Ukweli ni upi kuhusu Hospitali ya Mloganzila?

Ukweli ni upi kuhusu Hospitali ya Mloganzila?

Kuingiza siasa kwenye taaluma, msigano kati ya Muhimbili Upanga na Chuo cha MUHAS enzi hizo ndio kulifanya Hospitali ya Mloganzila mwanzo kufanya vibaya,

Kipindi Hospitali inafunguliwa kuna maagizo yalitoka juu ya kuwa hamisha wagonjwa kutoka MNH UPANGA kwenda MLOGANZILA, ili kupunguza msongamano wa wagonjwa MNH-UPANGA,
MNH-Upanga nao wakatumia mwanya ule waliopewa wakawa wanachagua wale terminal ill patients wa internal medicine(wagonjwa wa magonjwa ya ndani) ndio wakawa wanawapeleka Mloganzila, wakifika kule wakawa hawachukui muda wana fariki, ndio jina baya la Mloganzila lilianzia pale.

ila kwa sasa kwa Afrika Mashariki na kati hakuna Hospitali yenye mazingira na miundombinu bora kuizidi mloganzila, na kwa sasa inafanya vizuri nadhani ni hospitali chache sana hapa nchini zinazidi Mloganzila kwenye kutoa huduma.

Nendeni mkatibiwe Mloganzila mtakuja na majibu tofauti na mnayo yasikia na kuyasoma Mitandaoni, wana jitahidi sana kwenye kutoa huduma, watoa huduma wao wana kauli nzurI, na wanawajali wagonjwa, mimi binafsi ni shahidi, ndio imekuwa kimbilio langu napopata changamoto za kiafya.
Kipindi cha COVID-19 wagonjwa wa COVID walikuwa wakiponea pale, wengi ni mashahidi.

Kwa sasa chini ya Prof Janabi imekuwa na muelekeo mzuri zaidi, na staff wa pale wengi ukiohojiana nao wanamkubali sana huyu mwamba Prof Janabi, anajali maslahi wa wafanyakazi wake, na hii imeongeza morari ya watoa huduma pale Mloganzila na Upanga kwa ujumla,

Naskia kuna msigano unaendelea kati ya Chuo cha Muhimbili na Muhimbili Upanga nani anapaswa kuiendesha Hospitali,
Kama mdau wa Afya nawashauri mwacheni kwa sasa Prof Janabi aendeshe ile Hospitali ana maono na muelekeo mzuri zaidi, na amefanikiwa kuleta mabadiliko chanya toka akabidhiwe Hospitali ya Upanga na Mloganzila, ataleta mapinduzi makubwa sana kwenye hizi Hospitali mbili za Taifa, kama alivyo fanya pale Taasisi ya Moyo ya JKCI.
Maelezo yako yanatia moyo,lipo tumaini.
 
Ila hapo rabininsia sio mchezo,kwa experience niliyoipata siwezi recomend mtu especially mtoto kulazwa ila kitengule sina hakika
Tanzania ukienda hospital, unatakiwa kuwa mwangalifu kweli kweli. Hospital nyingi zina madaktari uchwara. Infact vyuo siku hizi vinazalisha madaktari wauaji na siyo madaktari waponyaji.
 
Mloganzila ni bonge la Hospital, lakini 80% , ya wagonjwa wanaopelekwa pale huwa hawatoboi ( Wanakufa), ndugu 2 kwangu wamekufa pale, na ukifikishwa pale haichukui ata siku 2 au 3 mgonjwa anakua ameaga dunia. Inavyoonesha wagonjwa wengi walio serious kutoka muhimbili upelekwa pale, na kwakuwa hospital ina tekinolojia nzuri sana, lakini madokta na manesi ni juniors (wanafunzi), basi kuna kupishana au kubabaika kwingi kwa utoaji huduma ambayo huleta kifo kwa baadhi ya wagonjwa ingawa wapo wanaopona. Gharama pia unaweza kukimbia, ndugu yangu alikaa siku moja na kufariki, tuliambiwa ni laki 9 tulipe. Hakuna kulala na mgonjwa (uzungu mwingi), wagonjwa wengi ufa kwa kustukiwa asubuhi(Ukaguzi Zero), na kama unavyojua mwafrika akiwa mgonjwa anapenda kuwaona wapendwa wake ukimuacha peke ake ufa kirahisi, na manesi hawana muda wa kuwaona wagonjwa, kiufupi naweza Sema ni CAPITALIST HOSPITAL (hawana huruma).

Sent from my TECNO B1g using JamiiForums mobile app
Dah,

Hili la manesi kuwa wanafunzi nilisita kuandika ila pia linasemwa Sana miongoni mwa watu.

Lakini pia,swala la mhudumu wa mgonjwa kutolala hospitali kuhudumia mgonjwa wake(umeita uzungu) lipo hospitali nyingi Sana Sasa hivi,hata za mitaani wameiga hili.
 
Kwanza mloganzila wameiga mfumo wa ulaya wa mgonjwa kulala mwenyewe muda mwingi bila msaidizi wakati wao wana wafanyakazi wasio na wito kabisa...imagine mgonjwa amezidiwa hadi anakata roho hakuna cha nesi wala nini anayekuja kuokoa jahazi.

Tuliwahi kuta maiti ya mgonjwa aliyefariki saa 8 usiku ipo kitandani hadi saa 12 asubuhi ule muda wanaoruhusu waleta menu.

Pia ni wazembe sana...niliuguza mama yangu pale japo hakufia pale.

Madaktari wengi wazuri wamegomea muhimbili ya upanga mloganzila kwa asilimia kubwa wamebaki wanafunzi.
Pole Sana kwa kufiwa na mama.

Sent from my CPH1923 using JamiiForums mobile app
 
Maneno tu hayo,kuna mgonjwa wetu sisi mpaka tulikua tumemkatia tamaa,ila kwa huduma aliyopewa pale mloganzila,mgojwa amepona na anadunda hadi leo.
 
Hizi story huwa nyingi sana. Hata mimi
Niliwahi kuskia wanasema hivyo hivyo kuhusu kitengule na rabininsia. Sasa kwakuwa sijawahi kutibiwa pale niliishia kuyapuuza
Rabininsia ni hospitali nzuri sana. Kwanza ukitaka kujua ni nzuri tazama vifaa tiba vyake, huduma zao hata mapokezi tu na marupurupu ya wafanyakazi wao yalivyo
 
dah ndugu yetu amekufa pale baada yakukosa huduma yakwanza.aligongwa na gari asubuhi aliemgonga akala mita.raia wakaita polisi polisi wakamchukua nakumpeleka hapo sisi tumejua kesho yake kwasababu mtoto alikuwa anasoma bweni.ilia yotekwayote basi tumemwachia mungu.
 
Zinaweza kweli kuwa ni story za mitaani lakini hata wewe umeleta story za mitaani. Huwezi kusema eti kwa sababu wanakwenda wagonjwa wa magonjwa fulani basi ni halali kuwe na vifo vingi. Hili jambo linahitaji research ya kina ndiyo ufikie hitimisho kama hili. Hata kwa wagonjwa wa magonjwa uliyoandika bado uzembe unaweza kutokea.
Mkuu, fatality rate unaita story za vijiweni. Research zilishafanyika hapo, usitegemee mgonjwa wa stage 4 coron cancer apone sawasawa na mgonjwa wa kichocho.
 
Nimesikia sana hizi hadithi...lakini nilichoshudia ni hiki kifutacho

Jamaa yangu alipata ajali ya bodaboda..tukapewa fomu na polisi tuende mloganzila,...tulipofika mloganzila tukapokelewa kitengo cha emergency,palepale nikaambiwa nilipie 15000 ya dokta mm sasa huyo ndugu wa mgonjwa nikatoa.,,,nikaambiwa nilipie kipimo cha kichwa,cha tumbo,cha kifua ambayo gharama ikawa 205000 wakuu hio ni mbali na 15k kumbuka ni usiku huo ila nilitoa...mgonjwa alikaa siku mbili bila ya kufanyiwa chchote hadi akapona tukasepa...kuhusu kufa sijui ila naona coast nyingi muachaliia
 
Kuingiza siasa kwenye taaluma, msigano kati ya Muhimbili Upanga na Chuo cha MUHAS enzi hizo ndio kulifanya Hospitali ya Mloganzila mwanzo kufanya vibaya,

Kipindi Hospitali inafunguliwa kuna maagizo yalitoka juu ya kuwa hamisha wagonjwa kutoka MNH UPANGA kwenda MLOGANZILA, ili kupunguza msongamano wa wagonjwa MNH-UPANGA,
MNH-Upanga nao wakatumia mwanya ule waliopewa wakawa wanachagua wale terminal ill patients wa internal medicine(wagonjwa wa magonjwa ya ndani) ndio wakawa wanawapeleka Mloganzila, wakifika kule wakawa hawachukui muda wana fariki, ndio jina baya la Mloganzila lilianzia pale.

ila kwa sasa kwa Afrika Mashariki na kati hakuna Hospitali yenye mazingira na miundombinu bora kuizidi mloganzila, na kwa sasa inafanya vizuri nadhani ni hospitali chache sana hapa nchini zinazidi Mloganzila kwenye kutoa huduma.

Nendeni mkatibiwe Mloganzila mtakuja na majibu tofauti na mnayo yasikia na kuyasoma Mitandaoni, wana jitahidi sana kwenye kutoa huduma, watoa huduma wao wana kauli nzurI, na wanawajali wagonjwa, mimi binafsi ni shahidi, ndio imekuwa kimbilio langu napopata changamoto za kiafya.
Kipindi cha COVID-19 wagonjwa wa COVID walikuwa wakiponea pale, wengi ni mashahidi.

Kwa sasa chini ya Prof Janabi imekuwa na muelekeo mzuri zaidi, na staff wa pale wengi ukiohojiana nao wanamkubali sana huyu mwamba Prof Janabi, anajali maslahi wa wafanyakazi wake, na hii imeongeza morari ya watoa huduma pale Mloganzila na Upanga kwa ujumla,

Naskia kuna msigano unaendelea kati ya Chuo cha Muhimbili na Muhimbili Upanga nani anapaswa kuiendesha Hospitali,
Kama mdau wa Afya nawashauri mwacheni kwa sasa Prof Janabi aendeshe ile Hospitali ana maono na muelekeo mzuri zaidi, na amefanikiwa kuleta mabadiliko chanya toka akabidhiwe Hospitali ya Upanga na Mloganzila, ataleta mapinduzi makubwa sana kwenye hizi Hospitali mbili za Taifa, kama alivyo fanya pale Taasisi ya Moyo ya JKCI.
Hii hospitali irudishwe MUHAS....kwani wao ndio wamiliki kuanzia wazo la ujenzi na pia isitoshe imejengwa kwenye plot yao.
 
Ni ujinga unatusubua watz, mloganzila ni teaching university hospital. Muhimbili iachie ifanye utafiti. Kwa nini wabunge hawaelewi.
 
Story za mtaani zisizo na maana.

Mloganzila ila mortality rate ndogo sana ukilinganisha na MNH Upanga.

Wakati hospitali ilipofunguliwa ikiwa chini ya MUHAS, ilianza na kitengo cha magonjwa ya ndani (Internal Medicine)

Kitenho hiki ndio kinapokea wagonjwa wengi wenye terminal illnesses - Idadi kubwa ya Saratani, Magonjwa ya Figo, Magonjwa ya ini n.k

Kumbuka hii ni hispitali ya taifa hivyo wengi wenye magonjwa tajwa hapo juu walikuwa wakifika na hali mbaya, na kwa sababu hospitali ilikuwa na kitengo hiko tu ikaonekana kwa juu juu na wabongo hawajui statistics kama vile kila mgonjwa anayekuja anachance kubwa wa kufa.

Wabongo wakashika hilo na kufanya ndo stori wa kila kijiwe.

Ujinga utatumaliza
Inaonekana unaijua hii hospital au uko huko. Ungekuwa umetusaidia kama ungeweka hizo statistics hapa tuweze kufanya huo ulinganifu unaosema. Hizi tetesi zipo sana na majuzi tuu nimemsikia Prof Janabi akizitolea ufafanuzi, yeye tofauti na wewe hakuna hata neno moja la kejeli alilotumia kama wewe ulivyofanya, pamoja na kwamba yeye ndiye mkurugenzi mkuu wa hizo Hospital.
 
Story za mtaani zisizo na maana.

Mloganzila ila mortality rate ndogo sana ukilinganisha na MNH Upanga.

Wakati hospitali ilipofunguliwa ikiwa chini ya MUHAS, ilianza na kitengo cha magonjwa ya ndani (Internal Medicine)

Kitenho hiki ndio kinapokea wagonjwa wengi wenye terminal illnesses - Idadi kubwa ya Saratani, Magonjwa ya Figo, Magonjwa ya ini n.k

Kumbuka hii ni hispitali ya taifa hivyo wengi wenye magonjwa tajwa hapo juu walikuwa wakifika na hali mbaya, na kwa sababu hospitali ilikuwa na kitengo hiko tu ikaonekana kwa juu juu na wabongo hawajui statistics kama vile kila mgonjwa anayekuja anachance kubwa wa kufa.

Wabongo wakashika hilo na kufanya ndo stori wa kila kijiwe.

Ujinga utatumaliza
Leo Gazeti ya Mwananchi wameandika nanukuu.
"Mloganzila yazidiwa wagonjwa wa Akili". Yaani vichaa!!
Je imekuwa kitengo ya Mirembe!?
Na mbona wagonjwa wa Akili wanaongezeka kila kukicha??

Matatizo na njaa ya akili.!!
 
Mkuu, fatality rate unaita story za vijiweni. Research zilishafanyika hapo, usitegemee mgonjwa wa stage 4 coron cancer apone sawasawa na mgonjwa wa kichocho.
Ilifanywa na nani? Lini? Naomba link nisome hiyo reseach kama ipo kwenye mtandao.
 
Ni ujinga unatusubua watz, mloganzila ni teaching university hospital. Muhimbili iachie ifanye utafiti. Kwa nini wabunge hawaelewi.
Elezea kwa kirefu mkuu. Unaonekana una hoja ila umefupisha sana. Wabunge,utafiti,teaching University,vyote umeviweka kwa pamoja.

Sent from my CPH1923 using JamiiForums mobile app
 
Hii hospitali irudishwe MUHAS....kwani wao ndio wamiliki kuanzia wazo la ujenzi na pia isitoshe imejengwa kwenye plot yao.

MUHAS pia wanaweza kuifanya ile taasisi ikaleta mapinduzi makubwa sana kwenye sekta ya Afya wasipoleta maslahi yao binafsi kama walivyofanya walipokabidhiwa ule mradi
Nimependekeza iendelee kuwa Chini ya Prof Janabi kwa sababu muelekeo chanya umeanza kuonekana,
anafanya vizuri kwa sababu anajali utu na maslahi ya wafanya kazi wake, JKCI ipo pale sababu ya maslahi bora, wala si vinginevyo, na pale MNH UPANGA na MLOGANZILA pameanza kuonesha mwanga sababu ameanza kuwalipa vizuri wafanya kazi wake, wala hakuna muujiza mwingine,
Hospitali ya Taifa Muhimbili Upanga na Mloganzila ndio icon la Taifa letu kwenye kutoa huduma, haziitaji majaribio kwenye utendaji, zinahitaji mtu smart kuziongoza, Hospitali zilizo chini zinatakiwa zijifunze kutoka kwao, mambo mazuri yanatakiwa yaanzie kwao yashuke hadi ngazi ya zahanati na vituo vya Afya.

Hospitali nyingi Duniani zinazo milikiwa na vyuo ndio zinaongoza kwa kutoa matibabu ya hari ya juu, sipingi MUHAS kurudishiwa hospitali yao, ila wanatakiwa wajipange haswa.

Ile hospitali kuiendesha si mchezo, imewekewa mazingira kama ya First World, AC kila mahali, escalator, ventilation, system za moto, nk, hivyo vyote vinakula umeme wakutosha,

Kuendesha Hospitali ile kunahitaji ubunifu wa hari ya juu, na si kwa kutegemea ruzuku ,

Inahitaji kuwa na huduma za ziada amabazo hazipatikani nchini, pamoja na nchi zinazo tuzunguka,

Watengeneze mazingira yatayowavutia wateja kwenda pale, badala ya watu kukimbilia kwenda kutibiwa nje ya nchi,

kwa hadhi ya hospitali yenu Agakhan inatakiwa iwe inakuja kujifunza kwenu mkitumia fursa mliyo nayo.

Mfano kuhusu malazi, eneo la kibamba hakuna hotel na lodge za maana, hospitali inaweza kuingia ubia na sekta binafsi wajenge lodge na hotel za kueleweka, ndugu wa wagonjwa wasisumbuke sehemu za kufikia,

Ile stand ya pale, nayo inawachafulia mandhari ya pale, ombeni mjengewe stand inayo endana na hadhi ya hospitali yenu.

Sehemu za kupata chakula nazo zipo chache, ikifika saa 12 wameshafunga, hadi uamue kwenda kibamba chama ndio unaweza ukapata chakula cha kueleweka,

Wafundisheni staff wenu customer care nzuri, hii dunia ya ubepari, mgonjwa akija leo mkamzingua kupata majibu na matibabu kwa haraka kesho harudi kwenu, ataenda aghkhan, rabininsia, n.k

Waondoleeni staff wenu njaa njaa zisizo za maana, walipeni stahiki zao kwa wakati, hili nchi za wenzetu ndio walipotuzidia, nurse, daktari, mtoa huduma wa afya kama kipato hakieleweki msitegemee miujiza kwenye kutoa huduma bora, wataishia kupiga part-time (vijiwe) na kuacha taasisi za umma zikiendelea kujikongoja kutoa huduma,

majibu mabovu kwa wagonjwa na customer care mbovu asilimia 90% inachangiwa na vipato duni vya watoa huduma, asilimia 10% ni tabia ya mtu mmoja mmoja.

tukumbuke wanatumia muda wao mwingi hospitali, wengi wao hawana sehem nyingine za kuwaongezea vipato, wanatoka kazini muda umeenda, ukiongeza changamoto za usafiri wanafika majumbani usiku,

kesho yake saa moja anatakiwa kuwahi kazini, bado hajaingia night shift, hakuna kulala usiku mzima, na bado wapo wachache, ikifika jioni mtoa huduma hoi, kila kiungo kinamuuma,

maslahi kiduchu, anawaza atarudi vipi nyumbani, na kesho ataacha nini nyumbani watoto wapate chakula.

Tembeleeni hospitali mkajionee wanayo yapitia watoa huduma wa afya, muda ambao sisi tumelala wao wanapigania uhai wa ndugu zetu, bado hatujawananga mitandaoni,

inahitaji miujiza kupata customer care nzuri kwa mtoa huduma wa afya anayepitia mazingira hayo.

Niwape kongole watoa huduma wote wa Afya nchini, kwa kuendelea kuokoa uhai wa ndugu nzetu, japo mnapitia changamoto nyingi na mazingira magumu ya utendaji kazi,

Msichoke mna Hazina yenu mbinguni, mnafanya kazi ya Mungu ya uponyaji, japo mnapitia changamoto nyingi za maisha.

Nchi za wenzetu katika kada zinazolipwa vizuri kada ya Afya inaongoza,

"A healthy nation is a wealthy nation, and every life matters. If you’re healthy, you can wish anything. If you’re not healthy, you wish only to have your health back. That’s why health is the foundation."
 
Back
Top Bottom