Ukweli mchungu: Zanzibar tunaishi kwa kudra za Tanganyika!

Ukweli mchungu: Zanzibar tunaishi kwa kudra za Tanganyika!

Kwamba tukikopa nje tunawapa 4% ya pesa za mikopo anadai sio sawa,
Hayo ya Zitto ni porojo..

Halafu inapokuja suala la kulipa mikopo Tanganyika pekee ndo hulipa. Fikiria itakuwaje kama Znz wakitakiwa walipe mikopo yote waliyowahi kupokea kupitia Tanganyika, si visiwa vitapigwa mnada?!

Kumbuka pia kuna mikopo huwa inakopwa na Tanganyika kwa ajili ya Znz tuu, ingawa hata hii mlipaji ni Tanganyika pekee
 
Wanasem Wazenji kwamba wakipewa uhuru wao, watawaita Waarabu wa Dubai na Oman wapabadirishe hapo pawe kama Dubai...

Sasa akili zao zilivyo fupi, chakula kinatoka Bara.. na Wazenji wengi hawana kazi za maana nikimaanisha hakuna mzunguko wa hela unaoeleweka ukiweka pembeni shughuli za Utalii na Uvuvi.

Mazao yao hayo ya karafuu, mwani etc havitoshi kuingiza kipato kwa mtu mmoja mmoja.

Ikumbukwe karibu nusu yao wapo huku Bara.. wakipewa uhuru wao na sisi tunawatimua huku warudi kwao hivyo overpopulation itakuwepo na ufinyu wa resources lazima uzidi kuwadidimiza.

I wish siku ifike kila mtu abebe chake.
Dubai ni Dubai tu na ZNZ itabakia ZNZ. Kwanza ZNZ ikitolewa kwenye Muungano tambua kuwa nayo itakufa na kuzaa Pemba na Unguja.

Ni rahisi kuwa na Muungano wa Tanzania na ZNZ kuliko muungano wa Pemba na Unguja. Tofauti za kihistoria za hivi visiwa viwili inamezwa na Muungano. Watagawana mbao halafu baada ya hapo tutaanza kubeba mzigo wa UNHCR kama inavyotokea Kigoma na ngara kwa kambi za wahutu na watusi kutoka Burundi/ Rwanda
 
Hayo ya Zitto ni porojo..

Halafu inapokuja suala la kulipa mikopo Tanganyika pekee ndo hulipa. Fikiria itakuwaje kama Znz wakitakiwa walipe mikopo yote waliyowahi kupokea, si visiwa vitapigwa mnada?!

Kumbuka pia kuna mikopo huwa inakopwa na Tanganyika kwa ajili ya Znz tuu, ingawa hata hii mlipaji ni Tanganyika pekee
Wazanzibari wanaojielewa hawataki huu muungano uvunjike, wachache wasiojitambua wanalia na kulalama kwa kusema wanaminywa, ukiwauliza wanaminywa wapi hawajui na hawasemi...

Mfano leo hii muungano ufe

1. Hawana jeshi imara la ulinzi na usalama, sababu 80% jeshi hili kiutawala limebase bara kuliko visiwani... Hapa watahangaika sana, na ndio utakuwa mwanya kwa wasiotaka amani huko kuleta vurugu

2. Hawana uchumi imara wa kusema wanaweza kujitegemea na mambo yakaenda, watalazimika kuingiza wahisani wengi visiwani + madeni + kugawa visiwa kwa kisingizio cha uwekezaji, matokeo yake kuwa na madeni mazito kisha kuwa taifa tegemezi kwa kiasi kikubwa

3. Hawana ardhi ya kilimo cha kutosheleza, chakula kwa kiasi kikubwa kinatoka nje ya Zanzibar, vinaingia kutoka bara na nchi nyingine, so vyovyote vile ndani ya muda mchache kutatokea mfumuko wa bei na kusababisha hali ngumu ya maisha

4. kunawezekana kukawepo kundi la watu/wafanya biashara/viongozi linasubiri wazanzibari wajichanganye wafuate mihemko ya kuvunja muungano kisha kuwe na kukomoana, cha huku ni cha huku na cha huko ni cha huko...

Watu watafakari kabla ya kutaka kuvunja Muungano wasije kuja kujuta hapo baadae... Hasa wazanzibari mjitafakari sana
 
Nakwambia hivi, Tanganyika kwa sasa ndio inatusitiri sisi wazanzibar. Bila Tanganyika hatuna ulinzi, usalama wala umeme.

Karafuu iliyokuwa inatupa jeuri ilishakufa kitambo sana, na kwa uvivu wetu tumeshindwa kuifufua, na sasa tunasikia huko Tanganyika mlishaanza kuotesha na kuvuna karafuu yenu kwa fujo.....

Bandari ya Zanzibar iko mahututi maana kila jirani yetu (Beira, Mombasa, Comoro, Eritrea, Djibout, Dar, Mtwara, Tanga) alisha imarisha bandari yake, Zanzibar hatuna tena upekee wa kibandari....

Zanzibar tumebakia na Utalii pekee yake (ambao ni wa msimu, na watalii wenyewe wengi huanzia bara au kumalizia bara maana huko wako huru kuvaa chochote, kula mwaka mzima (huku kula hadharani kipindi cha Ramandan ni mwiko!), kula chochote (hata kitimoto), kunywa chochote(pombe), hapa Zanzibar watalii wanapita kwa siku zisizozidi tatu (kushangaa mchanga mweupe wa beach ambao umegundulika umejaa vilivyo kule Tanganyika (Kigamboni), kutafuna machoko wakizenji na kubwia unga kwa uhuru kisha kusepa zao). Bahati mbaya sana na huo utalii pekee hautoshi kuendesha maisha ya wazanzibar zaidi ya 1.5milioni kwa siku zaidi ya 90.

Yote kwa yote, mmasai ameshaingia Zanzibar na sasa anataka kutawala utaliii wote.

Nasema hivi, Zanzibar bila Tanganyika twafaa!
Mtanganyika anatujali mnooo.
"kutafuna machoko wakizenji na kubwia unga kwa uhuru kisha kusepa zao"

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]aisee wakikukamata[emoji23][emoji23][emoji1787][emoji1787]
 
Kumtegemea binadamu ni dhambi
Mimi naamini mtaishi na mnaweza kuwa mbali sana kwa kujitegemea wenyewe
Hata huku tunaishi kwa kudra za Mungu tu kupitia kwa wazungu na misaada yao
 
Back
Top Bottom