Ukweli Mchungu: Serikali Haiwezi Kuendesha SGR Kwa Watanzania Tuliopo. Tujifunze Kutoka Kwenye Mwendokasi

Hii miradi inaweza kuendeshwa kwa faida lakini si na serikali ya CCM

Ttcl, sgr, mwendo kasi, bandari, hii yote inaweza kuwa ya faida sana lakini si kwa akili hizi za maccm yanayowaza upigaji kwenye kila mradi
Na hapo bado wamiliki wa mabasi ambao wengi ni Makada wa chama awajaanza fitina za kuifitini treni ya mwendo kasi.
 
82% ya shehena za Mizigo zinazohudumiwa na Bandari ya Dar es Salaam kwa ajili ya Nchi jirani zinakwenda/kutoka Nchi 3 tu. Nazo ni JK Kongo, Zambia na Rwanda. Jumla ya Tani 8.2M zilipita Bandari ya Dar kwenda/kutoka Nchi jirani - DRC 3.4M- Zambia 2M- Rwanda 1.5M Shehena za Mizigo ya Nchi jirani kupitia Bandari zetu imekua kwa 28%


Sijui huyo mnayemuita Shujaa au sijui mbeba maono alikuwa anatumia vigezo gani katika kuamua SGR iende Mwanza.
 
Ikibinafsishwa nauli utaiweza,juzi tu hapa nauli zimetangazwa watu mmepiga kelele nauli zipunguzwe,na mfanyabiashara yeye siku zote anaangalia faida,wacha tu serikali iendeshe na sisi wengine huku Kidugalo tufaidi...
 
Ikibinafsishwa nauli utaiweza,juzi tu hapa nauli zimetangazwa watu mmepiga kelele nauli zipunguzwe,na mfanyabiashara yeye siku zote anaangalia faida,wacha tu serikali iendeshe na sisi wengine huku Kidugalo tufaidi...
Kuna namna nyingi ya ku subsidise nauli kwa raise tozo mbali mbali kwenye huduma. Sioni kama hiyo ni issue kubwa
 
Na swali watawekeza wazawa au?
Mnapoanza kufikiria wazawa au wageni kwenye biashara mnakosea. Hili ni soko huria, muache mwenye mtaji wake aje ashindanishwe kutoka popote
 
Mnapoanza kufikiria wazawa au wageni kwenye biashara mnakosea. Hili ni soko huria, muache mwenye mtaji wake aje ashindanishwe kutoka popote
Tatizo hapa bongo tunawapa kipaumbele wageni kuliko wazawa
 
Mbona barabarani kuna makampuni kibao, Makampuni kwenye SGR yawe mengi, yalipe tu kiwango fulani serikalini kisha yapige kazi.
Barabarani kuna uwezekano wa gari kupita muda wowote, wala haupangiwi muda wa kuanza safari. Treni zinategemea njia moja, kupishana hadi kituo maalum, yaani treni moja ikae isubiri hadi nyingine ipite ndio iendelee na safari. Kwa mtindo huo hakutakuwa na uokoaji wa muda, maana Dar-Morogoro inaweza ikachukua masaa matano
 
Mtu hajawahi kumili duka kama la Mangi ni Mkurugenzi Au Mwenyekiti wa shirika lenye thamani ya Matrilioni ya fedha,Mtu alizaliwa kabla ya kompyuta(bc)na anologia ni boss wa digital coy na madigitali,kampuni imejaa madigitali wenye umri chini 50 ila kiongozi wao ana miaka zaidi 75,si atapigwa,tuajiri watanzania wenye uwezo kielimu na kiujuzi wako wengi,pia naikubali hiyo speech ya Waziri hapo
 
Lini serikali ilitangaza tenda wakashinda UDART ?


ALIEKWAMBIA MWENDO KASI INAENDESHWA NA SERIKALI 100% NI NANI? UDART SIO SERIKALI NDUGU NI KAMPUNI TANZU, NDIO MAANA MABASI YAO HAYANA PLATE NUMBER YA SU, NA KODI YA IMPORTATION WANALIPA
 
Inasikitisha sana. Ina maana sasa imeshakubalika kuwa serikali haitakuwa tena na uwiano katika mipango ya kitaifa maendeleo (national integrated development planning)? Serikali ya CCM imejenga SGR kwa gharama kubwa sana inayojumuisha mass passenger transportation component. Halafu serikali hiyo hiyo inapanga kutumia gharama kubwa tena kujenga expressway kwenye corridor hiyo hiyo kama vile hii ni nchi yenye uchumi wa dunia ya kwanza! Inahitaji miundombinu shindani kuwapa raia wake “wide choice”! Tena kwa mikopo zaidi!

What’s going on? Umuhimu wa kugawa pesa za umma za maendeleo kwa sekta mbali mbali kwa uwiano sahihi umetupiliwa mbali? Sasa kila Rais anataka kufanya “miradi yake” kuwapiku wenzake wa awamu zingine? Yaani, tunakubaliana na wajinga/wapumbavu waliozuka na kutamalaki miaka hii wanaofikiri Rais bora ni yule “mwenye maono; anayebuni miradi ya ‘kimkakati’”?

Halafu hayo mahangaiko ya kutaka SGR ionekane ikisafirisha abiria ni ujinga mwingine usioelezeka. Taaluma zimetupiliwa mbali enzi hizi! Watu hawajiulizi ilikuwaje reli zetu za awali za TRC na TAZARA zikafikia hapo zilipo? Bahati mbaya hakuna documentary clip ya TAZARA watu waone ilivyokuwa wakati TAZARA inazinduliwa ikiwa brand new na kila kitu kimekamilika.

Kiuchumi, gharama ya kuendesha treni ni kubwa sana inaweza kufidiwa tu na kiwango kikubwa cha usafirishaji mizigo mizito (bulky) kwa umbali mrefu (=>1000km). Vinginevyo, inabidi abiria watozwe nauli kubwa sana kufidia gharama za uendeshaji na faida kidogo. Tanzania miaka yote gharama za safari za treni ya abiria (TRC/TZR) zimekuwa zikifidiwa (subsidised) na safari za treni ya mizigo. Ulaya waliachana na mchezo wa cross-subsidisation miaka mingi tu. Nauli za abiria katika treni ni ghali kuliko za mabasi.

Baada ya mageuzi makubwa ya kiuchumi yaliyochagizwa na IMF na Benki ya Dunia, makampuni binafsi ya malori yalivamia soko ndio ikawa mwanzo wa kudorora kwa TRC na TZR. Hakuna hatua za kisera zilizochukuliwa kubadilisha hali hiyo. Lakini viongozi wetu wamekimbilia kumwaga matrilioni ya mikopo kujenga SGR. (Sijui kama feasibility study ilifanyika). Sasa hao wanasiasa na wananchi wanaona raha kuanza kupanda treni kwenda Morogoro na Dodoma bila kujiuliza hatma ya huo mradi!

Ni hasara sana kwa nchi kama Tanzania kutekeleza mipango yake kwa propaganda za kisiasa badala ya uhalisia wa vigezo vya uchumi. It’s just a matter of time, the reality will finally settle on the SGR and ATCL, the most amazing follies that I know and still wondering at.
 
Hakuna tunachoweza,majibu kamili mtapata baada ya uchaguzi wa 2025 yaani ripoti ya CAG #2026.

Hii ni miradi cosmetics ya kufurahisha wajinga ila itaendelea kula Kodi na Kodi kuiendesha.
"Let us agreed that Blacks cannot rule themselves, Whites are born in order to rule and Blacks are born to be ruled."

Pieter W. Botha, a former President of South Africa during the Apartheid era
 
Kwa njaa hizi kila kitu kitahribika ndani ya miezi 3 tu. Hao wahudumu walipatioanaje? Kwanza tuanzie hapo.
 
"Let us agreed that Blacks cannot rule themselves, Whites are born in order to rule and Blacks are born to be ruled."

Pieter W. Botha, a former President of South Africa during the Apartheid era
Sometimes we have to swallow the bitter pill
 
"Let us agreed that Blacks cannot rule themselves, Whites are born in order to rule and Blacks are born to be ruled."

Pieter W. Botha, a former President of South Africa during the Apartheid era
Kuna kitu kinaitwa "subjective"na kingine kinaitwa "objective"Sasa sisi Waafrika wengi tunatenda tunavyofikiri inafaa na si kwa kufuata taaluma inavyotaka,Kanuni,Sheria nataka kusema mengi ni "utopian na mengi ni morriband".
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…