Ukweli tunaotakiwa kuujua: Rais atakayekuwa hana wabunge wa kutosha Bungeni hataweza kuleta au kufanya mabadiliko yoyote na Urais wake hautadumu

Ukweli tunaotakiwa kuujua: Rais atakayekuwa hana wabunge wa kutosha Bungeni hataweza kuleta au kufanya mabadiliko yoyote na Urais wake hautadumu

Utawala wa nchi yetu na nchi zote za kidemokrasia ni utawala wa sheria. Na sheria hizo tunazitunga wenyewe wananchi kupitia wawakilishi wetu kwenye bunge letu. Sisi ndiyo tunaoamua nchi yetu tuiendeshe namna gani kupitia sheria tutakazozitunga au kuzibadilisha kupitia wawakilishi wetu (wabunge) bungeni. Yaani mamlaka yote ya nchi ni ya kwetu sisi wananchi kupitia bunge letu. Yaani hata huyo rais atakayechaguliwa tuna mamlaka ya kumuondoa madarakani hata baada ya siku chache tu baada ya kuchaguliwa kupitia wawakilishi wetu bungeni. Hii ndiyo maana ya demokrasia. 'The government of the people by the people for the people'

Kwa msingi huo wa utawala wa sheria, kama rais atakayechaguliwa kama hatakuwa na wabunge wa kutosha bungeni hataweza hata kidogo kufanya mabadiliko ye yote ya utendaji kazi serikalini. Hataweza kutekeleza hata moja ya anayoyaahidi kwenye hizi kampeni hususani eti kufumua TRA, Traffic police, NHIF, kuongeza mishahara ya watumishi wa umma mara dufu, kutoa matibabu na ubwabwa bure kwa kila mtanzania, kuruhusu uvuvi wa nyanya ndogo utakaomalima samaki wote nk.

Ili hayo yote anayoahidi yaweze kutekelezwa ni lazima yaidhinishwe na wabunge wetu kupitia utungaji au marekebisho ya sheria. Ukweli tunaojua ni kuwa hawa jamaa zetu wanaotoa hizi ahadi za porojo zinazofurahisha lakini si za uhalisia hawataweza hata kidogo kuwa na wabunge wa kutosha huko bungeni. Yaani idadi ya wabunge wao watakaoshinda haitafika hata robo ya wabunge wote. Maana yake ni kuwa miswada yao bungeni itapigwa chini na wabunge wa ccm ambao idadi yao itazidi theruthi mbili, idadi inayoruhusu kubadili hata katiba kwa jinsi wanavyotaka. Idadi inayoruhusu kumtoa madarakani rais wa nchi saa yo yote wanayotaka

Huu ndiyo ukweli wananchi wanaopaswa kuujua. Wao ndiyo wenye nchi.
Kweli tupu, hapo uchaguzi bado mwenzake kashaweka point 3 na magoli kadhaa wabunge bila kupingwa wao 0.Uchaguzi ukija si ndio thunami kabisa. Wana saccos, endeleeni kujisifia nyomi tu, mwaka huu mnaambulia kura chache kuliko zile za 2015 kwa hizo porojo zenu..
 
Hizo teuzi zake zitakuwa batili. Na akiendelea kuleta fyoko fyoko wanaume wanamuweka lockdown nyumbani kwake kama ilivyofanyika kwa Mzee Mugabe huko Zimbabwe.
Ok
IMG_20200905_131243.jpeg
 
Kuna upotoshaji unaufanya, kwa kujua, kutokujua au labda kwa kuzidiwa na mapenzi! Hoja yako ina ukweli nusu tu, sehemu ya pili hujazingatia!
Ni wabunge wangapi watakao kuwa na uhakika wa kurudi bila kubebwa na mamlaka?! Kwa raisi wa chama chenye uchache wa wabunge, uchaguzi ukirudiwa atakua na advantage kubwa Kwa sababu;
Ana serikali na vyombo vyake.
Hofu ya watu kufanya mabadiliko imeisha
Wabunge waliopita bila kupingwa, sasa watapingwa!
Wale waliokua wanasifu kiunafiki wataonesha makucha yao!
Hii propaganda yako haitutishi, alafu siyo kweli kwamba UKAWA walipata wabunge 18, 2015, kasome takwimu zako vizuri, usije ukafanana na Baba ako anayesema Nyerere alitawala miaka 27!
 
Kwa katiba ya sasa, bunge likileta fyoko dhidi ya rais anao uwezo wa kulivunja.
Mfano Lissu awe Rais na wabunge wake kiduchu, anaweza kulivunja Bunge au Bunge litakuwa linamwendesha linavyotaka ili mradi yeye ni Rais.
 
Hataweza kufanya hayo maana bunge litakuwa limesha mu impeanch. Na katiba yetu haimuruhusu kuunda serikali yake pekee. Katiba inamtaka Waziri Mkuu atoke kwenye chama chenye wabunge wengi na nusu ya mawaziri watoke kwenye chama chenye wabunge wengi. Na bunge litalapo mu impeanch rais wa aina hiyo haruhusiwi kuwa mgombea urais tena. Huu ndiyo ukweli kwa mjibu wa katiba ndugu yangu, utake usitake.
Dr. Akili tumianakili Basi..kwà hii katiba na hata hatafikia kwenye hiyo impeachment..Hadi Bunge likutane tayari ameshafanya mabadiliko meengi tuu Sana mnoo. Anaweza vunja hilo Bunge hata kabla ya impeachment. Na sijui wajua safari ya impeachment au waisikia tuu. Bunge ni barabara ya kuanzia tu bosi..Kati a hii kila kitu kinawezekana bosii hata Kama huna mbunge hata mmoja.
 
..Raisi wa Tz ana mamlaka makubwa mno aliyopewa na Katiba.

..akiwa hana wabunge wengi itasaidia asitumie madaraka yake vibaya.

..kwa maoni yangu hili litakuwa ni jambo la heri. Litaibadilisha Tz for good.
 
Haohao mliowatolea wagombea wao kwa ghirba (Lissu na Maalim) ndio tunawapa kura. tegemeo lenu labda NEC tu.
Utawala wa nchi yetu na nchi zote za kidemokrasia ni utawala wa sheria. Na sheria hizo tunazitunga wenyewe wananchi kupitia wawakilishi wetu kwenye bunge letu. Sisi ndiyo tunaoamua nchi yetu tuiendeshe namna gani kupitia sheria tutakazozitunga au kuzibadilisha kupitia wawakilishi wetu (wabunge) bungeni. Yaani mamlaka yote ya nchi ni ya kwetu sisi wananchi kupitia bunge letu. Yaani hata huyo rais atakayechaguliwa tuna mamlaka ya kumuondoa madarakani hata baada ya siku chache tu baada ya kuchaguliwa kupitia wawakilishi wetu bungeni. Hii ndiyo maana ya demokrasia. 'The government of the people by the people for the people'

Kwa msingi huo wa utawala wa sheria, kama rais atakayechaguliwa kama hatakuwa na wabunge wa kutosha bungeni hataweza hata kidogo kufanya mabadiliko ye yote ya utendaji kazi serikalini. Hataweza kutekeleza hata moja ya anayoyaahidi kwenye hizi kampeni hususani eti kufumua TRA, Traffic police, NHIF, kuongeza mishahara ya watumishi wa umma mara dufu, kutoa matibabu na ubwabwa bure kwa kila mtanzania, kuruhusu uvuvi haramu na wa nyaya ndogo utakaomaliza samaki wote nk.

Ili hayo yote anayoahidi yaweze kutekelezwa ni lazima yaidhinishwe na wabunge wetu kupitia utungaji au marekebisho ya sheria. Ukweli tunaojua ni kuwa hawa jamaa zetu wanaotoa hizi ahadi za porojo zinazofurahisha lakini si za uhalisia hawataweza hata kidogo kuwa na wabunge wa kutosha huko bungeni. Yaani idadi ya wabunge wao watakaoshinda haitafika hata robo ya wabunge wote. Maana yake ni kuwa miswada yao bungeni itapigwa chini na wabunge wa ccm ambao idadi yao itazidi theruthi mbili, idadi inayoruhusu kubadili hata katiba kwa jinsi wanavyotaka. Idadi inayoruhusu kumtoa madarakani rais wa nchi saa yo yote wanayotaka

Huu ndiyo ukweli wananchi wanaopaswa kuujua. Wao ndiyo wenye nchi.
 
Haohao mliowatolea wagombea wao kwa ghirba (Lissu na Maalim) ndio tunawapa kura. tegemeo lenu labda NEC tu.
Kwani mlikuwa hamuwapi kura? Mwaka 2015 hamukuwapa kura?
Demokrasia ni utawala wa wale walo wengi. Sisi ndiyo tuliyo wengi.
 
Samahani, kwani bajeti ya kununulia ndege na kujenga uwanja Chato ilipitishwa lini bungeni?

Pia, maazimio ya kutokuwaongeza mishahara watumishi yalifanyika bunge la ngapi?

#MADARAKAYARAIS!
 
Utawala wa nchi yetu na nchi zote za kidemokrasia ni utawala wa sheria. Na sheria hizo tunazitunga wenyewe wananchi kupitia wawakilishi wetu kwenye bunge letu. Sisi ndiyo tunaoamua nchi yetu tuiendeshe namna gani kupitia sheria tutakazozitunga au kuzibadilisha kupitia wawakilishi wetu (wabunge) bungeni. Yaani mamlaka yote ya nchi ni ya kwetu sisi wananchi kupitia bunge letu. Yaani hata huyo rais atakayechaguliwa tuna mamlaka ya kumuondoa madarakani hata baada ya siku chache tu baada ya kuchaguliwa kupitia wawakilishi wetu bungeni. Hii ndiyo maana ya demokrasia. 'The government of the people by the people for the people'

Kwa msingi huo wa utawala wa sheria, kama rais atakayechaguliwa kama hatakuwa na wabunge wa kutosha bungeni hataweza hata kidogo kufanya mabadiliko ye yote ya utendaji kazi serikalini. Hataweza kutekeleza hata moja ya anayoyaahidi kwenye hizi kampeni hususani eti kufumua TRA, Traffic police, NHIF, kuongeza mishahara ya watumishi wa umma mara dufu, kutoa matibabu na ubwabwa bure kwa kila mtanzania, kuruhusu uvuvi haramu na wa nyaya ndogo utakaomaliza samaki wote nk.

Ili hayo yote anayoahidi yaweze kutekelezwa ni lazima yaidhinishwe na wabunge wetu kupitia utungaji au marekebisho ya sheria. Ukweli tunaojua ni kuwa hawa jamaa zetu wanaotoa hizi ahadi za porojo zinazofurahisha lakini si za uhalisia hawataweza hata kidogo kuwa na wabunge wa kutosha huko bungeni. Yaani idadi ya wabunge wao watakaoshinda haitafika hata robo ya wabunge wote. Maana yake ni kuwa miswada yao bungeni itapigwa chini na wabunge wa ccm ambao idadi yao itazidi theruthi mbili, idadi inayoruhusu kubadili hata katiba kwa jinsi wanavyotaka. Idadi inayoruhusu kumtoa madarakani rais wa nchi saa yo yote wanayotaka

Huu ndiyo ukweli wananchi wanaopaswa kuujua. Wao ndiyo wenye nchi.

Kwani hao watakao mchagua Rais watashindwaje kumchagua mbunge pia wa eneo hilo
 
Kwani hao watakao mchagua Rais watashindwaje kumchagua mbunge pia wa eneo hilo
Hicho chama hakikuweza kupata/ kuweka mgombea ubunge kila jimbo. Na wagombea iliyowaweka wengi wao hawakuwa na sifa au hawakuweza kutimiza vigezo vinavyotakiwa na hivyo kuondolewa baada ya kuwekewa pingamizi kwa mjibu wa katiba na sheria zetu za uchaguzi. Yaani wengi wao walishindwa hata kujaza ile fomu.
Wengi waliobaki kugombea hawakubaliki majimboni kwao ukiwalinganisha na hao wa chama tawala eg Mdee vs Gwajima.

Pia kumbuka wapiga kura walio wengi hawako chama cho chote cha siasa. Kwa walio kwenye vyama vya siasa: ccm ndicho chama kongwe kikiwa na wanachama millioni 12 wakati chadema kina wanachama wasiozidi laki 7 tu! Huo ndiyo ukweli ndugu yangu.
 
Back
Top Bottom