Aaaah nashukuru the power ya Mtandao.... Nimefanya ku google na nimepata kipande hiki kuthibitisha kile nilichosema mimi....
Monday, 19 April 2010
KARUME MWANZILISHI WA YANGA NA JINA LA SIMBA SPORTS CLUB
Na Ibrahim Mkamba
HISTORIA yetu katika mambo mengi imepotoshwa ama kwa makusudi au kwa bahati mbaya.Ni upotoshaji wa historia mtu anapoizungumzia klabu ya Young Africans maarufu kama Yanga bila kumzungumzia hayati Sheikh Abeid Aman Karume ambaye tangu atutoke kwa kupigwa risasi mwaka 1972, tarehe 7 mwezi huu na mwak huu ilitimia miaka 38 kamili.Ni upotoshaji wa historia mtu anapozungumzia jina la Simba Sports Club bila kumtaja Rais huyo wa kwanza wa Zanzibar na Makamu wa Kwanza, wa kwanza, wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Aidha,ni kosa kubwa kiimani na kimaadili mtu kuzipongeza klabu za Simba na Yanga kuwa na majengo yake bila kumhusisha kwa kiwango kikubwa hayati Karume.Kutomhusisha huko,kiimani ni dhambi ambapo kimaadili ni utovu mkubwa wa shukrani.Kwa maneno mengine,klabu za Yanga na Simba zilifanyiwa makubwa mno na hayati Karume kinyume cha jinsi historia inavyofanyiwa jitihada kwa Mwenyekiti huyo wa kwanza wa Baraza la Mapinduzi ya Zanzibar kutosikika sana ndani ya klabu hizo za soka zenye mashabiki wengi ndani ya Jamhuri nzima ya Muungano wa Tanzania.
Aliyoyafanya Karume kwa Yanga
Historia iliyoandikwa haielezi vizuri ukweli kwamba Sheikh Abeid Aman Karume alikuwa mhamasishaji mkubwa wa kuanzishwa kwa klabu ya soka ambayo sasa ndiyo hii inayoitwa Young Africans yaani Yanga.Baada ya kufanya kazi ya ubaharia iliyomuwezesha kuzunguka karibu dunia nzima kwa miaka kadhaa akiwa kijana mdogo, Karume alipata uzoefu wa yaliyotokea kwenye nchi mbalimbali alizozunguka duniani na kugundua kwamba serikali za kikoloni zilipiga vita uanzishwaji wa vyama vya siasa na wananchi wazawa lakini zilikuwa hazipingi vyama vya kijamii kama klabu za michezo.
Baada ya kuufahamu ukweli huo,akiwa nyumbani Zanzibar,Karume alijiunga na wenzake na kuunda klabu ya soka iliyojulikana kama African Sports Club,mwenyewe akiwa mchezaji mahiri wa timu ya klabu hiyo.Humo humo kwenye mikutano ya kisoka ndimo yeye na Wazanzibari wenzake walikuwa wakijadili jinsi ya kujinasua toka kwenye utawala wa kisultani uliokuwa ukilindwa na Waingereza.
Ni hayati Karume ndiye aliyehamasisha kuanzishwa kwa matawi ya hiyo African Sports ya Zanzibar na akafanikiwa kuanzishwa kwa tawi la timu hiyo jijini Dar es Salaam ambalo kwa sasa ndilo hii klabu kubwa sana ya Yanga na kule Tanga alifanikisha kuanzishwa kwa tawi jingine ambalo ni African Sports ya Tanga.Kumbuka kuwa kwenye miaka hiyo ya nyuma miji ya Dar es Salaam,Bagamoyo,Pangani na Tanga ilikuwa na ukaribu sana wa kimahusiano na miji ya visiwa vya Unguja na Pemba.
Baada ya kuanzishwa,timu hizo tatu za Yanga ya sasa,African Sports ya Zanzibar na African Sports ya Tanga zilitengeneza undugu wa damu mkubwa mno.Zote tatu zilikuwa chimbuko la hayati Karume ingawa historia haiuweki wazi ukweli huo.
Kwa Yanga pia, hayati Karume ndiye alitoa kiasi kikubwa cha pesa,kama siyo chote, mwaka 1971 kwa kufanikisha ujenzi wa jengo la makao makuu ya Yanga la sasa lililopo kwenye makutano ya mitaa ya Twiga na Jangwani,Kariakoo jijini Dar es Salaam.Alifanya hivyo kwa Yanga baada ya kushirikiana na wana Simba kupata jengo lao kwenye mtaa wa Msimbazi,Kariakoo,jijini Dar es Salaam mwaka huo 1971 kwa kuchangia kiasi cha pesa. Ki msingi,hayati Karume alishiriki kujenga majengo yote mawili ya klabu za Yanga na Simba ingawa historia iliyoandikwa haitaki kuuweka wazi ukweli huo.
Hivyo ndivyo hayati Karume alivyoifanyia klabu ya Yanga tangu kuanzishwa kwake mpaka kupata jengo la makao makuu yake.Ukitaka kuamini jinsi jengo la Yanga lilivyo na mahusiano na Wazanzibari,tangaza leo kupigwa kwake mnada,uone jinsi utakavyoshukiwa kwa hasira na Wazanzibari.Kama huamini,nitakukumbusha.Mwaka 1988 jengo hilo lilikuwa lipigwe mnada baada ya Yanga ya kina Ally Bwamkuu kudaiwa kiasi fulani kikubwa cha pesa.Kila kitu kilikamilika kwa hatua hiyo kutekelezwa lakini hilo halikufanyika baada ya jopo la Wazanzibari kadhaa kutia timu Dar es Salaam na kuweka pingamizi dhidi ya hatua hiyo kwa sababu kulikuwa na mkono wa Wazanzibari kwenye ujenzi wa jengo hilo.Mnada haukuwepo na deni lililipwa kwa njia nyingine.
Monday, 19 April 2010
KARUME MWANZILISHI WA YANGA NA JINA LA SIMBA SPORTS CLUB
Na Ibrahim Mkamba
HISTORIA yetu katika mambo mengi imepotoshwa ama kwa makusudi au kwa bahati mbaya.Ni upotoshaji wa historia mtu anapoizungumzia klabu ya Young Africans maarufu kama Yanga bila kumzungumzia hayati Sheikh Abeid Aman Karume ambaye tangu atutoke kwa kupigwa risasi mwaka 1972, tarehe 7 mwezi huu na mwak huu ilitimia miaka 38 kamili.Ni upotoshaji wa historia mtu anapozungumzia jina la Simba Sports Club bila kumtaja Rais huyo wa kwanza wa Zanzibar na Makamu wa Kwanza, wa kwanza, wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Aidha,ni kosa kubwa kiimani na kimaadili mtu kuzipongeza klabu za Simba na Yanga kuwa na majengo yake bila kumhusisha kwa kiwango kikubwa hayati Karume.Kutomhusisha huko,kiimani ni dhambi ambapo kimaadili ni utovu mkubwa wa shukrani.Kwa maneno mengine,klabu za Yanga na Simba zilifanyiwa makubwa mno na hayati Karume kinyume cha jinsi historia inavyofanyiwa jitihada kwa Mwenyekiti huyo wa kwanza wa Baraza la Mapinduzi ya Zanzibar kutosikika sana ndani ya klabu hizo za soka zenye mashabiki wengi ndani ya Jamhuri nzima ya Muungano wa Tanzania.
Aliyoyafanya Karume kwa Yanga
Historia iliyoandikwa haielezi vizuri ukweli kwamba Sheikh Abeid Aman Karume alikuwa mhamasishaji mkubwa wa kuanzishwa kwa klabu ya soka ambayo sasa ndiyo hii inayoitwa Young Africans yaani Yanga.Baada ya kufanya kazi ya ubaharia iliyomuwezesha kuzunguka karibu dunia nzima kwa miaka kadhaa akiwa kijana mdogo, Karume alipata uzoefu wa yaliyotokea kwenye nchi mbalimbali alizozunguka duniani na kugundua kwamba serikali za kikoloni zilipiga vita uanzishwaji wa vyama vya siasa na wananchi wazawa lakini zilikuwa hazipingi vyama vya kijamii kama klabu za michezo.
Baada ya kuufahamu ukweli huo,akiwa nyumbani Zanzibar,Karume alijiunga na wenzake na kuunda klabu ya soka iliyojulikana kama African Sports Club,mwenyewe akiwa mchezaji mahiri wa timu ya klabu hiyo.Humo humo kwenye mikutano ya kisoka ndimo yeye na Wazanzibari wenzake walikuwa wakijadili jinsi ya kujinasua toka kwenye utawala wa kisultani uliokuwa ukilindwa na Waingereza.
Ni hayati Karume ndiye aliyehamasisha kuanzishwa kwa matawi ya hiyo African Sports ya Zanzibar na akafanikiwa kuanzishwa kwa tawi la timu hiyo jijini Dar es Salaam ambalo kwa sasa ndilo hii klabu kubwa sana ya Yanga na kule Tanga alifanikisha kuanzishwa kwa tawi jingine ambalo ni African Sports ya Tanga.Kumbuka kuwa kwenye miaka hiyo ya nyuma miji ya Dar es Salaam,Bagamoyo,Pangani na Tanga ilikuwa na ukaribu sana wa kimahusiano na miji ya visiwa vya Unguja na Pemba.
Baada ya kuanzishwa,timu hizo tatu za Yanga ya sasa,African Sports ya Zanzibar na African Sports ya Tanga zilitengeneza undugu wa damu mkubwa mno.Zote tatu zilikuwa chimbuko la hayati Karume ingawa historia haiuweki wazi ukweli huo.
Kwa Yanga pia, hayati Karume ndiye alitoa kiasi kikubwa cha pesa,kama siyo chote, mwaka 1971 kwa kufanikisha ujenzi wa jengo la makao makuu ya Yanga la sasa lililopo kwenye makutano ya mitaa ya Twiga na Jangwani,Kariakoo jijini Dar es Salaam.Alifanya hivyo kwa Yanga baada ya kushirikiana na wana Simba kupata jengo lao kwenye mtaa wa Msimbazi,Kariakoo,jijini Dar es Salaam mwaka huo 1971 kwa kuchangia kiasi cha pesa. Ki msingi,hayati Karume alishiriki kujenga majengo yote mawili ya klabu za Yanga na Simba ingawa historia iliyoandikwa haitaki kuuweka wazi ukweli huo.
Hivyo ndivyo hayati Karume alivyoifanyia klabu ya Yanga tangu kuanzishwa kwake mpaka kupata jengo la makao makuu yake.Ukitaka kuamini jinsi jengo la Yanga lilivyo na mahusiano na Wazanzibari,tangaza leo kupigwa kwake mnada,uone jinsi utakavyoshukiwa kwa hasira na Wazanzibari.Kama huamini,nitakukumbusha.Mwaka 1988 jengo hilo lilikuwa lipigwe mnada baada ya Yanga ya kina Ally Bwamkuu kudaiwa kiasi fulani kikubwa cha pesa.Kila kitu kilikamilika kwa hatua hiyo kutekelezwa lakini hilo halikufanyika baada ya jopo la Wazanzibari kadhaa kutia timu Dar es Salaam na kuweka pingamizi dhidi ya hatua hiyo kwa sababu kulikuwa na mkono wa Wazanzibari kwenye ujenzi wa jengo hilo.Mnada haukuwepo na deni lililipwa kwa njia nyingine.
