Ukweli wa Kustaajabisha Kuhusu Nyota za Angani

Ukweli wa Kustaajabisha Kuhusu Nyota za Angani

Status
Not open for further replies.
mkuu monstagla ni muda mrefu sana toka watu waache kuchangia katika hili bandiko ila kuna kitu kinanchanganya sana katika earth beneath da sima joto linfikia 2000'c inafiatiwa na mentle rigid rock asthenosphere ni layer of molten material inafuata lower mentle sijui chochote kuhusu hii layer outer core ipo katika molten state na ina core ni solid kutokana na high presure ila
sijaelewa sababu zinazosababisha hilo joto ni kipi kinafanya baadhi ya leya ziwe katika molten state while others not
the same atmospheric layers nazo zinachanganya joyo jinsi limavvyopanda na linavyoshuka kwa baadhi ya layers naona celewi kabisa kwanini joto lisishuke continuasly as u go up ward na kwanini joto lisipande continuously as u go up ward
 
Hizi ndo mada interesting JF!! kwingine kule kumechoka na kuna fujo fujo
 
mkuu monstagla ni muda mrefu sana toka watu waache kuchangia katika hili bandiko ila kuna kitu kinanchanganya sana katika earth beneath da sima joto linfikia 2000'c inafiatiwa na mentle rigid rock asthenosphere ni layer of molten material inafuata lower mentle sijui chochote kuhusu hii layer outer core ipo katika molten state na ina core ni solid kutokana na high presure ila
sijaelewa sababu zinazosababisha hilo joto ni kipi kinafanya baadhi ya leya ziwe katika molten state while others not
the same atmospheric layers nazo zinachanganya joyo jinsi limavvyopanda na linavyoshuka kwa baadhi ya layers naona celewi kabisa kwanini joto lisishuke continuasly as u go up ward na kwanini joto lisipande continuously as u go up ward

Dunia kwa ndani ina layer nne, Crust, Mantle, Core na Inner core. Kwa jinsi unavyoenda ndani zaidi basi pia joto ni kali zaidi. Katika inner core joto likadiriwa kufikia nyuzi katika ya 6,000 mpaka 12,000 Fahrenheit. Ni joto kali pengine zaidi ya joto katika uso au layer ya juu ya jua.

Sababu ya joto hili ni kwamba tangu Dunia inaumbwa ilikuwa ni muunganiko wa miamba ya moto sana na pia kulikuwa na msuguano mkali sana wa gesi na miamba hivyo joto lilikuwa kali katika layer zote. Baada ya dunia kuform process ya kupoa ilichukua muda mrefu sana na kulikuwa hakukaliki kwenye uso wa Dunia. Sasa layers za juu zimepoa lakini inner core haijapoa na imekuwa hivyo kwa muda wote kwa nini? Wataalam wanasema hali hiyo inasababishwa na radioactivity ndani ya inner core. Atoms zinapodecay zinaachia joto kubwa sana. Technology iliyopo nyuma ya Atomic bombs ni hii ya kuzifanya atoms zianze kudecay yani ku-unstabilize atom hivyo kusababisha nucleus yake ianze ku-loose nishati kwa kufyatua miale yake na hapo ndio source ya mlipuko na joto kali sana. Hivyo katika inner circle kuna natural process of radioactivity na hii ndio haswa source ya joto hili. Hizi element za radioactive zinapoanza kudecay ni mpaka mabilioni ya miaka ndio process inaeza malizika. Inner core itaendelea kuwa ya moto kwa miaka na miaka lakini eventually radioactivity zikiacha basi kili chuma katikati kitapoa. Na ile inner core bila shaka ndio chanzo cha kuzifanya layer nyingine juu yake kubakia kuwa na joto kama inavyopimwa.
 
Dunia kwa ndani ina layer nne, Crust, Mantle, Core na Inner core. Kwa jinsi unavyoenda ndani zaidi basi pia joto ni kali zaidi. Katika inner core joto likadiriwa kufikia nyuzi katika ya 6,000 mpaka 12,000 Fahrenheit. Ni joto kali pengine zaidi ya joto katika uso au layer ya juu ya jua.

Sababu ya joto hili ni kwamba tangu Dunia inaumbwa ilikuwa ni muunganiko wa miamba ya moto sana na pia kulikuwa na msuguano mkali sana wa gesi na miamba hivyo joto lilikuwa kali katika layer zote. Baada ya dunia kuform process ya kupoa ilichukua muda mrefu sana na kulikuwa hakukaliki kwenye uso wa Dunia. Sasa layers za juu zimepoa lakini inner core haijapoa na imekuwa hivyo kwa muda wote kwa nini? Wataalam wanasema hali hiyo inasababishwa na radioactivity ndani ya inner core. Atoms zinapodecay zinaachia joto kubwa sana. Technology iliyopo nyuma ya Atomic bombs ni hii ya kuzifanya atoms zianze kudecay yani ku-unstabilize atom hivyo kusababisha nucleus yake ianze ku-loose nishati kwa kufyatua miale yake na hapo ndio source ya mlipuko na joto kali sana. Hivyo katika inner circle kuna natural process of radioactivity na hii ndio haswa source ya joto hili. Hizi element za radioactive zinapoanza kudecay ni mpaka mabilioni ya miaka ndio process inaeza malizika. Inner core itaendelea kuwa ya moto kwa miaka na miaka lakini eventually radioactivity zikiacha basi kili chuma katikati kitapoa. Na ile inner core bila shaka ndio chanzo cha kuzifanya layer nyingine juu yake kubakia kuwa na joto kama inavyopimwa.

Mkuu Monstgala/Mgalanjuka let me ask you
what if our beautiful planet (earth) had only one layer (let's say crust) ??
Je kungekua na matatizo yoyote katika life ya viumbe juu ya uso wa dunia??
(sorry if it's stupidy question)

.made in mby city.
 
yaani eti kuna midude mikubwa dunia mara milion+ for nothing sijajua hesabu za god zimekusudia nn??? (kama yupo)
 
Jana usiku mida ya saa sita usiku nilitoka nje na kuchagua kasehemu ambacho kilikuwa hakina nyota upande wa magharibi wa Dar nikiwa Kijitonyama na kukiangalia Sana na hata kukakazia macho. Baada ya muda wa Kama dakika 2 au 3 niliona kikundi cha nyota Kama 250- 500 kwa kukadilia kwa mbali sana yaani mwanga wake ulikuwa hafifu mno but I managed to see them clearly. Sasa hiki kikundi kinaweza kikawa ni part ya galaxy yetu au ndio galaxy nyingine?
Je kwa macho bila kifaa chochote cha darubini ni rahisi kuona galaxy nyingine?
monstgala na wengine karibuni.
 
yaani eti kuna midude mikubwa dunia mara milion+ for nothing sijajua hesabu za god zimekusudia nn??? (kama yupo)
Mkuu naamini kwenye hizo sayari zinazofanana na dunia kimazingira kuna viumbe vinaishi though vinaweza visiwe Kama sisi I mean viko in any form of life.
 
Moja kwa moja elimu kama hii inanifanya:
1-niamini kuwa Mungu yupo
2-Nisikubali kuwa Mmarekani amefika Mwezini
3-Kwa namna fulani, niwe na shauku na kifo. naamini kifo kitaifungua roho kutoka restrictions za mwili. Utaweza kutembelea sehemu hizo.
 
Jana usiku mida ya saa sita usiku nilitoka nje na kuchagua kasehemu ambacho kilikuwa hakina nyota upande wa magharibi wa Dar nikiwa Kijitonyama na kukiangalia Sana na hata kukakazia macho. Baada ya muda wa Kama dakika 2 au 3 niliona kikundi cha nyota Kama 250- 500 kwa kukadilia kwa mbali sana yaani mwanga wake ulikuwa hafifu mno but I managed to see them clearly. Sasa hiki kikundi kinaweza kikawa ni part ya galaxy yetu au ndio galaxy nyingine?
Je kwa macho bila kifaa chochote cha darubini ni rahisi kuona galaxy nyingine?
monstgala na wengine karibuni.

Nyota nyingi zinazoonekana kwa macho ni zile zilizoko ndani ya galaxy yetu (Milkyway). Pia unaweza kuona kwa macho nyota ambazo ziko katika galaxi nyingine za karibu bila kutumia telescope. Kuzitambua inahitaji utaalam kidogo au uwe umepata maelezo mazuri. Galaxi ndogo ndogo za karibu yetu sio zenye umbo la spiral na galaxi ya aina hiyo iliyoko karibu ni Andromeda. Unaweza ukaiona Andromeda kwa macho katika miezi fulani kutegemea na eneo ulipo na utaalam wa kuitambua. Lakini baada ya Andromeda galaxi na nyota zilizo mbali zaidi yake hazionekani kwa macho. Kwa ujumla kila kitu unachokiona kwa macho ni sehemu ndogo sana ya anga halisi. Unapokuwa na telescope kubwa utashangaa jinsi anga linavyoendelea mbali sana na nyota nyingi sana ambazo hatuna habari nazo.
 
Pale ambapo akili yetu inaishia,ndipo Mungu huanzia.
Kuwaza Mungu atakuwaje,ni sawa na kuchota maji baharini na kuyamwaga Kisimani,Hupunguzi hata theluthi ya Bahari.Mungu atabaki kuwa Mungu.

KWANZA KABISA AMEN
Pia lazima ujue ya kuwa ufanikishaji wa suala zima la kisayanzi ni mpango wa Mungu ili binadamu aweze kujua utukufu wa Mungu.Kumbuka ya kwamba kila kitu kina exist without any mistake...hata wewe binadamu umeumbwa with DNA zaidi ya billion zinazooperate ...Pia lazima ujue kuwa Mungu yupo na anaexist,,ungu ni roho ambayo inaexist kivyake na kama ni roho haifungamani na sheria zozote za physics in time and space mfano mdogo huu hapa Binadamu amegawanyika sehemu mbili moja mwili wake na roho yake ndo maana binadamu akifa wanazema mwili wake upo wapi?Roho yako iliumwa ili iishi milele na ndo maana hata ukifika roho yako inaishi milele kwa kuwa roho haifungamani na sheria za kifizikia yani time and space roho ya biandamu pia inaishi milele either in hell or in heaven


Ila amini usiamini kama ukisoma biblia kwa msaada wa roho mtakatifu utagundua sayanzi ilikuwepo kabla ya biandamu hao wanachokifanya ni kidogo sana

Pia lazima ujue kuwa hakuna kiumbe yotote kwenye universal nzima anayeishi uwepo wa universe si suala la bahati mbaya zote hizo ninasaidia kusimama kwa sayari yetu ni siri kubwa ambayo hata wanasayanzi bila Mungu mwenyewe kuwafungua hawawezi kutoa majibu hii ni kwa sababu yangu na wewe

Swali je wewe ni nani mbele za Mungu?Mungu alitengeneza the whole universe and its still expanding kwa jili yangu na wewe ili tuishi kwa raha mstarehe hapa duniani jambo la msingi ni kusema THANKS LORD

Kama kungekuwa na sayari yenye viumbe basi ungesha ijua lakini nakuhakikishia haitakuja patikana uwezo wa binadamu una kikomo chake bro

Nionyeshe kitu gani kilichoumwa na Mungu kina mistake???kama our life was coincidence basi kila kitu kingekuwa so roughly?if our life was coincidence then hata sayari zinginee kungekuwa na watu-umeishi siku zote lini uliona gesi tunayopumua ilipungua-kutoka mwanzo wa ulimwengu hakuna itilafu yoyote ni kwa sababu historia nzima ya ulimwengu ipo mikononi mwa Mungu na maisha yetu ni safari kama unataka kubaki kuamini kusubiri alienz wagunduliwe basi subiri safari yako duniani itakapokwisha -tuone utaishia wapi

BY THE END PRAISE TO LORD
 
Nimeonelea nipost mada hii kwa kiswahili ili wote wanaojua lugha hii wafaidike lakini katika kuchangia tutumie lugha yoyote inayotumika hapa jukwaani . Nilipata challenge katika ule uzi wa UFOs kwamba je nikiandika kiswahili nitakufa? Nikajibu "sitakufa" na hii ni jitihada za kuonesha hivyo. 🙂<br /><br />Tukirudi kwenye mada, watu wanapofikiri kuhusu ulimwengu basi wanafikiria nyota. Nyota ndizo zinazofanya sehemu kubwa ya yabisi, kiminika na hewa (matter) inayoonekana na ingawa nyota zote mbali na jua ziko katika umbali usiofikirika kutoka tulipo, bado tunaweza kuziona nyota maelfu kwa maelfu kwa macho yetu wenyewe. Kuna maajabu mengi ya ukweli kuhusu nyota lakini nitaongelea machache yanayovutia na wengine wanaweza kuongezea ili tijifunze au kueleweshana pamoja.<br /><br /><b>1.</b><b>Idadi ya nyota katika ulimwengu unaoonekana <br /></b><br />Katika usiku wenye giza tororo katika maeneo ya vijijini au mbali na mji unaweza kujionea nyota zisizo na idadi lakini katika mazingira ya kawaida hapo unakuwa unaangalia nyota kama 2500 na si zaidi ya hapo. Hizo ni moja ya billioni 1/100,000,000 ya jumla ya nyota zilizo katika galaxi tuishiyo (MilkyWay).<br /><br />Milky way ni moja ya galaxi kubwa sana katika universe na sisi tumebahatika kuwa ndani ya galaxi hii. Labda kidogo tuangalie kwa kifupi ukweli wa galaxi hii. Diameter (kipenyo) ya Milky Way kutoka upande mmoja mpaka mwingine ni umbali wa miaka laki moja (100,000) ya mwendo wa mwanga. Mwendo wa mwanga kwa mwaka ni jinsi mwanga unavyosafifi kwa mwaka mzima kutoka point moja mpaka nyingine. Mwanga husafiri kwa mwendo wa kasi kuliko mwendo wa kitu kingine chochote tunachokijua. Kwa mfano katika sekunde moja mwanga unasafiri umbali wa kuzunguka dunia mara saba. Hivyo mwaka mmoja wa kusafiri kwa mwanga (a light year) ni umbali wa kustaajabisha. Inaweza kuchukua miaka elfu kumi na nane kwa chombo chenye kasi zaidi cha anga kusafiri mwaka mmoja wa mwanga. Sasa hapa ku-cover distance ya kipenyo cha MilkyWay tunazungumzia umbali wa miaka 100,000 ya kusafiri kwa mwanga.<br /><br />Hii pia ina maana unapochukua telescope ukafanikiwa kuziona nyota zilizoko upande mwengine wa mwisho wa galaxi, basi unaziona jinsi zilivyokuwa miaka 100,000 iliyopita, kwa sababu mwanga uliotoka kwenye nyota hizo miaka laki moja iliyopita ndio kwanza unatufikia. hii ni sawa pia kwamba kama kuna kiumbe katika upande mwingine wa galaxi na anaiangalia dunia kwa telescope basi ataiona dunia kama ilivyokuwa miaka 100,000 iliyopita.<br /><br />
milky_way.jpg
<br /><br />Katika picha hiyo ya Milkyway galaxi unaweza kudhani mojawapo ya vidoti hivyo ni jua letu. Ukweli ni kwamba kama ukiikuza picha hiyo ifikie ukubwa wa saizi ya Dunia, bado ungehitaji microscope ili kuweza kuona kidoti cha mwanga wa jua letu. Hii ni kutokana na kwamba kama Milkyway galaxi ingepunguzwa iwe kama size ya Dunia, basi jua lingekuwa 1/50 ya millimita (kipenyo). Hii ni sawa na kidoti tusichoweza kukiona kwa macho.<br /><br />MilkyWay ni bonge la dude na lina idadi ya nyota kati ya bilioni 100 hadi 400 lakini kumbuka hii ni galaxi moja tu.<br /><br /><b>Kwani kuna Galaxi ngapi?</b><br /><br />Mwaka 1995, wanasayansi walichagua kajisehemu kadogo sana katika anga ambako kwa macho ya kawaida kalikuwa kanaonekana hakana nyota yoyote wala mwanga wowote. pia kwa telescope ya kawaida kaeneo haka bado kalionesha hakana kitu chochote yani ni giza tu. Eneo hili dogo ambalo lilionekana tupu ni kama vile eneo linaloweza kuzibwa na mpira wa tenis ukiwa juu yako kwa mita mia.<br />kw amuda wa siku kumi wanasayansi wakitumia Hubble telescope, walichunguza eneo hili ambalo lilidhaniwa halina kitu na picha nii chini ndicho walichovumbua:<br /><br />
hudf_hst_big-600x749.jpg
<br /><br /><br />Ajabu!<br /><br />Kila kinachoonekana katika picha hiyo si nyota tena, hata kidoti kidogo kabisa cha mwanga ni galaxi nzima. Katika picha hii tu kuna zaidi ya galaxi 10,000 na kila moja ikiwa na zaidi ya nyota billioni 100. Lakini kumbuka hiki ni kisehemu kidogo sana cha anga tunayoiona kama vile saizi ya kichwa cha pini.<br /><br />Hivyo picha hii ilisaidia makadirio ya ulimwengu uonekanao (observable universe) kwamba una zaidi ya galaxi bilioni 100, ambayo inafanya jumla ya nyota katika ulimwengu tunaoweza kuuona kuwa kwenye kati ya 100 sextillion stars.<br />Ili kuweka kiasi hiki katika njia inaweza kufikirika kirahisi, Chuo kikuu cha Hawaii kilitumia muda wa kutosha katika kukokotoa kadirio la kila punje ya mchanga duniani ambampo walipata jibu kuwa dunia ina quintillion 7.5 za mchanga.<br />Hivyo basi, <b>kwa kila punje moja ya mchanga duniani kuna nyota 10,000 katika universe.</b><br /><b><br />2. Nyota hazijakaribiana<br /></b><br />Ukiweka kando mfumo wa nyota pacha, nyota nyingi ziko pekee zikiwa hazina chochote pembeni kwa umbali mkubwa sana katika kila uelekeo, yani ziko pweke sana. Jua letu ni mojawapo, nyota iliyo karibu kabisa na sisi ni Proxima Centauri, umbali wa miaka minne na nusu ya kusafiri kwa mwanga au miaka elfu sabini ukisafiri na chombo chenye mwendo mkali cha NASA.<br /><br />Tukiweka mfano rahisi kama Jua ni mpira wa tennis uko katikati ya jiji la Dar es salaam basi Proxima centauri ni mpira mwingine wa tenis ukiwa katikati ya jiji la maputo Maputo umbali wa karibia kilomita 1600.<br /><br /><b>3. Baadhi ya nyota ni kubwa kuliko maelezo</b><br /><br />Nyota kubwa sana zinaitwa red hypergiants hizi ni kubwa kweli kweli. Mojawapo ya haya majidude makubwa kabisa linaitwa VY Canis Majoris. Kama ukizidisha saizi ya jua letu mara 1, 420 ndio unaweza kupata size ya VY Canis majoris.<br /><br />Tukirudisha mfano wa mpira wa tenis inakuwa kama jua ni size ya mpira wa tenis basi VY Canis majoris, ni sawa na jengo la ghorofa 16, Hapa sijui lipi litafit kama mfano kwa jiji letu la Dar, PPF Tower? Kama nyota hii ndo ingekuwa jua letu basi kwa maana ya kuwa katikakati ya solar system basi sayari zote zingemezwa.<br /> <br />Nyota nyingine kubwa katika level ya hypergiant ambayo saizi yake inakaribia VY Canis Majoris ni Betelgeuse. Hii inaonekana angani kwa macho kusipokuwa na mbalamwezi.<br /><br /><b>4. Baadhi ya nyota ni ndogo haswa lakini nzito kupindukia.</b><br /><br />Pale nyota kubwa inapokufa kwa kulipuka (supernova), mvuto wa ndani(gravitational collapse) unajitokeza na kusababisha nyota changa (netron star). Matter ambayo sijui kwa kiswahili inaitwa nini imeundwa kwa atoms na atoms zimeundwa kwa nafasi tupu kwa kiasi kikubwa. kitu pekee kinachoipa atom uzito wake ni kiini kidogo (nucleus) katikati yake. Kupata picha ya hii fikiriria atom ni duara kubwa la kilomita moja, kwa size hiyo atom itakuwa size ya mbegu kunde ikielea katikati. Uzito wa atom yote unakuwa sawa na uzito wa mbegu ya kunde.<br /><br />Sasa kinachotokea katika mvuto wa kuvunjika kwa nyota inayokufa ili kuwa nyota changa ni kwamba atoms zinakandamizwa pamoja kwa nguvu sana kiasi kwamba kila nafasi tupu kwenye atom inaachia na vile viini au kwa mfano tuliotumia, zile mbegu za kunde katikati ya miduara ya atoms zinagandamana pamoja. Sasa fikiria nafasi tupu zote katika duara la kilomita moja.moja zimeachia na zile mbegu sasa zimeshonana kwenye eneo dogo kabisa. Kwa hiyo badala ya kuwa na eneo la kilomita moja lenye uzito wa mbegu moja ya kunde sasa eneo hili lina uzito wa karibia mbegu za kunde 1,000,000,000,000,000,000.<br /><br />Hivyo ndivyo inavyokuwa nyota changa inapozaliwa kunakuwa hakuna nafasi tupu, ni neutrons ambazo zimegandana na uwiano wa uzito wake kwa kulinganisha ukubwa ni trillioni mara trillioni ya uzito wa nyota ya kawaida. Matokeo yake unakuta nyota changa yenye ukubwa wa kilomita 25 tu ina uzito wa mara tatu ya jua au sawa na uzito wa dunia millioni moja.<br /><br /><b>Mambo mengine ya kustaajabisha kabisa!</b><br /><br />Katika nyota changa (netron star) kijiko kimoja cha chai kina uzito sawa na mapiramidi mia tisa ya Giza kule Misri. Mkandamizo wa nyota changa ni sawa na kuweka meli moja kubwa ya mizigo juu ya punje moja ya mchanga. Nyota hizi hujizungusha kwa kasi sana (spinning) kufikia mara 642 kwa sekunde moja hii ikiwa na maana kidoti katika eneo la kati la nyota hii kinazungunguka kwa kasi ya umbali wa zaidi ya mzunguko mzima wa dunia kwa sekunde. Nyota hizi ni zenye joto kali sana 10,000,000,000,000 Kelvin, kama mara 1000 zaidi ya katikati ya jua.<br /><br />Mwenye kuongeza, maswali, kupungunguza kuhusu nyota haya karibuni&amp;#8230;
 
mkuu uzi wako una maswal meng sana em rud hapa izo nyota wanajuaje uo uzito wake na uzito wa jua na dunia pia wanaujua??

na kuna sehemu naona umesema wanachuo wamehesabu michanga yote dunian duuuh[emoji15][emoji15][emoji15][emoji15][emoji125][emoji125][emoji125] shikamoo
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom