Ulaghai na Ramli za Wanasiasa (The Finger Pointing Culture)

Ulaghai na Ramli za Wanasiasa (The Finger Pointing Culture)

Logikos

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2014
Posts
15,460
Reaction score
24,233
Nadhani wote tunaelewa Wanasiasa na Ulaghai / Kulaumu wengine ni pete na Kidole....; Mdau mmoja alisema.... To err is human. To blame someone else is politics.

Nashangaa pale Chama tawala wanapolaumu wapinzani ni kama dereva kulaumu abiria wakati yeye ndio anaendesha (lakini naelewa wanajilinda waendelee kutawala).

Na Wapinzani wanapopinga ndio kazi yao wala sishangai; lakini productively badala ya Watawala kupoteza muda labda wangejipima kwa kipi wamefanya kutokana na walichosema watafanya. Na wapinzani wangejikita kwenye kuonyesha nini hakijafanyika na wao wangefanya nini tofauti.

Tatizo imekuja hii Kasumba ya hawa Wanasiasa (Wapinzani) kuanza kulaumu maboss wao...; yaani sisi tunaowalipa Ruzuku na wabangaizaji ambao tumewaweka pale ili wafanye hilo wanalofanya na sisi tufanye mengine... Unasikia jamaa anasema Watanzania wanajua kuongelea tu Mpira (Sasa wanataka nini, labda hatuongelei Siasa hawajaifanya iweze kuongeleka) yaani wanasema kama vile wana-magic wand kwamba wao wakipewa uskani mambo yote yatakuwa Kosher.

Mwingine anasema hata taarifa hamuangalii ni miziki tu. Sasa kwa kinachoendelea Vijembe na Ulaghai si bora mtu ajiridhishe kwa kupunguza maumivu kwa hivi viburudisho? Najiuliza hivi bila hawa wadau (Mipira na Wasanii) kufanya kazi yao ipasavyo jambo ambalo wanasiasa hawafanyi si maisha yangekuwa magumu maradufu?

Angalizo; Endeleeni kunyosheana vidole lakini tusivunjiane heshima kwa kutaka kuingia kwenye starehe zetu chache zilizobaki na kutulaumu sisi wakati nyie ndio mna-under-perform. Sisi huku kitaa tumefanya yetu kwa kuwalipa na kuwaweka hapo mlipo, na mkizingatia Ulaghai wenu huenda hatuna Imani ya kwamba mtafanya mnachosema. Sasa it's up to you to convince us; na kama bado hatuwaelewi ongezeni bidii.
 
Nikiwaangalia huwa naona ni mapandikizi ya CCM .

1.Freeman Mbowe

2.Zitto kabwe

3.Prof Ibrahim Lipumba

Ni kipi kinafanya uwe na imani na hawa watu ?
Kwani unadhani wao wanakuelewa wewe au wanajua hata kama unaexist? Fanya yaupendezayo moyo wako, waache nao wafanye yawapendazayo. Hawapo pale kukuridhisha wewe.
 
Nikiwaangalia huwa naona ni mapandikizi ya CCM .

1.Freeman Mbowe

2.Zitto kabwe

3.Prof Ibrahim Lipumba

Ni kipi kinafanya uwe na imani na hawa watu ?
Wewe ni wale mandondocha ya kitanzania yasiyopenda mabadiliko yanapenda kuwa CCM tu kwasababu yanapenda vitu vilivyokwisha kuundwa hawapendi kuunda vya kwao, vivu type, akili mgando.
 
Huyo wa kwanza ni kitengo tangu akiwa kijana tu
 
Hata mm nikisoma katikati ya mistari ya hii mada naona kama mleta mada ni chawa wa ccm. Sina Imani na wewe kabisa.
 
Nikiwaangalia huwa naona ni mapandikizi ya CCM .

1.Freeman Mbowe

2.Zitto kabwe

3.Prof Ibrahim Lipumba

Ni kipi kinafanya uwe na imani na hawa watu ?
Mtoe Lipumba hapo, hao wengine ni wakuooopwa
 
Kwani unadhani wao wanakuelewa wewe au wanajua hata kama unaexist? Fanya yaupendezayo moyo wako, waache nao wafanye yawapendazayo. Hawapo pale kukuridhisha wewe.
Hivi unajua kwamba Kodi zako ndio zinalipia Demokrasia na kuwaweka pale ? Okay basi hilo tuachane nalo tunajua demokrasia ni gharama..., Sasa vipi hizi za kuanza kuvunjiana Heshima sijui watanzania hivi watanzania vile kana kwamba underperformance yao ni sababu ya wananchi au wananchi wakimuweka yeye anayelaumu sasa hivi ndio itakuwa magic wand na kila kitu kitakuwa Kosher
 
Hata mm nikisoma katikati ya mistari ya hii mada naona kama mleta mada ni chawa wa ccm. Sina Imani na wewe kabisa.
Huwe na Imani na mimi kwani unanilipa au nipo hapa kukutumikia wewe ? Tofauti na wanasiasa tunawalipa na wapo pale kututumikia sisi hivyo ulaghai wao una effect kubwa kwa jamii as a whole...; By the way umesoma sentensi ya kwanza ? Next time usisome between the line unaweza kupata maana yako unayotaka ambayo haipo:

Nashangaa pale Chama tawala wanapolaumu wapinzani ni kama dereva kulaumu abiria wakati yeye ndio anaendesha (lakini naelewa wanajilinda waendelee kutawala)
 
Nadhani wote tunaelewa Wanasiasa na Ulaghai / Kulaumu wengine ni pete na Kidole....; Mdau mmoja alisema.... To err is human. To blame someone else is politics.

Nashangaa pale Chama tawala wanapolaumu wapinzani ni kama dereva kulaumu abiria wakati yeye ndio anaendesha (lakini naelewa wanajilinda waendelee kutawala).

Na Wapinzani wanapopinga ndio kazi yao wala sishangai; lakini productively badala ya Watawala kupoteza muda labda wangejipima kwa kipi wamefanya kutokana na walichosema watafanya. Na wapinzani wangejikita kwenye kuonyesha nini hakijafanyika na wao wangefanya nini tofauti.

Tatizo imekuja hii Kasumba ya hawa Wanasiasa (Wapinzani) kuanza kulaumu maboss wao...; yaani sisi tunaowalipa Ruzuku na wabangaizaji ambao tumewaweka pale ili wafanye hilo wanalofanya na sisi tufanye mengine... Unasikia jamaa anasema Watanzania wanajua kuongelea tu Mpira (Sasa wanataka nini, labda hatuongelei Siasa hawajaifanya iweze kuongeleka) yaani wanasema kama vile wana-magic wand kwamba wao wakipewa uskani mambo yote yatakuwa Kosher.

Mwingine anasema hata taarifa hamuangalii ni miziki tu. Sasa kwa kinachoendelea Vijembe na Ulaghai si bora mtu ajiridhishe kwa kupunguza maumivu kwa hivi viburudisho? Najiuliza hivi bila hawa wadau (Mipira na Wasanii) kufanya kazi yao ipasavyo jambo ambalo wanasiasa hawafanyi si maisha yangekuwa magumu maradufu?

Angalizo; Endeleeni kunyosheana vidole lakini tusivunjiane heshima kwa kutaka kuingia kwenye starehe zetu chache zilizobaki na kutulaumu sisi wakati nyie ndio mna-under-perform. Sisi huku kitaa tumefanya yetu kwa kuwalipa na kuwaweka hapo mlipo, na mkizingatia Ulaghai wenu huenda hatuna Imani ya kwamba mtafanya mnachosema. Sasa it's up to you to convince us; na kama bado hatuwaelewi ongezeni bidii.
1727440645618.png
 
Kwani unadhani wao wanakuelewa wewe au wanajua hata kama unaexist? Fanya yaupendezayo moyo wako, waache nao wafanye yawapendazayo. Hawapo pale kukuridhisha wewe.
Anawalipa Pesa through Ruzuku (Kodi) ambazo ni pesa zake kwahio wanayofanya yanatakiwa kumpendeza.., Kulaumu kwake anafanya his / her civic duty...
 
Back
Top Bottom