Ukweli usemwe: Siasa za huko ni ngumu Rostam, CRDB na Dangote walishindwa

Nchi ya kijamaa hii,nani ana muda wa kunyanyua wafanyabiashara wa ndani?

Rais wa nchi anasema nataka matajiri waishi kama mashetani?Watu wa dizaini hio ndio uwaambie wanyanyue wazawa?
 
Kwa hiyo unataka Watanzania warudi Igunga na kuridhika?

Kweli wewe mtu wa mshahara.
 
Kuna wengine wako kama kasuku wakenya hata ukikaa nao ukiwanunulia kinywaji chako watakunywa ila chake huwezi kunywa kamwe ni wabinafsi wa hali ya juu sanasana wanavizia ardhi na fursa zilizoko Tanzania hivi nchi gani wanathubutu hadi kudanganya mlima kilimanjaro hupo nchini mwao ili wapate watalii
 
Rostam amepngea ukweli mtupu hakuna mtanzania ambaye ataweza wekeza kenya kirahisi!

Tanzania kuna mazingira rahisi sana ya kuwekeza sema watanzania kwakuwa hatutembei basi tunadhani kwetu ni pagumu sana...

Wakenya wanataka kufanya kazi nchini free ndio maana wanajidai kusema watanzania wasisumbuliwe hahaha

Hivi Rostam pamoja na kumuona Kenyatta bado alishindwa!

Kenyatta amethibitisha wazi kuwa mahindi yetu hayana sumukavu!
 
Hata kama kuna ugumu kufungua kampuni kule, bado tuna nafasi ya kufanya nao biashara na tukanufaika pia, maza kafungua nchi tumuunge mkono.

Nani aliifunga? Wao si ndio walianza? Mahindi yetu hayana sumukavu tena?
 
Azam juice ilipigwa vita kwa sasa haipo huko, waulize TBL wanajua figusi figusi za hao jamaa, TBL bia zake zilipigwa vita mbaya mno
 
Nani aliifunga? Wao si ndio walianza? Mahindi yetu hayana sumukavu tena?
Inatakiwa ujiulize kwanini alifunga na kwanini kafungua, kwa kukusaidia tu yote yale yalitokea kwa sababu marehemu dikiteta magufuli alikuwa mweupe ktk masuala ya diplomasia ya uchumi.
 
Hicho wanachofanya Wakenya huko kwao kwenye ushindani, ndio kinachofanywa na ccm hapa nchini kwenye siasa na unaona sawa. Kama unaona huku ni sawa, ni vyema ukae kwa kutulia kwenye hiyo tabia ya wakenya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…