Ukweli tunaotakiwa kuujua: Rais atakayekuwa hana wabunge wa kutosha Bungeni hataweza kuleta au kufanya mabadiliko yoyote na Urais wake hautadumu

Ukweli tunaotakiwa kuujua: Rais atakayekuwa hana wabunge wa kutosha Bungeni hataweza kuleta au kufanya mabadiliko yoyote na Urais wake hautadumu

Ubunge ni ajira siku hizi!
Ubunge hautakiwi kuwa ni ajira. Ni uwakilishi wa wananchi. Enzi za Mwalimu hakuwa analipwa mshahara wo wote na hakukuwa na posho ya kikao ya laki tatu kwa siku. Mbunge alikuwa lazima awe ni mtu ambaye ana kazi yake inayompa kipato.

Tatizo linalotusumbua kwa sasa ni hilo la serikali kuwa inawalipa wabunge wetu mishahara na marupurupu makubwa kuliko mtu mwingine ye yote nchini. Hili ninakubaliana nawe kwamba wawakilishi wetu hawa badala ya kuwa part of us wamekuwa part of serikali.

Tulitegemea Lissu badala ya kusema ataongeza mishahara ya watumishi wa umma mara dufu, angesema atafuta misharaha na marupurupu ya wabunge. Hapo tungalimuunga mkono na kumpatia kura. Kuongeza mishahara ya watumishi wa umma na askari wetu mara dufu mapato yote ya serikali kupitia kodi zetu yangeishia kulipa mishahara tu ya watumishi hawa na bado hayangalitosha na hivyo kulazimishwa kuongezewa kodi. Hili halikubaliki.
 
Ambacho hujui ni kuwa Rais wa nchi anaweza kulivunja bunge wakati wowote akijisikia na nchi ikarudi kwenye uchaguzi na akapiga spana wabunge wake wakapita kwa wingi kama ambavyo Magufuli amejipatia wabunge wa tume!
Yaani tuseme Lissu ndiye Rais,akisikia tu fyokofyoko za kuhujumiwa na wabunge,basi anaweza piga mkwara mmoja wa kulivunja bunge na wote wakanywea!Kumbuka hawa wabunge ni njaa mbele,hawawezi kurisk kurudi kwenye uchaguzi!
Au tuseme wabunge wa CCM ndio wanaanzisha mchakato wa kumuondoa,basi kabla hawajafika popote kesho yake wanakutana na habari kwenye gazeti la serikali kuwa bunge limevunjwa na wao sio wabunge tena!Nchi inarudi kwenye uchaguzi!
Rais wa aina hiyo kwa mjibu wa katiba yetu hana mamlaka hayo. See above threads.
 
Tunazungumzia utawala wa sheria. Bunge ndilo suprem. Ndiyo demokrasia. Rais akienda kinyume cha hapo anakuwa dictator. Hivyo ili Lissu aweze kuendesha nchi wakati ni lazima aiendeshe kidikiteta kwani hatakuwa na support la wabunge walio wengi. Na akifanya u dictator bunge litamu iimpeach mara moja.

Unapaswa pia kujua kuwa katiba yetu hairuhusu rais asiyekuwa na angalao nusu ya wabunge wa majimbo. Katiba yetu imeweka bayana kwa mfano kama Lissu ikatokea (Mungu apishe mbali) akapita kwenye kura za urais na CCM wakapata majority of votes za wabunge kama ilivyo kawaida yao, basi serikali itakayoundwa itakuwa ya mseto; Waziri Mkuu atatoka ccm na nusu ya mawaziri watatoka ccm. Haya ni kwa mjibu wa katiba yetu ya nchi. Na kwamba bunge litakapomu impeach Lissu na uchaguzi kurudiwa yeye Lissu katiba haimuruhusu kuwa mgombea urais tena bali Waziri Mkuu. Hivyo Lissu atakuwa rais wa muda mfupi sana kwa vyo vyote vile kwa mjibu wa katiba yetu.

..bunge haliwezi ku-impeach raisi anayeungwa mkono na wananchi.

..lakini itakuwa ni bahati njema kwa taifa kama tutalazimika kuunda serikali ya mseto.

..kwa kweli hilo likitokea tutaweza kuzi-sanitize siasa zetu ili ziwe kwa manufaa ya nchi na siyo vyama.

..naamini kila upande, kwa maana ya bunge na executive, watafanya kila jitihada kufanya kazi kwa mashirikiano.
 
Ni sawa kabisa. Rais tuliomchagua akiona kuwa wawakilishi wetu bungeni hawapikiki chungu kimoja, tumempa mamlaka ya kulivunja bunge na kuitisha uchaguzi mkuu wa urais na ubunge. Yaani anarudi kwetu tuamue kama yeye aendelee kuwa rais au hao wawakilishi wetu waendelee kuwa wabunge na tuchague rais wanayeendana nao.

Ndiyo demokrasia yenyewe. Kwa hiyo uchaguzi utakaporudiwa, iwe kwa wabunge wetu kumu impeach rais au kwa rais kuvunja bunge, sisi wenye nchi ndiyo tutaamua nani kati yao hafai kwa kupitia sanduku la kura. Na kwa vyo vyote ccm itatoa tena wabunge zaidi ya theluthi mbili ya wabunge wote bungeni. Huu ndiyo ukweli kwa hali yetu. Hivi vyama vingine bado vichanga sana kuweza kupata wabunge wa kutosha. Hivyo tukichagua rais kutoka vyama hivyo tutakuwa tunapoteza muda na pesa bure kwani uchaguzi mkuu mpya utabidi ufanyike. Tutake tusitake uchaguzi mkuu utabidi urudiwe.

Hadi sasa ccm ina wabunge tayari 18 kibindoni, kiasi ambacho ndiyo chadema na ukawa ilipata kwenye uchaguzi mkuu wa 2015. Mwaka huu ukawa haipo, imebaki kugawana hiyo 10% itakayoachwa na ccm kwa vyama vyote vya upinzani. Na kwa ukweli rais hatatoka chadema, ndiyo maana Mbowe akawa mjanja na kujitoa kugombea nafasi hiyo. Akaamua kujaribu karata yake jimbo la Hai ambako ana 30% chance ya kushinda. Huko kwenye urais chance ya kushinda ni 0%. Mwamba analijua hilo.
Hakuna mbunge atakubali bunge livunjwe.
 
Hata wana CCM wengi tu wanataka uhuru na haki wanamuogopa jiwe. Wakipata uhuru wa kusema utaona nchi itakavyochangamka.
Kwa hiyo jiwe huwa anawashikia mawe siku za uchaguzi
 
JPM hafanyi kampeni kwa ajili ya kuomba kura zake. Yeye tayari ni Rais kilichobaki ni kuapishwa tu. Anafanya kampeni kwa ajili ya kuwaombea kura Wabunge na Madiwani.
 
Kweli Katiba yetu inahitaji marekebisho makubwa Sana, endeleeni kushusha nondo wakuu, hoja zenu zinajenga
 
Hahahaaaaaa...lol. Kama kungekuwa na "OGP" katika awamu hii,hakika Watanzania wangelia. Ufisadi wa sasa ni zaidi ya EPA +Radar + Richmonds + Dowans + Escrow ukizijumlisha. Wabunge wa CCM "waliolazwa" wanajua,ni wabunge "maiti" tu ndio ndio hawajui lolote.
Wewe unatoka nchi gani? Dunia yote inajua jinsi Tanzania ilivyo uteketeza ufisadi. Hadi nchi mbali mbali za Afrika huwa zinatuomba tuwaazime JPM akawe rais wao angalao kwa kipindi kifupi ili akakomeshe ufisadi uliokithiri kwenye nchi zao.
 
Ubunge hautakiwi kuwa ni ajira. Ni uwakilishi wa wananchi. Enzi za Mwalimu hakuwa analipwa mshahara wo wote na hakukuwa na posho ya kikao ya laki tatu kwa siku. Mbunge alikuwa lazima awe ni mtu ambaye ana kazi yake inayompa kipato.

Tatizo linalotusumbua kwa sasa ni hilo la serikali kuwa inawalipa wabunge wetu mishahara na marupurupu makubwa kuliko mtu mwingine ye yote nchini. Hili ninakubaliana nawe kwamba wawakilishi wetu hawa badala ya kuwa part of us wamekuwa part of serikali.

Tulitegemea Lissu badala ya kusema ataongeza mishahara ya watumishi wa umma mara dufu, angesema atafuta misharaha na marupurupu ya wabunge. Hapo tungalimuunga mkono na kumpatia kura. Kuongeza mishahara ya watumishi wa umma na askari wetu mara dufu mapato yote ya serikali kupitia kodi zetu yangeishia kulipa mishahara tu ya watumishi hawa na bado hayangalitosha na hivyo kulazimishwa kuongezewa kodi. Hili halikubaliki.
Bwashee wabunge wanawakilisha matumbo yao hawakuwakilishi wewe!
 
Mbunge gani anataka bunge livunjwe? Wakishaingia hutawasikia maana wakileta ujinga Rais anavunja bunge tunarudi kwenye uchaguzi wa wabunge na yeye ndiye anasimamia uchaguzi. Thubutuuuuu!
Kwani hukuona au kusikia pale Zitto alipojaribu kukusanya sahihi za wabunge kutaka kupeleka hoja ya kumuondoa JPM kuwa rais wa JMT ili bunge livunjwe na uchaguzi urudiwe? Wabunge wote wa upinzani waliweka saini zao lakini idadi yao haikufikia ile idadi inayotakiwa na katiba kupeleka hoja hiyo bungeni. Wabunge wa chama tawala hawakusaini hilo likaratasi lake na likaishia hapo. Sasa Lissu akipata urais wabunge wote wa ccm watafanya kama alivyfanya Zitto, na kwa kuwa ni wengi idadi inayotakiwa kikatiba itafikiwa na Lissu atakuwa out!
 
..bunge haliwezi ku-impeach raisi anayeungwa mkono na wananchi.

..lakini itakuwa ni bahati njema kwa taifa kama tutalazimika kuunda serikali ya mseto.

..kwa kweli hilo likitokea tutaweza kuzi-sanitize siasa zetu ili ziwe kwa manufaa ya nchi na siyo vyama.

..naamini kila upande, kwa maana ya bunge na executive, watafanya kila jitihada kufanya kazi kwa mashirikiano.
CCM haitakubali kuwa pamoja na vibaraka wa mabeberu. Shida ndiyo inaanzia hapo. Angalikuwa Lipumba au Mbatia hapo ingalikuwa poa. Si hawa jamaa zetu.
 
CCM haitakubali kuwa pamoja na vibaraka wa mabeberu. Shida ndiyo inaazia hapo. Angalikuwa Lipumba au Mbatia hapo ingalikuwa poa. Si hawa jamaa zetu.

..raisi anayekuwa impeached ni yule asiyeungwa mkono na wananchi.

..na ccm wakijaribu kumu-impeach raisi wanaweza kukutana na resistance ya wenzao wanaounga mkono serikali ya mseto.

..na impeachment proceedings is a risky business, ukiijaribu na ikashindwa, chama kinaweza kupoteza uungwaji mkono na wananchi.

..njia bora ni kufanya kazi pamoja. kuweka mbele maslahi ya nchi badala ya maslahi ya vyama.
 
Ccm walishapoteza mwelekeo wamebakiza kiduchu waende chini
IMG_20200903_163731.jpg
 
..bunge haliwezi ku-impeach raisi anayeungwa mkono na wananchi.

..lakini itakuwa ni bahati njema kwa taifa kama tutalazimika kuunda serikali ya mseto.

..kwa kweli hilo likitokea tutaweza kuzi-sanitize siasa zetu ili ziwe kwa manufaa ya nchi na siyo vyama.

..naamini kila upande, kwa maana ya bunge na executive, watafanya kila jitihada kufanya kazi kwa mashirikiano.
Mmeshindwa kuipata hiyo demokrasia mnayoililia ndani ya Chadema mtaweza kuipata ya nchi nzima? Chadema ipo kwenye dictatorship ya Mbowe ingawa ukweli huu mkiambiwa mnachukia. Huyo mlevi wa konyagi sijui aliwaloga vipi.

Kubadili nchi yoyote ile ni rahisi sana kama huko kwenye chama chenu mko na demokrasia ya kweli, lakini huko kwenu wote mnawewesekaweweseka tu nani atawaamini? Angalia kina Zito Kabwe, Membe et al ni aibu tupu, uchu wa madaraka ndio umewatawala.

To be honest with you JPM and CCM hawana mshindani wanavinjari tu. You better cleanse your parties.
 
Kwani hukuona au kusikia pale Zitto alipojaribu kukusanya sahihi za wabunge kutaka kupeleka hoja ya kumuondoa JPM kuwa rais wa JMT ili bunge livunjwe na uchaguzi urudiwe? Wabunge wote wa upinzani waliweka saini zao lakini idadi yao haikufikia ile idadi inayotakiwa na katiba kupeleka hoja hiyo bungeni. Wabunge wa chama tawala hawakusaini hilo likaratasi lake na likaishia hapo. Sasa Lissu akipata urais wabunge wote wa ccm watafanya kama alivyfanya Zitto, na kwa kuwa ni wengi idadi inayotakiwa kikatiba itafikiwa na Lissu atakuwa out!
Akiwa out sheria inasemaje? Nani atashikilia uongozi ili kufanya uchaguzi wa Rais mwingine?
 
Kabla hawajamaliza kuweka sahihi rais anatangaza kulivunja bunge. Wakati huo yeye alishajiteulia madc wakurugenzi sasa hapo ndio ccm inaenda kufia hapo
Kwani hukuona au kusikia pale Zitto alipojaribu kukusanya sahihi za wabunge kutaka kupeleka hoja ya kumuondoa JPM kuwa rais wa JMT ili bunge livunjwe na uchaguzi urudiwe? Wabunge wote wa upinzani waliweka saini zao lakini idadi yao haikufikia ile idadi inayotakiwa na katiba kupeleka hoja hiyo bungeni. Wabunge wa chama tawala hawakusaini hilo likaratasi lake na likaishia hapo. Sasa Lissu akipata urais wabunge wote wa ccm watafanya kama alivyfanya Zitto, na kwa kuwa ni wengi idadi inayotakiwa kikatiba itafikiwa na Lissu atakuwa out!
 
Kabla hawajamaliza kuweka sahihi rais anatangaza kulivunja bunge. Wakati huo yeye alishajiteulia madc wakurugenzi sasa hapo ndio ccm inaenda kufia hapo
Hizo teuzi zake zitakuwa batili. Na akiendelea kuleta fyoko fyoko wanaume wanamuweka lockdown nyumbani kwake kama ilivyofanyika kwa Mzee Mugabe huko Zimbabwe.
 
Utawala wa nchi yetu na nchi zote za kidemokrasia ni utawala wa sheria. Na sheria hizo tunazitunga wenyewe wananchi kupitia wawakilishi wetu kwenye bunge letu. Sisi ndiyo tunaoamua nchi yetu tuiendeshe namna gani kupitia sheria tutakazozitunga au kuzibadilisha kupitia wawakilishi wetu (wabunge) bungeni. Yaani mamlaka yote ya nchi ni ya kwetu sisi wananchi kupitia bunge letu. Yaani hata huyo rais atakayechaguliwa tuna mamlaka ya kumuondoa madarakani hata baada ya siku chache tu baada ya kuchaguliwa kupitia wawakilishi wetu bungeni. Hii ndiyo maana ya demokrasia. 'The government of the people by the people for the people'

Kwa msingi huo wa utawala wa sheria, kama rais atakayechaguliwa kama hatakuwa na wabunge wa kutosha bungeni hataweza hata kidogo kufanya mabadiliko ye yote ya utendaji kazi serikalini. Hataweza kutekeleza hata moja ya anayoyaahidi kwenye hizi kampeni hususani eti kufumua TRA, Traffic police, NHIF, kuongeza mishahara ya watumishi wa umma mara dufu, kutoa matibabu na ubwabwa bure kwa kila mtanzania, kuruhusu uvuvi wa nyanya ndogo utakaomalima samaki wote nk.

Ili hayo yote anayoahidi yaweze kutekelezwa ni lazima yaidhinishwe na wabunge wetu kupitia utungaji au marekebisho ya sheria. Ukweli tunaojua ni kuwa hawa jamaa zetu wanaotoa hizi ahadi za porojo zinazofurahisha lakini si za uhalisia hawataweza hata kidogo kuwa na wabunge wa kutosha huko bungeni. Yaani idadi ya wabunge wao watakaoshinda haitafika hata robo ya wabunge wote. Maana yake ni kuwa miswada yao bungeni itapigwa chini na wabunge wa ccm ambao idadi yao itazidi theruthi mbili, idadi inayoruhusu kubadili hata katiba kwa jinsi wanavyotaka. Idadi inayoruhusu kumtoa madarakani rais wa nchi saa yo yote wanayotaka

Huu ndiyo ukweli wananchi wanaopaswa kuujua. Wao ndiyo wenye nchi.
Itakuwa serikali ya mseto, kwani katiba inasema waziri mkuu atatoka kwenye chama chenye wabunge wengi. Hivyo chama kitakacho mtoa waziri mkuu pia kitatoa mwaziri kadhaa. Na hapo nchi yetu itasitawi kidemokrasia na mijadala huru ya kibunge, maana hatutakuwa na bughudha au ubaguzi wa kichama. Kimoja kina prezidaa na kingine kina pm, halafu vyote vimechangia mawaziri.

Sent from my TECNO F3 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom