Ukweli usemwe, Yanga bado sana!

Peramiho yetu

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2018
Posts
5,303
Reaction score
14,983
Huenda nikashambuliwa na mashabiki wa yanga lakini ukweli usemwe, Yanga kimataifa bado sana! Anahtaji miaka kama miwil tena ya mikiki mikiki kama hii.

Yanga ni timu waoga sana, tena mno inapokuja kucheza mechi za nje ya nchi, hata iwe ya kirafiki hawapendi kuona udhaifu wao ukitokea mbele yao na haya ndiyo matokeo yake.

Huwezi kujipima na Mbuni FC halafu uende ukacheze CAFCL eti kiwe ndiyo kipimo, hapana nakataa kabisa. Simba haina uoga huo hata ikifungwa, kwao ni sehemu ya somo na kurekebisha tatizo.

Yanga wanataka ushindi tu ili kuwafurahisha mashabiki wao basi, ndiyo maana wanachagua timu za madaraja ya chini ili wapate ushindi. Ifike wakati mashabiki tuache kuwa sehemu ya ujinga huu, tuipigie kelele timu yetu izinduke.

Matarajio leo kwa mashabiki wa Yanga yalikuwa makubwa sana sababu ya maneno ya kuhadaa kutoka kwa viongozi wetu. Timu inawachezaji baadhi ni wazuri sana, sina haja ya kuwataja ila kwa mtindo huu hawatakaa hapo.

Beki zetu ni shida sana, zinajichanganya hazina uelewano mzuri, naomba liangaliwe hili. Kule Sudan asilimia za usindi ni 30% tu, kwa hiyo mech yetu likuwa hapa nyumbani. Ila tumeshindwa kutumia nafasi nyingi ikiwemo kona nyingi sana, lakini hakuna wamliziaji.

Kila la heri Simba hapo kesho, iheshimisheni nchi kesho. Tupo nyuma yenu.

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Mimi nafikiri yanga wamefungwa na kocha wao wenyewe kwa sababu zifuatazo.

1. Huwezi wachezesha Aziz ,morison and Fei pamoja. Kwakua wote siwakabaji wazuri nawote almost wanacheza style moja nahasa Fei na Azizi

2. Fei sio namba 8 or 6 ni bora sana akicheza 10 ambayo alikua anacheza Azizi.

3. Ukitaka mfumo wa namba 1 ufanye kazi wape free role wote halafu uwe na 6,8 ziwe natabia ya kukaba ilikuzuia counter attack.

4. Wachezaji walijiamini kua wanashinda bila kucheza.

5. Analyst wa yanga hakufanya kazi yake vzr sub za Ibenga zilikua6 bora kuliko za Nabi
 
Hii ligi ya nbc sio kipimo sahihi kwenda caf champion league, ndo maana simba sc wakiwa huko wanabadilika kabisa sio hawa wanaocheza hapa kwa mkapa na ihefu fc.
Huwa wanabadilika sana, huko huwa wanawasha mpaka moto uwanjani.
 
Bado sana kwaopi? Unbeaten ya ngapi hii unahesabu?
Yanga ni kubwa ndg

Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app
Nyinyi ni unbeaten wa mchongo . Kuna mechi za ndani mlistahili vipigo Ila mliokolewa na maamuzi mabovu ya waamuzi wa mchongo. Kiufupi timu lenu sio bora kama mnavyojidai na Leo mngeshinda refa angekuwa Arajiga.
 
Yanga hawezi kufungwa na Al hilal, Yanga anaingia Makundi kibabe.
 
Tokea lini kenge wa mikiani ukawa yanga, kwaiyo kucheza mechi za kirafiki kubwa ndo unafanikiwa kwenye mashindano nani kakuambia? Peleka utahira wako uko umbumbuni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…