Ukweli usemwe, Yanga wametuacha Mbali sana upande wa Jezi

Na tutanunua na tutavaa...
Nyoka nyie
 
Halafu jezi za Yanga ni picha tuu...mtaani huku ni mbayaa bora ile nyeusi..
 
Simba haitegemei mauzo ya jezi maana tayari VUNJABEI alishalipa pesa , akiharibu zisinunulike yeye ndo anapoteza sio Simba unlike GSM ambayo yenyewe inauza jezi ndo ipate pesa tena haina hata mkataba
 
Kwahiyo jezi ya liverpool ni ya kawaida?
Ya real madrid ni ya kawaida?
Muogope Mungu
 
Yaani umri huo unawaza jezi? Ingekuwa hivo polisi wa tz wasingevaa uniform zao mana ni mbaya sana. Jezi tunanunua sio sababu ya uzuri bali niuzalendo kuchangia timu. Kuna jezi mbaya kuliko zile za yanga za vinyago? Ni zilivalika sana tuu
Kwa mara ya kwanza safari hii mtanunua jez kwa ajili ya uzalendo.. Gud
 
Jesrey zenu nzuri ndio,ila swali ni je??????KUNA MASHINDANO YA JERSEY KWENYE SOKA??KAMA YAPO HONGERENI
Sawa amna mashindano ya jezi lakini lazima team ivalishwe vizuri ndio maana uwa inawekwa tenda na wabunifu wanapeleka maombi na viongozi wanaangalia sifa

Ingekuwa bora kuvaa tu kusingekuwa na haja ya kutoa tenda anachukuliwa yoyote tu af fresh

Sawa kwenye ubora na uzuri wa jezi tuuache je hili la mechi kuchezwa tar11 na jezi kuanza kuuzwa tar15 limekaaje?

Na unakumbuka msimu huu tulianza na ligi na jezi za msimu uliopita?

Kwenye hii ishu mkinga hatakiwi kulindwa kwa namna yoyote amefeli na ametufelisha
 
hivi vijezi anaokota kule mtaani China kwa bei ya 2000 ya TZ
 
Simba haitegemei mauzo ya jezi maana tayari VUNJABEI alishalipa pesa , akiharibu zisinunulike yeye ndo anapoteza sio Simba unlike GSM ambayo yenyewe inauza jezi ndo ipate pesa tena haina hata mkataba
Ushabiki usitufanye matahira jamani, uwezi ukaacha mtu atumie brand yako kutengeneza bidhaa mbovu eti kisa tu ashakulipa pesa yako. Leo ukitaka kufanya franchise ya mgahawa wa McDonald's lazima walete wataalamu wao kukuelekeza kila kitu kinavyofanyika na kukufatilia pia maana wanajua ukiaribu wewe umearibu na brand yao pia hawawezi kukuacha tu ufanye unavyotaka ilimradi wao ushawalipa pesa yao. Rage apewe phd ya heshima kwa kweli
 
AKILI KIDODA

JERSEY HAICHUKUI UBINGWA WA AFRICA.
HAICHEZI MPIRA..

WATU WANATAKA UBINGWA WA CAF.
 
Kwahiyo jezi ya liverpool ni ya kawaida?
Ya real madrid ni ya kawaida?
Muogope Mungu
Ndiyo. Mifano yote niliyosema na mingine niliyoacha kama Brazil, Arsenal, Man City jezi zao zinafanana kwa usimple wake. Tunaziona kali kwa sababu zinatumika na timu zinazojulikana kwa mpira wa hali ya juu.



 
W ni guluguja kweli, watu wanawaza malengo makubwa ya kufika mbali zaidi kimafanikio w unaongelea mambo ayo hayakupeleki kokote....ngoja tusubir utopolo kama hyo jezi itawasadia kufunga magoli. W ni utopolo bila kupepesa macho.
Hahahhaaaa,ila wakuu mlikuwa mna nafasi kubwa sana ya kutengeneza Jezi nzuri kuliko Yanga kwa kuwa Jezi zao mlishaziona kwenye upungufu pia mlishapaona,mngelitoa Jezi nzuri point yako ingekuwa ya kuwa mnafanya vizuri kwenye Jezi mpaka uwanjani
 
Kwani kuna kiongozi wa Simba amelalamika kuwa VB hawaletei bidhaa za viwango?

Tatizo mnataka mvae jezi mnapoenda club, kwenye harusi, kwenye misiba.....

Na kama ni quality ya material, mdogo mdogo tu atafika huko. Kumbuka Simba iliamua kumpa nafasi na kumkuza mzawa mwenzetu ili baadae tuwe na adidad na nike za kwetu. Ungeniambia jezi inachanika hovyo au inavuja rangi ningekuelewa.
 
Hahahhaaaa,ila wakuu mlikuwa mna nafasi kubwa sana ya kutengeneza Jezi nzuri kuliko Yanga kwa kuwa Jezi zao mlishaziona kwenye upungufu pia mlishapaona,mngelitoa Jezi nzuri point yako ingekuwa ya kuwa mnafanya vizuri kwenye Jezi mpaka uwanjani
Kwan ww zile jezi unaona zina shida gani? Usifosi tufanane, Utopolo ndio inatakiwa ipambane kwenye maendeleo ya club na sio kuzungumzia matambara hayo hayapeleki timu kokote
 
Hahahhaaaa,ila wakuu mlikuwa mna nafasi kubwa sana ya kutengeneza Jezi nzuri kuliko Yanga kwa kuwa Jezi zao mlishaziona kwenye upungufu pia mlishapaona,mngelitoa Jezi nzuri point yako ingekuwa ya kuwa mnafanya vizuri kwenye Jezi mpaka uwanjani
Tukiwaambiaga Simba hawawachukulii Yanga kama mshindani wao huwa hamuamini, mnataka ushahidi gani tena? Ndiyo maana tukio la jana lilikuwa simple sana halikuwa na mbwembwe nyingi. Nyie mmeokoteza mamodo wasiojua hata kusimama jukwaani, sisi tumeshusha jezi kwa drone, hatukuzi mambo wakati kuna mambo mengi muhimu zaidi ya kufanya.
 
Simba haitegemei mauzo ya jezi maana tayari VUNJABEI alishalipa pesa , akiharibu zisinunulike yeye ndo anapoteza sio Simba unlike GSM ambayo yenyewe inauza jezi ndo ipate pesa tena haina hata mkataba
Hichi ulichoandika una uhakika nacho?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…