Peramiho yetu
JF-Expert Member
- May 25, 2018
- 5,303
- 14,983
Huenda nikashambuliwa na mashabiki wa yanga lakini ukweli usemwe, Yanga kimataifa bado sana! Anahtaji miaka kama miwil tena ya mikiki mikiki kama hii.
Yanga ni timu waoga sana, tena mno inapokuja kucheza mechi za nje ya nchi, hata iwe ya kirafiki hawapendi kuona udhaifu wao ukitokea mbele yao na haya ndiyo matokeo yake.
Huwezi kujipima na Mbuni FC halafu uende ukacheze CAFCL eti kiwe ndiyo kipimo, hapana nakataa kabisa. Simba haina uoga huo hata ikifungwa, kwao ni sehemu ya somo na kurekebisha tatizo.
Yanga wanataka ushindi tu ili kuwafurahisha mashabiki wao basi, ndiyo maana wanachagua timu za madaraja ya chini ili wapate ushindi. Ifike wakati mashabiki tuache kuwa sehemu ya ujinga huu, tuipigie kelele timu yetu izinduke.
Matarajio leo kwa mashabiki wa Yanga yalikuwa makubwa sana sababu ya maneno ya kuhadaa kutoka kwa viongozi wetu. Timu inawachezaji baadhi ni wazuri sana, sina haja ya kuwataja ila kwa mtindo huu hawatakaa hapo.
Beki zetu ni shida sana, zinajichanganya hazina uelewano mzuri, naomba liangaliwe hili. Kule Sudan asilimia za usindi ni 30% tu, kwa hiyo mech yetu likuwa hapa nyumbani. Ila tumeshindwa kutumia nafasi nyingi ikiwemo kona nyingi sana, lakini hakuna wamliziaji.
Kila la heri Simba hapo kesho, iheshimisheni nchi kesho. Tupo nyuma yenu.
Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Yanga ni timu waoga sana, tena mno inapokuja kucheza mechi za nje ya nchi, hata iwe ya kirafiki hawapendi kuona udhaifu wao ukitokea mbele yao na haya ndiyo matokeo yake.
Huwezi kujipima na Mbuni FC halafu uende ukacheze CAFCL eti kiwe ndiyo kipimo, hapana nakataa kabisa. Simba haina uoga huo hata ikifungwa, kwao ni sehemu ya somo na kurekebisha tatizo.
Yanga wanataka ushindi tu ili kuwafurahisha mashabiki wao basi, ndiyo maana wanachagua timu za madaraja ya chini ili wapate ushindi. Ifike wakati mashabiki tuache kuwa sehemu ya ujinga huu, tuipigie kelele timu yetu izinduke.
Matarajio leo kwa mashabiki wa Yanga yalikuwa makubwa sana sababu ya maneno ya kuhadaa kutoka kwa viongozi wetu. Timu inawachezaji baadhi ni wazuri sana, sina haja ya kuwataja ila kwa mtindo huu hawatakaa hapo.
Beki zetu ni shida sana, zinajichanganya hazina uelewano mzuri, naomba liangaliwe hili. Kule Sudan asilimia za usindi ni 30% tu, kwa hiyo mech yetu likuwa hapa nyumbani. Ila tumeshindwa kutumia nafasi nyingi ikiwemo kona nyingi sana, lakini hakuna wamliziaji.
Kila la heri Simba hapo kesho, iheshimisheni nchi kesho. Tupo nyuma yenu.
Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app