 100 students selected to join government secondary schools only 21 were Muslim while 79 were Christian. The MP wanted to know whether Muslim children were inherently dull (An-Nuur, February 5-11, 1999).
Unless my math teacher was dumb something is wrong with these figures. If there were 100 students doing the standard 7 exam and 79 of them are Muslims and 21 Christians, then where did the other 58 Christian students come from to make a figure of 71 Christians going to secondary school? Did the school system convert former Muslim students to christianity?
 
...Fundi nafikiri unashindwa Kujua situation za wakati wa Mwalim na Hao unaowaita "Waislam"...hao wote unaosema walikuwa hawafuruki kwa Nyerere. Ikiwa Nyerere aliweza mficha Jumbe....hayo mengine madogo angeshindwaje? Hao walikuwa wapokea Order tu....!!!

Mohammed Said kaandika tukio lingine la AGIP, Aziz...Nyerere alitoa order ya Kukamatwa Muft wa Tanganyika Shekh Hassan Bin Ameir...AGIP Aziz alikataa hio order...lkn nini kimefanyika...?Nyerere akafanya lake?

Ukisoma vema kitabu utajua Fitna za Nyerere...ilikuwa ukimpinga order zake anakutengenezea Zengwe...unatiwa ndani au kusahaulika kabisa....so hao unaowataja walikuwa Rubber Stamp.

Mzee Jumbe ameandika Kitabu..kitafute pia ukisome...!!!

Hivi waweza kunieleza kuwa Mahakama ya Kadhi na OIC ktk Utawala wa Jakaya umezuiwa na Jakaya?....!!!
Misamaha ya Kodi ya Makanisa imeruhusiwa kwa Serikali kupenda?.....Na hii ndio Christian Lobby anaiyozungumza Mohammed Said...!!!
Chuma,
Sijasoma kitabu cha Jumbe. Lakini tatizo langu na Jumbe ni kwamba alikuwa miongoni mwa viongozi waliokuwa karibu sana na Nyerere kuanzia 1972 alipouliwa Karume mpaka alipoondolewa na kuchafuka kwa hewa Zanzibar. Huyu huyu Jumbe kuna wakati tulidhania alikuwa anajiandaa kumrithi Nyerere. Tatizo langu ni kwamba wakati wote ule aliokuwa karibu na Nyerere alimpa ushauri gani kuhusu hii "imbalance inayolalamikiwa baina ya waislamu na wakristo Tanzania?" Ningependa kusikia Jumbe anasema kuwa alimshauri Nyerere A and B lakini Nyerere hakumsikiliza. Hii ya kuandika kitabu baada ya kuondolewa mamlakani inampunguzia sana mzee Jumbe credibiliity.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom