Ukweli wa Kustaajabisha Kuhusu Nyota za Angani

Ukweli wa Kustaajabisha Kuhusu Nyota za Angani

Status
Not open for further replies.
Mkuu monstgala Shukrani sana
hivi Nyota nazo zinadondoka kama ilivyo kwavimondo ?

kama unaweza nisaidia pia Vimondo vinatofautigani na nyota ?
hivMon stgalaj
mikonomiwili katika mada hii Post ya 117 nilijibu swali linalofanana na lako kama ifuatavyo:

Asili ya vimwondo

Vimwondo ni miamba, mawe, mchanga au maumbo ya mkusanyiko wa madini yanalolizunguka jua ama yanayozunguka sayari nyinginezo, inategemeana tu na umbali lakini yote yako katika mizunguko (orbits) tofauti. Kuna wakati vinasogea karibu na hivyo kuingia kwenye mzunguko wa sayari yetu. Vinakuwa na majina tofauti kitaalam kutokana na size composition eneo vinapozungukia na hata vile vinavyoangukia duniani basi jina linabadilika kama tayari kimeshaanguka. Mfano meteor (ule mwanga wake kikiwa kinaanguka na kuwaka moto) alafu meteorite kile kipisi cha mwamba au jiwe au chuma kilichobaki baada ya kuanguka.

Vimwondo vipo siku zote katika solar system na pale vinapochomoka kwenye orbit zake mara nyingi vinakuwa either vimetokea katika Oort cloud au kwenye Kuiper belt ile inayozunguka sayari ya Neptune. Lakini kuna belts nyingine ambazo zimejaza haya mawe na mabonge ya barafu kuanzia kwenye mzunguko wa sayari ya Mars mpaka ile ya Jupiter. Asili ya vimwondo inasemekana ni wakati ule Big-Bang ilipotokea na ni mabaki ya sayari ndogo zilizopasuka na vipande vyake vimekuwa vikigongana na kuvunjana mpaka sasa hivyo sio matokeo ya nyota moja kwa moja.

Mara nyingi vimwondo vinaishia hewani.

Dunia imeshagongwa na vimwondo mara nyingi sana na hata ushahidi tunao pale mbozi Mbeya na sehemu nyingine maarufu lakini kwa silimia kubwa huishia na kuyeyuka hewani kabla ya kugonga dunia. Binafsi nimesha tembelea pale Mbozi na kwa kweli ni kitu cha kujivunia kuwa na kivutio kama kile lakini hakijajengewa au kutengewa eneo linaloendana nacho (hadhi). Kama ingekuwa sehemu nyingine pale pasingekuwa vile.

Kile kilichoanguka Urusi mwaka jana (February 15, 2013) katika mji mdogo wa Chelyabinsk ndio kilitoa somo zuri maana tayari kuna technology zenye kupima na kurekodi karibu kila kitu kinachotakiwa. Ukubwa wake ulikuwa mita 15 na uzito wake kama 7000 metric tons kabla ya kuingia katika anga la dunia. Mwendo wake ulikuwa 65,000km/h hiyo ni velocity kali sana na ndio pona pona yetu maana kwa mwendo huo kikiingia tu kwenye anga la dunia "Earth atmosphere" kinaanza kuungua kutokana na msuguano mkali sana. Kumbuka mwendo wa risasi ni kilomita elfu moja na mia mbili kwa saa (1,200km/h) hivyo ni wazi kimwondo kile kilikuwa na mwendo mkali mara nyingi sana zaidi ya risasi. Vipande vidogo tu viligusa ardhi baada ya kuungua na kulipuka ila shockwave na sauti yake watu wengi waliumia kwa kupanic, madidisha ya vioo yalipasuka na kuta za nyumba nyingi zilianguka. Na kama kingetua kama kilivyo bila kuungua na kulipuka basi ni impact yake ingekuwa zaidi ya bomu lilioangushwa hiroshima.

Wastani wa vimwondo kugonga Dunia.

Kila mwaka zaidi ya tani mia moja za vumbi na mchanga kutoka angani zinatua duniani na kwa wastani wa mara moja kwa mwaka kimwondo chenye size ya gari dogo huingia kwenye anga la dunia (Earth atmosphere) lakini huungua chote kabla ya kutua duniani. Kwa wastani wa kila miaka 2000 kimwondo cha ukubwa wa saizi ya uwanja wa mpira hugonga dunia na kusababisha madhara makubwa katika eneo husika.

Na katika wastani wa miaka milioni 10 hadi 100 kimwondo kikubwa zaidi kama saizi ya jiwe kubwa lenye upana wa kilomita 2 hadi 7 hugonga dunia na kutengeneza shimo kubwa sana, mlipuko zaidi ya bomu la nuclear, tetemeko, moto, vumbi, hewa chafu na moshi mzito ambao unaweza kukaa duniani kwa zaidi ya miaka elfu moja na hivyo kubadili majira ya dunia kwa kutoruhusu mwanga wa jua kupenya. Hiki ndicho kinachohofiwa sana maana ni wazi viumbe vingi vitafutika lakini sio maisha kwa ujumla.

Mfano mzuri wa hili unaelekezwa kwenye kimwondo kikubwa zaidi kilichoanguka zamani sana kabla binadamu hatujawa katika hali hii ambacho kinadhaniwa kuchangia kufuta wale reptiles wakubwa waliokuwa wametapakaa duniani (Dinosaurs) miaka millioni 65 iliyopita na pia kubadili majira na hali ya hewa ya dunia. Ingawa uwezekano wa kugongwa na kimwondo kikubwa ambacho kitaleta madhara mazito ni mdogo sana, lakini upon na inadhaniwa hutokea mara moja kwa kipindi kirefu labda miaka millioni mia moja. Kwa kuhofia hilo kuna baadhi ya programs zenye technologia ya juu sana zimejikita kuchunguza mwenendo wa vimwondo hasa vile vikubwa vinavyoweza kuleta madhara.

Labda pia labda ni bahati kwamba kimwondo kilibadili mazingira ya dunia na kutufanya binadamu taratibu tuongezeke kwa kuwa wale kina T-rex wasingetuacha. Si ajabu kujificha
 
Last edited by a moderator:
Nilipata challenge katika ule uzi wa UFOs kwamba je nikiandika kiswahili nitakufa? Nikajibu ”sitakufa” na hii ni jitihada za kuonesha hivyo. 🙂

You went through all the trouble kutafsiri material for some anonymous internet persona who thinks kuongea lugha nyingine ni ulimbukeni??

you have alot of time on your hands.

kutafsiri kwaajili ya watu wasio familiar na lugha ni vema sana. Nafikiria how long it took you. I know its not as easy as it looks when finally posted.

So hats off for Monstgala

but I was wondering, wewe ni astrophysicist??Hahaaa. No I'm serious. Jinsi umeelezea orbitals kwa lugha rahisi fascinates me.
 
Last edited by a moderator:
You went through all the trouble kutafsiri material for some anonymous internet persona who thinks kuongea lugha nyingine ni ulimbukeni??

you have alot of time on your hands.

kutafsiri kwaajili ya watu wasio familiar na lugha ni vema sana. Nafikiria how long it took you. I know its not as easy as it looks when finally posted.

So hats off for Monstgala

but I was wondering, wewe ni astrophysicist??Hahaaa. No I'm serious. Jinsi umeelezea orbitals kwa lugha rahisi fascinates me.
housegirl , Mfasiri anaweza kutafsiri lakini hawezi kujibu maswali. Niamini, kuna watu wanajua vitu vingi sana na wako humu humu majukwaani, na wana muda pia wa kubadilishana mawazo.
 
Last edited by a moderator:
kuna jambo moja nimeskia ya kuwa ukubwa wa dunia na jua unaongezeka na kuongezska
kwa ukubwa wa jua ndio huko kizeeka ambapo itafika siku nuru ya jua itazimika na kupotea
hivi hili swala ni la kweli alafu kuna swala linaloangazia mwisho wa dunia ambalo mpaka sasa sijajikinaisha kuna wanaosema itganda tena barasfu na maisha kusimama sijajua ikiyeyuka maisha yataemdelea ---- wanosema itawaka moto sijajua moto huo utaanzia juu due to atmospheric impact au chini katika uji wa volcano wakuu wa jf naomba msaada kwenu
 
kuna jambo moja nimeskia ya kuwa ukubwa wa dunia na jua unaongezeka na kuongezska
kwa ukubwa wa jua ndio huko kizeeka ambapo itafika siku nuru ya jua itazimika na kupotea
hivi hili swala ni la kweli alafu kuna swala linaloangazia mwisho wa dunia ambalo mpaka sasa sijajikinaisha kuna wanaosema itganda tena barasfu na maisha kusimama sijajua ikiyeyuka maisha yataemdelea ---- wanosema itawaka moto sijajua moto huo utaanzia juu due to atmospheric impact au chini katika uji wa volcano wakuu wa jf naomba msaada kwenu

Mkuu Sajumo angalia post ya 33 alafu angalia mada ya Muda wa ulimwengu na Matukio yake nadhani utapata mwanga kuhusu swali lako au maswali yako. Unaweza kuuliza chochote kutokana na hizo hoja na dhana.
 
mikonomiwili katika mada hii Post ya 117 nilijibu swali linalofanana na lako kama ifuatavyo:

Asili ya vimwondo

Vimwondo ni miamba, mawe, mchanga au maumbo ya mkusanyiko wa madini yanalolizunguka jua ama yanayozunguka sayari nyinginezo, inategemeana tu na umbali lakini yote yako katika mizunguko (orbits) tofauti. Kuna wakati vinasogea karibu na hivyo kuingia kwenye mzunguko wa sayari yetu. Vinakuwa na majina tofauti kitaalam kutokana na size composition eneo vinapozungukia na hata vile vinavyoangukia duniani basi jina linabadilika kama tayari kimeshaanguka. Mfano meteor (ule mwanga wake kikiwa kinaanguka na kuwaka moto) alafu meteorite kile kipisi cha mwamba au jiwe au chuma kilichobaki baada ya kuanguka.

Vimwondo vipo siku zote katika solar system na pale vinapochomoka kwenye orbit zake mara nyingi vinakuwa either vimetokea katika Oort cloud au kwenye Kuiper belt ile inayozunguka sayari ya Neptune. Lakini kuna belts nyingine ambazo zimejaza haya mawe na mabonge ya barafu kuanzia kwenye mzunguko wa sayari ya Mars mpaka ile ya Jupiter. Asili ya vimwondo inasemekana ni wakati ule Big-Bang ilipotokea na ni mabaki ya sayari ndogo zilizopasuka na vipande vyake vimekuwa vikigongana na kuvunjana mpaka sasa hivyo sio matokeo ya nyota moja kwa moja.

Mara nyingi vimwondo vinaishia hewani.

Dunia imeshagongwa na vimwondo mara nyingi sana na hata ushahidi tunao pale mbozi Mbeya na sehemu nyingine maarufu lakini kwa silimia kubwa huishia na kuyeyuka hewani kabla ya kugonga dunia. Binafsi nimesha tembelea pale Mbozi na kwa kweli ni kitu cha kujivunia kuwa na kivutio kama kile lakini hakijajengewa au kutengewa eneo linaloendana nacho (hadhi). Kama ingekuwa sehemu nyingine pale pasingekuwa vile.

Kile kilichoanguka Urusi mwaka jana (February 15, 2013) katika mji mdogo wa Chelyabinsk ndio kilitoa somo zuri maana tayari kuna technology zenye kupima na kurekodi karibu kila kitu kinachotakiwa. Ukubwa wake ulikuwa mita 15 na uzito wake kama 7000 metric tons kabla ya kuingia katika anga la dunia. Mwendo wake ulikuwa 65,000km/h hiyo ni velocity kali sana na ndio pona pona yetu maana kwa mwendo huo kikiingia tu kwenye anga la dunia "Earth atmosphere" kinaanza kuungua kutokana na msuguano mkali sana. Kumbuka mwendo wa risasi ni kilomita elfu moja na mia mbili kwa saa (1,200km/h) hivyo ni wazi kimwondo kile kilikuwa na mwendo mkali mara nyingi sana zaidi ya risasi. Vipande vidogo tu viligusa ardhi baada ya kuungua na kulipuka ila shockwave na sauti yake watu wengi waliumia kwa kupanic, madidisha ya vioo yalipasuka na kuta za nyumba nyingi zilianguka. Na kama kingetua kama kilivyo bila kuungua na kulipuka basi ni impact yake ingekuwa zaidi ya bomu lilioangushwa hiroshima.

Wastani wa vimwondo kugonga Dunia.

Kila mwaka zaidi ya tani mia moja za vumbi na mchanga kutoka angani zinatua duniani na kwa wastani wa mara moja kwa mwaka kimwondo chenye size ya gari dogo huingia kwenye anga la dunia (Earth atmosphere) lakini huungua chote kabla ya kutua duniani. Kwa wastani wa kila miaka 2000 kimwondo cha ukubwa wa saizi ya uwanja wa mpira hugonga dunia na kusababisha madhara makubwa katika eneo husika.

Na katika wastani wa miaka milioni 10 hadi 100 kimwondo kikubwa zaidi kama saizi ya jiwe kubwa lenye upana wa kilomita 2 hadi 7 hugonga dunia na kutengeneza shimo kubwa sana, mlipuko zaidi ya bomu la nuclear, tetemeko, moto, vumbi, hewa chafu na moshi mzito ambao unaweza kukaa duniani kwa zaidi ya miaka elfu moja na hivyo kubadili majira ya dunia kwa kutoruhusu mwanga wa jua kupenya. Hiki ndicho kinachohofiwa sana maana ni wazi viumbe vingi vitafutika lakini sio maisha kwa ujumla.

Mfano mzuri wa hili unaelekezwa kwenye kimwondo kikubwa zaidi kilichoanguka zamani sana kabla binadamu hatujawa katika hali hii ambacho kinadhaniwa kuchangia kufuta wale reptiles wakubwa waliokuwa wametapakaa duniani (Dinosaurs) miaka millioni 65 iliyopita na pia kubadili majira na hali ya hewa ya dunia. Ingawa uwezekano wa kugongwa na kimwondo kikubwa ambacho kitaleta madhara mazito ni mdogo sana, lakini upon na inadhaniwa hutokea mara moja kwa kipindi kirefu labda miaka millioni mia moja. Kwa kuhofia hilo kuna baadhi ya programs zenye technologia ya juu sana zimejikita kuchunguza mwenendo wa vimwondo hasa vile vikubwa vinavyoweza kuleta madhara.

Labda pia labda ni bahati kwamba kimwondo kilibadili mazingira ya dunia na kutufanya binadamu taratibu tuongezeke kwa kuwa wale kina T-rex wasingetuacha. Si ajabu kujificha
Aisee Kama itakuja kutokea kwa asteroid yenye ukubwa wa 2km tu kuigonga dunia, disaster itakayoipata Hilo eneo na dunia kwa ujumla mh. Mungu tuepushie hii kitu kwa kweli maana ni zaidi ya bomu la nyuklia. Everything will be wiped away... Just type" could an asteroid impact event mass extinction on earth? YouTube mjionee wenyewe
 
Sasa mkuu Monstagala..kuna sehemu niliwahigi kusomaga wanasema kwamba wale ancient creatures walipotea baada ya comet kuipiga dunia pande za Magharibi ya North Amerika na ile shock na wind waves na moto uliozalishwa pale hadi Katika Bahali ya Pasific, viumbe wote walikufa na wachache sana waliokuwa deep water ndio walisalimika. Sasa swali langu je Hawa viumbe walipoteaje kwenye other parts of the world?
 
Sasa mkuu Monstagala..kuna sehemu niliwahigi kusomaga wanasema kwamba wale ancient creatures walipotea baada ya comet kuipiga dunia pande za Magharibi ya North Amerika na ile shock na wind waves na moto uliozalishwa pale hadi Katika Bahali ya Pasific, viumbe wote walikufa na wachache sana waliokuwa deep water ndio walisalimika. Sasa swali langu je Hawa viumbe walipoteaje kwenye other parts of the world?

Mkuu fyddell, Wale viumbe hawakupotea siku moja baada ya ile impact ya kimwondo miaka milioni 90 mpaka 110 iliyopita. Wala si wiki au mwaka au hata karne moja tu bali muda mrefu baada ya dunia kugongwa. Kuna wale waliokufa pale pale katika dakika ile ya tukio na hao ni wale waliokuwa eneo lile. Alafu kuna wale walikufa dakika chache kidogo baadae hawa ni wale waliokuwa umbali fulani lakini shockwave iliwafikia. Na kuna wale waliokuwa siku saa hadi mwaka hao ni wale waliotegemea eneo lile kama mazalia, sehemu ya chakula na maji na hawakuweza kwenda eneo lingine kwa urahisi. Pia kuwa waliofuka kwa mabadiliko yale maana kidogo kulianza kuwa na upungufu wa chakula hao sasa ni kutokana na kubadilika kwa eco-system kwa ghafla.

Kubwa zaidi lilifuta viumbe hawa maeneo yote ya dunia ni kubadilika kwa kwa mazingira ya Dunia baada kugongwa na kimwondo hiki. Kwa muda mrefu sana windu zito lilitanda duniani na hewa ya Carbondioxide iliyotokana na moto na kuungua kwa eneo lile ilisambaa Dunia nzima baada ya muda mrefu. Hili wingu halikuondoka haraka lilikaa duniani kwa muda mrefu. Mwanga wa jua haukupenya vizuri katika maeneo mengi ya dunia na hivyo kusababisha halijoto kushuka kwa muda mrefu. Mazingira haya mapya hayakuwa mazuri kwa viumbe hawa na food chain iliathirika vibaya sana. Baada ya karne nyingi sana viumbe hawa waliisha kabisa. Ni kama jinsi uvuaji wa samaki wa aina fulani baharini unavoweza kuathiri eco-system ya baadhi ya species na baada ya muda species hizo zinaweza kutoweka Dunia nzima ingawa bahari ni kubwa kuliko hata nchi kavu. Ipo mifano hai katika hili.

Lakini kitu kimoja cha muhimu kunote kutoka katika dhana hii ni kwamba kipindi walishoishi viumbe hawa mamalia wengi walikuwa ni wale wadogo wadogo jamii ya panya. Hivyo baada ya kimwondo hali hii mpya ndio ilipelekea jamii ya mamalia kuanza kuongezeka na kutawanyika zaidi sehemu mbalimbali za Dunia. Hivyo kimwondo kilileta balaa kwa aina moja ya viumbe na kuleta heri kwa jamii nyingine ya vuimbe. Ndivyo wataalamu wa dhana hii wanavyo-hypothesize hii kitu. Niliwahi kuandika kidogo kuhusu hii ya mamalia katika mada ya muda wa ulimwengu.
 
Mkuu fyddell, Wale viumbe hawakupotea siku moja baada ya ile impact ya kimwondo miaka milioni 90 mpaka 110 iliyopita. Wala si wiki au mwaka au hata karne moja tu bali muda mrefu baada ya dunia kugongwa. Kuna wale waliokufa pale pale katika dakika ile ya tukio na hao ni wale waliokuwa eneo lile. Alafu kuna wale walikufa dakika chache kidogo baadae hawa ni wale waliokuwa umbali fulani lakini shockwave iliwafikia. Na kuna wale waliokuwa siku saa hadi mwaka hao ni wale waliotegemea eneo lile kama mazalia, sehemu ya chakula na maji na hawakuweza kwenda eneo lingine kwa urahisi. Pia kuwa waliofuka kwa mabadiliko yale maana kidogo kulianza kuwa na upungufu wa chakula hao sasa ni kutokana na kubadilika kwa eco-system kwa ghafla.

Kubwa zaidi lilifuta viumbe hawa maeneo yote ya dunia ni kubadilika kwa kwa mazingira ya Dunia baada kugongwa na kimwondo hiki. Kwa muda mrefu sana windu zito lilitanda duniani na hewa ya Carbondioxide iliyotokana na moto na kuungua kwa eneo lile ilisambaa Dunia nzima baada ya muda mrefu. Hili wingu halikuondoka haraka lilikaa duniani kwa muda mrefu. Mwanga wa jua haukupenya vizuri katika maeneo mengi ya dunia na hivyo kusababisha halijoto kushuka kwa muda mrefu. Mazingira haya mapya hayakuwa mazuri kwa viumbe hawa na food chain iliathirika vibaya sana. Baada ya karne nyingi sana viumbe hawa waliisha kabisa. Ni kama jinsi uvuaji wa samaki wa aina fulani baharini unavoweza kuathiri eco-system ya baadhi ya species na baada ya muda species hizo zinaweza kutoweka Dunia nzima ingawa bahari ni kubwa kuliko hata nchi kavu. Ipo mifano hai katika hili.

Lakini kitu kimoja cha muhimu kunote kutoka katika dhana hii ni kwamba kipindi walishoishi viumbe hawa mamalia wengi walikuwa ni wale wadogo wadogo jamii ya panya. Hivyo baada ya kimwondo hali hii mpya ndio ilipelekea jamii ya mamalia kuanza kuongezeka na kutawanyika zaidi sehemu mbalimbali za Dunia. Hivyo kimwondo kilileta balaa kwa aina moja ya viumbe na kuleta heri kwa jamii nyingine ya vuimbe. Ndivyo wataalamu wa dhana hii wanavyo-hypothesize hii kitu. Niliwahi kuandika kidogo kuhusu hii ya mamalia katika mada ya muda wa ulimwengu.
Thanks maana nimeelewa na unachoniambia ni kweli kabisa kuwa it did take long time for those mammals to be wiped on land. Hiyo mada nyingine sijawahi ipitia, Ngoja nichukue muda huu kuipitia ili nijifunze kitu kutoka huko.
 
Kama kwenye observable universe kuna galaxy zaidi ya billion 100 na kila galaxy ina nyota zaidi ya sextillion 100 na kila nyota inazungukwa na midude mikubwa iitwayo sayari that means kuna zaidi ya quintollions 100 of planets in only observable universe na vyote vinaelea katika mpangilio wa kipekee bila kuingiliana; what might balancing power be?!! ( This is really astonishing). Sidhani Kama tutaweza kumaliza kuzichunguza na kugundua kama kuna any form of life out there. Hakika kwa akili ya kibinadamu lazima tustaajabishwe na haya mambo, I am trying to thing and rethink how God great He is mpaka akayaumba yote haya kwa utukufu wake mwenyewe daaaaah.
 
Mungu ana siri kubwa Sana kuhusu hii dunia haya yote yanaonyesha ni jinsi gani Tuna paswa kujianda ili tuje kwenda mbinguni na kujifunza uumbaji wake kuhusu haya yote tunayo ona ni maajabu.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom