Ukweli Usiosemwa: Hali Halisi ya Matukio Muhimbili November 2016 Kuhusu Janeth Magufuli

Ukweli Usiosemwa: Hali Halisi ya Matukio Muhimbili November 2016 Kuhusu Janeth Magufuli

[@moderator nimeshindwa niweke wapi hii comment, unaweza unganisha na uzi wowote]

Tukio la Janeth Magufuli kulazwa Muhimbili Novemba 2016 linapaswa kufafanuliwa kwa muktadha wa ukweli na uwazi. Huwa inahuzunisha sana kuona watu wanaweza wakawa wanaongelea tukio la kusimuliwa, wakalifanya ukweli wakati halina ukweli. Magufuli pamoja na madhaifu mengi aliyokuwa nayo, alisingiziwa mengi sana, na wengi hayo waliyoyasikia wameyafanya kuwa ndio maisha ya Magufuli wakati wa Uhai wake. Na mmoja wa waliodanganywa, lakini anadhani ana habari ya kweli ni Erick Kabendera. Lakini unaelewa kwa namna Erick alivyopita katika tanuru la moto, anaweza asiyafikirie vyema hata yale aliyosimuliwa.

Wakati Mama Janeth Magufuli analazwa Muhimbili Novemba 2016, huyu Mama hakupata kipigo chochote, lakini ndio ilikuwa habari ya mjini. Ni muhimu kwa wale waliohusika kwa namna moja au nyingine na matibabu yake bila kusimuliwa kuweka wazi kwamba hali yake ya kiafya kipindi kile haikuwa na uhusiano wowote na kipigo au ukatili wa aina yoyote. Badala yake, lilikuwa jambo la kiafya ambalo lilihitaji matibabu ya kitaalamu na uangalizi wa karibu. Kama kila mtu siri zake za matibabu zingetolewa nje, basi labda tungekuwa na mtazamo tofauti kuhusu mambo mengi sana kuhusu watu na vitu. Mfano kwa waliofariki unaweza ukaondoa imani za kurogwa, kupigwa n.k, na kwa wale wanaoishi unaweza gundua kwamba wengine labda wamebakiza siku chache, na hata ukisikia wamefariki, hutoshtuka.

Kwa wale waliokuwa karibu na mazingira hayo ya hospitali wakati Janeth amelazwa, dalili na hali iliyoshughulikiwa hospitalini kipindi hicho haikuonyesha ishara yoyote ya majeraha yanayoweza kuhusishwa na ukatili wa kimwili. Uchunguzi uliofanywa ulionyesha sababu za kiafya zinazohusiana na matatizo ya kawaida yanayoweza kumpata mtu yeyote na hakika yanawapata watu wengi tu kila siku. Shida ukiwa mke wa Rais, watu wanadhani haupaswi kulazwa.

Katika kipindi hicho, Janeth akiwa amelazwa, Magufuli alionekana kujali sana na alikuwa karibu na mkewe, akihakikisha kuwa anapata huduma bora. Hayati Magufuli, alitumia muda wake mwingi usiku kukaa na mkewe wodini Muhimbili. Hakuna waandishi wa habari wajualo hilo, maana walilishwa matango pori. Taarifa za uvumi zinazohusiana na tukio hili hazina msingi wowote wa kweli, na ni muhimu kutozizingatia ili kuepuka kueneza dhana potofu.

Kutokana na Erick Kabendera kulishwa tango pori hilo (najua anajiamini sana na aliloandika), inaonesha hata habari nyingine kuhusu Magufuli, zitakuwa ni hekaya, zisizokuwa na ukweli.

Ni muhimu sana sisi binadamu kuacha kuongelea habari tusizokuwa na uhakika nazo hasa za kifamilia. Ukiwa na hizo tabia, usishangae watu wakiongelea habari zako, ambazo nawe hata huzijui. Karma is real.


Kabendera ana maumivu na magufuli
But Kwa upande mwingine hata waliochapisha hiko kitabu nao wanamakosa coz sidhani kama ni Sawa Sawa kupublish taarifa ambazo hazina uhakika wa 100%
 
leta uchunguzi wako pia tuupime Gentleman kama Tlaatlaah anavosemaga humu ndani.
Iruhusiwe timu Dkt Magufuli na timu yenu ya wezi tufanye mijadala tuone nani ataibuka mshindi. Nyie ni ka kikundi ka wajinga wajinga yaani mlimuua Dkt Magufuli na bado mnaendelea kutusimanga, inauma sana tena sana. Ila Mungu wetu yupo hai anatuona machozi yetu
 
Shida ya serikali yenu haipendi kuambiwa ukweli na inafichaficha sana mambo kwa manufaa yake.

Ingekua inaweka wazi walau baadhi ya mambo au kutofumbia macho mabaya yanayofanywa na viongozi wake, hizi zinazoitwa porojo za Erick hakuna ambae angeziamini hata kidogo.

Ila sasa kuna tetesi tetesi tu zinazosemwa kwa mafumbo huku wengine hawayaelewi hayo mafumbo, mwisho wa siku akija mtu kupoint kidole kwa wahusika moja kwa moja ndio itakua reference hiyo.
 
Iruhusiwe timu Dkt Magufuli na timu yenu ya wezi tufanye mijadala tuone nani ataibuka mshindi. Nyie ni ka kikundi ka wajinga wajinga yaani mlimuua Dkt Magufuli na bado mnaendelea kutusimanga, inauma sana tena sana. Ila Mungu wetu yupo hai anatuona machozi yetu
mimi sio mwizi na sijawahi kuwa mwizi ndugu yangu- hebu futa hiyi kauli yako. Sijashiriki kwa namna yeyote kwenye hayo mauwaji ya JPM kama ulivyo andika. Kuuliza swali au kutoa suggestion sio kukusimanga, hebu jiongezi kidogo tafadhari. kuhusu" wajinga" acha matusi- comment bila matusi itapendeza sana. Machozi ni wote wanalia, wasitendewa haki na waliompoteza JPM- equlibrium iko wapi? Hisia pembeni, mshika uskani anafaa sana kuwaleta watu pamoja... Wateswa wa JPM sasa wanaongea, huko ndani ndani wanaruka na kukanyagana- acheni nao pia wateme nyongo. kuchapwa wachapwe na kulia pia wazuiwe kulia, hii uliiona wapi?
 
Kwanini mpk aandike madhaifu yake,
Kuna shida gani kuyaandika mapungufu yake? Mbona nyinyi mlikuwa makasuku wa kuimba mapambio ya kusifu na kuabudu?
ukumbuke tayari huyu mtu ni marehemu,nini kiko nyuma yake,kuna kiongozi ambaye amepita hakuwa na mapungufu?
Kwa mtu ambaye alitumia vibaya vyombo vya dola, akatisha, akakamata, akatesa, akafunga na kuua wengine, basi mtu huyo akifa ndiyo wakati sahihi wa kumlipizia kisasi. Ili mlio baki mjifunze kwamba kumbe kuna masha baada ya kifo, kumbe kufa siyo mwisho wa kila kitu.
Tunapoongelea Kutesa na kuua watu, hayo siyo mapungufu. Huo ni uuaji, ukatili. Mapungufu husaheka lakini siyo uuaji na ukatili wa aina ya Magufuli.
tulisikia ya Nyerere,Mwinyi,Mkapa na hata Kikwete,sasa kwanini ya Magufuli ayavalie njuga mpaka aandike kitabu,
Kwanini umlazimishe aandike kuhusu Kikwete, Mwinyi, Nerere na Mkapa? Hao ndiyo walimtesa yeye?
Ukitaka unaweza wewe ukaandika kitabu cha hao, yeye ameshaandika cha Magufuli.
kwahiyo na huyu tulie naye pia akipita ataandika kitabu.
Akiendeleza ujinga wake na asipojitoa kugombea mwaka huu, haitasubiriwa afe, bali kitaandikwa akiwa madarakani tena huyu taarifa zake ni kama zipo kwenye oublic domain tu. Ni mwepesi kuliko unyoya mama wa watu, unaweza ukadhani hata siyo rais, sijui ndiyo mfumo haumtaki hivyo umeamua kutomlinda taatifa zake?
Hakuna binadamu asiye na mapungufu,mazuri yapo na mabaya yapo,atuache tujenge nchi asituletee chuki ili kutuharibia amani ya nchi yetu...
Uuaji, ukattili, unyanyasij siyo mapunguffu.

Hata kipindi anafanya mauaji bado wazalendo waliendelea kujenga nchi huku wakiwa hawana uhakika wa ka watafika kesho.
 
Unajua kabendera kwa ufupi kajichimbia shimo na kujifuta Tanganyika. Anadhani kama ilivyokuwa kwa utawala wa mwanzo wa Dkt Samia kudhani Dkt Magufuli anachukiwa ila baadaye kaja kujua wanaomchukia ni wale waovu ambao hata kura hawapigi wengine hawapo hata Tanzania. Kabendera kama anapitia hizi thread ajue kabisa amejiharibia sana akitaka ushahidi aje ajaribu kusimama kariakoo aseme kuhusu kitabu chake watamuua kwa kummwagia petroli afe na kitabu chake cha kijinga kitachomwa moto
Hakuna kitu kama hicho binti yangu nikuambie kitu kimoja katika watu walioongoza kufurahia kifo cha magufuli ni pamoja na wafanyabiashara mimi nakueleza hivyo nipo sokoni sio saluni kama wewe
 
leta uchunguzi wako pia tuupime Gentleman kama Tlaatlaah anavosemaga humu ndani.
Gentleman,
ni muhimu zaidi kwanza,
huyo bendera akapata usaidizi wa kisaikojia kabla hali yake kuaelekea kua mbaya ziada tuendako ni hatari kwa afya na maisha yake 🐒
 
Mwamba yukowapi aje amweke Erick kwenye Mfuko wa salfeti...hakika kila mtu njia yetu ni moja, anaekuua anakusaidia kupumzika mapema hii Tanzania inachosha asikwambie mtu.
 
[@moderator nimeshindwa niweke wapi hii comment, unaweza unganisha na uzi wowote]

Tukio la Janeth Magufuli kulazwa Muhimbili Novemba 2016 linapaswa kufafanuliwa kwa muktadha wa ukweli na uwazi. Huwa inahuzunisha sana kuona watu wanaweza wakawa wanaongelea tukio la kusimuliwa, wakalifanya ukweli wakati halina ukweli. Magufuli pamoja na madhaifu mengi aliyokuwa nayo, alisingiziwa mengi sana, na wengi hayo waliyoyasikia wameyafanya kuwa ndio maisha ya Magufuli wakati wa Uhai wake. Na mmoja wa waliodanganywa, lakini anadhani ana habari ya kweli ni Erick Kabendera. Lakini unaelewa kwa namna Erick alivyopita katika tanuru la moto, anaweza asiyafikirie vyema hata yale aliyosimuliwa.

Wakati Mama Janeth Magufuli analazwa Muhimbili Novemba 2016, huyu Mama hakupata kipigo chochote, lakini ndio ilikuwa habari ya mjini. Ni muhimu kwa wale waliohusika kwa namna moja au nyingine na matibabu yake bila kusimuliwa kuweka wazi kwamba hali yake ya kiafya kipindi kile haikuwa na uhusiano wowote na kipigo au ukatili wa aina yoyote. Badala yake, lilikuwa jambo la kiafya ambalo lilihitaji matibabu ya kitaalamu na uangalizi wa karibu. Kama kila mtu siri zake za matibabu zingetolewa nje, basi labda tungekuwa na mtazamo tofauti kuhusu mambo mengi sana kuhusu watu na vitu. Mfano kwa waliofariki unaweza ukaondoa imani za kurogwa, kupigwa n.k, na kwa wale wanaoishi unaweza gundua kwamba wengine labda wamebakiza siku chache, na hata ukisikia wamefariki, hutoshtuka.

Kwa wale waliokuwa karibu na mazingira hayo ya hospitali wakati Janeth amelazwa, dalili na hali iliyoshughulikiwa hospitalini kipindi hicho haikuonyesha ishara yoyote ya majeraha yanayoweza kuhusishwa na ukatili wa kimwili. Uchunguzi uliofanywa ulionyesha sababu za kiafya zinazohusiana na matatizo ya kawaida yanayoweza kumpata mtu yeyote na hakika yanawapata watu wengi tu kila siku. Shida ukiwa mke wa Rais, watu wanadhani haupaswi kulazwa.

Katika kipindi hicho, Janeth akiwa amelazwa, Magufuli alionekana kujali sana na alikuwa karibu na mkewe, akihakikisha kuwa anapata huduma bora. Hayati Magufuli, alitumia muda wake mwingi usiku kukaa na mkewe wodini Muhimbili. Hakuna waandishi wa habari wajualo hilo, maana walilishwa matango pori. Taarifa za uvumi zinazohusiana na tukio hili hazina msingi wowote wa kweli, na ni muhimu kutozizingatia ili kuepuka kueneza dhana potofu.

Kutokana na Erick Kabendera kulishwa tango pori hilo (najua anajiamini sana na aliloandika), inaonesha hata habari nyingine kuhusu Magufuli, zitakuwa ni hekaya, zisizokuwa na ukweli.

Ni muhimu sana sisi binadamu kuacha kuongelea habari tusizokuwa na uhakika nazo hasa za kifamilia. Ukiwa na hizo tabia, usishangae watu wakiongelea habari zako, ambazo nawe hata huzijui. Karma is real.

Mbona haikukanushwa ilipotolewa mwanzo mpaka chapisho linatoka ndiyo mnataka kutuaminisha kivingine ....!!
 
Umeandika ujinga. Nilitegemea uweke ushahidi wa kile alichokuwa anaumwa mama Janeth hapa jukwaani kwa kulipiga picha Hilo faili la wagonjwa (maana ishakuwa old stori na ashapona ugonjwa wenyewe).

Kumbe unasimuliwa na uchawa wako kwa Magufuli.
 
Kabendera ana maumivu na magufuli
But Kwa upande mwingine hata waliochapisha hiko kitabu nao wanamakosa coz sidhani kama ni Sawa Sawa kupublish taarifa ambazo hazina uhakika wa 100%
Hivi una uhakika gani kuwa hazina uhakika?

Kwa mtu ambaye amepiga ruti za mahakamani kama zote na amesota sana mahabusu unafikiri haelewi nini maana ya ushahidi?
 
[@moderator nimeshindwa niweke wapi hii comment, unaweza unganisha na uzi wowote]

Tukio la Janeth Magufuli kulazwa Muhimbili Novemba 2016 linapaswa kufafanuliwa kwa muktadha wa ukweli na uwazi. Huwa inahuzunisha sana kuona watu wanaweza wakawa wanaongelea tukio la kusimuliwa, wakalifanya ukweli wakati halina ukweli. Magufuli pamoja na madhaifu mengi aliyokuwa nayo, alisingiziwa mengi sana, na wengi hayo waliyoyasikia wameyafanya kuwa ndio maisha ya Magufuli wakati wa Uhai wake. Na mmoja wa waliodanganywa, lakini anadhani ana habari ya kweli ni Erick Kabendera. Lakini unaelewa kwa namna Erick alivyopita katika tanuru la moto, anaweza asiyafikirie vyema hata yale aliyosimuliwa.

Wakati Mama Janeth Magufuli analazwa Muhimbili Novemba 2016, huyu Mama hakupata kipigo chochote, lakini ndio ilikuwa habari ya mjini. Ni muhimu kwa wale waliohusika kwa namna moja au nyingine na matibabu yake bila kusimuliwa kuweka wazi kwamba hali yake ya kiafya kipindi kile haikuwa na uhusiano wowote na kipigo au ukatili wa aina yoyote. Badala yake, lilikuwa jambo la kiafya ambalo lilihitaji matibabu ya kitaalamu na uangalizi wa karibu. Kama kila mtu siri zake za matibabu zingetolewa nje, basi labda tungekuwa na mtazamo tofauti kuhusu mambo mengi sana kuhusu watu na vitu. Mfano kwa waliofariki unaweza ukaondoa imani za kurogwa, kupigwa n.k, na kwa wale wanaoishi unaweza gundua kwamba wengine labda wamebakiza siku chache, na hata ukisikia wamefariki, hutoshtuka.

Kwa wale waliokuwa karibu na mazingira hayo ya hospitali wakati Janeth amelazwa, dalili na hali iliyoshughulikiwa hospitalini kipindi hicho haikuonyesha ishara yoyote ya majeraha yanayoweza kuhusishwa na ukatili wa kimwili. Uchunguzi uliofanywa ulionyesha sababu za kiafya zinazohusiana na matatizo ya kawaida yanayoweza kumpata mtu yeyote na hakika yanawapata watu wengi tu kila siku. Shida ukiwa mke wa Rais, watu wanadhani haupaswi kulazwa.

Katika kipindi hicho, Janeth akiwa amelazwa, Magufuli alionekana kujali sana na alikuwa karibu na mkewe, akihakikisha kuwa anapata huduma bora. Hayati Magufuli, alitumia muda wake mwingi usiku kukaa na mkewe wodini Muhimbili. Hakuna waandishi wa habari wajualo hilo, maana walilishwa matango pori. Taarifa za uvumi zinazohusiana na tukio hili hazina msingi wowote wa kweli, na ni muhimu kutozizingatia ili kuepuka kueneza dhana potofu.

Kutokana na Erick Kabendera kulishwa tango pori hilo (najua anajiamini sana na aliloandika), inaonesha hata habari nyingine kuhusu Magufuli, zitakuwa ni hekaya, zisizokuwa na ukweli.

Ni muhimu sana sisi binadamu kuacha kuongelea habari tusizokuwa na uhakika nazo hasa za kifamilia. Ukiwa na hizo tabia, usishangae watu wakiongelea habari zako, ambazo nawe hata huzijui. Karma is real.
Mwenye Picha ya Erick Kabendera Tafadhali!
 
Mimi sikuupenda utawala wa kidhalimu wa awamu ya 5 lakini naona kama kwa siku hizi chache kuna mashambulizi makali sana dhidi ya mwendakuzimu. Ninadhani tujikite kuongelea yanayotupasa kufanya kwa sisi tulio hai ili kuwa na kesho nzuri zaidi.
 
uwe na akili za kufikiri mbali...unategemea mkewe akilazwa aonesha negative response kuanika ugomvi wao? janet ana wandani wake, aliwasimulia, nao wakasema kwa wandani wao_mlolongo huo mpaka ..............ikawa public....
Kagera yakliwahi majanga, taasisi mbalimbali na raia wakachanga kwa ajili ya majanga yale. Magufuli akachukua zile pesa zote ambazo zilichangwa kwa ajili ya watu waliopata yale majanga. 2
 
Hivi una uhakika gani kuwa hazina uhakika?

Kwa mtu ambaye amepiga ruti za mahakamani kama zote na amesota sana mahabusu unafikiri haelewi nini maana ya ushahidi?

Mbowe amekaa jela mara ngapi?
Ishu yake ya Ugaidi ilikuwa na ushahidi?

Sheria ya Ugaidi inasemaje? Mbona Leo mbowe Yuko huru?
 
Back
Top Bottom