Ukweli tunaotakiwa kuujua: Rais atakayekuwa hana wabunge wa kutosha Bungeni hataweza kuleta au kufanya mabadiliko yoyote na Urais wake hautadumu

Ukweli tunaotakiwa kuujua: Rais atakayekuwa hana wabunge wa kutosha Bungeni hataweza kuleta au kufanya mabadiliko yoyote na Urais wake hautadumu

Dr Akili

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2011
Posts
5,119
Reaction score
4,569
Utawala wa nchi yetu na nchi zote za kidemokrasia ni utawala wa sheria. Na sheria hizo tunazitunga wenyewe wananchi kupitia wawakilishi wetu kwenye bunge letu. Sisi ndiyo tunaoamua nchi yetu tuiendeshe namna gani kupitia sheria tutakazozitunga au kuzibadilisha kupitia wawakilishi wetu (wabunge) bungeni. Yaani mamlaka yote ya nchi ni ya kwetu sisi wananchi kupitia bunge letu. Yaani hata huyo rais atakayechaguliwa tuna mamlaka ya kumuondoa madarakani hata baada ya siku chache tu baada ya kuchaguliwa kupitia wawakilishi wetu bungeni. Hii ndiyo maana ya demokrasia. 'The government of the people by the people for the people'

Kwa msingi huo wa utawala wa sheria, kama rais atakayechaguliwa kama hatakuwa na wabunge wa kutosha bungeni hataweza hata kidogo kufanya mabadiliko ye yote ya utendaji kazi serikalini. Hataweza kutekeleza hata moja ya anayoyaahidi kwenye hizi kampeni hususani eti kufumua TRA, Traffic police, NHIF, kuongeza mishahara ya watumishi wa umma mara dufu, kutoa matibabu na ubwabwa bure kwa kila mtanzania, kuruhusu uvuvi haramu na wa nyaya ndogo utakaomaliza samaki wote nk.

Ili hayo yote anayoahidi yaweze kutekelezwa ni lazima yaidhinishwe na wabunge wetu kupitia utungaji au marekebisho ya sheria. Ukweli tunaojua ni kuwa hawa jamaa zetu wanaotoa hizi ahadi za porojo zinazofurahisha lakini si za uhalisia hawataweza hata kidogo kuwa na wabunge wa kutosha huko bungeni. Yaani idadi ya wabunge wao watakaoshinda haitafika hata robo ya wabunge wote. Maana yake ni kuwa miswada yao bungeni itapigwa chini na wabunge wa ccm ambao idadi yao itazidi theruthi mbili, idadi inayoruhusu kubadili hata katiba kwa jinsi wanavyotaka. Idadi inayoruhusu kumtoa madarakani rais wa nchi saa yo yote wanayotaka

Huu ndiyo ukweli wananchi wanaopaswa kuujua. Wao ndiyo wenye nchi.
 
Nauliza hivi ni majimbo mangapi mzee wa ubweche kasimamisha wabunge? Maana nchi tushampa tayari! Jiwe atateuliwa kuwa waziri wa bara bara na madaraja kwenye serikali ya mzee wa ubwabwa ili aongeze madaraja mpunga uje mjini kwa wingi
 
Kwa katiba ya sasa, bunge likileta fyoko dhidi ya rais anao uwezo wa kulivunja.
Ni sawa kabisa. Rais tuliomchagua akiona kuwa wawakilishi wetu bungeni hawapikiki chungu kimoja, tumempa mamlaka ya kulivunja bunge na kuitisha uchaguzi mkuu wa urais na ubunge. Yaani anarudi kwetu tuamue kama yeye aendelee kuwa rais au hao wawakilishi wetu waendelee kuwa wabunge na tuchague rais wanayeendana nao.

Ndiyo demokrasia yenyewe. Kwa hiyo uchaguzi utakaporudiwa, iwe kwa wabunge wetu kumu impeach rais au kwa rais kuvunja bunge, sisi wenye nchi ndiyo tutaamua nani kati yao hafai kwa kupitia sanduku la kura. Na kwa vyo vyote ccm itatoa tena wabunge zaidi ya theluthi mbili ya wabunge wote bungeni. Huu ndiyo ukweli kwa hali yetu. Hivi vyama vingine bado vichanga sana kuweza kupata wabunge wa kutosha. Hivyo tukichagua rais kutoka vyama hivyo tutakuwa tunapoteza muda na pesa bure kwani uchaguzi mkuu mpya utabidi ufanyike. Tutake tusitake uchaguzi mkuu utabidi urudiwe.

Hadi sasa ccm ina wabunge tayari 18 kibindoni, kiasi ambacho ndiyo chadema na ukawa ilipata kwenye uchaguzi mkuu wa 2015. Mwaka huu ukawa haipo, imebaki kugawana hiyo 10% itakayoachwa na ccm kwa vyama vyote vya upinzani. Na kwa ukweli rais hatatoka chadema, ndiyo maana Mbowe akawa mjanja na kujitoa kugombea nafasi hiyo. Akaamua kujaribu karata yake jimbo la Hai ambako ana 30% chance ya kushinda. Huko kwenye urais chance ya kushinda ni 0%. Mwamba analijua hilo.
 
Ni sawa kabisa. Rais tuliomchagua akiona kuwa wawakilishi wetu bungeni hawapikiki chungu kimoja, tumempa mamlaka ya kulivunja bunge na kuitisha uchaguzi mkuu wa urais na ubunge. Yaani anarudi kwetu tuamue kama yeye aendelee kuwa rais au hao wawakilishi wetu waendelee kuwa wabunge na tuchague rais wanayeendana nao.

Ndiyo demokrasia yenyewe. Kwa hiyo uchaguzi utakaporudiwa, iwe kwa wabunge wetu kumu impeach rais au kwa rais kuvunja bunge, sisi wenye nchi ndiyo tutaamua nani kati yao hafai kwa kupitia sanduku la kura. Na kwa vyo vyote ccm itatoa tena wabunge zaidi ya theluthi mbili ya wabunge wote bungeni. Huu ndiyo ukweli kwa hali yetu. Hivi vyama vingine bado vichanga sana kuweza kupata wabunge wa kutosha. Hivyo tukichagua rais kutoka vyama hivyo tutakuwa tunapoteza muda na pesa bure kwani uchaguzi mkuu mpya utabidi ufanyike.
Kukiwa na uchaguzi huru na wa haki + tume huru ya uchaguzi,CCM hawapati "one third" ya bunge zima.
 
Kukiwa na uchaguzi huru na wa haki + tume huru ya uchaguzi,CCM hawapati "one third" ya bunge zima.
Hizo ni ngonjera ambazo hazina maana yo yote. Uhuru wa NEC au chombo cho chote cha serikali unatolewa na katiba na sheria za nchi. Kwa mfano mahakama na CAG ni vyombo huru kikatiba na wakuu wa vyombo hivyo huteuliwa na mkuu wa nchi. Tatizo lenu ni kuwa hamujui kwamba kuna mkuu wa nchi na kuna rais wa JMT.

Zanzibar waliingia kwenye matata baada ya kuingiza wawakilishi wa vyama mbali mbali kwenye ZEC eti ili kuifanya ZEC kuwa chombo huru. Matokeo yake tuliyaona uchaguzi wa 2015. Wajumbe wa ZEC walitwangana makonde, nguo na nyaraka munimu zote zilichanika na mwisho wa yote mwenyekiti wao akafuta uchaguzi wote. Ikabidi urudiwe, CUF wakasusa na kwenda kushitaki Amerika ambao hadi sasa hawajatoa hukumu. Ikabidi CUF kipande kimoja kumeguka na kujiunga na ACT na Zitto Kabwe kufurahia mafanikio hayo ya ZEC 'huru'. Angependa na huku bara yatokee kwa NEC yetu kuwa'huru'! Wapinzani wote wangependa yatokee hayo. Hatudanganyiki nyoo!
 
Pia kumbuka CCM kuna wabunge wenye akili zao timamu tu, ila kwa ajili ya kuwapendeza mabosi wao, akili zao wameziifadhia matakoni,

Endapo RAIS akatoka upinzani CCM watavurugana hakutakuwa na kauli moja, hakutakuwa na wakuwashika masikio, akili zao zitarudi utimamu

REFER Bunge la escrow nakumbuka CCM akili zao zilirudishwa kwa masaa kadhaa, tundu lissu alishamgeuzia pinda kibra, wabunge wa CCM wakaridhia....mbowe akakimbia na kisu kwapani

Sent from my TECNO KD6 using JamiiForums mobile app
 
Pia kumbuka CCM kuna wabunge wenye akili zao timamu tu, ila kwa ajili ya kuwapendeza mabosi wao, akili zao wameziifadhia matakoni,

Endapo RAIS akatoka upinzani CCM watavurugana hakutakuwa na kauli moja, hakutakuwa na wakuwashika masikio, akili zao zitarudi utimamu

REFER Bunge la escrow nakumbuka CCM akili zao zilirudishwa kwa masaa kadhaa, tundu lissu alishamgeuzia pinda kibra, wabunge wa CCM wakaridhia....mbowe akakimbia na kisu kwapani

Sent from my TECNO KD6 using JamiiForums mobile app
Lazima pia ujue kwamba bunge la 2020 litakuwa funga kazi. Mbunge wa chadema atakayerudi mjengoni ni Halima Mdee peke yake tena kupitia viti maalum. Na madudu kama ya Escrow kamwe hayatatokea katika utawala wa JPM. Yatatumbuliwa kabla hayajachipuka. Huu ndiyo ukweli na msema ukweli ni mpenzi wa Mungu.
 
Lazima pia ujue kwamba bunge la 2020 litakuwa funga kazi. Mbunge wa chadema atakayerudi mjengoni ni Halima Mdee peke yake tena kupitia viti maalum. Na madudu kama ya Escrow kamwe hayatatokea katika utawala wa JPM. Yatatumbuliwa kabla hayajachipuka. Huu ndiyo ukweli na msema ukweli ni mpenzi wa Mungu.
Labda ukimsikiliza Lissu hapa utajikuta unaelewa kitu Fulani katika ufahamu wako.
Msikilize kwa makini, fungua mawazo yako mihemko weka pembeni kisha tafakari kama Mtanzania na sio kama kada wa chama chochote especially CCM.

 
Utawala wa nchi yetu na nchi zote za kidemokrasia ni utawala wa sheria. Na sheria hizo tunazitunga wenyewe wananchi kupitia wawakilishi wetu kwenye bunge letu. Sisi ndiyo tunaoamua nchi yetu tuiendeshe namna gani kupitia sheria tutakazozitunga au kuzibadilisha kupitia wawakilishi wetu (wabunge) bungeni. Yaani mamlaka yote ya nchi ni ya kwetu sisi wananchi kupitia bunge letu. Yaani hata huyo rais atakayechaguliwa tuna mamlaka ya kumuondoa madarakani hata baada ya siku chache tu baada ya kuchaguliwa kupitia wawakilishi wetu bungeni. Hii ndiyo maana ya demokrasia. 'The government of the people by the people for the people'.

Kwa msingi huo wa utawala wa sheria, kama rais atakayechaguliwa kama hatakuwa na wabunge wa kutosha bungeni hataweza hata kidogo kufanya mabadiliko ye yote ya utendaji kazi serikalini. Hataweza kutekeleza hata moja ya anayoyaahidi kwenye hizi kampeni hususani eti kufumua TRA, Traffic police, NHIF, kuongeza mishahara ya watumishi wa umma mara dufu, kutoa matibabu na ubwabwa bure kwa kila mtanzania, kuruhusu uvuvi wa nyanya ndogo utakaomalima samaki wote nk.

Ili hayo yote anayoahidi yaweze kutekelezwa ni lazima yaidhinishwe na wabunge wetu kupitia utungaji au marekebisho ya sheria. Ukweli tunaojua ni kuwa hawa jamaa zetu wanaotoa hizi ahadi za porojo zinazofurahisha lakini si za uhalisia hawataweza hata kidogo kuwa na wabunge wa kutosha huko bungeni. Yaani idadi ya wabunge wao watakaoshinda haitafika hata robo ya wabunge wote. Maana yake ni kuwa miswada yao bungeni itapigwa chini na wabunge wa ccm ambao idadi yao itazidi theruthi mbili, idadi inayoruhusu kubadili hata katiba kwa jinsi wanavyotaka. Idadi inayoruhusu kumtoa madarakani rais wa nchi saa yo yote wanayotaka.

Huu ndiyo ukweli wananchi wanaopaswa kuujua. Wao ndiyo wenye nchi.
Mbunge gani anataka bunge livunjwe? Wakishaingia hutawasikia maana wakileta ujinga Rais anavunja bunge tunarudi kwenye uchaguzi wa wabunge na yeye ndiye anasimamia uchaguzi. Thubutuuuuu!
 
Kwa nchi hii na katiba yake au???
Utawala wa nchi yetu na nchi zote za kidemokrasia ni utawala wa sheria. Na sheria hizo tunazitunga wenyewe wananchi kupitia wawakilishi wetu kwenye bunge letu. Sisi ndiyo tunaoamua nchi yetu tuiendeshe namna gani kupitia sheria tutakazozitunga au kuzibadilisha kupitia wawakilishi wetu (wabunge) bungeni. Yaani mamlaka yote ya nchi ni ya kwetu sisi wananchi kupitia bunge letu. Yaani hata huyo rais atakayechaguliwa tuna mamlaka ya kumuondoa madarakani hata baada ya siku chache tu baada ya kuchaguliwa kupitia wawakilishi wetu bungeni. Hii ndiyo maana ya demokrasia. 'The government of the people by the people for the people'.

Kwa msingi huo wa utawala wa sheria, kama rais atakayechaguliwa kama hatakuwa na wabunge wa kutosha bungeni hataweza hata kidogo kufanya mabadiliko ye yote ya utendaji kazi serikalini. Hataweza kutekeleza hata moja ya anayoyaahidi kwenye hizi kampeni hususani eti kufumua TRA, Traffic police, NHIF, kuongeza mishahara ya watumishi wa umma mara dufu, kutoa matibabu na ubwabwa bure kwa kila mtanzania, kuruhusu uvuvi wa nyanya ndogo utakaomalima samaki wote nk.

Ili hayo yote anayoahidi yaweze kutekelezwa ni lazima yaidhinishwe na wabunge wetu kupitia utungaji au marekebisho ya sheria. Ukweli tunaojua ni kuwa hawa jamaa zetu wanaotoa hizi ahadi za porojo zinazofurahisha lakini si za uhalisia hawataweza hata kidogo kuwa na wabunge wa kutosha huko bungeni. Yaani idadi ya wabunge wao watakaoshinda haitafika hata robo ya wabunge wote. Maana yake ni kuwa miswada yao bungeni itapigwa chini na wabunge wa ccm ambao idadi yao itazidi theruthi mbili, idadi inayoruhusu kubadili hata katiba kwa jinsi wanavyotaka. Idadi inayoruhusu kumtoa madarakani rais wa nchi saa yo yote wanayotaka.

Huu ndiyo ukweli wananchi wanaopaswa kuujua. Wao ndiyo wenye nchi.
 
Wawakilishi wanawawakilisha wapiga kura. Wapiga kura Wakisema nenda katufanyie uliyoahidi wawakilishi kwa nn wakatae?
 
Uchaguzi unakuwa ni kwa wabunge tu, Rais anawacheck tu kwa kideo akiwa Chamwino
Ni sawa kabisa. Rais tuliomchagua akiona kuwa wawakilishi wetu bungeni hawapikiki chungu kimoja, tumempa mamlaka ya kulivunja bunge na kuitisha uchaguzi mkuu wa urais na ubunge. Yaani anarudi kwetu tuamue kama yeye aendelee kuwa rais au hao wawakilishi wetu waendelee kuwa wabunge na tuchague rais wanayeendana nao.

Ndiyo demokrasia yenyewe. Kwa hiyo uchaguzi utakaporudiwa, iwe kwa wabunge wetu kumu impeach rais au kwa rais kuvunja bunge, sisi wenye nchi ndiyo tutaamua nani kati yao hafai kwa kupitia sanduku la kura. Na kwa vyo vyote ccm itatoa tena wabunge zaidi ya theluthi mbili ya wabunge wote bungeni. Huu ndiyo ukweli kwa hali yetu. Hivi vyama vingine bado vichanga sana kuweza kupata wabunge wa kutosha. Hivyo tukichagua rais kutoka vyama hivyo tutakuwa tunapoteza muda na pesa bure kwani uchaguzi mkuu mpya utabidi ufanyike. Tutake tusitake uchaguzi mkuu utabidi urudiwe. Hadi sasa ccm ina wabunge tayari 18 kibindoni, kiasi ambacho ndiyo chadema na ukawa ilipata kwenye uchaguzi mkuu wa 2015. Mwaka huu ukawa haipo, imebaki kugawana hiyo 10% itakayoachwa na ccm kwa vyama vyote vya upinzani. Na kwa ukweli rais hatatoka chadema, ndiyo maana Mbowe akawa mjanja na kujitoa kugombea nafasi hiyo. Akaamua kujaribu karata yake jimbo la Hai ambako ana 30% chance ya kushinda. Huko kwenye urais chance ya kushinda ni 0%. Mwamba analijua hilo.
 
Lazima pia ujue kwamba bunge la 2020 litakuwa funga kazi. Mbunge wa chadema atakayerudi mjengoni ni Halima Mdee peke yake tena kupitia viti maalum. Na madudu kama ya Escrow kamwe hayatatokea katika utawala wa JPM. Yatatumbuliwa kabla hayajachipuka. Huu ndiyo ukweli na msema ukweli ni mpenzi wa Mungu.
Hahahaaaaaa...lol. Kama kungekuwa na "OGP" katika awamu hii,hakika Watanzania wangelia. Ufisadi wa sasa ni zaidi ya EPA +Radar + Richmonds + Dowans + Escrow ukizijumlisha. Wabunge wa CCM "waliolazwa" wanajua,ni wabunge "maiti" tu ndio ndio hawajui lolote.
 
Utawala wa nchi yetu na nchi zote za kidemokrasia ni utawala wa sheria. Na sheria hizo tunazitunga wenyewe wananchi kupitia wawakilishi wetu kwenye bunge letu. Sisi ndiyo tunaoamua nchi yetu tuiendeshe namna gani kupitia sheria tutakazozitunga au kuzibadilisha kupitia wawakilishi wetu (wabunge) bungeni. Yaani mamlaka yote ya nchi ni ya kwetu sisi wananchi kupitia bunge letu. Yaani hata huyo rais atakayechaguliwa tuna mamlaka ya kumuondoa madarakani hata baada ya siku chache tu baada ya kuchaguliwa kupitia wawakilishi wetu bungeni. Hii ndiyo maana ya demokrasia. 'The government of the people by the people for the people'.

Kwa msingi huo wa utawala wa sheria, kama rais atakayechaguliwa kama hatakuwa na wabunge wa kutosha bungeni hataweza hata kidogo kufanya mabadiliko ye yote ya utendaji kazi serikalini. Hataweza kutekeleza hata moja ya anayoyaahidi kwenye hizi kampeni hususani eti kufumua TRA, Traffic police, NHIF, kuongeza mishahara ya watumishi wa umma mara dufu, kutoa matibabu na ubwabwa bure kwa kila mtanzania, kuruhusu uvuvi wa nyanya ndogo utakaomalima samaki wote nk.

Ili hayo yote anayoahidi yaweze kutekelezwa ni lazima yaidhinishwe na wabunge wetu kupitia utungaji au marekebisho ya sheria. Ukweli tunaojua ni kuwa hawa jamaa zetu wanaotoa hizi ahadi za porojo zinazofurahisha lakini si za uhalisia hawataweza hata kidogo kuwa na wabunge wa kutosha huko bungeni. Yaani idadi ya wabunge wao watakaoshinda haitafika hata robo ya wabunge wote. Maana yake ni kuwa miswada yao bungeni itapigwa chini na wabunge wa ccm ambao idadi yao itazidi theruthi mbili, idadi inayoruhusu kubadili hata katiba kwa jinsi wanavyotaka. Idadi inayoruhusu kumtoa madarakani rais wa nchi saa yo yote wanayotaka.

Huu ndiyo ukweli wananchi wanaopaswa kuujua. Wao ndiyo wenye nchi.
Ambacho hujui ni kuwa Rais wa nchi anaweza kulivunja bunge wakati wowote akijisikia na nchi ikarudi kwenye uchaguzi na akapiga spana wabunge wake wakapita kwa wingi kama ambavyo Magufuli amejipatia wabunge wa tume!
Yaani tuseme Lissu ndiye Rais,akisikia tu fyokofyoko za kuhujumiwa na wabunge,basi anaweza piga mkwara mmoja wa kulivunja bunge na wote wakanywea!Kumbuka hawa wabunge ni njaa mbele,hawawezi kurisk kurudi kwenye uchaguzi!
Au tuseme wabunge wa CCM ndio wanaanzisha mchakato wa kumuondoa,basi kabla hawajafika popote kesho yake wanakutana na habari kwenye gazeti la serikali kuwa bunge limevunjwa na wao sio wabunge tena!Nchi inarudi kwenye uchaguzi!
 
wote. Maana yake ni kuwa miswada yao bungeni itapigwa chini na wabunge wa ccm ambao idadi yao itazidi theruthi mbili, idadi inayoruhusu kubadili hata katiba kwa jinsi wanavyotaka. Idadi inayoruhusu kumtoa madarakani rais wa nchi saa yo yote wanayotaka.
Dr. Akili;
 
Utawala wa nchi yetu na nchi zote za kidemokrasia ni utawala wa sheria. Na sheria hizo tunazitunga wenyewe wananchi kupitia wawakilishi wetu kwenye bunge letu. Sisi ndiyo tunaoamua nchi yetu tuiendeshe namna gani kupitia sheria tutakazozitunga au kuzibadilisha kupitia wawakilishi wetu (wabunge) bungeni. Yaani mamlaka yote ya nchi ni ya kwetu sisi wananchi kupitia bunge letu. Yaani hata huyo rais atakayechaguliwa tuna mamlaka ya kumuondoa madarakani hata baada ya siku chache tu baada ya kuchaguliwa kupitia wawakilishi wetu bungeni. Hii ndiyo maana ya demokrasia. 'The government of the people by the people for the people'.

Kwa msingi huo wa utawala wa sheria, kama rais atakayechaguliwa kama hatakuwa na wabunge wa kutosha bungeni hataweza hata kidogo kufanya mabadiliko ye yote ya utendaji kazi serikalini. Hataweza kutekeleza hata moja ya anayoyaahidi kwenye hizi kampeni hususani eti kufumua TRA, Traffic police, NHIF, kuongeza mishahara ya watumishi wa umma mara dufu, kutoa matibabu na ubwabwa bure kwa kila mtanzania, kuruhusu uvuvi wa nyanya ndogo utakaomalima samaki wote nk.

Ili hayo yote anayoahidi yaweze kutekelezwa ni lazima yaidhinishwe na wabunge wetu kupitia utungaji au marekebisho ya sheria. Ukweli tunaojua ni kuwa hawa jamaa zetu wanaotoa hizi ahadi za porojo zinazofurahisha lakini si za uhalisia hawataweza hata kidogo kuwa na wabunge wa kutosha huko bungeni. Yaani idadi ya wabunge wao watakaoshinda haitafika hata robo ya wabunge wote. Maana yake ni kuwa miswada yao bungeni itapigwa chini na wabunge wa ccm ambao idadi yao itazidi theruthi mbili, idadi inayoruhusu kubadili hata katiba kwa jinsi wanavyotaka. Idadi inayoruhusu kumtoa madarakani rais wa nchi saa yo yote wanayotaka.

Huu ndiyo ukweli wananchi wanaopaswa kuujua. Wao ndiyo wenye nchi.
Ubunge ni ajira siku hizi!
 
Back
Top Bottom