Ukweli ni kwamba, mkuu wa wilaya ya Kinondoni hafiti kabisa kuongoza wilaya yetu

Ukweli ni kwamba, mkuu wa wilaya ya Kinondoni hafiti kabisa kuongoza wilaya yetu

Wasalaam Mkuu,
Binafsi naona post yako imejaa majungu. Mimi kama mkazi wa Kinondoni nampongeza sana Mkuu wa Wilaya Mh. Saad kwa namna anavyoongoza. Tangu amehamia hapa ame-perfom vizuri sana tena bila mbwembwe tofauti na watangulizi wake.

Mh. Saad amejitengea siku ya Alhamisi kusikiliza kero mbalimbali hususani migogoro ya Ardhi na kuzitatua hapohapo. Ni kiongozi mwenye hofu na Mungu ni ngumu kuingilika kifisadi. Mungu mbariki Mh. Saad, Mungu wabariki wakazi wa Kinondoni.
Labda huwa anachagua baadhi ya maeneo hasa kwa kuangalia yale maeneo yenye wakubwa wengi, ili wasije kumshtaki kwa aliemteua na matokeo yake kitumbua chake kiingie mchanga.
 
Habari zenu wanaJF wenzangu,

Wakubwa leo sina mengi ya kuelezea, ila ukweli ni kwamba mkuu wa wilaya yetu ya Kinondoni aliepo ofisini sasa hafai hata robo kuongoza wilaya yetu.

Kila mtu anafahamu kwamba wilaya ya Kinondoni ndio wilaya inayoongoza kuwa na wasomi wengi nchini, ndio wilaya inayoishi viongozi wengi nchini, ndio wilaya inayoongoza kuwa na matajiri wengi nchini na ndio wilaya iliyoendelea kimakazi kuliko wilaya yoyote ile nchini.

Hivyo nilitarajia kutokana na sifa hizo nilizotaja hapo juu, pengine serikali ingekuletea kiongozi au mkuu wa wilaya ambae atakuwa na elimu pamoja na ujuzi wa ku deal na watu wenye sifa nilizozitaja hapo juu, na badala yake naona tumeletewa mtu ambae ni kama vile hajui ni nini alichotakiwa au anachotakiwa kukifanya katika wilaya hii.

Maeneo mengi ambayo yanatakiwa kupatiwa ufumbuzi yeye hana maono wala muda nayo, hashirikiani na mamlaka kubwa za serikali kutatua kero za sisi anaotuongoza kama vile kupigania na kusimamia miundo mbinu ya ujenzi wa barabara mbali mbali ambazo zinatakiwa kujengwa, utatuaji wa migogoro ya ardhi, changamoto za usafiri katika maeneo ambayo hayafikiki, upatikanaji wa maji nk.

Najua kuna watu watasema kwamba ooh toka lini mkuu wa wilaya akajenga barabara, lkn ukweli ni kwamba juhudi zake na uambanaji wake vinaweza kubusti na kuchangia ujengaji huo.

Yani jamaa anashindwa kupambania wilaya yake hata na wakuu wa wilaya wenzake kina DC Komba (Ubungo) , DC Matinyi (Temeke) , DC Bulembo (Kigamboni) nk ambao kila siku hukutana na wananchi wao kwa ajili ya kuwasikiliza kero zao na baadae kuangalia njia ya kuzitatua kero hizo.

Yeyote ambae yupo karibu na DC huyo hapa JF, naomba amfikishie ujumbe na kumwambia mh DC ajitafakari vizuri kama yeye kwa elimu yake na uwezo wake anao uwezo wa kweli wa kuongoza wilaya yetu, au ameamua tu kukaa ofisini kutafuna kodi za wavuja jasho bila tija yoyote.

Bora DC Godwin Gondwe alijitahidi kushirikiana na wananchi kwa namna moja au nyingine, lkn huyu wa sasa hamna kitu na ni kama vile kaletwa mahala asipopajua au kupapenda.

Wana Kinondoni safari hii tumeamua kuwa kitu kimoja katika kufuatilia na kusimamia maendeleo yetu. Kamwe hatutokubali kuona vichelema mbali mbali vinaletwa katika wilaya zetu kuja tu kupiga picha na kukaa ofisini kusubiri mshahara wa mwezi bila kupigania maendeleo yetu na haki zetu.

Asanteni wakuu.
hivi wewe kunguni una akili kweli? Umesema ni Wilaya yenye maendeleo na ina matajiri na viongozi wengi kuliko Wilaya zote nchini.

Sasa ni nini kinakufanya ulalamikie miundombinu? Hutaki Wilaya zingine ambazo zipo nyuma zipate?

Huna akili
 
MKUU WA WILAYA YA KINONDONI SAAD MTAMBULE KABLA YA HAPO ALITOKEA WILAYA YA MUFINDI NI MCHAPAKAZI SANA ALIKUSANYA MAPATO KUZIDI MALENGO KWA MIAKA MIWILI RAISI ALIVUTIWA NA UCHAPAKAZI WAKE AKAMPELEKA KINONDONI
PIA AKAMTEUA Mr COMRADE JAMES MGEGO ALIYEKUWA KATIBU WA CCM WILAYA YA MUFINDI AKAMPELEKA KINONDONI KWASABABU ILIKUWA NI MUUNGANIKO WA TIMU NZURI KWA MAENDELEO YA MUFINDI NADHANI PIA HUKO KINONDONI WANAFANYA VIZURI SANA HAPENDI RUSHWA
NB mkuu wa wilaya wa sasa wa mufindi DR linda salekwa ni KIMEO
 
Mwandishi mzuri wa umbea kama huu unatakiwa utupe jina kamili la muhusika na historia yake fupi,halafu ndio utuletee fact za anavyofeli utendaji Kwa Sasa.
 
Hua nasema

Kiongozi wa bara la Afrika akisema anakutana na wananchi ili kujua kero/ matatizo/ shida zao huyo hafai kabisa.

Ameishi nchini kabla hajawa kiongozi? Mbona changamoto zetu zipo nje nje? Ukimchukua kijana wa diploma ukamuambia nakupa uDC na resources za kudeal na changamoto za wilaya yako ila nitajie mbili utazoanza nazo atataja ndani ya dk 3.
 
Huyu DC alikua DED Arusha DC baadae akateuliwa DC NJOMBE halafu akaletwa Kinondoni. Kiukweli uwezo wake ni mdogo sana hana command ya DC. Afadhali awe DAS tuuu.
 
Back
Top Bottom