Ukweli ni upi kuhusu Hospitali ya Mloganzila?

Ukweli ni upi kuhusu Hospitali ya Mloganzila?

Kwanza mloganzila wameiga mfumo wa ulaya wa mgonjwa kulala mwenyewe muda mwingi bila msaidizi wakati wao wana wafanyakazi wasio na wito kabisa...imagine mgonjwa amezidiwa hadi anakata roho hakuna cha nesi wala nini anayekuja kuokoa jahazi.

Tuliwahi kuta maiti ya mgonjwa aliyefariki saa 8 usiku ipo kitandani hadi saa 12 asubuhi ule muda wanaoruhusu waleta menu.

Pia ni wazembe sana...niliuguza mama yangu pale japo hakufia pale.

Madaktari wengi wazuri wamegomea muhimbili ya upanga mloganzila kwa asilimia kubwa wamebaki wanafunzi.
 
Walipelekwa kwa magonjwa gani tusiwe tu tunalaumu
Wa kwanza alidondoka tu nyumbani kwake,
Wa pili alikua anavimba miguu ikatakiwa afanyiwe operation, siku ya kwanza wakamover dose. baadae sijui iliendelea vipi.
Wa tatu huyu ni mama, alikua na shinikizo la damu
RIP wapendwa.😭😭😭
 
Mloganzila ni bonge la Hospital, lakini 80% , ya wagonjwa wanaopelekwa pale huwa hawatoboi ( Wanakufa), ndugu 2 kwangu wamekufa pale, na ukifikishwa pale haichukui ata siku 2 au 3 mgonjwa anakua ameaga dunia. Inavyoonesha wagonjwa wengi walio serious kutoka muhimbili upelekwa pale, na kwakuwa hospital ina tekinolojia nzuri sana, lakini madokta na manesi ni juniors (wanafunzi), basi kuna kupishana au kubabaika kwingi kwa utoaji huduma ambayo huleta kifo kwa baadhi ya wagonjwa ingawa wapo wanaopona. Gharama pia unaweza kukimbia, ndugu yangu alikaa siku moja na kufariki, tuliambiwa ni laki 9 tulipe. Hakuna kulala na mgonjwa (uzungu mwingi), wagonjwa wengi ufa kwa kustukiwa asubuhi(Ukaguzi Zero), na kama unavyojua mwafrika akiwa mgonjwa anapenda kuwaona wapendwa wake ukimuacha peke ake ufa kirahisi, na manesi hawana muda wa kuwaona wagonjwa, kiufupi naweza Sema ni CAPITALIST HOSPITAL (hawana huruma).

Sent from my TECNO B1g using JamiiForums mobile app
 
Kwanza mloganzila wameiga mfumo wa ulaya wa mgonjwa kulala mwenyewe muda mwingi bila msaidizi wakati wao wana wafanyakazi wasio na wito kabisa...imagine mgonjwa amezidiwa hadi anakata roho hakuna cha nesi wala nini anayekuja kuokoa jahazi.

Tuliwahi kuta maiti ya mgonjwa aliyefariki saa 8 usiku ipo kitandani hadi saa 12 asubuhi ule muda wanaoruhusu waleta menu.

Pia ni wazembe sana...niliuguza mama yangu pale japo hakufia pale.

Madaktari wengi wazuri wamegomea muhimbili ya upanga mloganzila kwa asilimia kubwa wamebaki wanafunzi.
Naona ushauri wako ni mzuri waende hapo hospitali ni nzuri, iko ngazi ya kitaifa.
Nafikri usichanganye, mambo kuhusu Prof Janabi. Yeye sio kiongozi wa moja kwa moja Mlongazila bali ni Muhimbili yote (MNH) inawezekana pamoja na Mlongazila, nadhani kuna mtendaji mkuu wa Mlongazila.
Ingawa nilisikia kwa Waziri Ummy Mwalimu akipendekeza Mlongazila ijitegemee. Sijui imefikia wapi.
Mlongazila ni jina la mahali ilipojengwa hiyo hospitali. Hospitali nyingi ndivyo zimepewa majina ya aina hiyo.
 
Kuingiza siasa kwenye taaluma, msigano kati ya Muhimbili Upanga na Chuo cha MUHAS enzi hizo ndio kulifanya Hospitali ya Mloganzila mwanzo kufanya vibaya,

Kipindi Hospitali inafunguliwa kuna maagizo yalitoka juu ya kuwa hamisha wagonjwa kutoka MNH UPANGA kwenda MLOGANZILA, ili kupunguza msongamano wa wagonjwa MNH-UPANGA,
MNH-Upanga nao wakatumia mwanya ule waliopewa wakawa wanachagua wale terminal ill patients wa internal medicine(wagonjwa wa magonjwa ya ndani) ndio wakawa wanawapeleka Mloganzila, wakifika kule wakawa hawachukui muda wana fariki, ndio jina baya la Mloganzila lilianzia pale.

ila kwa sasa kwa Afrika Mashariki na kati hakuna Hospitali yenye mazingira na miundombinu bora kuizidi mloganzila, na kwa sasa inafanya vizuri nadhani ni hospitali chache sana hapa nchini zinazidi Mloganzila kwenye kutoa huduma.

Nendeni mkatibiwe Mloganzila mtakuja na majibu tofauti na mnayo yasikia na kuyasoma Mitandaoni, wana jitahidi sana kwenye kutoa huduma, watoa huduma wao wana kauli nzurI, na wanawajali wagonjwa, mimi binafsi ni shahidi, ndio imekuwa kimbilio langu napopata changamoto za kiafya.
Kipindi cha COVID-19 wagonjwa wa COVID walikuwa wakiponea pale, wengi ni mashahidi.

Kwa sasa chini ya Prof Janabi imekuwa na muelekeo mzuri zaidi, na staff wa pale wengi ukiohojiana nao wanamkubali sana huyu mwamba Prof Janabi, anajali maslahi wa wafanyakazi wake, na hii imeongeza morari ya watoa huduma pale Mloganzila na Upanga kwa ujumla,

Naskia kuna msigano unaendelea kati ya Chuo cha Muhimbili na Muhimbili Upanga nani anapaswa kuiendesha Hospitali,
Kama mdau wa Afya nawashauri mwacheni kwa sasa Prof Janabi aendeshe ile Hospitali ana maono na muelekeo mzuri zaidi, na amefanikiwa kuleta mabadiliko chanya toka akabidhiwe Hospitali ya Upanga na Mloganzila, ataleta mapinduzi makubwa sana kwenye hizi Hospitali mbili za Taifa, kama alivyo fanya pale Taasisi ya Moyo ya JKCI.
Mkuu naungana na wewe kwa %zote mapema mwaka juzi dada yangu alipata maradhi mazito yanayohusiana na ubongo alianzia huko mtaani hadi m/nyamala hosp hajitambui chochote akapokelewa pale kila ndugu anaeingia ndani akirudi ni vilio ikatoka rufaa mloganzila tukasema dah habari imeishia hapa tunaenda kukamilisha ratiba tu,ebana eeeh mdada kapokelewa mloganzila kaanza vipimo docta huyu kule huyu hapa nesi kimbia kule leta kile lete hiki yani kazungukwa na jopo la wataalam,zile mishe mishe za wauguzi tu tukaanza kupata faraja ndugu Mungu si ujugu mgonjwa akaanza kuhisi siku nne tano anageuza macho mara geuza kichwa mara hivi mara vile hadi hapa ninavyotext yupo anapiga mishe zake,nishahudhuria sana clinic na mdada huduma nilizoziona pale ni classic kama vifo au errors za kibinadamu hata St Thomas zipo
 
Haya ni MAJUNGU,

Kipindi Hii hospital inafunguliwa wagonjwa wengi walihamishwa Muhimbili UPANGA kwa mabasi wengi walikuwa na hali mbaya tena saana ndio waliokufa

Ilipofunguliwa RASMI madaktari wengi walitoka Mhimbili Upanga na hopsitali nyingine za UMMA, huko walikotoka si walikuwa wanahudumia wagonjwa hao hao

Ni maoni yangu binafsi wanajitahidi tena saana wapo madaktari very dedicated, nilishafika IDARA YAO YA DHARURA huduma niliyopata utafikiri sio Tanganyika.madaktari walionihudumia walikuwa lugha ilikuwa ni njema na kila wanachofanya wanaongea na wewe na kukuelewesha tofauti na huko kwingine

OMBI kwa serekali hii hospitali iwe Teaching HOspital ya chuo kikuu cha tiba Mhimbili, waipewe waiendeshe wenyewe naamini ikifanyika hivyo watabibu watakuwa na wakati wa kufanya tafiti, na kuleta matokeo chanya ya changamoto mbalimbali
Kwa nini wao tu wapigwe majungu? Mbona waliofika hospital ya Benjamin Mkapa Dodoma wanaisifu kwa huduma nzuri. Kwa nini mloganzila ndo wapigwe majungu?
 
Story za mtaani zisizo na maana.

Mloganzila ila mortality rate ndogo sana ukilinganisha na MNH Upanga.

Wakati hospitali ilipofunguliwa ikiwa chini ya MUHAS, ilianza na kitengo cha magonjwa ya ndani (Internal Medicine)

Kitenho hiki ndio kinapokea wagonjwa wengi wenye terminal illnesses - Idadi kubwa ya Saratani, Magonjwa ya Figo, Magonjwa ya ini n.k

Kumbuka hii ni hispitali ya taifa hivyo wengi wenye magonjwa tajwa hapo juu walikuwa wakifika na hali mbaya, na kwa sababu hospitali ilikuwa na kitengo hiko tu ikaonekana kwa juu juu na wabongo hawajui statistics kama vile kila mgonjwa anayekuja anachance kubwa wa kufa.

Wabongo wakashika hilo na kufanya ndo stori wa kila kijiwe.

Ujinga utatumaliza
Ujinga utaisha vipi bila nyie kutoa elimu kama hivi??hapa nimepata elimu today kwako ujinga umenitoka kuhusu kufikiria ill kuhusu mloganzila
 
Inaweza kua stories za vijiweni; Ila kiukweli nina watu wangu watatu wa karibu, wote walipelekwa mloganzila kwa matibabu , hakuna alietoboa. Wote ni marhum, lisemwalo lipo na kama halipo laja.Ila issue haijakaa vizuri kwa hio hospitali...mloganzila = mchawi wa njia/barabara..
NB: Kuna biashara tajwa ya figo.
Ni hospital ya mwisho nchini,yaani vikishindikana kote huko mgonjwa hupelekwa mloganzila,watu wapumbavu tu..ni Kama pale ICU muhimbili,Kuna vitanda vitano,Imani iliyojengeka ni kwamba huwa wanapona wawili tu,nilipokua na mgonjwa pale walupona wanne
 
Kwanza mloganzila wameiga mfumo wa ulaya wa mgonjwa kulala mwenyewe muda mwingi bila msaidizi wakati wao wana wafanyakazi wasio na wito kabisa...imagine mgonjwa amezidiwa hadi anakata roho hakuna cha nesi wala nini anayekuja kuokoa jahazi.

Tuliwahi kuta maiti ya mgonjwa aliyefariki saa 8 usiku ipo kitandani hadi saa 12 asubuhi ule muda wanaoruhusu waleta menu.

Pia ni wazembe sana...niliuguza mama yangu pale japo hakufia pale.

Madaktari wengi wazuri wamegomea muhimbili ya upanga mloganzila kwa asilimia kubwa wamebaki wanafunzi.
Daktari mtumishi wa umma hawezi gomea kituo Cha kazi, mloganzila ni hospital ambayo wanafunzi huchukulia masomo pia...labda useme uzembe lakini siyo hizo tuhuma zingine
 
Story za mtaani zisizo na maana.

Mloganzila ila mortality rate ndogo sana ukilinganisha na MNH Upanga.

Wakati hospitali ilipofunguliwa ikiwa chini ya MUHAS, ilianza na kitengo cha magonjwa ya ndani (Internal Medicine)

Kitenho hiki ndio kinapokea wagonjwa wengi wenye terminal illnesses - Idadi kubwa ya Saratani, Magonjwa ya Figo, Magonjwa ya ini n.k

Kumbuka hii ni hispitali ya taifa hivyo wengi wenye magonjwa tajwa hapo juu walikuwa wakifika na hali mbaya, na kwa sababu hospitali ilikuwa na kitengo hiko tu ikaonekana kwa juu juu na wabongo hawajui statistics kama vile kila mgonjwa anayekuja anachance kubwa wa kufa.

Wabongo wakashika hilo na kufanya ndo stori wa kila kijiwe.

Ujinga utatumaliza
Wewe umeelezea vizuri na nimekuelewa Sana mkuu.

Ila nakusaihisha Aya ya mwisho uliyosema wabongo uninga utatumaliza..kwa maelezo haya wana Haki ya kuongea wanayoyaona,so elimu inahitajka sana maana imani huku mtaani Hakuna kabisa.Mtu Ukiambiwa unaenda kutibiwa Mloganzila unapata ganzi ya moyo.
 
Story za mtaani zisizo na maana.

Mloganzila ila mortality rate ndogo sana ukilinganisha na MNH Upanga.

Wakati hospitali ilipofunguliwa ikiwa chini ya MUHAS, ilianza na kitengo cha magonjwa ya ndani (Internal Medicine)

Kitenho hiki ndio kinapokea wagonjwa wengi wenye terminal illnesses - Idadi kubwa ya Saratani, Magonjwa ya Figo, Magonjwa ya ini n.k

Kumbuka hii ni hispitali ya taifa hivyo wengi wenye magonjwa tajwa hapo juu walikuwa wakifika na hali mbaya, na kwa sababu hospitali ilikuwa na kitengo hiko tu ikaonekana kwa juu juu na wabongo hawajui statistics kama vile kila mgonjwa anayekuja anachance kubwa wa kufa.

Wabongo wakashika hilo na kufanya ndo stori wa kila kijiwe.

Ujinga utatumaliza
Zinaweza kweli kuwa ni story za mitaani lakini hata wewe umeleta story za mitaani. Huwezi kusema eti kwa sababu wanakwenda wagonjwa wa magonjwa fulani basi ni halali kuwe na vifo vingi. Hili jambo linahitaji research ya kina ndiyo ufikie hitimisho kama hili. Hata kwa wagonjwa wa magonjwa uliyoandika bado uzembe unaweza kutokea.
 
Hizi story huwa nyingi sana. Hata mimi
Niliwahi kuskia wanasema hivyo hivyo kuhusu kitengule na rabininsia. Sasa kwakuwa sijawahi kutibiwa pale niliishia kuyapuuza
Ila hapo rabininsia sio mchezo,kwa experience niliyoipata siwezi recomend mtu especially mtoto kulazwa ila kitengule sina hakika
 
Nijuavyo kuhusu MLOGANZILA

Kuna kijana alipasuka kichwa na mguu pamoja na mbavu alitapata rufaa ya kupelekwa mloganzila kipindi anatoka hapo hospitali alikuwa hata fahamu ile haipo lakini alipofika mloganzila ilichukua siku tatu tu kuanza kuongea na siku ya nne alirudi na familia yake Home na siji nilivyoona ule mshono wa kichwani alikuwa si wa kupona yule ila yupo fresh kabisa

Hongera sana madokta wote tanzania
 
Back
Top Bottom