Ukweli usiosemwa juu ya dini za Kiafrika


Inaonekana hichi ulichokiandika huna elimu nacho.

Msingi wingi wake ni misingi,kwa maana ya haraka haraka juu yake kunajengwa mengine. Si kweli dini ni jina tu,ndio maana wewe leo hii ukajua dini si ada na desturi za watu. Kwa minajili hiyo dini ni zaidi ya hivyo unavyofikiria.

Umemgusia Mungu wa Afrika ni kwa waafrika,hili naomba unithibitishie na umejuaje kwamba Mungu wa Afrika ni tofauti na wa wazungu na mfano wake ?

Sasa kama Mungu wa wa afrika ni mmoja kwanini kila kabila lina dini yake kama ulivyoashiria huko juu ?

Ilikuwaje Miungu ikagawana mabara ? Hapa unatakiwa ujue kila jambo linataka elimu,sasa kama unaleta habari za kutunga na wasi wasi useme mapema,usije kushindwa kutetea hiki unachokisema.

Kama ulikubali ya kuwa uchawi uliletwa a wageni hasa wazungu kwanini unaleta uhusiano wa dini za kiafrika na matambiko ? Angalizo usijibu swali hili kama hujaelewa,usije kufanya kama kwenye swali langu la awali.

Nipo ....
 
Hao wazungu na waarabu wametuharibia sana maisha yetu
Hakuna kitu nakichukia kama utumwa. Uwe ule wa kiuchumi, ule wa kiutamaduni, ule wa kisiasa na hata wa kifikra. Mtu mtumwa huonekana dhalili kabisa mbele ya mtwana. Mtwana humfanya atakavyo mtumwa wake! Ndio maana siku ikitokea mtwana kasafiri au kaondoka basi mtumwa ataiga ayafanyayo mtwana kama vile kujitupa katika kitanda cha mtwana, kuzungumza kwa kumwiga mtwana, kulia chakula vyombo vya mtwana n.k, n.k. Kitimtim ni pale atakapojua mtwana amerejea tena ghafla! Atakuwa na mashaka makubwa huyo!

Bado tuna kautumwa fulani ndani yetu, pamoja na kuwa angalau tuna uhuru na tunaweza kujiamulia mambo yetu wenyewe ila bado tunawaza kama watwana wetu! Afrika lazima iamke. Wale jamaa walishatuchezea akili sana! Hadi sa hivi hapa Tanzania utasikia mtu akifanya jambo zuri litavikwa "uzungu" kana kwamba sisi hatuwezi kufanya jambo zuri.
 
Wameharibu mfumo mzima wa maisha yetu kuanzia kufikiri hadi tunavyokula

Hapo kabla sisi tulikuwa tunafikiri vipi na tulikuwa tunakulaje ?
Naomba unipe faida,maana nijuavyo mimi ni kuwa kurudi katika asili ni jambo rahisi sana.
 

Uko sahihi iwapo tu takribani miaka 2019 iliyopita, Yesu hakuwahi kuwepo Duniani, ila kama unakubali kuwa aliwahi kuwepo, basi wazungu wako sahihi zaidi ya 100%
 
Hakuna kitu kibaya kama utumwa wa kifikra na hicho ndicho huleta utumwa wa kiuchumi,kiutamaduni na mengine yote.wazungu wametuteka kifikra tuamini wao ni zaidi yetu na ndo maana tukiona mzungu amevaa suruali imetoboka tunaita ni fashion ila mwafrika mwenzetu akivaa tunamuita maskini.

Utumwa huu wa kifikra umetufanya tusahau ulikotoka na kufikiri tunajua tuendako ,hebu tujiulize kidogo hili swali"kabla ya wazungu kutuletea hizi dini zao tulikuwa tunawasilianaje na mungu?" alikuwa anatujibu vipi maombi yetu tuliokuwa tunafanya kupitia tambiko na mila zingine? Na je walioishi kabla ya ujio wa dini hizi wote wataenda moto?

Waafrika tuamuke tutukuze vilivyo vyetu na kama wazungu ni ndugu zetu na hizi dini zao zipo kwa wote mbona sisi tu ndo tunaita majina yao na wao hawaiti watoto wao masawe,mapunda,mwita,nyambura,akothi ?
 
wametuteka
Usipo elewa-ukikosa elimu utaona dini ya Kristo ni kinyume na dini ya asili. Wafrika kwasababu ya kutokuwa na elimu na pia wao kwa wao yaani wafrika wenyewe kutofundishana kutoka kizazi hadi kizazi ndiyo maana, siyo nyakati zetu;

Hata mababu waliotutangulia waliishi na kutumikia upotofu huu, ambao leo nasi tunaishi na kutumikia. Kudai kwamba wafrika tuna dini yetu ni upotofu unaotokana na ujinga, lakini pia unatokana na uzushi wa baadhi ya wafrika kwa kujua au kutojua wanawapotosha wafrika wenzao wengi (majority) kwa manufaa ya utawala na uchumi.
 
Labda kwa mtazamo wako dini ni nini?
 
Unaposoma, unaposikia, unapojua au unapoelewa dini unakuwa unarejelea Mungu au miungu. Kwahiyo, dini ni mafundisho yote ya utaratibu wa mtu kuabudu Mungu au miungu,mafundisho ya maonyo na jinsi ya kuishi na kuenenda katika maisha.

Dini inaporejelea Mungu inarejelea ukweli-ndiye Mungu aliyeumba vitu vyote. Yeye ndiye mwanga, elimu, maarifa, maisha, uhai, usalama, uzima na umilele wa mtu. Dini inaporejelea miungu inarejelea upotofu na uongo wa mtu kukataa ukweli na kuelekea uharibifu. Kwa kuishi miungu mtu anamkataa Mungu na hivyo ana haribu uhai, uzima, usalama, umilele na maisha yake yeye na wanaomfuata badae.

Dini ikirejelea Mungu inarejelea muumba wa vitu vyote na mwenye utaratibu na watu wenye kufanya tambiko wanayo sifa ya pekee inayowatofautisha na ndugu zao wengine.
 
Uko sahihi kwa mtazamo wako ila kwa mtazamo wangu naamini dini za mababu zetu na jinsi walivyoweza kufikisha matatizo yao kwa mungu wao na kuyatatua na hiyo ndo naita dini ya kiafrika.
Kabla ya kuingia wamisionari na waarabu Afrika na kuanza kuzieneza hizo dini zilizotupatia majina mazuri na ya kuvutia tulikuwa na utaratibu wetu na imani .
 
Uko sahihi iwapo tu takribani miaka 2019 iliyopita, Yesu hakuwahi kuwepo Duniani, ila kama unakubali kuwa aliwahi kuwepo, basi wazungu wako sahihi zaidi ya 100%
Hakuwa kuwepo kwetu huku hata na sisi kulikuwa na watu wenye miujiza ya kugeuka mawe,mara kinu, mara mtoto na mbwembwe za kila aina,so Yesu kama alikuwepo hakuwepo hiyo ni imani yao na haituhusu kiongozi.

Nabii K.Ngwale, Mkwawa, Mangungo,e.t.c. walikuwepo ila sisi tuliwaita viongozi wao wakawaita mitume na manabii. Wao waliamini uwezo wa Yesu/Muhammad ulitokana na Mungu wao na sisi tuliamini akina Kinjeketile walipewa uwezo wa ziada na Mungu wetu.
Au unafikili wale walitwaa wapi ule uwezo? na kama hapakuwahi tokea mtu nyuma yao i.e Baba,babu,mama,bibi, etc. Mungu wetu aliwainua ili kuleta mwanga na ukombozi katika bara letu. Ndio maana shida za Afrika ni the same but zipo tofauti sana na mabara mengine.
 
Mungu yupo,Mizimu ipo na Shetani yupo..
Dini ni kama daraja tu la kukufikisha kwa hivyo hapo juu nilivyotaja.
Dini inaweza kuwa batili kulingana na matakwa ya mtu..
Kama hautumii akili Dini itakuumiza.
 
Huyo labda atakuwa anatoka bara la Asia ila kama ni Afrika na ni mwafrika basi anatakiwa afanyiwe mila na desturi nyingi za kiafrika(dini ya Afrika). Anazungumza kwa kutumia maneno ya Asia huyo namwonea huruma sana kwani yy anafikili ni mueshia?

Hao na uzao wao ni wasaliti wa bara letu na ndio familia zao zinatumia mawese ya kubadili ngozi ili awe kama wa Asia. Amekopi kila kitu na sasa hadi Rangi anataka. We're handing to nowhere.
 
Mungu yupo,Mizimu ipo na Shetani yupo..
Dini ni kama daraja tu la kukufikisha kwa hivyo hapo juu nilivyotaja.
Dini inaweza kuwa batili kulingana na matakwa ya mtu..
Kama hautumii akili Dini itakuumiza.
Mizimu haipo duniani ndg,mizimu ndio nn sasa.
 

Maana ya dini inaachaniana ila kwa ujumla naweza sema ni "Mfumo uliopangiliwa wa kiimani,sherehe na sheria mbalimbali ambazo zinatumika katika kuabudu mungu au kundi la miungu'. Hiyo ni maana ya dini na dini ni applicable only in this world, sisi hatuna mafundisho sijui ukifa kuna moto mara kuna bata noooo my fellow citizen. Hivyo kupitia tafsiri hii bila shaka sasa umejua pia Dini za Afrika zilikuwa 1000% sahihi.. Mungu wa bara la Afrika ni yupi.

Hapa hakuna wa kutoa jibu sahihi hata ww huyo mungu wa wazungu ni yupi na yupo vipi,huwezi ni jibu. Niliposema kuwa kunautofauti kwa sababu hawaivi chungu kimoja, na kila mmoja anamkataa wa mwenzake. Wazungu wanadai mungu wetu ni feki ilihali wao ndio feki zaidi. Wao hawakuwa na haja ya kutaka kujua wakwetu anataka nn na yupo vipi wali mpuuzia na wakatupandikizia wao. Kwa nn kuna sects(madhehebu) mengi kwa kila kabira? Sijui kuna haja ya kukujibu hapa kwa sababu hata wao wana madhehebu mengi pia na haijalishi hata kama sisi mazehebu yalikuwa mengi zaidi ila ni mpango wa mungu kutokana na mazingira yenyewe. Kwa nn miungu iligawa mabara? swali hili ni sawa na kuuliza kwa nn mungu haonikani. Swali is too spiritual hili kulijibu.

Matambiko ni jina tu hata watu wa Asia wanatumia ubani,udi n.k ilikufanikisha mambo yao. Matumizi ya haya ni matambiko pia angalia albadiri sijui ubatizo sijui upako n.k haya yote ni matambiko. Sitaki niseme mengi hapa sijui kwenda maka n.k ila tambua pia hizi pia ni taratibu katika dini.

NB: Yawezekana mungu ni mmoja ila alitenda katika mataifa tofauti tofauti kwa namna ya kiutofautitofauti na kipekee. Haikuwa sahihi sisi kuiga mambo ya mataifa mengine ilihali mungu alitupa utaratibu wa kufanya. Waafrika ni watulivu wanyenyekevu na hakuna adhabu zozote kubwa kutoka kwa mungu. Angalia Afrika ilivyorehemewa na ilivyo green it's godish land.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…