Ukweli mchungu kuhusu KINANA

Mleta uzi umetumwa kuja kumsafisha JANGILI ila kumbuka Chama Cha Majangili hamkubaliki tena ktk jamii.
Hata mfanye nini hakunj anayeweza kukubali Majangili na Chama chenu
 
mojawapo ya ukomavu wa kisiasa ni kuwa mtulivu,ustahimilivu,maono,kuthubutu na kuwa na maamuzi sahihi.sifa hizi kinana naona mungu amemjalia.
 
Siasa za kuchafuana zilizoibuka hivi karibuni hapa nchini zinazofanywa na vyama vya upinzani hazitaufikisha mbali upinzani

Hata mume wako mr dhaifu alisema kuwa ni vyama vya msimu lakini akisikia chadema anatetemeka ndio ukawe wewe mkewe?
 
Nadhani kwa bahati mbaya hujamwelewa mtoa mada. Kama wewe ni mchambuzi utaona kuwa anaijenga CDM kwa njia tofauti

Huku ni kujenga cdm bila kudhamiria. Inaingia akilini kulinganisha upinzani enzi za Mrema na huu wa sasa kweli?
 
Bado sijaelewa lengo la mleta uzi huu
Kwamba kinana ni mtu makini, hodari, ametumika na marais wote
Je, sifa hizo ndizo tunazotakiwa kuzizingatia na kuacha kuhoji kama kweli amehusika na ujangili wa tembo?

Hata hivyo nadhani kuna sifa moja mleta uzi ameisahau. Kinana ameongozoza kampeni za urais ambazo zote kura ziliibiwa kupindukia, wapiga kura walichakachuliwa sana, na matokeo mengi yalitangazwa kwa nguvu. Kampeni zote za uchaguzi alizoongoza alitekeleza mikakati yake iliyogawa wapiga kura kwa dini na makabila yao. Mtu wa sifa hizi mimi simuoni kama ni mtu makini.

Unaweza kuwa na akili sana kichwani lakini usiwe na utu moyoni. Pima vyote viwili, utu na akili
 
Tufike mahali tufikirie kama taifa, vizazi vijavyo vinategemea fikara zetu na namna ya kuyaendea mambo.
 
Tunachohitaji Watanzania ni mtu ambaye ataweza kuilinda katiba yetu na rasilimali zetu kwa manufaa yetu . Unadhani Kinana kwa nafasi yake anaweza kuisaidia Tanzania ikafikia hiyo ndoto ? Basi na atuonyeshe kwa muda huu mfupi uliobaki
 
Mleta uzi amekopy makala ya Kibanda wakati anaelekea kuondoka tanzania daima
 
Namkubali Mh Kinana, lakini Nape na Mwigulu wanamwaribia sana katika discipline ndani ya CCM.
 
Huku ni kujenga cdm bila kudhamiria. Inaingia akilini kulinganisha upinzani enzi za Mrema na huu wa sasa kweli?
Ni kosa kubwa maishani kumdharau adui. Hivyo mtoa mada alitaka kutueleza kuwa makini ili CDM kupata ushindi 2015. Kwa mfano mwepesi kabla ya mchezo wa watani wa jadi, Yanga ikitaka ushindi, basi Yanga inatakiwa kuwa makini na lolote lisemwalo hasa zuri kuhusu Simba kama inataka kupata ushindi. Vile vile Yanga inatakiwa kutoa taarifa potofu kuhusu yenyewe ili Simba ijisahau kuwa Yanga si lolote.
 
Tutaendelea kumbeza pamoja na ustaafu wake wa jeshi maana amechafuka, zamani enzi za Nyerere alikuwa mtu makini sana lakini sasa hana umakini wowote na hasa alipoingia kwenye genge la wezi wa rasilimali za nchi. Amepewa ukatibu mkuu kama shukrani za kumpigia kampeni JK na ndiyo maana anafanya anavyotaka kusafirisha nyara za serikali. Atakisaidia sana chama cha mapinduzi maana anachangia pesa nyingi kwenye chama. Ukitaka kujua kwamba Kinana si yule wa 2005 sikiliza hotuba yake ya mkutano wa Morogoro... Huwezi kuwa mtu makini ukiwa ndani ya CCM, muulize Samuel Sitta, Mwakyembe, Mama Kilango, Nape, Mwandosya watakuambia nini kilichomo ndani ya CCM. Hata wale ambao huwadhanii kabisa kwamba wanaweza kufanya madudu ukielezwa mambo wanayofanya hutaamini!! Endeleeni kumsifia Kinana.
Mmesahau mlivyomsifia Mkama kwamba alifanya mambo makubwa Dar akiwa Mkurugenzi wa jiji wengine wakasema sasa chama kimepata Jembe, akatoa na siku 90 wakiwa na Nnauye.... hovyoooo. Leo Kinana!!! poleni wapambe
 
Mleta uzi hata sijakuelewa kwa sababu hujaweza kutuonesha namna ambavyo uadilifu wake huo wa kuanzia miaka ya 1960's unaweza kumsafisha na matendo yake ya sasa ya ujangili kuua na kusafirisha meno ya tembo wetu ambayo sasa ndiyo agenda kuu inayomuhusu yeye kwa muda huu.We are talking about the present,what Kinana is doing now.Hiyo habari ya miaka ile haina maana sana kwetu sasa kwa sababu kama ulitenda mema milioni kadhaa kuanzia jana na ukatenda ovu baya leo hakika hilo baya moja pekee linafuta mema yote uliyotenda miaka milioni uliyoishi.Na hii ndiyo kanuni atakayotumia MUNGU MUUMBA WA BINGU NA NCHI kumhukumu kila aliye kiumbe wake

So, mimi sijaelewa hata kidogo uadilifu wa Kinana wa miaka yote leo unahalalisha kwa namna gani matendo yake maovu ya sasa....UJANGILI WA TEMBO WETU kwa sababu mleta uzi katika kila setensi aliyoandika hapo juu sijaona alipojaribu kusema usafi wa Kinana katika hujuma dhidi ya uchumi wa nchi yetu anazohusishwa nazo sasa zaidi ya hoja nyepesi sana za juujuu za kumtakasa kwa kutumia historia ambayo kwa namna yeyote hakuna mwenye tatizo na hilo hata kama kweli ndivyo alivyo.Nasema kwa sbb ni lazima tufahamu kwamba kwa sasa tuna-deal na kizazi cha dot.com.....vijana wengi wa kuanzia miaka ya 1980 to date ambao hiyo historia kwao si ishu wala hawana haja nayo...na hili maana yake ni kuwa hujaweza kumsaidia Kinana na CCM yake kuwa safi na free na uchafu alioubeba sasa ambao by any means kwa nafasi yake kama mtendaji mkuu wa chama kinachotawala na kinachosimamia serikali inayotekeleza sera ambazo zinamuathiri kila mmoja wetu,hakustahili kuwa na tuhuma kama hizi bila ya hatua za haraka,zilizowazi na zisizotia hata chembe ya shaka kuchukuliwa na chama chake kumsafisha ili aendelee kuaminika na umma!!.

Lakini kinachofanyika sasa ni upuuzi na kuwafanya watu wote ni wajinga hawawezi kuchanganua na kupima mambo katika mizani sawia ya weledi wa mambo.Wewe cheki hata kule ambako hili jambo limeibukia(bungeni) hakuna hata mmoja katika serikali au wabunge wa chama chake aliyesimama kwa kutumia kanuni za chombo(bunge) ili kuleta hoja thabiti chao ya kumtetea na kumkinga huyu bwana dhidi ya tuhuma zake ikiwa ni pamoja na kumtaka mtoa tuhuma kuleta ushahidi wa tuhuma.Lakini tulichokiona,tunachokiona sasa na tutakachoendelea kukiona baadaye ni taharuki na kejeli kuelekezwa kwa mtoa hoja na CHADEMA jambo ambalo kwa watu wanaofikiri kwa kutumia vichwa wanatambua mara moja kuwa nyoka kapigwa jiwe la kichwa sasa anatapatapa ili afe tu.
 
Nani ana mpuuza? Kama kauza pembe si kauza tu? Kwani shida iko wapi na huo umaarufu alionao?
 
Umejitahidi kumremba lakini mwisho wa siku mbivu na mbichi zitajulikana, uzoefu wake katika siasa tutaona utatusaidia vipi kujikwamua na umaskini ilionao Tanzania. Pia tutaona ni kwa namna gani atairudisha heshima ya CCM ambayo inaelekea kupotea kabisa hata kwa wanakijiji ambao walikua wanategemewa.
 
Teh teh teeh..! Kweli ukweli mchungu, mtachonga sana mwaka huu ila ukweli utabakia kuwa ukweli daima, Kinana ni jembe na ni pigo takatifu kwa upinzani..!

Nakubaliana na wewe kuwa hili ni pigo takatifu,lakini si kwa wapinzani bali kwa watanzania wote! kwa maliasili zetu zote, ni pigo takatifu kwa tembo wetu.
NAkubali pia kama Kinana ni mtu makini,madhubuti ,jasiri na hodari wa mipango na mikakati lakini je wajuwa kuwa wahalifu wananidhamu ya hali ya juu linapokuja suala la mambo yao?
In short uhodari na umakini unomnasibisha mtu huyu si wa kuijenga nchi yetu bali kuiangamiza usinitake nikupe ushahidi kwani kwa uhodari wao ushahidi sina ,kutokana na umahiri wao k sina uwezo wa kuwazuia,kutokana na umakini wao sina uwezo wa kuwatia hatiani ,kutokana na mikakati yao sina uwezo wa kuondoa ulindanaji wao .
LAKINI kutokana na uwezo mkubwa wa KISANDUKU CHA KURA 2015 UWEZO WANGU UTAKUWA MKUBWA KUYASHINDA YOTE HAYO TUSUBIRI!
 
Jana nilimsikia kijana moja wa Lumumba akilalamika buku saba yake aijaingizwa kwa Mpesa. Wanajitaidi sana kuosha kinyesi Nape hawa vijana walipeni kwa wakati kwani wanaumia sana hasa kwa hili sakata. Hawa vijana wa UVCCM awalali kwa sasa. Usiku mchana wanashinda kwenye mitandao
 
Wanaompuuza kinana ni mambumbu wa kufikiri,na hiyo ndio hulka ya atanzania na kwanini msigwa asipeleke ushahidi huo kwenye vyombo vya dola ni kutaka kujichukulia ujiko kwa wajinga wasio weza kufikiri, apeleke kama ulivyopelekwa wa lwakatare??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…