Ukweli Mchungu: Serikali Haiwezi Kuendesha SGR Kwa Watanzania Tuliopo. Tujifunze Kutoka Kwenye Mwendokasi

Ukweli Mchungu: Serikali Haiwezi Kuendesha SGR Kwa Watanzania Tuliopo. Tujifunze Kutoka Kwenye Mwendokasi

Hii miradi inaweza kuendeshwa kwa faida lakini si na serikali ya CCM

Ttcl, sgr, mwendo kasi, bandari, hii yote inaweza kuwa ya faida sana lakini si kwa akili hizi za maccm yanayowaza upigaji kwenye kila mradi
Na hapo bado wamiliki wa mabasi ambao wengi ni Makada wa chama awajaanza fitina za kuifitini treni ya mwendo kasi.
 
Unaelewa maana ya kampuni tanzu?
Unadhani nikijibu hilo swali litafuta ujinga wako? Kwa hiyo Rais wa JMT siku hizi anateua ma CEO wa Sekta Binafsi
Screenshot_20240615_084031_Chrome.jpg
 
SGR inatakiwa kufika Mwanza na Kigoma haraka na kusafirisha mizigo ya nchi jirani kwa haraka na tuanze kuchota pesa za majirani na kuua uchumi wa Kenya hizo ndio zilikuwa ndoto za Magu , hii ya kutubeba abiria ni ziada tu ya SGR sasa mwenyewe kaenda mbwembwe kama zote.

Inapaswa mkubwa aambiwe tukope bila hofu SGR imalizwe haraka kujengwa ifike Mwanza na Kigoma kwakuwa ni reli ya kimkakati kubeba mizigo ndio lengo mama na kuifanya bongo kama Ulaya yaani donor country. Yule mwamba hakunaga!he had royal dreams ambazo Mama amezielewa,amezibeba na anazitekeleza kwa nguvu zote !

Mbwembwe za kubeba abiria kwa buku teni hazitalipa mkopo na kwa maana hiyo tozo tulizochoka za mwanayanga zitaendelea kutudidimiza kwenye umaskini. Wakumbuke duniani tunapita tu

Mama ameweza, maua mengi kwake, Mama mitano mingine!
82% ya shehena za Mizigo zinazohudumiwa na Bandari ya Dar es Salaam kwa ajili ya Nchi jirani zinakwenda/kutoka Nchi 3 tu. Nazo ni JK Kongo, Zambia na Rwanda. Jumla ya Tani 8.2M zilipita Bandari ya Dar kwenda/kutoka Nchi jirani - DRC 3.4M- Zambia 2M- Rwanda 1.5M Shehena za Mizigo ya Nchi jirani kupitia Bandari zetu imekua kwa 28%
Screenshot_20240615_085129_Instagram.jpg
Screenshot_20240615_085218_Chrome.jpg


Sijui huyo mnayemuita Shujaa au sijui mbeba maono alikuwa anatumia vigezo gani katika kuamua SGR iende Mwanza.
 
View attachment 3017687
Mbona barabarani kuna makampuni kibao,
Makampuni kwenye SGR yawe mengi, yalipe tu kiwango fulani serikalini kisha yapige kazi.

View attachment 3017688

Tumeona kinachoendelea kwenye Mwendokasi ni aibu tu na mateso kwa abiria. Tusikubali SGR ifike huko. BINAFSISHA mara MOJA kama anavyosema Waziri Mbarawa
Ikibinafsishwa nauli utaiweza,juzi tu hapa nauli zimetangazwa watu mmepiga kelele nauli zipunguzwe,na mfanyabiashara yeye siku zote anaangalia faida,wacha tu serikali iendeshe na sisi wengine huku Kidugalo tufaidi...
 
Ikibinafsishwa nauli utaiweza,juzi tu hapa nauli zimetangazwa watu mmepiga kelele nauli zipunguzwe,na mfanyabiashara yeye siku zote anaangalia faida,wacha tu serikali iendeshe na sisi wengine huku Kidugalo tufaidi...
Kuna namna nyingi ya ku subsidise nauli kwa raise tozo mbali mbali kwenye huduma. Sioni kama hiyo ni issue kubwa
 
Mnapoanza kufikiria wazawa au wageni kwenye biashara mnakosea. Hili ni soko huria, muache mwenye mtaji wake aje ashindanishwe kutoka popote
Tatizo hapa bongo tunawapa kipaumbele wageni kuliko wazawa
 
Mbona barabarani kuna makampuni kibao, Makampuni kwenye SGR yawe mengi, yalipe tu kiwango fulani serikalini kisha yapige kazi.
Barabarani kuna uwezekano wa gari kupita muda wowote, wala haupangiwi muda wa kuanza safari. Treni zinategemea njia moja, kupishana hadi kituo maalum, yaani treni moja ikae isubiri hadi nyingine ipite ndio iendelee na safari. Kwa mtindo huo hakutakuwa na uokoaji wa muda, maana Dar-Morogoro inaweza ikachukua masaa matano
 
Hii miradi inaweza kuendeshwa kwa faida lakini si na serikali ya CCM

Ttcl, sgr, mwendo kasi, bandari, hii yote inaweza kuwa ya faida sana lakini si kwa akili hizi za maccm yanayowaza upigaji kwenye kila mradi
Na hapo bado wamiliki wa mabasi ambao wengi ni Makada wa chama awajaanza fitina za kuifitini treni ya mwendo kasi.
Mtu hajawahi kumili duka kama la Mangi ni Mkurugenzi Au Mwenyekiti wa shirika lenye thamani ya Matrilioni ya fedha,Mtu alizaliwa kabla ya kompyuta(bc)na anologia ni boss wa digital coy na madigitali,kampuni imejaa madigitali wenye umri chini 50 ila kiongozi wao ana miaka zaidi 75,si atapigwa,tuajiri watanzania wenye uwezo kielimu na kiujuzi wako wengi,pia naikubali hiyo speech ya Waziri hapo
 
Lini serikali ilitangaza tenda wakashinda UDART ?


ALIEKWAMBIA MWENDO KASI INAENDESHWA NA SERIKALI 100% NI NANI? UDART SIO SERIKALI NDUGU NI KAMPUNI TANZU, NDIO MAANA MABASI YAO HAYANA PLATE NUMBER YA SU, NA KODI YA IMPORTATION WANALIPA
 
Swala sio vilaza Bali Mwendazake Alikurupuka,wrong timing and decion na mara nyingi watu wasio na akili hukombilia hizi structures Ili kuwapumbaza mbulula.

Reli zote Duniani hujengwa kuliwa na uhitaji wa kiuchumi na sio vinginevyo

Mwisho tunaenda kujenga expressway ya kulipia Dom-Dar kabla ya 2030 itakuwa tayari nani atapanda hiyo treni yenu hususani VIP? Mtu ataona Bora alipie toll kwenye Barabara ajiachie na km 120-200/hr.
Inasikitisha sana. Ina maana sasa imeshakubalika kuwa serikali haitakuwa tena na uwiano katika mipango ya kitaifa maendeleo (national integrated development planning)? Serikali ya CCM imejenga SGR kwa gharama kubwa sana inayojumuisha mass passenger transportation component. Halafu serikali hiyo hiyo inapanga kutumia gharama kubwa tena kujenga expressway kwenye corridor hiyo hiyo kama vile hii ni nchi yenye uchumi wa dunia ya kwanza! Inahitaji miundombinu shindani kuwapa raia wake “wide choice”! Tena kwa mikopo zaidi!

What’s going on? Umuhimu wa kugawa pesa za umma za maendeleo kwa sekta mbali mbali kwa uwiano sahihi umetupiliwa mbali? Sasa kila Rais anataka kufanya “miradi yake” kuwapiku wenzake wa awamu zingine? Yaani, tunakubaliana na wajinga/wapumbavu waliozuka na kutamalaki miaka hii wanaofikiri Rais bora ni yule “mwenye maono; anayebuni miradi ya ‘kimkakati’”?

Halafu hayo mahangaiko ya kutaka SGR ionekane ikisafirisha abiria ni ujinga mwingine usioelezeka. Taaluma zimetupiliwa mbali enzi hizi! Watu hawajiulizi ilikuwaje reli zetu za awali za TRC na TAZARA zikafikia hapo zilipo? Bahati mbaya hakuna documentary clip ya TAZARA watu waone ilivyokuwa wakati TAZARA inazinduliwa ikiwa brand new na kila kitu kimekamilika.

Kiuchumi, gharama ya kuendesha treni ni kubwa sana inaweza kufidiwa tu na kiwango kikubwa cha usafirishaji mizigo mizito (bulky) kwa umbali mrefu (=>1000km). Vinginevyo, inabidi abiria watozwe nauli kubwa sana kufidia gharama za uendeshaji na faida kidogo. Tanzania miaka yote gharama za safari za treni ya abiria (TRC/TZR) zimekuwa zikifidiwa (subsidised) na safari za treni ya mizigo. Ulaya waliachana na mchezo wa cross-subsidisation miaka mingi tu. Nauli za abiria katika treni ni ghali kuliko za mabasi.

Baada ya mageuzi makubwa ya kiuchumi yaliyochagizwa na IMF na Benki ya Dunia, makampuni binafsi ya malori yalivamia soko ndio ikawa mwanzo wa kudorora kwa TRC na TZR. Hakuna hatua za kisera zilizochukuliwa kubadilisha hali hiyo. Lakini viongozi wetu wamekimbilia kumwaga matrilioni ya mikopo kujenga SGR. (Sijui kama feasibility study ilifanyika). Sasa hao wanasiasa na wananchi wanaona raha kuanza kupanda treni kwenda Morogoro na Dodoma bila kujiuliza hatma ya huo mradi!

Ni hasara sana kwa nchi kama Tanzania kutekeleza mipango yake kwa propaganda za kisiasa badala ya uhalisia wa vigezo vya uchumi. It’s just a matter of time, the reality will finally settle on the SGR and ATCL, the most amazing follies that I know and still wondering at.
 
View attachment 3017687
Mbona barabarani kuna makampuni kibao,
Makampuni kwenye SGR yawe mengi, yalipe tu kiwango fulani serikalini kisha yapige kazi.

View attachment 3017688

Tumeona kinachoendelea kwenye Mwendokasi ni aibu tu na mateso kwa abiria. Tusikubali SGR ifike huko. BINAFSISHA mara MOJA kama anavyosema Waziri Mbarawa
Serikali haijawahi kufanikiwa kwenye mradi wowote kuanzia ndege,mwendokasi,madini,gesi,treni,meli,uvuvi,utalii nk. nk.

Huu niuthibitisho kuwa viongozi wajuu serikalini hawana uwezo,ujuzi wala maarifa katika kusimamia miradi na kuipeleka nchi mbele.

Kimsingi serikali yetu inatumia pesa nyingi mmmno kutufanyia kazi ndooogo sana ndomana ikipewa miradi yoote inafilisika!!

Mfano Ikulu ingepewa mradi uuendeshe ili kupata mapato ya kujihudumia ninauhakika ikulu ingegeuka gofu chakavu na watumishi wake wangelala njaa...
Nivile inajiendesha Kwa kodizetu na wanazila bila kujali maana hawana uchungu nazo
Tizama raisi anasafiri kilaleo Tena saanyingine anasafiri na wasanii ughaibuni bila kujali gharama kuubwa bila tija kwakuwa hawazitafuti pesa wanazichota tuu!!!

Kila taasisi(wizara) ya serikali ingekabidhiwa mradi mmoja kama chanzochake pekee cha pesa za matumizi na kodizetu zikatumika tuu kwa huduma nyingine kunaviongozi/mawaziri wangekondeana, wangevaa viraka na kuendesha baiskeli chakavuu.
Narudia Tena "Hatuna viongozi wenye uhodari wowote labda wakuvaa masuti na kumsifu alowapa kulayao".
TURUDI KWENYE ELIMU YETU...
Hakuna tunachoweza,majibu kamili mtapata baada ya uchaguzi wa 2025 yaani ripoti ya CAG #2026.

Hii ni miradi cosmetics ya kufurahisha wajinga ila itaendelea kula Kodi na Kodi kuiendesha.
"Let us agreed that Blacks cannot rule themselves, Whites are born in order to rule and Blacks are born to be ruled."

Pieter W. Botha, a former President of South Africa during the Apartheid era
 
Kwa njaa hizi kila kitu kitahribika ndani ya miezi 3 tu. Hao wahudumu walipatioanaje? Kwanza tuanzie hapo.
 
"Let us agreed that Blacks cannot rule themselves, Whites are born in order to rule and Blacks are born to be ruled."

Pieter W. Botha, a former President of South Africa during the Apartheid era
Sometimes we have to swallow the bitter pill
 
"Let us agreed that Blacks cannot rule themselves, Whites are born in order to rule and Blacks are born to be ruled."

Pieter W. Botha, a former President of South Africa during the Apartheid era
Kuna kitu kinaitwa "subjective"na kingine kinaitwa "objective"Sasa sisi Waafrika wengi tunatenda tunavyofikiri inafaa na si kwa kufuata taaluma inavyotaka,Kanuni,Sheria nataka kusema mengi ni "utopian na mengi ni morriband".
 
Back
Top Bottom