SI KWELI Ulaji wa Chips husababisha ugonjwa wa Macho

SI KWELI Ulaji wa Chips husababisha ugonjwa wa Macho

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Chips ni chakula maarufu sana kinachotumiwa na watu wengi, hasa vijana. Baadhi ya watu huamini kuwa chakula hiki husababisha ugonjwa wa macho hasa kutoa machozi, maumivu ya mishipa ya macho pamoja na upofu.

0275C5CE-E906-4586-88D3-65CDAB810A90.jpeg

Je, kuna ukweli wowote kuhusu madai haya?
 
Tunachokijua
Kwa mujibu wa takwimu za WHO, takriban watu bilioni 2.2 duniani ni waathirika wa magonjwa ya macho yanayohusisha upofu na uoni hafifu.

Kwa kiasi kikubwa, sababu zinazopelekea upofu, uoni hafifu pamoja na changamoto zingine za macho ni-
  • Uzee
  • Mtoto wa jicho
  • Kisukari
  • Glaucoma
  • Sababu zingine zinazoharibu neva za fahamu pamoja na mishipa ya damu ya macho
Pia, takriban watoto 250,000-500,000 kila mwaka hupatwa na upofu kutokana na upungufu wa virutubisho vya Vitamini A. Hii inatoa maana kuwa vyakula pia huchukua sehemu muhimu katika kuamua uimara wa afya ya macho.

Kwa mujibu wa USDA, viazi huwa na mjumuiko wa nishati, aina mbalimbali za madini muhimu kwa mwili, vitamini pamoja na sukari. Ni virutubisho muhimu katika kujenga mwili wa binadamu ambapo macho ni sehemu ya viungo vinavyo uunda.

Kwa kuzingatia mgawanyiko wa virutubisho hivyo pamoja na kazi zake mwilini, JamiiForums imebaini kuwa madai ya chips kusababisha changamoto za macho hayana mashiko, hivyo ni uzushi. Ukaangaji wa viazi kwenye mafuta hauwezi kuleta madhara hasi yanayoweza kunasibishwa na magonjwa ya macho.

Hata hivyo, kwa mujibu wa tafiti mbalimbali, aina hii ya chakula huhusishwa na kuongeza uzito na mafuta mabaya mwilini, shinikizo kubwa la damu pamoja na magonjwa ya mfumo wa damu na moyo.
Ongeza na hii... Ulaji wa chipsi hupunguza nguvu za kiume (huu ni uzushi)
 
Dah watu Wana nongwa ndo nasikia Leo kuwa chips zina athar katika macho
 
MADAI
Chips ni chakula maarufu sana kinachotumiwa na watu wengi, hasa vijana. Baadhi ya watu huamini kuwa chakula hiki husababisha ugonjwa wa macho hasa kutoa machozi, maumivu ya mishipa ya macho pamoja na upofu.

View attachment 2404967

Je, kuna ukweli wowote kuhusu madai haya?
chips siyo chakula, na haijawahi kuwa chakula CHIPS ni KIBWAGIZO kitumiwacho unapokuwa unasubiri mlo au baada ya mlo unashushia, its not food at all.
 
Watu wapaswa kufahamu kuwa chips ni viazi vilivyo kaangwa. Ni sawa tu na ndizi za kukaanga ama mihogo ya kukaanga. Lawama zoote zinapelekwa kwenye viazi, bila maelezo ya kitaalam juu ya madai hayo na ni kivipi hayo yasemwayo kwenye chips yasiwe pia kwenye mihogo n.k
 
hayo mafuta ya transformer wanayotumia kukaangia chips na hayo mayai ya kizungu hayana madhara ?

maana naona mumeongelea viazi tu.

vp kuhusu watoto wa kiume wanaokula chips kua na elements za kike kuna siri gani kwenye chips ?

tuwekeni wazi bhana acheni kuzipamba pamba sana
 
Back
Top Bottom