Ukweli na Uwongo upi hudumisha ndoa? Au vyote?

Ukweli na Uwongo upi hudumisha ndoa? Au vyote?

Hmaster

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2010
Posts
346
Reaction score
86
Juzi nilikuwa maeneo ya Ubungo ambapo nilikutana na dada furani akiwa na watoto wa2 na mizigo kadhaa na baada ya kusalimiana aliniomba nauli ya daladala ili aende Tegeta kwa dada yake kwani alikuwa ameibiwa pochi yake ambayo ilikuwa na pesa akiwa safarini kutokea Songea. Mimi kwa vile nilikuwa na gari na kwa namna alivyoonyesha huzuni niliona bora nimchukue tu kwenye gari yangu hadi Tegeta kisha nikarudi hadi Magomeni ninapoishi. Kwa sababu ya foleni nyingi na muda ulipita sana kabla ya kurudi home, hata hivyo my wife wangu nilimweleza kila kitu lakini badala ya kuona umuhimu wa mimi kumsaidia mwanamke mwenzake yeye alikwenda mbali zaidi na aliamua kukata simu na hakupatikana hadi nafika home. Baada ya kufika nikamkuta tayari yupo kitandani akiwa na nguo zake zote, eti ndo keshakasirika na kuamua kulala hiyo saa tatu na wakati huwa tunalala hata saa 5 kila siku. Nilipojaribu kumwamsha ili aniandalie chakula alinijibu niende kula kwa malaya niliyemsindikiza Tegeta. Nilijitahidi kumwelewesha lakini ilishindikana. Nikajiandalia chakula mwenyewe, nikaoga na kisha kulala kwa maana kwa hali hiyo hata kumchombeza sikuweza. Sasa swali ni je Ukweli na Uwongo upi hudumisha ndoa, au vyote? Wenye experince na mambo haya waweke hapa maana sasa najiandaa kuwa mwongo kwa vile ukweli umenitokea puani. Na kama wanawake humu jf watueleze wenyewe kipi wanataka kutoka kwetu kati ya hivyo vitatu ili wawe na amani. Nawasilisha!
 
Juzi nilikuwa maeneo ya Ubungo ambapo nilikutana na dada furani akiwa na watoto wa2 na mizigo kadhaa na baada ya kusalimiana aliniomba nauli ya daladala ili aende Tegeta kwa dada yake kwani alikuwa ameibiwa pochi yake ambayo ilikuwa na pesa akiwa safarini kutokea Songea. Mimi kwa vile nilikuwa na gari na kwa namna alivyoonyesha huzuni niliona bora nimchukue tu kwenye gari yangu hadi Tegeta kisha nikarudi hadi Magomeni ninapoishi. Kwa sababu ya foleni nyingi na muda ulipita sana kabla ya kurudi home, hata hivyo my wife wangu nilimweleza kila kitu lakini badala ya kuona umuhimu wa mimi kumsaidia mwanamke mwenzake yeye alikwenda mbali zaidi na aliamua kukata simu na hakupatikana hadi nafika home. Baada ya kufika nikamkuta tayari yupo kitandani akiwa na nguo zake zote, eti ndo keshakasirika na kuamua kulala hiyo saa tatu na wakati huwa tunalala hata saa 5 kila siku. Nilipojaribu kumwamsha ili aniandalie chakula alinijibu niende kula kwa malaya niliyemsindikiza Tegeta. Nilijitahidi kumwelewesha lakini ilishindikana. Nikajiandalia chakula mwenyewe, nikaoga na kisha kulala kwa maana kwa hali hiyo hata kumchombeza sikuweza. Sasa swali ni je Ukweli na Uwongo upi hudumisha ndoa, au vyote? Wenye experince na mambo haya waweke hapa maana sasa najiandaa kuwa mwongo kwa vile ukweli umenitokea puani. Na kama wanawake humu jf watueleze wenyewe kipi wanataka kutoka kwetu kati ya hivyo vitatu ili wawe na amani. Nawasilisha!

Mhhh! pole sana Mkuu kwa kesi yako hii labda ungesema uongo kwa mfano gari lilikuharibikia usingeweza kujibiwa majibu hayo ambayo yangeweza kabisa kuongeza purukushani ndani ya nyumba. Hongera sana kwa moyo wako wa huruma.
 
Hapa i see nimekosa la kusema...heri nikae kimya

Wewe kama mdada mwenye uzoefu wa ndoa miaka mi4 sasa tunahitaji sana mchango wako hapa ili na sisi ambao hatujaoa tujue tuseme nini likitutokea ili mtuelewe akina dada. Tafadhali FL1, usifiche hekima zako hapa, tunawapenda sana na tunataka tuwaelewe vizuri
 
Hapa i see nimekosa la kusema...heri nikae kimya

sema tu usiogope.........
ni kweli kwamba kila sekunde,kila dakika tuseme ukweli,
je kwa kusema uongo japo kiduchu tu pale inapobidi, si unaweza jikuta umesalimisha mambo mengi ya hatari?

....ila UWONGO hata mungu hapendi ...lol...
 
Inawezekana umezoea kutumia staili hiyo hiyo kumdanganya kiasi kwamba hata unaposema ukweli anakuwa hakuamini. Vinginevyo Hongera kwa moyo wa huruma uliuonyesha
 
Siku hizi uongo ndo ukweli na ukweli ndo uongo kwa hiyo kwenye ukweli unareplace uongo na penye uongo unareplace ukweli
 
Juzi nilikuwa maeneo ya Ubungo ambapo nilikutana na dada furani akiwa na watoto wa2 na mizigo kadhaa na baada ya kusalimiana aliniomba nauli ya daladala ili aende Tegeta kwa dada yake kwani alikuwa ameibiwa pochi yake ambayo ilikuwa na pesa akiwa safarini kutokea Songea. Mimi kwa vile nilikuwa na gari na kwa namna alivyoonyesha huzuni niliona bora nimchukue tu kwenye gari yangu hadi Tegeta kisha nikarudi hadi Magomeni ninapoishi. Kwa sababu ya foleni nyingi na muda ulipita sana kabla ya kurudi home, hata hivyo my wife wangu nilimweleza kila kitu lakini badala ya kuona umuhimu wa mimi kumsaidia mwanamke mwenzake yeye alikwenda mbali zaidi na aliamua kukata simu na hakupatikana hadi nafika home. Baada ya kufika nikamkuta tayari yupo kitandani akiwa na nguo zake zote, eti ndo keshakasirika na kuamua kulala hiyo saa tatu na wakati huwa tunalala hata saa 5 kila siku. Nilipojaribu kumwamsha ili aniandalie chakula alinijibu niende kula kwa malaya niliyemsindikiza Tegeta. Nilijitahidi kumwelewesha lakini ilishindikana. Nikajiandalia chakula mwenyewe, nikaoga na kisha kulala kwa maana kwa hali hiyo hata kumchombeza sikuweza. Sasa swali ni je Ukweli na Uwongo upi hudumisha ndoa, au vyote? Wenye experince na mambo haya waweke hapa maana sasa najiandaa kuwa mwongo kwa vile ukweli umenitokea puani. Na kama wanawake humu jf watueleze wenyewe kipi wanataka kutoka kwetu kati ya hivyo vitatu ili wawe na amani. Nawasilisha!


Kumbe unaweza, ila bado unamfumo dume.

Kani kabla ya kuoa nani alikua anakufanyia hayo yote?
 
Ukweli daima utakuweka huru! Pamoja na gharama zake kama hizo ulizoingia wewe....lakini gharama za kudanganya huwa ni kubwa zaidi. ukidanganya mara moja unaweza kujikuta unaingia gharama ya kudanganya tena na tena...ili kulinda uongo uliofanya awali (kwa mfano)...and you will never be free! Sema ukweli na simama kwenye ukweli....hata Mungu anakuona. Labda cha kujifunza ni namna na wakati wa kusema unachotaka kusema hata kama ni ukweli.
 
Mi kwanza nakupa pole na hongera pia kwa kuwa na moyo wa huruma kiasi hicho mkuuu mi naona ni vyema uilesama ukweli wanasema TELL THE TRUTH AND THE TRUTH WILL SET YOU FREE sawa hakukuelewa ila baadae atakuelewa kama huna mazoea ya kuwa na mambo ya kazi za nje siunajua tena.Ndoa zinzdumishwa na ukweli kwani hutadanganya kila siku ipo siku utakamatwa tuu km ulimpeleka huyo dada Tegeta labda kuna watu walikuona uje kumwambie wife wako kuwa gari ilipata shida afu wale watu waliokuona wamwambie wife wako hapo napo vipi.ALWAYS TELL THE TRUTH...
 
Kama unaona ukweli unaweze kuvunja ndoa yako au kumpa karaha au kumuumiza mwenzako utakuwa punguani kusema ukweli... sababu utakuwa haujengi bali unabomoa... Honesty is the Best Policy............ (Well not Always.........)
 
Inategemea wewe ukoje kama ni mtu wa kumfix tu unategemea nini .................binadamu wamebadilika ................mtu ukishang'atwa sijui kugongwa ukiguswa na unyasi tu unashtuka
 
Mimi kwa kweli siku zote napenda mume wangu aniambie ukweli, uongo kwangu mwiko. Sasa kwa kesi yako inategemea, kama siku zote wewe ni muongo ndiyo maana hakuamini, au inawezekana kuna tabia zako flani ambazo yeye anaziwekea mashaka ndiyo maana ulipomuambia hiyo habari pamoja na kumtaarifu toka mwanzo, alinuna.

Ila take time uongee naye esp siku akiwa amefurahi, umwambie kilichotokea siku hiyo na yeye anachokifikiria ni vitu viwili tofauti. Na kwa upande wake, unatakiwa umsome mkeo, kama ni mtu wa wivu sana basi jitahidi ku-avoid mazingira yatakayomfanya ahisi vinginevyo. Wivu ni sehemu ya mapenzi usimlaumu sana, she loves you, ila wivu ukipiliza ni kero kwa kweli
 
Kumbe unaweza, ila bado unamfumo dume.

Kani kabla ya kuoa nani alikua anakufanyia hayo yote?

Sio mfumo dume, sisi tuliokulia vijijini tulipewa mafunzo wakati wa jando kwamba si jambo jema kufunua chakula kilichoandaliwa na mwingine hata akiwa mkeo.
 
Kumbe unaweza, ila bado unamfumo dume.

Kani kabla ya kuoa nani alikua anakufanyia hayo yote?

Kaka hiyo ni topic nyingine
Huwezi jua walikubaliana vp kuhusu kupika
Turudi tu kwenye mada kuu . . . . kudanganywa
 
Ukweli daima utakuweka huru! Pamoja na gharama zake kama hizo ulizoingia wewe....lakini gharama za kudanganya huwa ni kubwa zaidi. ukidanganya mara moja unaweza kujikuta unaingia gharama ya kudanganya tena na tena...ili kulinda uongo uliofanya awali (kwa mfano)...and you will never be free! Sema ukweli na simama kwenye ukweli....hata Mungu anakuona. Labda cha kujifunza ni namna na wakati wa kusema unachotaka kusema hata kama ni ukweli.

Upo sahihi na hasa kiroho, lakini ndoa inayumba sana kupitia kusema ukweli ingawa yeye (mungu) ndo anavyotaka. Hakutakuwa na mwisho mbaya?
 
Kumbe unaweza, ila bado unamfumo dume.

Kani kabla ya kuoa nani alikua anakufanyia hayo yote?

KJ hapo napingana na wewe kabisa, ni kawaida ya mwanamke kumuandalia mume wake chakula. Inapotokea mume kaamua kujiandalia mwenyewe chakula sio mbaya kwani ni makubaliano ya mume na mke, lakini si kuambiwa kaniandalie chakula halafu akatae. Mwanamke anatakiwa hata awe amechukia namna gani kumuandalia mume wake chakula ni wajibu wake, ugomvi anatakiwa auweke pembeni wakamalizane huko chumbani siyo mezani na watoto wakiwa wanashuhudia eti mama kakasirika leo baba anajiandalia mwenyewe chakula no thank you!!
 
Kama unaona ukweli unaweze kuvunja ndoa yako au kumpa karaha au kumuumiza mwenzako utakuwa punguani kusema ukweli... sababu utakuwa haujengi bali unabomoa... Honesty is the Best Policy............ (Well not Always.........)
Lakini mheshimiwa kudanganya nako kuna madhala yake. Kwa kesi kama hii yangu: kumbuka gari ina namba na kwamba wife anaweza kukupigia simu baada ya kukuona umepita ili akutege, alafu wewe ndo unamdanganya eti gari limeharibika barabarani, si utachochea moto hapo?
 
...Hakutakuwa na mwisho mbaya?
Kama tukizungumzia hii kadhia yako specifically, hicho unachokishuhudia (kununiwa) hasa sio tatizo bali dalili ya tatizo lililopo kwenye mahusiano yenu. Katika hali ya kawaida mwenza kumsaidia binaadamu mwingine hata kama ni wa jinsia tofauti haipaswi kuleta manung'uniko asilani! Ukweli kwamba mkeo anabnung'unika kwa kitendo ulichokifanya kinaashiria matatizo katika mawasiliano yenu....kwa nini hakuamini?
 
Lakini mheshimiwa kudanganya nako kuna madhala yake. Kwa kesi kama hii yangu: kumbuka gari ina namba na kwamba wife anaweza kukupigia simu baada ya kukuona umepita ili akutege, alafu wewe ndo unamdanganya eti gari limeharibika barabarani, si utachochea moto hapo?

nadhani hujamwelewa vizuri VoR,
Hebu msome tena,
sidhani kama alimaanisha uwongo wa style hiyo....................
 
Back
Top Bottom