Ukweli kuhusu waasisi wa TANU na harakati za kupigania uhuru

Ukweli kuhusu waasisi wa TANU na harakati za kupigania uhuru

Status
Not open for further replies.
KWA waliosoma history ya TANU,iliyochapishwa na chuo cha kivukoni,je ni kweli hawa akina SYKES are hardly mentioned,mimi historia sijui,but from what i have been reading in this thread,kama kweli hawapo,then for once niki omit udini wake i am ready to give mohamed said a positive benefit of doubt

SOA
Hakuna anayemkatalia Mkuu Mohammed Said anavyojaribu kuweka sawa Historia ya ukombozi wa Tanganyika.......Kitabu cha Chuo cha Kuvukoni SIO MSAHAFU..............na hakuna pahala paliposemwa/kutamkwa kuwa kilichoandikwa pale Kivukoni ni FINAL.............
Hivyo hakuna hapa anayepinga yanayoandikwa na M'med Said..........kinachopingwa hapa ni approach na picha anayotaka kuonyesha na hasa kwa umma wa Waislam kuwa ukombozi wa Tanganyika umeletwa na Waislam lakini Waislam hao hao hawana haki kwenye Keki ya Taifa i.e. matunda ya uhuru..............

Baadhi ya wana JF nikiwemo mimi tunamwambia kuwa Kuandika historia.....mtu yeyote atakayefanya utafiti na kupata facts anaweza rekebisha yale yaliyoachwa......kama anavyofanya yeye......kwa hiyo......dhana ya M'med kuwa ni dhulma Chuo Cha Kuvukoni kutomu/waandika watu wengine kwenye historia...........HAINA MSINGI..............kwani hata yeye kuna mambo hajayazungumza kwenye historia kuwa Waislam walipinga uhuru usipatikane ili nao waje wawe sawa na Wakristo kimaendeleo.............
 
In 1987 Prof. Malima became the first Muslim Minister of Education. By MS

Wakati Prof anakuwa Waziri wa Elimu, kwenye mitihani ZILITUMIKA NAMBA NA SI MAJINA kama ndg yetu MS/Prof. alivodai unavyodai....................HUU NI UONGO........tena wa mchana KWEUPE

 
Kichuguu: Karibu katika mjadala ila ombi langu moja kwako ni hili. Hapa ukumbini ni hoja kwa hoja hatutukanani kwa lugha za "upuuzi huu" pombe utaitia maji mnakasha hautonoga utadorora. Wako wanaoweza kusoma hata kuandika matusi na kuyajibu na kuna wengine hatuwezi.

Turudi katika mjadala. Kweli Nyerere alitaifisha shule za Wakatoliki lakini Waislam hawakusoma kwa wingi ule ule waliosoma Wakristo. Takwimu zipo ikiwa utazihitaji Insha Allah nitazitoa hapa ukumbini kwa faida yetu sote.

Ama kwa hilo la mimi kutafuta umaarufu niutafute umaarufu kwa nani na vipi maana mimi ni maarufu si leo labda toka nina miaka takriban 15. Nimezaliwa Dar es Salaam, nimekulia Dar es Salaam watu wengi wananijua na si mimi tu hadi wazee wangu ambao takriban historia yao sasa inaweza kufika hata miaka mia moja. Hii ni vizazi vingapi sijui. Hapana sitafuti umaarufu. Natafuta haki na amani ya kweli kwa nchi yetu.

Sijaona jambo unalozungumza hapa lenye mantiki ambalo ni balanced.

Kuhusu waislamu kuzuiwa kusoma wakati milango ya shule ilikuwa imefunguliwa kwa watoto wote sioni ukweli wowote. Nimesoma katika shule hizo hizo kuanzia mwaka 1966 hadi chuo kikuu mwaka 1984; madarasa yote niliyopitia nilikuwa na marafiki wa dini zote. Tulikuwa na vipindi vya dini ambavyo vilikuwa vinafundishwa na waalimu wa dini wanaotumwa na misikiti au makanisa. Unaweza kuwa na takwimu ambazo ni sahihi lakini unazitafsiri vibaya, watoto waliokuwa hawawendelei na shule baada ya darasa la saba ilikuwa ni kwa sababu ya kutokufanya vizuri kwani wakati huo shule za sekondari zilikuwa chache kwa hiyo ni wale tu waliokuwa wakifanya vizuri ndio waliokuwa wakiendelea. Ilikuwa ni kawaida sana shule moja kutoa mwanafunzi mmja wawili au hakuna kabisa wa kwenda sekondari. Haingewezekana mwanafunzi aliyekuwa wa kwanza shuleni kwenye mitihani yote hata ile ya Mock eti akanyimwa nafasi ya kwenda sekondari kwa sababu ya dini yake. After-all mitihani yote ilikuwa inatumia namba ambazo zinaficha identity ya mwanafunzi wakati wa kusahihisha.
 
In 1987 Prof. Malima became the first Muslim Minister of Education. By MS

Wakati Prof anakuwa Waziri wa Elimu, kwenye mitihani ZILITUMIKA NAMBA NA SI MAJINA kama ndg yetu MS/Prof. alivodai unavyodai....................HUU NI UONGO........tena wa mchana KWEUPE


Hili swala la namba kuna watu wamekuwa wanalikuza sana wakati mimi nilianza kutumia namba hizo kwenye mtihani wa darasa la nne miaka ya sitini, wakati Malima mwenyewe bado anasoma. Namba zangu za darasa la saba, form 4 na Form 6 ziko kwenye vyeti vyangu na nimemaliza form 6 kabla Malima hajawa Waziri wa elimu; lakini mtu huyu ndiye aliyeplant hii chuki kuwa Waislamu walikuwa wanayimwa nafasi za kusoma wakati yeye mwenyewe alisomeshwa kwa skolaship aliyotafutiwa na Nyerere wakati akiwa katibu mtendaji wa TANU wa wilaya.
 
Mimi niliwaomba hao ndugu zetu wanaolalamika kuwa wakristu wanapendelewa watutajia shule angalau moja ambayo waislamu walikuwa wakifanya vizuri kuliko wakristu darasani lakini kila mara ni wakristu peke yao waliokuwa wakichaguliwa! Hauwezi mtu ukachakua statistics za mwaka mmoja halafu ukadai ndio ushahidi wa institutional bias. Watuambie kama toka wakati Profesa Malima alikuwa waziri wa elimu na namba zikazaanza kutumika kama wanavyodai, je pamekuwa na uwiano katika matokeo ya mtihani ya darasa la saba? Hali ikoje katika mitihani ya sekondari n.k.?

Amandla.......
 
In 1987 Prof. Malima became the first Muslim Minister of Education. By MS

Wakati Prof anakuwa Waziri wa Elimu, kwenye mitihani ZILITUMIKA NAMBA NA SI MAJINA kama ndg yetu MS/Prof. alivodai unavyodai....................HUU NI UONGO........tena wa mchana KWEUPE





Heshima kwako Ogah,

Nadhani ungetuambia ukweli baada ya kujua MS kutudanganya.Jamvi linanoga sana unapogundua mwenzako kakosea unatakiwa kusahihisha kwa kuweka ushahidi usiokuwa na shaka.Tafadhali mwenye kujua namba za mitihani zilianza kutumika lini badala ya majina atusaidie.Vile vile naomba kujua baraza la mawaziri tangu tupate uhuru wizara ya elimu iliongozwa na mawaziri wangapi na majina nikielezwa kwa ufasaha hoja ya MS itakuwa imepata majibu ya uhakika badala ya kumwita mwongo bila ushahidi wowote.

Mkuu naomba kujua ukweli mchana kweupe.
 
Hili swala la namba kuna watu wamekuwa wanalikuza sana wakati mimi nilianza kutumia namba hizo kwenye mtihani wa darasa la nne miaka ya sitini, wakati Malima mwenyewe bado anasoma. Namba zangu za darasa la saba, form 4 na Form 6 ziko kwenye vyeti vyangu na nimemaliza form 6 kabla Malima hajawa Waziri wa elimu; lakini mtu huyu ndiye aliyeplant hii chuki kuwa Waislamu walikuwa wanayimwa nafasi za kusoma wakati yeye mwenyewe alisomeshwa kwa skolaship aliyotafutiwa na Nyerere wakati akiwa katibu mtendaji wa TANU wa wilaya.

Heshima kwako Kichuguu,

Umenisaidia kujua namba hazikuanza wakati Marehemu Kighoma Malima.Binafsi nilifanya mtihani yangu yote kwa namba kuanzia darasa la saba mwaka 1985 hadi kidato cha sita sikuwahi kutumia jina langu hata siku moja.Kighoma Malima kwa mujibu wa MS alishika madaraka ya wizara ya elimu mwaka 1987 ???????????.

Mkuu MS kama kitabu chako unachosisitiza tukinunue utakuwa umefanya makosa makubwa kiasi hiki itakuwa si vibaya ukakiondoa sokoni kwaajili ya masahihisho yaliyo wazi au toleo lijalo ikiwezekana.
 
no, namba za mtihani zimeanza baada ya malima kuingia wizarani. kabala ya hapo tukitumia majina . kama huamini nenda ukaanglie record ktk baraza la mitihani
naomba hili jambo liwekwe sawa,hii ni serious case of omission,kama itabainika kwamba for the sake of proving a non existent point,we are being fed lies
 
no, namba za mtihani zimeanza baada ya malima kuingia wizarani. kabala ya hapo tukitumia majina . kama huamini nenda ukaanglie record ktk baraza la mitihani
Mkuu you were misled, na wewe ukaamini mambo yasiyokuwepo.
Sisi tuloanza kusoma mara tu baada ya uhuru, na system ya mitihani ya nchi hii inafuata system ya mitihani ya cambridge.Mtahiniwa ni lazima atumie namba ya mtihani na si jina lake.
Hawa Islamic zealots watawalisha pumba nyingi sana, sasa ni juu yako kupembua pumba na mchele.
Ikiwa kama wewe ulitumia jina kwenye mitihani ya kiserikali basi nina wasi wasi na standards za hiyo shule.
 
no, namba za mtihani zimeanza baada ya malima kuingia wizarani. kabala ya hapo tukitumia majina . kama huamini nenda ukaanglie record ktk baraza la mitihani

......unajua dini zinatufundisha kutokuwa Wanafiki.................sasa huu ni UNAFIKI WA MCHANA KWEUPE...............ukitaka kujua specifics.....zinaanzia kwangu mwenyewe.............na siwezi kuwa mnafik kwa imani yangu bila sababu yeyote ya msingii.............
 
sasa si nakwambia uende ukaulize, halafu utuletee data? nani alietumia no kabla ya malima?

Sehemu ya Mtihani ni pamoja na kufuata Instructions.................kama wewe uliambiwa andika namba ukaandika jina.......pole sana.........

Inaonekana ulianza kufanya mithani ya Taifa baada ya Kighoma Malima kuwa waziri wa Elimu 1987.............na wakti huo unamsikiliza kwenye mhadhara.............na umri wako............

Anyway Fundi kauliza swali................

Mimi niliwaomba hao ndugu zetu wanaolalamika kuwa wakristu wanapendelewa watutajia shule angalau moja ambayo waislamu walikuwa wakifanya vizuri kuliko wakristu darasani lakini kila mara ni wakristu peke yao waliokuwa wakichaguliwa!.............
Amandla.......
 
FM: Uzuri wa mjadala kama huu ni kuweka ukweli wazi kwa manufaa ya baadae hapahitajiki mtu kupewa mlima kubeba. Wanaohusika wakisoma watajua ala kumbe sasa mambo yanajulikana! Na wale wasiojua watakuwa weshajua kuwa lipo tatizo mahali. Waungwana hawafanyiani mchezo "wa hide and seek" katika mambo mazito ya nchi. Ila muhimiu ni kuwa walipokwenda kumjadili Prof. Malima dhulma dhidi ya Waislam katika Wizara ya Elimu haikujadiliwa kwa "maslahi makubwa na endelevu ya taifa." Hamza Njozi alivyodokeza mchezo unavyochezwa kitabu "Mwembechai Killings" kikapigwa marufuku. Mzee Kitwana Kondo na yeye alipolileta tatizo hilo la ubaguzi katika elimu dhidi ya Waislam ikahakikishwa kuwa bunge lifuatalo anaangushwa. Huu ndiyo mchezo wenyewe. Kwa sasa tuna fursa ya kufanya maskhara na kutaka ushahidi na data etc. etc. Mungu apishie mbali lakini iko siku tutasema, "Ilikuwaje sisi hatukuiona hatari hii hadi gharika hii imetukumba?" Lakini kwa wakati huo itakuwa majuto mjukuu.
 
Prof. Malima kayasema yote hayo hadharani lakini magazeti binafsi na ya chama na serikali hayakuwa wanayachapa kwa sababu zilizo wazi. Ala kuli hali Wizara ya Elimu ilizisikia shutuma hizo na imekaa kimya hadi leo. Lakini kwetu Waislam hayo si muhimu. Muhimu kwetu Waislam wajue tu kuwa ipo dhulma hiyo inatosha sana. Kama kuna mtu anaona kubeza ndiyo njia nzuri na ya kiungwana katika hali kama hii ahlan wahsaalan na aendelee kubeza.
 
Wanaukumbi niliahidi kukiweka hapa ukumbini kisa cha AMNUT. Hayo yaliyopo hapo chini ni baada ya TANU kurejea kutoka Mkutano wa Tabora wa mwaka 1958 ambao uliamua TANU iingie katika Uchaguzi wa Kura Tatu. Huu ulikuwa uchaguzi wa kwanza katika Tanganyika. Someni kwa furaha:


Baada ya kurejea kutoka Tabora, Sheikh Suleiman Takadir, Bibi Titi Mohamed, Elias Kassenge na Bhoke Munanka walifuatana na Nyerere kwenye ziara ya Jimbo la Mashariki kuwaeleza watu umuhimu na maana halisi ya uchaguzi uliokuwa mbele yao. Nyerere aliwafafanulia watu kile ambacho Waafrika wangepoteza endapo TANU ingesusia uchaguzi. Lakini Sheikh Takadir alikuwa akishiriki katika mikutano ile kimwili tu; moyo na fikra zake havikuwa pale. Alikuwa na wasiwasi jinsi matukio yalivyokuwa yakitokea katika TANU na namna siasa ilivyokuwa ikichukua mwelekeo mpya. Sheikh Takadir alikuwa anautazama kwa hofu uongozi wa Wakristo katika TANU ambao ulikuwa ukielekea kuchukua uongozi baada kuingia katika Baraza la Kutunga Sheria. Kwa sababu ya yale masharti magumu ya uchaguzi, TANU ilibidi itazame nje ya uongozi wake ili kupata wagombea uchaguzi wenye sifa zilizohitajika kugombea uchaguzi dhidi ya UTP. TANU iliwachagua Julius Nyerere, Chief Abdallah Said Fundikira, John Ketto, Nesmo Eliufoo, John Mwakangale, Lawi Sijaona, Paul Bomani na George Kahama kusimama kama wagombea wa TANU. Baadhi ya hawa walikuwa watu ambao hawakuinukia katika TANU au harakati za siasa. Sheikh Takadir alihofu kuwa hawa Wakristo walioelimishwa na wamisionari na ukuzingatia kuwa walikuwa watu wapya katika harakati, mara watakaposhika madaraka watafanya juhudi kudumisha hali ile ile ya ukoloni, wakiwa hawana dhima ya kuongoza harakati kufikia lengo lake lake lililokusudiwa. Sheikh Takadir alikuwa kiongozi wa kwanza katika TANU kuwatanabaisha Waislam kuhusu hatari hii mpya iliyokuwa ikiwabili.

Sheikh Haidar Mwinyimvua, mjumbe wa Baraza la Wazee wa TANU na mjumbe wa Kamati Kuu ya TANU katika mwaka 1958na aliyekuwa rafiki mkubwa wa Sheikh Suleiman Takadir, anakumbuka jinsi Sheikh Takadir ghafla alipotoa dukuduku lake kwa Nyerere, dukuduku ambalo lilionekana lilikuwa halina sababu:

"Ilikuwa katika ofisi ya zamani ya TANU tukisubiri kufanya mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa. Ghafla tu Sheikh Takadir alisimama wima akishikilia fimbo yake ya kutembea akimuelekezea Nyerere huku akisema, ”Huyu mtu katu hatakuja kutujali sisi atakuja kuwajali ndugu zake. Usipoziba ufa utajenga ukuta.” Sheikh Takadir alirudia maneno haya mara mbili. Sisi sote katika kile chumba cha mkutano tulipigwa na butwaa kutokana na maneno yale. Nilimwona Nyerere akilia. Nyerere alitugeukia sisi na kutuuliza, ”Je, Sheikh Suleiman amesema maneno yale kwa niaba yenu?” Tulijibu kwa pamoja kuwa hatukuwa na habari kuhusu shauri lile; na mkutano ukavunjika hapo hapo."

Sheikh Takadir alikuwa miongoni mwa watu wa mwanzo kabisa kumuunga mkono Nyerere na alikuwa ameifanyia kampeni TANU kwa bidii kubwa, akihutubia mikutano jukwaa moja na Nyerere. Halikadhalika alikuwa amesaidia kufutilia mbali Ukristo wa Nyerere kwa watu wa Dar es Salaam kiasi kwamba watu mjini Dar es Salaam hawakumnasibisha Nyerere na Kanisa Katoliki ila na TANU kama chama cha wananchi. Wadhifa wa Sheikh Takadir mwenyewe kama mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU ulikuwa wa heshima kubwa. Haikuwa kwamba wale wote waliokuwemo ndani ya chumba kile hawakuelewa kile alichodokeza Sheikh Takadir. Walielewa kila neno alilotamka na maana yake halisi hasa kwa uongozi wa TANU. Kile ambacho hawakufahamu, kutambua au kusadiki kilikuwa ule ukweli kuwa Nyerere, mtoto wao mpendwa na kiongozi wao, iko siku moja atawageuka Waislam na kuwatazama kama adui zake na mahasimu kwa imani yake ya Kikristo. Lakini kwa wakati ule hili lilikuwa wazo lililokuwa mbali sana na lisilokuwa na maana yeyote kwao. TANU na chama kilichotangulia, African Association, hazikuundwa kwa ajili ya masilahi ya kikundi fulani pamoja na ukweli kuwa Waislam ndiyo waliounda vyama hivyo viwili na kuviongoza. Sheikh Takadir alikuwa ametonesha jambo nyeti sana. Njia pekee ya kuzuia mgogoro huu mpya usikue ilikuwa kwa Nyerere kuthibitisha kuwa Waislam watatendewa haki baada ya uhuru kupatikana. Kwa wakati ule, umoja wa wananachi ulikuwa muhimu kwa ajili ya harakati. Umoja wa Watanganyika ukawa ndiyo hoja kuu ya Nyerere katika hotuba zake zote kuanzia mkasa wa Takadir utokee na alishikilia hoja ya umoja katika kila hotuba yake hadi kufikia uchaguzi wa kura tatu.

Halmashauri Kuu ya Taifa ya TANU iliamua kuunda kamati ya haraka haraka kwenda nyumbani kwa Sheikh Takadir Mtaa wa Msimbazi kumuuliza kwa nini alimshutumu Nyerere. Miongoni mwa wajumbe wa kamati hiyo walikuwa Idd Faiz, Mwenyekiti wa Halmashauri ya TANU, Idd Tulio na Jumbe Tambaza. Sheikh Takadir aliiambia kamati hiyo kuwa Nyerere alikuwa akitumia sharti la elimu katika uchaguzi wa kura tatu ili kuwaweka Wakristo wenzake madarakani kwa hoja kwamba wanazo zile sifa zitakiwazo kushika majukumu ya serikali. Kisha Sheikh Takadir akarudia tena maneno yale yale aliyomwelezea Nyerere, neno kwa neno, akiongeza kwamba hana majuto yoyote kwa msimamo wake huo. Wajumbe wa kamati hiyo wakiongozwa na Idd Tulio walisimama na kuondoka kimya kimya. Matokeo yake ikawa Sheikh Takadir kufukuzwa kutoka TANU kwa kuanzisha suala la udini, ambalo lilidhaniwa lingewagawa wananchi. Idd Tulio akachaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU kushika nafasi ya Sheikh Takadir.

Kuingizwa kwa watu kama Eliofoo, Mwakangale, Sijaona, Bomani, Kahama na wengine katika Baraza la Kutunga Sheria ili kuwakilisha TANU kuliwatia wasiwasi idadi kubwa ya wanachama Waislam waliokuwepo makao makuu ya TANU. Lakini kwa hakika viongozi hawa walikuwa wazalendo wakiwakilisha sehemu muhimu nchini Tanganyika ambazo kwa mfano wale kutoka vyama vya ushirika kama Bomani kutoka Jimbo la Ziwa, walijitoa mhanga sana katika harakati. Hakuna namna ambayo Nyerere angeweza kuwakwepa kwa hofu ya kuujaza uongozi katika TANU na Baraza la Kutunga Sheria na Wakristo. Kwa upande mwingnine halikadhalika haikufikiriwa kuwa ni lazima kuwa na uwakilishi ulio sawasawa baina ya Waislam na Wakristo katika TANU au katika Baraza la Kutunga Sheria. Wakati ule tatizo la udini lilikuwa halijulikani kabisa.

Ghafla Sheikh Takadir akageuka kuwa kama mkoma. Watu wa Dar es Salaam wakampiga pande. Sheikh Takadir alikuwa dalali na alikuwa akifanya shughuli zake nyumbani kwake. Siku za nyuma mnadani kwake kulikuwa ndiyo baraza la mazungumzo la wana-TANU. Katika siku za mwanzo za TANU Sheikh Takadir alikuwa akiendesha biashara hiyo nyumba iliyokuwa Mtaa wa Nyamwezi mali ya Mwinjuma Digosi, jumbe wa serikali ya kikoloni. Mwinjuma Digosi alipotambua kuwa Nyerere alikuwa akifika pale kumfuata Sheikh Takadir, Digosi akamueleza Sheikh Takadir kuwa itabidi ahame kwa kuwa yeye ni jumbe wa serikali hawezi kuwa na mpangaji ambae anaigeuza nyumba yake mahali pa kukutana na watu wakorofi kama Nyerere.

Wanachama wa TANU walikuwa wakikutana kwa Sheikh Takadir kunywa kahawa, kupoteza wakati na kujadili siasa. Baada ya yeye kufukuzwa kutoka TANU mahali hapo palihamwa na hakuna aliyekwenda pale kama ilivyokuwa mazoea hapo siku za nyuma. Sheikh Takadir alipokwenda sokoni Kariakoo kununua mahitaji yake hakuna mfanyabiashara aliyegusa fedha zake au hata kule kumtizama tu. Alipotoa salam hakuna aliyemwitikia. Sheikh Takadir alisuswa na jamii yake na TANU. Sheikh Takadir aliuhisi hasa uzito kamili wa kupigwa pande na jamii. Biashara yake ikaanza kuanguka na vivyo hivyo afya yake ikaanza kuathirika. Akawa mpweke sana na mtu mwenye fadhaha. Enzi zile alipokuwa akisoma surat fatíha na kusoma dua kabla ya kumtambulisha Nyerere kwa watu wa Dar es Salaam katika mikutano ya awali ya TANU katika viwanja vya Mnazi Mmoja zilikuwa zimepita. Yalikuwa ya kale wakati Sheikh Takadir akijenga vyema taswira ya Nyerere akimkweza hadi kufikia kiwango cha kumnasibisha na mtume. Haukupita muda mrefu Sheikh Takadir alifariki. Lakini kabla ya kufariki Sheikh Takadir aliwaachia usia.

Kikundi cha Waislam walikuwa wamekwenda nyumbani kwake kumdhihaki, wakimtukana na kumkebehi, wakipiga makele huku wakiimba kwa sauti kubwa mwimbo, ëTakadir mtaka dini!í Kikundi hiki kilivamia nyumba yake baada ya kutoka mkutanoni ambako Nyerere alitoa hotuba ya kumshambulia Sheikh Takadir. Sheikh Takadir, inasemekana, alitoka nje ya nyumba yake kuwakabili wale Waislam na akawaambia, ”Iko siku mtanikumbuka.”

"Mwafrika" gazeti la kila wiki chini ya uhariri wa Heri Rashid Baghdelleh na Robert Makange, lilichapisha habari za Sheikh Suleiman Takadir katika ukurasa wa kwanza, likitangaza kufukuzwa kwake kutoka TANU kwa wino mzito, picha yake akiwa amevaa kanzu na kofia ya mkono akikodoa macho ikachapishwa gazetini. Picha ya Sheikh Takadir iliwekwa pale ili wote wauone uso wa ”msaliti” anaetaka kuchelewesha uhuru kwa kutaka Waislam wapewe uthibitisho wa hali yao ya baadae kwa sababu ya mchango wao katika harakati za kudai uhuru. Mtu mmoja tu ndiyo aliyejitokeza kumuunga mkono Sheikh Takadir na huyo alikuwa Ramadhan Mashado Plantan. Akiandika katika gazeti lake la Zuhra alihoji ile harara ya Nyerere kuwatumbukiza wananchi ndani ya uchaguzi wa kura tatu ingawa ilikuwa wazi kuwa yale masharti ya kupiga kura yalikuwa ya kuchukiza na ile haraka ambayo kwayo Sheikh Takadir alifukuzwa kutoka TANU.

Wakati wa mkasa wa Sheikh Takadir, "Mwafrika" lilikuwa likifaidi mauzo makubwa kwa sababu TANU ilisusia gazeti la Baraza gazeti la kila wiki la serikali. Baghdelleh na Makange walikuwa wamechapisha makala moja ambayo serikali iliiona ni ya uchochezi. Baghdelleh na Makange walipatikana na hatia na kufungwa miezi sita gerezani. TANU ililipa kisasi kwa kuwataka wananchi wasusie gazeti la Baraza. Hakuna Mwafrika aliyenunua gazeti hilo na kwa ajili hii yake mauzo ya "Mwafrika" yalipanda sana, hivyo kuipa sakata ya Sheikh Takadir nafasi kubwa gazetini. Baraza ilikuwa katika ukingo wa kufa kabisa kama isingelikuwa juhudi na mbinu za kidiplomasia za meneja wake, Page Jones na Meneja wa Tanganyika Standard, Nihill waliokwenda makao makuu ya TANU kusuluhisha baina ya gazeti hilo la serikali na TANU. Nihill alifanya mazungumzo na makamu wa rais wa TANU, John Rupia; kaimu katibu mwenezi, Amos Kissenge; katibu wa TANU Youth League, Dr. Michael Lugazia; Dossa Aziz na Mwenyekiti wa Halmashauri Kuu ya TANU Idd Faiz. Hawa viongozi waandamizi wa TANU walitoa amri ya kusitisha ususiaji wa gazeti la Baraza. Kwa kitendo hiki TANU ilikuwa imeojieleza vyema na ilikuwa imeonyesha nguvu zake.

Katika kipindi hiki mashambulizi kwa wale Waislam walionekana wanaipinga TANU na Nyerere yalizidishwa. Sheikh Hussein Juma makamu wa rais wa UTP alikuwa na pacha mwenzake, Sheikh Hassan Juma. Sheikh Hassan Juma alikuwa akiendesha madrasa pamoja na shule ikiitwa Al Hassanein Muslim School, moja ya majaribio ingawa hafifu ya Waislam kujiendeleza katika elimu. Shule nyingi zilikuwa mikononi mwa wamisionari. Watoto wengi waliozaliwa mjini Dar es Salaam baada ya vita ya pili walisomeshwa Qurían katika Al Hassanein chini ya Sheikh Hassan Juma. Wazazi waliwatoa watoto wao katika shule hii kwa sababu waliihusisha madrasa hii na upinzani dhidi ya TANU. Watoto hawa hawakuishia katika kuacha kuhudhuria madrasa bali walitunga nyimbo za kebehi ambazo waliziimba kwa sauti kubwa walipokuwa wakipita katika shule yao ya zamani ili kuwakebehi, Sheikh Hussein Juma na nduguye pacha Sheikh Hassan. Wazee wao hawakuona haja ya kuwakataza watoto wao tabia hii isiyofaa. Kwa kawaida ilionekana kwamba yeyote aliyekuwa anaipinga au hakujinasibisha na TANU, alikuwa adui.

Huu ndiyo ukuwa mwanzo wa upinzani wa chini chini dhidi ya TANU. Mwaka 1959, Ramadhani Mashado Plantan, mhariri hodari wa gazeti la Zuhra wakati mmoja gazeti hili likiwa ndiyo sauti ya TANU na wananchi wa Tanganyika, pamoja na kikundi kidogo cha Waislam akiwemo Saleh Muhsin walijiuzulu kutoka TANU na kuunda chama chao cha upinzani, All Muslim National Union of Tanganyika (AMNUT). Wanachama wengine waasisi walikuwa Abdallah Mohammed ambaye alichaguliwa kuwa rais na Plantan akiwa katibu. Plantan alijitolea chumba kimoja nyumbani kwake Kirk Street, Gerezani kama ofisi ya kwanza ya AMNUT. Mara tu baada ya kuundwa kwa AMNUT, ulizuka mgogoro katika uongozi na ofisi hiyo ilibidi ihamishwe kutoka nyumbani kwa Plantan hadi Libya Street, eneo lenye Wahindi wengi katikati ya mji. Uongozi mpya ulikuja madarakani na katibu mpya Abduwahid Abdulkarim. Abduwahid Abdulkarim, kijana mwenye umri wa miaka 25 alichaguliwa kuchukua nafasi ya Plantan. Abdallah Mohamed alibakia na cheo chake kama rais. AMNUT haikuweza kumudu kodi ya nyumba katika eneo lile la matajiri wa Kihindi. AMNUT ikaihamisha ofisi yake na kwenda Kariakoo, Narungíombe Street, karibu na msikiti wa Sheikh Idris bin Saad.

Lengo kuu la AMNUT lilikuwa ni kulinda haki na maslahi ya Waislam ambayo ilikuwa ikihisi yalikuwa hatarini katika serikali iliyoshikiliwa na Wakristo. Abdulkarim alikwenda Tabora kujaribu kutafuta kuungwa mkono AMNUT lakini matokeo yalikuwa ya kukatisha tamaa. Abdulkarim alichagua Tabora kwa sababu ilikuwa mahali penye athari kubwa ya Uislamu. Hata hivyo Abdulkarim alifanikiwa kupokea mwaliko kutoka kwa Ali Muhsin Al Barwani kiongozi wa Zanzibar Nationality Party (ZNP) ahudhurie mkutano wa kamati kuu na awakilishe suala la AMNUT. Mkutano huu ulifanyika katika ofisi ya ZNP Darajani huko Zanzibar. Ali Muhsin alimwambia Abdulkarim kwamba ZNP haiwezi kujifungamanisha na tatizo la Uislam kwa sababu ZNP haikuwa inaamini kama Ukristo una uwezo wa kuhatarisha Uislam hasa ukichukulia kuwa Waislam ni wengi nchini Tanganyika. Waislam wa Tanganyika walikataa kuiunga mkono AMNUT wakihisi sera zake zilikuwa za kuwagawa watu kwa misingi ya dini. Kwa ajili hii basi AMNUT haikuwa na maslahi ya wananchi.

Lakini pigo kubwa kwa AMNUT lilikuja kutoka kwa masheikh wa Tanga. Masheikh na waalimu wa Qurían mjini Tanga walitia sahihi azimio la pamoja kuipinga AMNUT. Azimio hilo lilisema kuwa AMNUT ingezua janga. Masheikh walisisitiza kwamba wataiunga mkono TANU mpaka uhuru upatikane kwa sababu wana imani na malengo yake. AMNUT ikikabiliwa na mashambulio kama hayo kutoka tabaka ambayo ilidai inawakilisha maslahi yao, chama hicho hakikuweza kustawi. Haukupita muda mrefu AMNUT ikafa.

Mwaka 1960, Plantan sasa akiwa nje ya AMNUT na siasa, alitoa kauli moja iliyokuwa kama anatoa buriani kuteremsha pazia na kuaga jukwaa la siasa. Plantan aliwaambia Waislam kwamba hata kwa miaka mia moja hawataweza kuwafikia Wakristo. Baada ya kauli hiii hakuna kilichosikika kuhusu Ramadhani Mashado Plantan. Aliishi miaka ya mwisho ya maisha yake hapo Gerezani, akitumia wakati wake baina ya nyumba yake na msikiti wa jirani ambao alikuwa akiufagia kuuweka safi akisubiri mauti yaje akasimame mbele ya haki.

Nyerere alikubali ukweli kuwa kulikuwa na upogo baina ya Waislam na Wakristo hususan katika elimu ambayo itawazuia Waislam kushika nafasi za uongozi katika serikali ya wananchi. Nyerere aliwaomba Waislam waweke matumaini yao kwa TANU ambayo itaanzisha mabadiliko ya lazima kuwainua Waislam kwenye nafasi za usawa pamoja na Wakristo mara tu uhuru utakapopatikana. Lakini hili, Nyerere aliwakumbusha Waislam mara kwa mara kuwa linaweza kufanyika tu kwenye Tanganyika huru na siyo chini ya utawala wa Kiingereza. Waislam katika TANU, kwa upande wao, waliamini kwamba ilikuwa kinyume kwao kuanzisha chama cha kisiasa chini ya maslahi ya kikundi kimoja kama ndiyo lengo la kudai uhuru. Hili, wengi waliamini, lingesaidia kuunda vikundi vingi na kusababisha mfarakano. Kwa kweli madai yaliyokuwa yakitolewa na AMNUT hayakuwa madai ambayo yangetolewa kwa TANU katika wakati ule. Vita vya mwaka 1947 kati ya India na Pakistan vilivyosababisha kupoteza maisha ya watu wengi, vilikuwa bado vinakumbukwa na watu wengi. Chanzo cha ugomvi huo kilikuwa ushindani baina ya Waislam na Wahindu. Kabla ya mwaka 1947 India na Pakistan zilikuwa nchi moja chini ya ukoloni wa Mwingereza. Waislam na Wahindu walipigania uhuru pamoja na walifarakana mara tu ilipokuwa wazi kuwa Uingereza ingetoa uhuru kwa India. Watu wengi nchini Tanganyika walihofia kwamba kuruhusu fikra kama zile zilizotolewa na Sheikh Takadir kuota mizizi kulikuwa kukaribisha ile hali ya India na Pakistan Tanganyika. Nyerere alionya kuwa hakutaka hali kama ile ije kuisibu Tanganyika.

***

Wanaukumbi hii ndiyo historia ya wazee wangu na kama nilivyosema hapo awali mimi simsubiri Nimtz atoke Canada aje kuniandikia historia ya wazee wangu. Mimi nimeipokea hiyo kutoka katika ndimi zao wenyewe waliolipindua gurudumu la historia. Sheikh Haidar Mwinyimvua nikimfahamu hadi anafariki. Heri Baghadeleh alikuwa rafiki ya baba yangu na katika vitu vilivyokuwa vigumu kwake ni pale mwaka 1964 babu yangu alipowekwa kizuizini jela ya Uyui Tabora kwa shutuma za kutaka kuipindua serikali ya Nyerere. Bwana Jela alikuwa Mzee Munthali baba yake Kwege Muthali aliyekuwa mtangazaji wa TBC akafa katika ajali ya treni ilipogongana na gari yao ndogo pale Shaurimoyo. Baghdelleh alikuwa Regional Commissioner akienda pale jela kuwaona waliokuwa kizuizini na Mzee Munthali kama Bwana Jela alikuwa akimsindikiza. Anasema Baghdelleh akipata tabu sana kuutazama uso wa babu yangu kwa aibu. Baghdelleh alikuwa akijua kuwa hapakuwa na njama yoyote ya kumpindua Nyerere ila ni uongo mtupu. Hata hivyo akimtia moyo baba yangu kwa kumwambia, "Mzee ataachiwa hivi karibuni ondoa wasiwasi." Kadi yake ya TANU baba yangu kainunua kwa Abdulwahid Sykes tena kwa siri maana yeye alikuwa mfanyakazi wa serikali. Anaogopa akijulikana atafukuzwa kazi. Akikutana na Abdulwahid wote vinywa vinawajaa mate hawana la kusema. Nyerere amekuwa mkubwa sana hawamuwezi kamwe si yule ambae Abdulwahid alimjulisha baba yangu pale Mtaa wa Aggrey/Sikukuu nyumbani kwa Abdu mwaka 1952 siku ile usiku.

Mimi hupenda kuwakumbuka wazee wangu kwa namna hii. Kwa kuhadithia habari zao na ninamshukuru Mungu kwa kunipa historia. Wengi wetu hatukubahatika hivi. Historia hii kwangu mimi ni amana. Kitu nilichowekeshwa. Mwenyewe akijakitaka basi sina budi kumpa.
 
Mimi niliwaomba hao ndugu zetu wanaolalamika kuwa wakristu wanapendelewa watutajia shule angalau moja ambayo waislamu walikuwa wakifanya vizuri kuliko wakristu darasani lakini kila mara ni wakristu peke yao waliokuwa wakichaguliwa! Hauwezi mtu ukachakua statistics za mwaka mmoja halafu ukadai ndio ushahidi wa institutional bias. Watuambie kama toka wakati Profesa Malima alikuwa waziri wa elimu na namba zikazaanza kutumika kama wanavyodai, je pamekuwa na uwiano katika matokeo ya mtihani ya darasa la saba? Hali ikoje katika mitihani ya sekondari n.k.?

Amandla.......
Hii dhulma katika elimu imeanza zamani na mashahidi ni wengi kila mmoja na mwaka wake.Hatimae idadi ya miaka inakuwa mingi kama upendavyo wewe ili dhulma iitwe dhulma.
Nyerere alipojidai kutaifisha mashule,alifanya hivyo kwa kujitoa kimasomaso tu akijua kuwa hizo shule za kanisa wala si za kanisa kweli bali kuna haki nyingi za waislamu.Hata hivyo ilikuwa mbinu yake tu ya kujificha.Angekuwa mkweli basi baada ya uhuru angezigawa kwa waislamu waziendeshe wenyewe.Kwani kwa kuzitaifisha alikuwa tayari ametayarisha mtandao mwengine wa kuendeleza dhulma kwa waislamu.
Angalia hapo:
Roland (1970), The Missionery Factor in East Africa.
Shule za Wakristo zilijengwa na kuendeshwa kwa kodi za Watanganyika. Angalia kitabu cha akina Dodd ukurasa wa 76. Pia rejea ukurasa wa 114 ambapo wanasema, "... there can be no denying that, educational system, even under government had a great Christian bias...". Tafsiri. "Hakuna upinzani kuwa mfumo wa elimu hata pale serikali iliposimamia ulikuwa unawapendelea Wakristo....". Pia ukurasa wa 25 wanasema: "The British government having taken all the burden both recurrent and capital for the mission schools ...". Tafsiri. "Baada ya serikali kikoloni ya Uingereza kuchukua mzigo wote wa kugharimia shule za Kikristo katika matumizi ya kawaida na ya maendeleo...". Katika ukurasa wa 76 Bwana Dodd anasema. "In 1957, Muslim Association Agencies received only Pound 6,848, out of total government expenditure in education in grant - in - aid of pound 1,338,925 ...Christian missions ... greately expanded their education services by the means of grant-in-aid received from the government". Tafsiri. "Katika mwaka 1957 mawakala wa Jumuia za Kiislamu walipokea paundi 6,848 kati ya paundi 1,338,925 zilizotolewa na serikali kusaidia shule za mashirika ya dini ... hivyo Wakristo walitumia fedha hizo kupanua huduma zao za elimu.
Sababu ya wakoloni kufanya hivyo inaelezwa tena katikakitabu cha Roland ukurasa wa 205, utaona maneno yafuatayo:
"In British territories, strongly it was the governments rather than the missions which saw the dangers of the Islamic expansion and which took whatever steps they could to forestall it". Tafsiri; "Katika makoloni ya Waingereza ndio walioona hatari ya kupanuka Uislamu (kuliko wamisheni) na walichukua kila hatua waliyoweza kuzuia hali hiyo".
 
Wanaukumbi niliahidi kukiweka hapa ukumbini kisa cha AMNUT. Hayo yaliyopo hapo chini ni baada ya TANU kurejea kutoka Mkutano wa Tabora wa mwaka 1958 ambao uliamua TANU iingie katika Uchaguzi wa Kura Tatu. Huu ulikuwa uchaguzi wa kwanza katika Tanganyika. Someni kwa furaha:


Baada ya kurejea kutoka Tabora, Sheikh Suleiman Takadir, Bibi Titi Mohamed, Elias Kassenge na Bhoke Munanka walifuatana na Nyerere kwenye ziara ya Jimbo la Mashariki kuwaeleza watu umuhimu na maana halisi ya uchaguzi uliokuwa mbele yao. Nyerere aliwafafanulia watu kile ambacho Waafrika wangepoteza endapo TANU ingesusia uchaguzi. Lakini Sheikh Takadir alikuwa akishiriki katika mikutano ile kimwili tu; moyo na fikra zake havikuwa pale. Alikuwa na wasiwasi jinsi matukio yalivyokuwa yakitokea katika TANU na namna siasa ilivyokuwa ikichukua mwelekeo mpya. Sheikh Takadir alikuwa anautazama kwa hofu uongozi wa Wakristo katika TANU ambao ulikuwa ukielekea kuchukua uongozi baada kuingia katika Baraza la Kutunga Sheria. Kwa sababu ya yale masharti magumu ya uchaguzi, TANU ilibidi itazame nje ya uongozi wake ili kupata wagombea uchaguzi wenye sifa zilizohitajika kugombea uchaguzi dhidi ya UTP. TANU iliwachagua Julius Nyerere, Chief Abdallah Said Fundikira, John Ketto, Nesmo Eliufoo, John Mwakangale, Lawi Sijaona, Paul Bomani na George Kahama kusimama kama wagombea wa TANU. Baadhi ya hawa walikuwa watu ambao hawakuinukia katika TANU au harakati za siasa. Sheikh Takadir alihofu kuwa hawa Wakristo walioelimishwa na wamisionari na ukuzingatia kuwa walikuwa watu wapya katika harakati, mara watakaposhika madaraka watafanya juhudi kudumisha hali ile ile ya ukoloni, wakiwa hawana dhima ya kuongoza harakati kufikia lengo lake lake lililokusudiwa. Sheikh Takadir alikuwa kiongozi wa kwanza katika TANU kuwatanabaisha Waislam kuhusu hatari hii mpya iliyokuwa ikiwabili.

Sheikh Haidar Mwinyimvua, mjumbe wa Baraza la Wazee wa TANU na mjumbe wa Kamati Kuu ya TANU katika mwaka 1958na aliyekuwa rafiki mkubwa wa Sheikh Suleiman Takadir, anakumbuka jinsi Sheikh Takadir ghafla alipotoa dukuduku lake kwa Nyerere, dukuduku ambalo lilionekana lilikuwa halina sababu:

"Ilikuwa katika ofisi ya zamani ya TANU tukisubiri kufanya mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa. Ghafla tu Sheikh Takadir alisimama wima akishikilia fimbo yake ya kutembea akimuelekezea Nyerere huku akisema, "Huyu mtu katu hatakuja kutujali sisi atakuja kuwajali ndugu zake. Usipoziba ufa utajenga ukuta." Sheikh Takadir alirudia maneno haya mara mbili. Sisi sote katika kile chumba cha mkutano tulipigwa na butwaa kutokana na maneno yale. Nilimwona Nyerere akilia. Nyerere alitugeukia sisi na kutuuliza, "Je, Sheikh Suleiman amesema maneno yale kwa niaba yenu?" Tulijibu kwa pamoja kuwa hatukuwa na habari kuhusu shauri lile; na mkutano ukavunjika hapo hapo."

Sheikh Takadir alikuwa miongoni mwa watu wa mwanzo kabisa kumuunga mkono Nyerere na alikuwa ameifanyia kampeni TANU kwa bidii kubwa, akihutubia mikutano jukwaa moja na Nyerere. Halikadhalika alikuwa amesaidia kufutilia mbali Ukristo wa Nyerere kwa watu wa Dar es Salaam kiasi kwamba watu mjini Dar es Salaam hawakumnasibisha Nyerere na Kanisa Katoliki ila na TANU kama chama cha wananchi. Wadhifa wa Sheikh Takadir mwenyewe kama mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU ulikuwa wa heshima kubwa. Haikuwa kwamba wale wote waliokuwemo ndani ya chumba kile hawakuelewa kile alichodokeza Sheikh Takadir. Walielewa kila neno alilotamka na maana yake halisi hasa kwa uongozi wa TANU. Kile ambacho hawakufahamu, kutambua au kusadiki kilikuwa ule ukweli kuwa Nyerere, mtoto wao mpendwa na kiongozi wao, iko siku moja atawageuka Waislam na kuwatazama kama adui zake na mahasimu kwa imani yake ya Kikristo. Lakini kwa wakati ule hili lilikuwa wazo lililokuwa mbali sana na lisilokuwa na maana yeyote kwao. TANU na chama kilichotangulia, African Association, hazikuundwa kwa ajili ya masilahi ya kikundi fulani pamoja na ukweli kuwa Waislam ndiyo waliounda vyama hivyo viwili na kuviongoza. Sheikh Takadir alikuwa ametonesha jambo nyeti sana. Njia pekee ya kuzuia mgogoro huu mpya usikue ilikuwa kwa Nyerere kuthibitisha kuwa Waislam watatendewa haki baada ya uhuru kupatikana. Kwa wakati ule, umoja wa wananachi ulikuwa muhimu kwa ajili ya harakati. Umoja wa Watanganyika ukawa ndiyo hoja kuu ya Nyerere katika hotuba zake zote kuanzia mkasa wa Takadir utokee na alishikilia hoja ya umoja katika kila hotuba yake hadi kufikia uchaguzi wa kura tatu.

Halmashauri Kuu ya Taifa ya TANU iliamua kuunda kamati ya haraka haraka kwenda nyumbani kwa Sheikh Takadir Mtaa wa Msimbazi kumuuliza kwa nini alimshutumu Nyerere. Miongoni mwa wajumbe wa kamati hiyo walikuwa Idd Faiz, Mwenyekiti wa Halmashauri ya TANU, Idd Tulio na Jumbe Tambaza. Sheikh Takadir aliiambia kamati hiyo kuwa Nyerere alikuwa akitumia sharti la elimu katika uchaguzi wa kura tatu ili kuwaweka Wakristo wenzake madarakani kwa hoja kwamba wanazo zile sifa zitakiwazo kushika majukumu ya serikali. Kisha Sheikh Takadir akarudia tena maneno yale yale aliyomwelezea Nyerere, neno kwa neno, akiongeza kwamba hana majuto yoyote kwa msimamo wake huo. Wajumbe wa kamati hiyo wakiongozwa na Idd Tulio walisimama na kuondoka kimya kimya. Matokeo yake ikawa Sheikh Takadir kufukuzwa kutoka TANU kwa kuanzisha suala la udini, ambalo lilidhaniwa lingewagawa wananchi. Idd Tulio akachaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU kushika nafasi ya Sheikh Takadir.

Kuingizwa kwa watu kama Eliofoo, Mwakangale, Sijaona, Bomani, Kahama na wengine katika Baraza la Kutunga Sheria ili kuwakilisha TANU kuliwatia wasiwasi idadi kubwa ya wanachama Waislam waliokuwepo makao makuu ya TANU. Lakini kwa hakika viongozi hawa walikuwa wazalendo wakiwakilisha sehemu muhimu nchini Tanganyika ambazo kwa mfano wale kutoka vyama vya ushirika kama Bomani kutoka Jimbo la Ziwa, walijitoa mhanga sana katika harakati. Hakuna namna ambayo Nyerere angeweza kuwakwepa kwa hofu ya kuujaza uongozi katika TANU na Baraza la Kutunga Sheria na Wakristo. Kwa upande mwingnine halikadhalika haikufikiriwa kuwa ni lazima kuwa na uwakilishi ulio sawasawa baina ya Waislam na Wakristo katika TANU au katika Baraza la Kutunga Sheria. Wakati ule tatizo la udini lilikuwa halijulikani kabisa.

Ghafla Sheikh Takadir akageuka kuwa kama mkoma. Watu wa Dar es Salaam wakampiga pande. Sheikh Takadir alikuwa dalali na alikuwa akifanya shughuli zake nyumbani kwake. Siku za nyuma mnadani kwake kulikuwa ndiyo baraza la mazungumzo la wana-TANU. Katika siku za mwanzo za TANU Sheikh Takadir alikuwa akiendesha biashara hiyo nyumba iliyokuwa Mtaa wa Nyamwezi mali ya Mwinjuma Digosi, jumbe wa serikali ya kikoloni. Mwinjuma Digosi alipotambua kuwa Nyerere alikuwa akifika pale kumfuata Sheikh Takadir, Digosi akamueleza Sheikh Takadir kuwa itabidi ahame kwa kuwa yeye ni jumbe wa serikali hawezi kuwa na mpangaji ambae anaigeuza nyumba yake mahali pa kukutana na watu wakorofi kama Nyerere.

Wanachama wa TANU walikuwa wakikutana kwa Sheikh Takadir kunywa kahawa, kupoteza wakati na kujadili siasa. Baada ya yeye kufukuzwa kutoka TANU mahali hapo palihamwa na hakuna aliyekwenda pale kama ilivyokuwa mazoea hapo siku za nyuma. Sheikh Takadir alipokwenda sokoni Kariakoo kununua mahitaji yake hakuna mfanyabiashara aliyegusa fedha zake au hata kule kumtizama tu. Alipotoa salam hakuna aliyemwitikia. Sheikh Takadir alisuswa na jamii yake na TANU. Sheikh Takadir aliuhisi hasa uzito kamili wa kupigwa pande na jamii. Biashara yake ikaanza kuanguka na vivyo hivyo afya yake ikaanza kuathirika. Akawa mpweke sana na mtu mwenye fadhaha. Enzi zile alipokuwa akisoma surat fatíha na kusoma dua kabla ya kumtambulisha Nyerere kwa watu wa Dar es Salaam katika mikutano ya awali ya TANU katika viwanja vya Mnazi Mmoja zilikuwa zimepita. Yalikuwa ya kale wakati Sheikh Takadir akijenga vyema taswira ya Nyerere akimkweza hadi kufikia kiwango cha kumnasibisha na mtume. Haukupita muda mrefu Sheikh Takadir alifariki. Lakini kabla ya kufariki Sheikh Takadir aliwaachia usia.

Kikundi cha Waislam walikuwa wamekwenda nyumbani kwake kumdhihaki, wakimtukana na kumkebehi, wakipiga makele huku wakiimba kwa sauti kubwa mwimbo, ëTakadir mtaka dini!í Kikundi hiki kilivamia nyumba yake baada ya kutoka mkutanoni ambako Nyerere alitoa hotuba ya kumshambulia Sheikh Takadir. Sheikh Takadir, inasemekana, alitoka nje ya nyumba yake kuwakabili wale Waislam na akawaambia, "Iko siku mtanikumbuka."

"Mwafrika" gazeti la kila wiki chini ya uhariri wa Heri Rashid Baghdelleh na Robert Makange, lilichapisha habari za Sheikh Suleiman Takadir katika ukurasa wa kwanza, likitangaza kufukuzwa kwake kutoka TANU kwa wino mzito, picha yake akiwa amevaa kanzu na kofia ya mkono akikodoa macho ikachapishwa gazetini. Picha ya Sheikh Takadir iliwekwa pale ili wote wauone uso wa "msaliti" anaetaka kuchelewesha uhuru kwa kutaka Waislam wapewe uthibitisho wa hali yao ya baadae kwa sababu ya mchango wao katika harakati za kudai uhuru. Mtu mmoja tu ndiyo aliyejitokeza kumuunga mkono Sheikh Takadir na huyo alikuwa Ramadhan Mashado Plantan. Akiandika katika gazeti lake la Zuhra alihoji ile harara ya Nyerere kuwatumbukiza wananchi ndani ya uchaguzi wa kura tatu ingawa ilikuwa wazi kuwa yale masharti ya kupiga kura yalikuwa ya kuchukiza na ile haraka ambayo kwayo Sheikh Takadir alifukuzwa kutoka TANU.

Wakati wa mkasa wa Sheikh Takadir, "Mwafrika" lilikuwa likifaidi mauzo makubwa kwa sababu TANU ilisusia gazeti la Baraza gazeti la kila wiki la serikali. Baghdelleh na Makange walikuwa wamechapisha makala moja ambayo serikali iliiona ni ya uchochezi. Baghdelleh na Makange walipatikana na hatia na kufungwa miezi sita gerezani. TANU ililipa kisasi kwa kuwataka wananchi wasusie gazeti la Baraza. Hakuna Mwafrika aliyenunua gazeti hilo na kwa ajili hii yake mauzo ya "Mwafrika" yalipanda sana, hivyo kuipa sakata ya Sheikh Takadir nafasi kubwa gazetini. Baraza ilikuwa katika ukingo wa kufa kabisa kama isingelikuwa juhudi na mbinu za kidiplomasia za meneja wake, Page Jones na Meneja wa Tanganyika Standard, Nihill waliokwenda makao makuu ya TANU kusuluhisha baina ya gazeti hilo la serikali na TANU. Nihill alifanya mazungumzo na makamu wa rais wa TANU, John Rupia; kaimu katibu mwenezi, Amos Kissenge; katibu wa TANU Youth League, Dr. Michael Lugazia; Dossa Aziz na Mwenyekiti wa Halmashauri Kuu ya TANU Idd Faiz. Hawa viongozi waandamizi wa TANU walitoa amri ya kusitisha ususiaji wa gazeti la Baraza. Kwa kitendo hiki TANU ilikuwa imeojieleza vyema na ilikuwa imeonyesha nguvu zake.

Katika kipindi hiki mashambulizi kwa wale Waislam walionekana wanaipinga TANU na Nyerere yalizidishwa. Sheikh Hussein Juma makamu wa rais wa UTP alikuwa na pacha mwenzake, Sheikh Hassan Juma. Sheikh Hassan Juma alikuwa akiendesha madrasa pamoja na shule ikiitwa Al Hassanein Muslim School, moja ya majaribio ingawa hafifu ya Waislam kujiendeleza katika elimu. Shule nyingi zilikuwa mikononi mwa wamisionari. Watoto wengi waliozaliwa mjini Dar es Salaam baada ya vita ya pili walisomeshwa Qurían katika Al Hassanein chini ya Sheikh Hassan Juma. Wazazi waliwatoa watoto wao katika shule hii kwa sababu waliihusisha madrasa hii na upinzani dhidi ya TANU. Watoto hawa hawakuishia katika kuacha kuhudhuria madrasa bali walitunga nyimbo za kebehi ambazo waliziimba kwa sauti kubwa walipokuwa wakipita katika shule yao ya zamani ili kuwakebehi, Sheikh Hussein Juma na nduguye pacha Sheikh Hassan. Wazee wao hawakuona haja ya kuwakataza watoto wao tabia hii isiyofaa. Kwa kawaida ilionekana kwamba yeyote aliyekuwa anaipinga au hakujinasibisha na TANU, alikuwa adui.

Huu ndiyo ukuwa mwanzo wa upinzani wa chini chini dhidi ya TANU. Mwaka 1959, Ramadhani Mashado Plantan, mhariri hodari wa gazeti la Zuhra wakati mmoja gazeti hili likiwa ndiyo sauti ya TANU na wananchi wa Tanganyika, pamoja na kikundi kidogo cha Waislam akiwemo Saleh Muhsin walijiuzulu kutoka TANU na kuunda chama chao cha upinzani, All Muslim National Union of Tanganyika (AMNUT). Wanachama wengine waasisi walikuwa Abdallah Mohammed ambaye alichaguliwa kuwa rais na Plantan akiwa katibu. Plantan alijitolea chumba kimoja nyumbani kwake Kirk Street, Gerezani kama ofisi ya kwanza ya AMNUT. Mara tu baada ya kuundwa kwa AMNUT, ulizuka mgogoro katika uongozi na ofisi hiyo ilibidi ihamishwe kutoka nyumbani kwa Plantan hadi Libya Street, eneo lenye Wahindi wengi katikati ya mji. Uongozi mpya ulikuja madarakani na katibu mpya Abduwahid Abdulkarim. Abduwahid Abdulkarim, kijana mwenye umri wa miaka 25 alichaguliwa kuchukua nafasi ya Plantan. Abdallah Mohamed alibakia na cheo chake kama rais. AMNUT haikuweza kumudu kodi ya nyumba katika eneo lile la matajiri wa Kihindi. AMNUT ikaihamisha ofisi yake na kwenda Kariakoo, Narungíombe Street, karibu na msikiti wa Sheikh Idris bin Saad.

Lengo kuu la AMNUT lilikuwa ni kulinda haki na maslahi ya Waislam ambayo ilikuwa ikihisi yalikuwa hatarini katika serikali iliyoshikiliwa na Wakristo. Abdulkarim alikwenda Tabora kujaribu kutafuta kuungwa mkono AMNUT lakini matokeo yalikuwa ya kukatisha tamaa. Abdulkarim alichagua Tabora kwa sababu ilikuwa mahali penye athari kubwa ya Uislamu. Hata hivyo Abdulkarim alifanikiwa kupokea mwaliko kutoka kwa Ali Muhsin Al Barwani kiongozi wa Zanzibar Nationality Party (ZNP) ahudhurie mkutano wa kamati kuu na awakilishe suala la AMNUT. Mkutano huu ulifanyika katika ofisi ya ZNP Darajani huko Zanzibar. Ali Muhsin alimwambia Abdulkarim kwamba ZNP haiwezi kujifungamanisha na tatizo la Uislam kwa sababu ZNP haikuwa inaamini kama Ukristo una uwezo wa kuhatarisha Uislam hasa ukichukulia kuwa Waislam ni wengi nchini Tanganyika. Waislam wa Tanganyika walikataa kuiunga mkono AMNUT wakihisi sera zake zilikuwa za kuwagawa watu kwa misingi ya dini. Kwa ajili hii basi AMNUT haikuwa na maslahi ya wananchi.

Lakini pigo kubwa kwa AMNUT lilikuja kutoka kwa masheikh wa Tanga. Masheikh na waalimu wa Qurían mjini Tanga walitia sahihi azimio la pamoja kuipinga AMNUT. Azimio hilo lilisema kuwa AMNUT ingezua janga. Masheikh walisisitiza kwamba wataiunga mkono TANU mpaka uhuru upatikane kwa sababu wana imani na malengo yake. AMNUT ikikabiliwa na mashambulio kama hayo kutoka tabaka ambayo ilidai inawakilisha maslahi yao, chama hicho hakikuweza kustawi. Haukupita muda mrefu AMNUT ikafa.

Mwaka 1960, Plantan sasa akiwa nje ya AMNUT na siasa, alitoa kauli moja iliyokuwa kama anatoa buriani kuteremsha pazia na kuaga jukwaa la siasa. Plantan aliwaambia Waislam kwamba hata kwa miaka mia moja hawataweza kuwafikia Wakristo. Baada ya kauli hiii hakuna kilichosikika kuhusu Ramadhani Mashado Plantan. Aliishi miaka ya mwisho ya maisha yake hapo Gerezani, akitumia wakati wake baina ya nyumba yake na msikiti wa jirani ambao alikuwa akiufagia kuuweka safi akisubiri mauti yaje akasimame mbele ya haki.

Nyerere alikubali ukweli kuwa kulikuwa na upogo baina ya Waislam na Wakristo hususan katika elimu ambayo itawazuia Waislam kushika nafasi za uongozi katika serikali ya wananchi. Nyerere aliwaomba Waislam waweke matumaini yao kwa TANU ambayo itaanzisha mabadiliko ya lazima kuwainua Waislam kwenye nafasi za usawa pamoja na Wakristo mara tu uhuru utakapopatikana. Lakini hili, Nyerere aliwakumbusha Waislam mara kwa mara kuwa linaweza kufanyika tu kwenye Tanganyika huru na siyo chini ya utawala wa Kiingereza. Waislam katika TANU, kwa upande wao, waliamini kwamba ilikuwa kinyume kwao kuanzisha chama cha kisiasa chini ya maslahi ya kikundi kimoja kama ndiyo lengo la kudai uhuru. Hili, wengi waliamini, lingesaidia kuunda vikundi vingi na kusababisha mfarakano. Kwa kweli madai yaliyokuwa yakitolewa na AMNUT hayakuwa madai ambayo yangetolewa kwa TANU katika wakati ule. Vita vya mwaka 1947 kati ya India na Pakistan vilivyosababisha kupoteza maisha ya watu wengi, vilikuwa bado vinakumbukwa na watu wengi. Chanzo cha ugomvi huo kilikuwa ushindani baina ya Waislam na Wahindu. Kabla ya mwaka 1947 India na Pakistan zilikuwa nchi moja chini ya ukoloni wa Mwingereza. Waislam na Wahindu walipigania uhuru pamoja na walifarakana mara tu ilipokuwa wazi kuwa Uingereza ingetoa uhuru kwa India. Watu wengi nchini Tanganyika walihofia kwamba kuruhusu fikra kama zile zilizotolewa na Sheikh Takadir kuota mizizi kulikuwa kukaribisha ile hali ya India na Pakistan Tanganyika. Nyerere alionya kuwa hakutaka hali kama ile ije kuisibu Tanganyika.

***

Wanaukumbi hii ndiyo historia ya wazee wangu na kama nilivyosema hapo awali mimi simsubiri Nimtz atoke Canada aje kuniandikia historia ya wazee wangu. Mimi nimeipokea hiyo kutoka katika ndimi zao wenyewe waliolipindua gurudumu la historia. Sheikh Haidar Mwinyimvua nikimfahamu hadi anafariki. Heri Baghadeleh alikuwa rafiki ya baba yangu na katika vitu vilivyokuwa vigumu kwake ni pale mwaka 1964 babu yangu alipowekwa kizuizini jela ya Uyui Tabora kwa shutuma za kutaka kuipindua serikali ya Nyerere. Bwana Jela alikuwa Mzee Munthali baba yake Kwege Muthali aliyekuwa mtangazaji wa TBC akafa katika ajali ya treni ilipogongana na gari yao ndogo pale Shaurimoyo. Baghdelleh alikuwa Regional Commissioner akienda pale jela kuwaona waliokuwa kizuizini na Mzee Munthali kama Bwana Jela alikuwa akimsindikiza. Anasema Baghdelleh akipata tabu sana kuutazama uso wa babu yangu kwa aibu. Baghdelleh alikuwa akijua kuwa hapakuwa na njama yoyote ya kumpindua Nyerere ila ni uongo mtupu. Hata hivyo akimtia moyo baba yangu kwa kumwambia, "Mzee ataachiwa hivi karibuni ondoa wasiwasi." Kadi yake ya TANU baba yangu kainunua kwa Abdulwahid Sykes tena kwa siri maana yeye alikuwa mfanyakazi wa serikali. Anaogopa akijulikana atafukuzwa kazi. Akikutana na Abdulwahid wote vinywa vinawajaa mate hawana la kusema. Nyerere amekuwa mkubwa sana hawamuwezi kamwe si yule ambae Abdulwahid alimjulisha baba yangu pale Mtaa wa Aggrey/Sikukuu nyumbani kwa Abdu mwaka 1952 siku ile usiku.

Mimi hupenda kuwakumbuka wazee wangu kwa namna hii. Kwa kuhadithia habari zao na ninamshukuru Mungu kwa kunipa historia. Wengi wetu hatukubahatika hivi. Historia hii kwangu mimi ni amana. Kitu nilichowekeshwa. Mwenyewe akijakitaka basi sina budi kumpa.

Wee bwana kweli fundi wa hadithi.Mungu amekujalia Inshallah.
Kitumie kipaji chako vizuri wIslamu na waKristo waishi vizuri kwa upendo na amani.
Katika hadithi hii unathibitisha niliyo kuambia , kuwa waIslamu wengi walipigania uhuru kama waAfrika na si kwa dini zao.
Pamoja na yote haya hatuwezi kuishi in the past, yaliyopita si ndwele tugange yajayo!
Vinginevyo sidhani kama utashabikia msemo wa yaliyopita NI ndwele tusigange yajayo!!!!
Ni vema waTanzania tukashabikia yale yanayotuunganisha ili tuwe na nguvu na umoja.Matatizo yaliyowapata waIslamu wengine na anyohadithia ndugu Mohammed Salim yanaweza kutatuliwa with a change in ones mind set.
Mimi nimesoma na kukua na waIslamu wengi tu, na wengine wana vyeo vya juu sana serikalini, sitowataja kwa majina lakini umakini wao katika maisha unani-impress, na hawa jamaa ni watu wa juhudi kubwa kimaisha na kimaendeleo.
Inshallah kuna siku nitawataja ili wengi muone mafanikio yao,ambayo hawakuyapata kwa kulalamika bali kwa kufanya kazi kwa bidii sana.
 
Hii dhulma katika elimu imeanza zamani na mashahidi ni wengi kila mmoja na mwaka wake.Hatimae idadi ya miaka inakuwa mingi kama upendavyo wewe ili dhulma iitwe dhulma.
Nyerere alipojidai kutaifisha mashule,alifanya hivyo kwa kujitoa kimasomaso tu akijua kuwa hizo shule za kanisa wala si za kanisa kweli bali kuna haki nyingi za waislamu.Hata hivyo ilikuwa mbinu yake tu ya kujificha.Angekuwa mkweli basi baada ya uhuru angezigawa kwa waislamu waziendeshe wenyewe.Kwani kwa kuzitaifisha alikuwa tayari ametayarisha mtandao mwengine wa kuendeleza dhulma kwa waislamu.
Angalia hapo:
Roland (1970), The Missionery Factor in East Africa.
Shule za Wakristo zilijengwa na kuendeshwa kwa kodi za Watanganyika. Angalia kitabu cha akina Dodd ukurasa wa 76. Pia rejea ukurasa wa 114 ambapo wanasema, "... there can be no denying that, educational system, even under government had a great Christian bias...". Tafsiri. "Hakuna upinzani kuwa mfumo wa elimu hata pale serikali iliposimamia ulikuwa unawapendelea Wakristo....". Pia ukurasa wa 25 wanasema: "The British government having taken all the burden both recurrent and capital for the mission schools ...". Tafsiri. "Baada ya serikali kikoloni ya Uingereza kuchukua mzigo wote wa kugharimia shule za Kikristo katika matumizi ya kawaida na ya maendeleo...". Katika ukurasa wa 76 Bwana Dodd anasema. "In 1957, Muslim Association Agencies received only Pound 6,848, out of total government expenditure in education in grant - in - aid of pound 1,338,925 ...Christian missions ... greately expanded their education services by the means of grant-in-aid received from the government". Tafsiri. "Katika mwaka 1957 mawakala wa Jumuia za Kiislamu walipokea paundi 6,848 kati ya paundi 1,338,925 zilizotolewa na serikali kusaidia shule za mashirika ya dini ... hivyo Wakristo walitumia fedha hizo kupanua huduma zao za elimu.
Sababu ya wakoloni kufanya hivyo inaelezwa tena katikakitabu cha Roland ukurasa wa 205, utaona maneno yafuatayo:
"In British territories, strongly it was the governments rather than the missions which saw the dangers of the Islamic expansion and which took whatever steps they could to forestall it". Tafsiri; "Katika makoloni ya Waingereza ndio walioona hatari ya kupanuka Uislamu (kuliko wamisheni) na walichukua kila hatua waliyoweza kuzuia hali hiyo".

Sasa Nyerere anaingiaje katika grants za serikali ya uingereza? Tunachosema ni kuwa Nyerere alikuta mfumo wa elimu ambao ulikuwa hautoi mwanya kwa watanzania wote, akaamua kutaifisha shule zote na kufungua milango kwa watoto wote. Alifanya hivyo kuanzia shule za msingi, za sekondari, vyuo na mahospitali. Shule ya sekondari ya Rugambwa ilikuwa ya askofu wa kikatoliki lakini ikawa ya umma, Shule ya Sekondari ya Ndanda ilikuwa ya kikatoliki ikawa ya serikali, shule zote za Aghakhan zilikuwa za wahindi zikawa za umma watoto wote wakawa na fursa sawa. Hospitali ya Bugando ilikuwa ilikuwa ya wakatoliki lakini nayo ikafanywa ya umma kusudi watanzania wote wahudumiwe sawa. Chuo cha Nyegezi kilikuwa cha kikatoliki, kikageuzwa kuwa cha umma na watoto wote wakapewa fursa sawa. Sana sana unachoweza kulaumu ni kuwa kwa kuzitafisha shule hizo serikali ilizirudisha nyuma sana, lakini ilikuwa nia njema kuwa watoto wote wasome. Kila siku Nyerere anasemwa mtu alishaondoka madarakani miaka 25 iliyopita, na katikati kumekuwa na maraisi waisilamu wawili, makamu wa rais waislamu wengi tu kwani wao haoni kama kweli serikali inabagua waislamu.
 
no, namba za mtihani zimeanza baada ya malima kuingia wizarani. kabala ya hapo tukitumia majina . kama huamini nenda ukaanglie record ktk baraza la mitihani

Wewe husemi ukweli kwa sababu namba zetu zilikuwa na format ya S.***/***. Mimi nimemaliza shule za sekondari miaka ya sabini wakati uongozi wa Nyerere ukiwa kwenye peak akisadiana na Aboud Jumbe aliyekuwa anatembelea nchi nzima karibu kila baada ya miezi miwili. Namba hizo ndizo pia tulikuwa tunatumia kwenye Sel-Form za kuombea kazi, Mwaka 1984 nilishiriki katika kusahihisha mithani ya Physics ya form 6 na wanafunzi wote walikuwa wakitumia namba.
 
Jamani sisi vijana wa miaka ya 80 tunaufutilia kwa makini huu mjadala naomba tu! mslielemee upande wowote kuna mwananchi hapo juu ameongea point to be NOTED "WAISLAM WALIPIGINIA UHURU WA NCHI KAMA WAAFRIKA NA SI KAMA WAISLAM" Lets move on kwani tukiishi kutoka na history kamwe hatuoendelea
 
LG: Ahsante kwa kunisifia lakini isiwe unanivisha kilemba cha ukoka. Mambo ndiyo kama ulivyosoma. Nilipoona historia hiyo yote imezikwa nikatia nia ya kuifufua. Leo hii Alhamdulilah historia hii imehifadhika.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom