Ukweli kuhusu waasisi wa TANU na harakati za kupigania uhuru

Ukweli kuhusu waasisi wa TANU na harakati za kupigania uhuru

Status
Not open for further replies.
LG: Ahsante kwa mchango wako. Nia ya kuandika kitabu kile ni kuiweka sawa historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika kuwa Waislam ndiyo waliotoa mchango mkubwa hili sikulitaka mimi. Labda swali liwe kwa nini Waislam walilkuwa mbele katika kuupiga vita ukoloni? Msitishike na ukweli huu. Nachoshukuru ni kuwa waliokuwa hawatuelewi leo hii wanatuelewa. Vyuo vyote vinavyosomesha "African History" na "Islam and Politics" kitabu hiki ni mashuhuri na baadhi ya walimu wa vyuo hivyo ni marafiki zangu wakubwa na urafiki umekuja kwa sababu nimechangia katika dunia ya usomi, kitabu cha maana ambacho kimeongeza elimu. Jonathan Glassman, James Brenan, Brenan Mcsherry, Prof. Ali Mazrui ni watu ambao nisingewajua kama si kwa kitabu hicho. Hawa hawakupata kunikejeli wala kunizomea. Kwao wao nimepokea heshima, na mialiko. Ajabu naiona kwenu kila mkisoma hoja zangu hamaki zinapanda. Nimelipeleka hili jambo kwa mmoja wa maprofessa wa pyschology kutaka kujua ni nini hasa kinasababisha hali hii yenu na nimemuuliza kwa nini mimi sikasiriki kama hawa wenzangu. Kaniomba nimpelekee majibu yenu na hoja zangu. Nimefanya hivyo na sasa nasubiri jibu lake.
 
Ogah: Jitulize na fanya fikra. Usiuachie moyo ukakutawala toa nafasi kwa kichwa chako. Kuna mengi utanufaikanayo katika kufanya hivyo. Kwa kuanzia rejea katika michango yako kisha fananisha na majibu ninayotoa. Mjadala utadorora kwa matumizi ya lugha zisizo za kiungwana. Mjadala utastawi kwa kushindanisha hoja kwa hoja. Nimesomeshwa na walimu wazuri sana (madras na shule) na nawashukuru kwa elimu na maarifa waliyonipa ndiyo maana leo unanisoma humu. Haipendezi kuwatusi. Kwa kumaliza napenda nikufahamishe kuwa tafsiri ya Qur'an nilisoma kwa Sheikh Abdallah Iddi Chaurembo mwanafunzi wa Mufti Sheikh Hassan bin Ameir (hawa wote walikuwa mstari wa mbele katika TANU). Uongozi nimesomeshwa na Sheikh Hussein Malik (muasisi wa Warsha). Historia nimesomeshwa na Prof. Kaijage Dar es Salaam University na nilikuwa mmoja wa wanafunzi wake alowapenda sana.

....kusema kwamba walimu wako WAKO WRONG haimaanishi MATUSI..........ni mtizamo.........ungejituliza wewe na kufanya FIKRA ungejua jinsi gani ya kujibu mtizamo wangu.........sasa kwa kuwa wewe umeachia moyo wako kutawala na kuondoa nafasi ya kichwa chako..................ndio kunasababisha kutukana MATUSI HAPO JUU...............

Walimu wetu..........both kwenye elimu dunia na elimu ya dini..........wanakuwa challenged................wao sio MWISHO WA FIKRA (na wao hukosea).............watu wanachallenge na hata kujibu AYA na JUMBE za vitabu depending on the facts............na huwezi kum-ignore mtu anayekuchallenge kwa facts eti kwakuwa hajakujibu kwa kutumia kitabu kama ulivyoandika wewe..........again hao WALIMU ARE WRONG.........kukuambia KITABU HUJIBIWA KWA KITABU..............

Kitabu chako cha kurasa say 200....chaweza kuwa na facts 10 (tena kumi ni nyingi) tu.........nyingine ni strories tu (kama kukunja miguu nyumba numba 36).......na si lazima kujibu facts 10 kwa kurasa 200!........wengine sio ma-story tellers.............
 
Ogah: Nakushukuru kwa mchango wako na nathamini sana juhudi zako. Tuendelee kujadiliana.
 
Safari: Ahsante kwa mchango wako. Nakuwekea kipande hiki kutoka kitabu changu kinachohusu Yanga na Sunderland ya miaka ya 1950. Soma kisha nipe fikra zako:

Baada ya vyama hivyo vya wanawake kuingizwa katika TANU ndipo iliamuliwa kuwa vilabu viwili maarufu vya mpira na vilivyokuwa na ushindani mkubwa mjini Dar es Salaam, Young Africans na Sunderland navyo vijumuishwe katika kuiunga mkono TANU. Young Africans ilikuwa kilabu isiyo na wafuasi wenye elimu sana. Wengi wa wanachama na mashabiki wake walikuwa watu wa kawaida kutoka mitaa ya Dar es Salaam. Yanga kama ilivyokuwa ikijulikana ilichukua wachezaji wake mashuhuri kutoka vijana waliozaliwa na kulelewa mjini Dar es Salaam na pembezoni mwake. Vijana waliokua na kucheza mpira pamoja katika viwanja vya tifutifu katika mitaa ya Kariakoo. Kandanda ndiyo iliwafanya watu wa Tanganyika na Zanzibar wakutane. Kulikuwa na uhusiano baina ya Yanga na chama cha African Association huko Zanzibar tangu miaka ya 1930. Wengi wa viongozi wa African Association walikuwa washabiki wa mpira na wengi wa viongozi wa Yanga walikuwa wapenzi wa taarabu na Zanzibar ndiyo walikuwa mabingwa wa muziki huo. Haya ndiyo mambo yaliyowakutanisha wananchi wa pande mbili hizi pamoja na mwamko wa siasa. Kama TANU, rangi za Yanga ilikuwa kijani na nyeusi. Mwaka 1954 TANU ilipopandisha bendera yake ya kijani na nyeusi mtu wa kawaida hakuwa na khiyari ila kuifunganisha TANU na Yanga. Kwa hiyo, kuwa mwanachama wa Yanga au shabiki wake kuwa mwananchama wa Yanga ilikuwa sawasawa na kuwa mwanachama wa TANU. Inaaminika kwamba ilikuwa wakati wa uongozi wa Mohamed Sultan kama rais wa Yanga ndipo Mohamed Sultan alimtambulisha Nyerere kwa Karume, Rais wa Afro-Shiraz Party ndani ya kilabu ya Yanga Mtaa wa Mafia na Sukuma, Kariakoo.
 
FM: Uchochezi si moja ya sifa zangu.
.......... ilikuwa wazi kuwa Pacha, kama Mkristo na kabila yake Mlulwa kutoka Mpanda, hawezi kukubalika na Wamanyema wa Tabora. Wamanyema walikuwa wanajulikana kwa tabia yao ya ukaidi.
Need we explain more?
I suppose I rest my case
 
Ogah: Jitulize na fanya fikra. Usiuachie moyo ukakutawala toa nafasi kwa kichwa chako. Kuna mengi utanufaikanayo katika kufanya hivyo. Kwa kuanzia rejea katika michango yako kisha fananisha na majibu ninayotoa. Mjadala utadorora kwa matumizi ya lugha zisizo za kiungwana. Mjadala utastawi kwa kushindanisha hoja kwa hoja. Nimesomeshwa na walimu wazuri sana (madras na shule) na nawashukuru kwa elimu na maarifa waliyonipa ndiyo maana leo unanisoma humu. Haipendezi kuwatusi. Kwa kumaliza napenda nikufahamishe kuwa tafsiri ya Qur'an nilisoma kwa Sheikh Abdallah Iddi Chaurembo mwanafunzi wa Mufti Sheikh Hassan bin Ameir (hawa wote walikuwa mstari wa mbele katika TANU). Uongozi nimesomeshwa na Sheikh Hussein Malik (muasisi wa Warsha). Historia nimesomeshwa na Prof. Kaijage Dar es Salaam University na nilikuwa mmoja wa wanafunzi wake alowapenda sana.

BTW........Uzuri wa Walimu angalia products zao.............however products zilizozalishwa na product zao zaweza ku-deceive umma..........kwa kuamini uzuri wa Walimu hao.........my point is naheshimu sana mchango wa Walimu notwithstanding............
 
labda niwe tofauti kidogo katika kuchangia kwa kuuliza swali, kusema ni waislam ndio waliopigania uhuru na si nyerere kwa mfano unataka ku achieve nini regardless hoja yako ni kweli au si kweli? pili, sijui kama hata ushawai ku gogolise kujua sababu kubwa iliyowafanya waingereza watupe uhuru bila kumwaga damu, ni hoja za nyerere kwenye majukwaa ya kimataifa hadi akaonekana ni mtu anaweza ondoka, kuongoza mapambano ya uhuru wakati tungekua tunaonekana ni ma mbumbumbu sidhan kama huo uhuru tungeupata mkuu! kua na hoja jenga hasa ktk jamii kwani unakua kama unataka kuonyesha waislam wameonewa na wanaendelea kuonewa nchi hii bila sababu! unazungumzia vitu vilivyovunjwa vya waislam mbona huzungumzii mali za kanisa zilivyotaifishwa na zingine kulazimishwa kuwahudumia wananchi wote kiujumla bila kujali itikadi zao baada ya azimio la arusha! sera ya nchi ilikua ni kujenga mfumo usioruhusu dini kuingilia mifumo ambayo itawagawa watu kama nchi changa tulitaka umoja, je tunakoelekea sasa unakupenda, watu wanajali udini zaidi ktk siasa, michezo, ajira na karibu kila nyanja ya uchumi?
 
Mohamed Said said:
Ajabu naiona kwenu kila mkisoma hoja zangu hamaki zinapanda. Nimelipeleka hili jambo kwa mmoja wa maprofessa wa pyschology kutaka kujua ni nini hasa kinasababisha hali hii yenu na nimemuuliza kwa nini mimi sikasiriki kama hawa wenzangu. Kaniomba nimpelekee majibu yenu na hoja zangu. Nimefanya hivyo na sasa nasubiri jibu lake.

Mohamed Said,

..hapa umenichanganya kwelikweli.

..pamoja na kuelewa saikolojia ya wale wanaokupinga ungetafuta ushauri ili kuelewa saikolojia yako binafsi.

..hakikisha huyo mtaalamu wa psychology yuko independent, ili kupata ushauri wa uhakika na wenye msaada kwako.

..ktk video clip kuna mahali umejitambulisha kama Mmanyema, na zaidi ukadai hujawahi kukutana na Mkristo ktk kabila la Wamanyema. mimi kauli ile, na maneno mengine ya kuwazungumzia Wakristo kama "hawa," inanipa mashaka kama unaweza kuyaangalia masuala ya mahusiano kati ya dini hizi mbili with an "independent and unbiased" view.

..maadam umelileta mwenyewe suala la PSYCHOLOGIST, kwa heshima na taadhima, nashauri upeleke hizi video clips zako zikaangaliwe na wataalam na kupata maoni yao.
 
FM: Uchochezi si moja ya sifa zangu. Nakuwekea kiapnde hiki uone ukoloni ulivyokuwa ukitazamwa na Waislam na uone vipi dini hizi mbili zilivyoathiriwa na utawala wa Waingereza. Huu ni muhtasari tu:

Mwaka 1951 mgogoro wa ardhi ya Wameru ulipoanza tawi la TAA mjini Tabora lilikabili changamoto hiyo kupitia juhudi binafsi za Saadan Abdu Kandoro. Kandoro aliitisha mkutano wa matawi ya TAA ya Mwanza, Kigoma na Tabora kujadili suala hilo. Uongozi wa TAA Tabora, kwa kujihusisha katika mgogoro kama huu, ilikuja kuwa ngome ya upinzani dhidi ya ukoloni. Germano Pacha, katibu wa TAA katika Jimbo la Magharibi, alikuwa miongoni mwa wale wajumbe ambao tarehe 29 Oktoba, 1953 walikwenda Government House kuonana na Gavana Edward Twining ili kujadili ule waraka wa serikali, yaani Government Circular No. 5 uliopiga marufuku wafanyakazi serikalini kujishughulisha na siasa. Mwaka uliofuata TAA ilibadilishwa kuwa TANU na Pacha alikuwa miongoni mwa wanachama waasisi. Pacha alianza kuifanyia kampeni TANU mara tu aliporudi kutoka mkutano wa TAA ulioasisi TANU. Akiwa mhitimu wa Seminari ya Kipalapala ilikuwa rahisi sana kwake kupata kumbi za kanisani, Tabora vijijijni ambamo alifanya baadhi ya mikutano yake ya mwanzoni ya kampeni za TANU. Jambo hili lilizusha ugomvi dhidi ya Pacha. Jambo lile liliwaudhi viongozi Waislam katika TANU mjini Tabora. Wamishonari walijulikana kuwa makachero wa wakoloni na wapinzani wa Uislamu. Kwa hiyo uongozi wa Waislam mjini Tabora ukamsusa Pacha na kwa muda kwa ajili ya kufanya baadhi ya mikutano ya TANU katika kumbi za makanisa. Ususiaji huu ukaifanya TANU katika Jimbo la Magharibi kuzorota. TANU haikuweza kupamba moto Tabora kama ilivyotarajiwa. Moto wa siasa uliokuwa Tabora tangu mwaka 1945 ulionekana kufifia kwa kuzuka chama kipya cha siasa.

Juhudi za kuihuisha TANU zilikuja mwaka 1955 mwaka mmoja baadae kupitia Young New Strong Football Club -kilabu ya kandanda iliyoanzishwa miaka mingi nyuma ambayo ilikuwa maarufu pale mjini. Wanachama wa kilabu hiyo baadhi yao ndiyo walikuwa waasisi wa African Association, mashuhuri miongoni mwao walikuwa Fundi Mhindi na Maulidi Kivuruga. Mwenyekiti wa kilabu hiyo alikuwa Juma Mrisho, mcheza kandanda mashuhuri kwa siku zile. Shaaban Mohamed Silabu na Bilali Rehani Waikela walikuwa katibu na naibu katibu. Uongozi huu wa klabu hiyo ya kandanda ulikutana katika nyumba ya Abeid Kazimoto aliyekuwa akifanya kazi Medical Department, kujadili jinsi ya kuifufua TANU. Sasa ilikuwa wazi kuwa Pacha, kama Mkristo na kabila yake Mlulwa kutoka Mpanda, hawezi kukubalika na Wamanyema wa Tabora. Wamanyema walikuwa wanajulikana kwa tabia yao ya ukaidi. Wakati huo TANU ilibidi ikubaliwe na Waislam wakazi wa mijini kabla ya kusambaa kwenye sehemu nyinginezo. Wamanyema kama Waislam wa mijini walikuwa nguvu thabiti ya kisiasa ambayo haikuwa raihisi kupuuzwa. Alichokuwa akikabiliana nacho Pacha kilikuwa sawasa na kile Nyerere kilimkabili baada ya kumshinda Abdulwahid Sykes katika ule uchaguzi wa TAA wa mwaka 1953. Waislam waliacha kuiunga mkono TANU kwa sababu zile zile zilizomsibu Nyerere. Uongozi wa kilabu uliamua kumualika Julius Nyerere na Bibi Titi Mohammed kuja Tabora ili kujadili tatizo hilo na kulitafutia jawabu.

Mwaka 1955 Bibi Titi Mohamed na Julius Nyerere waliitika mwaliko na kuja Tabora. Mkutano ulifanyika katika ile kilabu ya kandanda. Waliohudhuria mkutano ule walikuwa Germano Pacha, Juma Mrisho, Shaaban Mohamed Silabu, Bilali Rehani Waikela, Mohamed Mataka wakati ule akiwa muadhin wa Masjid Nur - msikiti wa Wamanyema pale Tabora, Hassan Mohamed Ikunji, Ramadhani Mussa Wajaku, Swedi Mambosasa, Said Ali Kiruwi na Hamis Khalfan. Uongozi wa kilabu ulimwambia Nyerere na Bibi Titi kuwa kilabu hiyo ya kandanda ilikuwa ikitaka udugu na TANU ili ifanye kampeni ya kuipatia TANU wanachama wengi. Uongozi huo wa TANU kutoka makao makuu Dar es Salaam uliambiwa kuwa maadam kilabu hiyo ilikuwa ikipendwa na kuungwa mkono na watu wa Tabora na ilikuwa maarufu sana, sifa hizo zingeweza kutumiwa kwa manufaa ya TANU. Vilevile Nyerere alifahamishwa kuwa kilabu hiyo ingependa kuvijumuisha vyama vitatu vya lelemama na vikundi vya taarabu, Nujum ul Azhar, Waridatil Hubb na Egyptian Club. Nyerere na Titi waliyakubali mapendekezo haya na usiku ule akifuatana na uongozi wa kilabu Nyerere alizungumza na kikundi cha watu waliyokusanyika nje ya nyumba ya kilabu juu ya hali ya Tanganyika katika siku zijazo. Nyerere alikuwa amerudi Tabora ambapo alianza siasa kiasi cha miaka minane nyuma. Jambo muhimu katika kipindi hiki pale Tabora ni kuwa wasomi wa Makerere waliokuwa St. Maryís School hawakuwapo katika harakati hizi na katika mikakati iliyokuwa ikipangwa.

Bibi mmoja wa Kiganda, Nyange bint Chande, mwanachama wa moja ya vikundi vya lelemama mjini Tabora alijitolea nyumba yake kama ofisi ya kwanza ya TANU katika Jimbo la Magharibi. Uchaguzi ulifanyika na Shaabani Marijani alichaguliwa Mwenyekiti wa Wilaya na Idd Said Ludete Katibu wa TANU. Bilali Waikela akawa mjumbe wa kamati. Kadi za kwanza za uanachama wa TANU ziliuzwa ndani ya soko la Tabora na Amani Idd na Pacha, Katibu wa Jimbo wa TANU. Pacha alikuwa na lingo la kuni pale sokoni kama biashara yake. Baadae Amani Idd alisaidiwa kazi hiyo ya kuuza kadi za TANU na Dharura bint Abdulrahman.
'

Tatizo si unachokiandika bali hizo hitimisho zako. Unamlaume Nyerere kwa kuwatenga waislamu lakini kila ulichoandika ni kuwa waislamu ndio waliowatenga wakristu wakina Pacha na Nyerere! Pamoja na Tabora kuwa na waislamu wengi, lakini bado tunaona mmisheni alikuwemo kwenye juhudi za kugombea uhuru! Hii yote inathibitisha msimamo wetu kuwa uhuru uliletwa kwa juhudi za kushirikiana wakristu na waislamu. Si waislamu peke yao kama unavyotaka kupindisha! Kwangu mimi huo ni uchochezi.

Amandla..........
 
duh huu mjadala unapoelekea sijui.

ila nnajua kwa haraka hakuna kitu ambacho kizito kukijadili kwa amani hadi mwisho kama masuali ya dini.

sasa tujadiliane bila ya kupambana kwa ngumi
 
Mtu wa Pwani: Ahsante kwa kuingia katika mjadala. Usiwe na hofu na mimi mie si mgomvi najibu hoja jwa hoja yenye mantiki wala sithubutu kutumia lugha isiyo ya kiungwana. Waamerika wana msemo: It takes two to Tango.
 
FM: Hakika umesema kweli. Nimekuwekea hiyo ili uone mambo yalivyokuwa wakati ule. Wabague uwatawale.
 
JK: Ahsante kwa ushauri. Huyu professor keshanipitia na moja katika taarifa yake alinambia: "You are a man of exceptional courage." Yapo mengi alisema kuhusu mimi na hadi leo namshukuru mtu aliyenijulisha kwake na mimi nimejitahidi sana kuwaeleza marafiki zangu kuhusu mtaalam huyu. Baadhi ya mabadilishano yetu yeye ametumia katika kusomesha. Hivi sasa anaandika kitabu ambacho Tanzania na woga wa viongozi wetu kuogopa vivuli utaelezwa. Yako mengi kanieleza kuhusu tabia yangu mazuri na mabaya. Insha Allah ikitokea nafasi ntakujuvya.
 
Safari: Ahsante kwa mchango wako. Nakuwekea kipande hiki kutoka kitabu changu kinachohusu Yanga na Sunderland ya miaka ya 1950. Soma kisha nipe fikra zako:

Baada ya vyama hivyo vya wanawake kuingizwa katika TANU ndipo iliamuliwa kuwa vilabu viwili maarufu vya mpira na vilivyokuwa na ushindani mkubwa mjini Dar es Salaam, Young Africans na Sunderland navyo vijumuishwe katika kuiunga mkono TANU. Young Africans ilikuwa kilabu isiyo na wafuasi wenye elimu sana. Wengi wa wanachama na mashabiki wake walikuwa watu wa kawaida kutoka mitaa ya Dar es Salaam. Yanga kama ilivyokuwa ikijulikana ilichukua wachezaji wake mashuhuri kutoka vijana waliozaliwa na kulelewa mjini Dar es Salaam na pembezoni mwake. Vijana waliokua na kucheza mpira pamoja katika viwanja vya tifutifu katika mitaa ya Kariakoo. Kandanda ndiyo iliwafanya watu wa Tanganyika na Zanzibar wakutane. Kulikuwa na uhusiano baina ya Yanga na chama cha African Association huko Zanzibar tangu miaka ya 1930. Wengi wa viongozi wa African Association walikuwa washabiki wa mpira na wengi wa viongozi wa Yanga walikuwa wapenzi wa taarabu na Zanzibar ndiyo walikuwa mabingwa wa muziki huo. Haya ndiyo mambo yaliyowakutanisha wananchi wa pande mbili hizi pamoja na mwamko wa siasa. Kama TANU, rangi za Yanga ilikuwa kijani na nyeusi. Mwaka 1954 TANU ilipopandisha bendera yake ya kijani na nyeusi mtu wa kawaida hakuwa na khiyari ila kuifunganisha TANU na Yanga. Kwa hiyo, kuwa mwanachama wa Yanga au shabiki wake kuwa mwananchama wa Yanga ilikuwa sawasawa na kuwa mwanachama wa TANU. Inaaminika kwamba ilikuwa wakati wa uongozi wa Mohamed Sultan kama rais wa Yanga ndipo Mohamed Sultan alimtambulisha Nyerere kwa Karume, Rais wa Afro-Shiraz Party ndani ya kilabu ya Yanga Mtaa wa Mafia na Sukuma, Kariakoo.
Mkuu hata hii story yako nashindwa kukubaliana nayo kwa sababu navyojua mimi Marehemu Sheikh Abeid Karume na African Sports ya Zanzibar ndio waanzilishi wa club ya Yanga ya Dar Es Salaam na ile Africa Sports ya Tanga zikiwa kama ni matawi la African Sports ya Zanzibar. Hii ilitokana na kuwa mzee yule (Baharia) baada ya kurudi Unguja alijiunga na wenzake kuunda team ya mpira kwa sababu jumuiya za kisiasa zilikuwa ni marufuku.

Nakuomba fanya utafiti kwa wana Yanga wenyewe utakuta historia hii na kama sikosei nilipokuwa Tanzania kabla sijaondoka (mwezi April) Yanga walimuenzi Marehemu Karume akahudhulia mkewe ktk maandimisho hayo, na nilimwona mke wa marehemu Abeid Karume akihutubia mkutano uloandaliwa na Yanga (on TV). Katika hotuba yake alisema wazi na kuwakumbusha wanachama mchango wa marehemu ktk Ujenzi wa team hiyo na akimalizia kwamba Karume was Assassinated na akiomba historia kamili ya kuawa kwake iandikwe na wahusika watajwe pasipo kuficha. Kwa hiyo sioni kabisa mahusiano ya Yanga na TANU hapa unatuongezea tu kwa sababu rangi zao zinafanana na ni ktk dhana hiyo hiyo unatumia kumlaumu Nyerere kwa sababu ni rangi ya Yanga, sii rangi ya Simba.
 
quote_icon.png
Originally Posted by Mohamed Said

FM: Uchochezi si moja ya sifa zangu. (kweli?)
.......... ilikuwa wazi kuwa Pacha, kama Mkristo na kabila yake Mlulwa kutoka Mpanda, hawezi kukubalika na Wamanyema wa Tabora. Wamanyema walikuwa wanajulikana kwa tabia yao ya ukaidi.
...........
harakati za pili za Waislam, safari hii kuchukua serikali kutoka kwa Wakristo. Harakati za kwanza zilikuwa zile za kumngíoa Mwingereza katika ardhi ya Tanganyika

.............
Katika miaka ya 1950, jiji la Dar-es-Salaam lilikua na la Waislamu. Hata mabibi wa Kikristo walikua wakivaa mabuibui, kivazi cha Waislamu.
.................

[/QUOTE]
Mohammed Said[/I]
..pamoja na kuelewa saikolojia ya wale wanaokupinga ungetafuta ushauri ili kuelewa saikolojia yako binafsi.

..hakikisha huyo mtaalamu wa psychology yuko independent, ili kupata ushauri wa uhakika na wenye msaada kwako.

..ktk video clip kuna mahali umejitambulisha kama Mmanyema, na zaidi ukadai hujawahi kukutana na Mkristo ktk kabila la Wamanyema. mimi kauli ile, na maneno mengine ya kuwazungumzia Wakristo kama "hawa," inanipa mashaka kama unaweza kuyaangalia masuala ya mahusiano kati ya dini hizi mbili with an "independent and unbiased" view.

..maadam umelileta mwenyewe suala la PSYCHOLOGIST, kwa heshima na taadhima, nashauri upeleke hizi video clips zako zikaangaliwe na wataalam na kupata maoni yao.

Hizo ndio zake Mohammed Said,mwandishi who is basking in the sunshine of inconsequential foreigners and half cooked admirers.
Elewa tu muheshimiwa Mohammed kuwa siku ya siku , tutakapokula sahani moja hawa jamaa watakuwa wakila kuku huko makwao.


In general huyu ndugu yetu Mohammed Said is unstable upstairs.Nimejaribu kumuweka katika bahasha inayoeleweka lakini sipati anuani.

Kwa vile kwa mambo anayoandika anaomba msaada wa wataalam zaidi yake..PSYCHOLOGISTS mimi namshauri aende mbali zaidi apate ushauri wa PSYCHIATRISTS.
 
JK: Ahsante kwa ushauri wako. Insha Allah na tuendelee kujadiliana na kupeana nasaha kama hizi. Najifunza mengi. Wamanyema kama Warufiji na Wangazija huwezi kupata Mkristo. Huu ni ukweli ingawa huenda wengine wasiupende. Naitakia nchi yangu amani ya kweli ndiyo maana niliandika kitabu kile. Haiwezekani Wakristo wahodhi kila kitu halafu useme hivi ndivyo ilivyotakiwa na mtegemee Waislam waridhie na hali hiyo miaka nenda miaka rudi. Allah anawakataza Waislam kudhulumu na vilevile amewakataza kukubali kudhulumiwa. Wanaodhulumu hawathubutu kutoa majibu sana sana wameishia kupiga vitabu marufuku (Mwembechai Killings) na kukusanya magazeti (Africa Events).
 
Mkandara kwa hili wala sihitaji kumuuliza mtu. Yanga iko Mtaa wa Sukuma chuo chetu kwa Shariff Abdulrahman milango inatazamana. Nimuulize nani? Shariff Abdulrahman akicheza Yanga. Baba yangu kasoma Qur'an kwa Mwalimu Mzinga mtoto wake (Mambo Mzinga) alikuwa mchezaji wa Yanga hao wote ni wazee wangu. Mambo Mzinga na baba yangu wamesoma chuo kimoja hapo Mtaa wa Mafia na Chura. Sikuwa na haja ya kutafuta habari za Yanga kwa yeyote yule ni historia iliyokuwa ndani ya nyumba yetu. Hao watu wa magazeti masikini ya Mungu wanajiandikia tu bila ya hata kufanya utafiti. Ikiwa mtataka kujua historia yetu iko wazi tutaieleza na kama inakupeni shida haipendezi kwenu hiyo ni bahati mbaya. Mzee Kitwana Kondo wakati alipokuwa Mayor wa Dar es Salaam alilalamikiwa kwa kubadili baadhi ya majina ya mitaa ya Dar es Salaam na kuipa majina ya wazalendo waliopigania uhuru wa Tanganyika. Katika mahojiano na Sarah Dumbah wa RTD Mzee Kondo alisema kama kuna mtu hajui Mshume Kiyate alikuwa nani katika TANU na aulize tutamwambia. Kwa hasad zao hadi leo wamekataa kubadili kibao cha Mtaa wa Tandamti na kuuita jina la Mshume Kiyate. Katika khutba niliyotoa Msikiti wa Idris bin Saad mwaka huu mwanzoni niliwaambia Waislam mara nyingine mkinialika hapa nataka nikione kibao cha Kiyate Mshume kimewekwa (Msikiti wa Idris bin Saad upo Mtaa wa Tandamiti na Donge. Tandamti ndiyo mtaa akiishi Mzee Mshume Kiyate.) Ukipenda naweza kukuwekea kipande cha mchango wake katika kupigania uhuru wa Tanganyika. Mzee Mshume ni mmoja wa mashujaa wetu waliofutwa katika historia.
 
Mkandara kwa hili wala sihitaji kumuuliza mtu. Yanga iko Mtaa wa Sukuma chuo chetu kwa Shariff Abdulrahman milango inatazamana. Nimuulize nani? Shariff Abdulrahman akicheza Yanga. Baba yangu kasoma Qur;an kwa Mwalimu Mzinga mtoto wake (Mambo Mzinga) alikuwa mchezaji wa Yanga hao wote ni wazee wangu. Mambo Mzinga na baba yangu wamesoma chuo kimoja hapo Mtaa wa Mafia na Chura. Sikuwa na haja ya kutafuta habari za Yanga kwa yeyote yule ni historia iliyokuwa ndani ya nyumba yetu.
Mkuu wangu kuwa mchezaji wa Yanga haina maana ataajua historia ya Timu hiyo. Nakwambia wewe tafuta ukweli haiwezekani ukweli wako ndio pekee kwa sababu ulienda chuoni karibu na hapo.. Hii akili gani mkuu wangu. Nasema hivi, mimi nimeona ktk TV - Yanga wenyewe wakim enzi marehemu Karume live on TV April mwaka huu..na historia ikazungumzwa kwa kumpongeza Marehemu. Leo wewe unakuja na mambo ya Yanga na TANU hali havihusiani kabisa isipokuwa rangi zake. sasa utakuja sema hata haya nayoandika ni uongo tafuta ukweli mkuu wangu tafuta ukweli na sio wewe kufanya maamuzi ya mwisho.
 
Bona: Ahsante kwa mchango wako umechelewa kuingia katika mjadala. Swali lako nishalijibu huko nyuma. Nimeandika historia ya wazee wangu ili niweke kumbukumbu zao kwa faida ya kizazi kijacho. Historia rasmi ilikuwa inamtukuza Nyerere peke yake. Nikaona ni vyema nami niandike ili na ya wazee wetu ijulikane pia. Kwa bahati mbaya historia hii inawachoma watu wengine kwa kuwa waliokuwa mstari wa mbele kupambana na ukoloni walikuwa Waislam. Wao hawataki Waislam watajwe kwao wao ni kuingiza udini.
 
Mkandara: Mimi sina ugomvi na mawazo kama hayo uwanja ni wa kila mtu na mtu ana ruhusa ya kueleza lile analojua. Wanaotusoma watapima nani anasema kweli. Mwinyi Mangara mtoto wa Tabu Mangara mchezaji wa Yanga 1940s na Rais wa Yanga 1960/70 yu hai yuko pale Ilala waandishi wamfuate kwa mahojiano. Mtoto wa Kondo Kipwata aliekuwa kiongozi kabla ya Mangara Tabu wanae wapo na wawatafute kwa mahojiano. Captain Maliki aliecheza Yanga sisi bado wadogo sana yuko pale Club ya Pan African na akahojiwe. Hapana shaka ni hivi ndivyo inavyotakiwa.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom