SI KWELI Ulaji wa Limao na Ndimu husababisha upungufu wa Damu Mwilini

SI KWELI Ulaji wa Limao na Ndimu husababisha upungufu wa Damu Mwilini

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Source #1
View Source #1
Baadhi ya jamii huamini kuwa ulaji wa limao na ndimu husababisha upungufu wa damu mwilini.

6B7371F5-2DAE-4F6B-B319-54712849FF74.jpeg

Uvumi huu uliosambaa kwenye maeneo mengi hutoa maonyo makali hasa kwa watoto na wanawake wenye ujauzito wanaojaribu kutumia matunda haya.

Je, ni kweli kuwa matunda haya hukausha damu mwilini?
 
Tunachokijua
Kwa mujibu wa Idara ya Kilimo ya Marekani (USDA, ) limao (ndimu) huwa na mjumuiko wa nishati, protini, wanga, nyuzilishe, madini ya calcium, magnesium, phosphorus, potassium, sodium, zinc, copper, selenium na kiasi kidogo cha sukari.

Huwa na vitamini C, citric acid, vitamini B12, folate pamoja na viondoa sumu vya carotene, vitamini E, lutein na zeaxanthin.

Madini ya chuma, folate na vitamini B12 hufanya kazi kwa pamoja katika kuwezesha utengenezwaji wa damu mwilini.

Aidha, vitamini C na citric acid huhitajika kwenye kuzuia tatizo la Anemia linaloweza kutokea baada ya mwili kushindwa kufyonza madini ya chuma yanayopatikana kwenye mlo kisha kusababisha upungufu wa damu.

Taasisi ya Chakula la Lishe Tanzania inazungumziaje suala hili?
JamiiCheck pia imefuatilia ukweli wa madai haya kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania, TFNC, ambayo kwa mujibu wa Maelezo yanayopatikana kwenye tovuti yake rasmi, matunda haya hayasababishi upungufu wa Damu, bali huusaidia mwili kuongeza damu zaidi.

“Ndimu na limau ni matunda yenye vitamini C ambayo husaidia katika ufyonzwaji wa madini ya chuma yanayopatikana kwenye vyakula. Madini ya chuma ni muhimu katika kutengeneza chembechembe nyekundu za damu. Kwa mantiki hiyo matumizi ya ndimu na limau hutumika kama kichocheo kimajawapo cha kuongeza damu mwilini na wala si kupunguza damu mwilini.

Pia ifahamike kwamba ndimu na limau husaidia kuongeza hamu ya kula hasa kwa mtu anayepata kichefuchefu na kutapika”
wanaandika TFNC

Taasisi hii inawataka watu kupuuza madai hayo kwani hayana ukweli.

Kwa kurejea vyanzo hivi, JamiiCheck imebaini sio kweli kuwa matunda haya hakausha damu, bali huusaidia mwili kutengeneza damu pamoja na kuzuia upungufu wake.
MADAI
Baadhi ya jamii huamini kuwa ulaji wa limao na ndimu husababisha upungufu wa damu mwilini.


Uvumi huu uliosambaa kwenye maeneo mengi hutoa maonyo makali hasa kwa watoto na wanawake wenye ujauzito wanaojaribu kutumia matunda haya.

Je, ni kweli kuwa matunda haya hukausha damu mwilini?
Si kweli, limao linaongeza acid mwilini, nyongo tu na si kausha damu.
 
Hawako mbali sana na ukweli sema tu kuna matukio hutokea pamoja(association) na sio kusababishana causation
Screenshot_20230328-101547_Chrome.jpg


Ukiingiza malaria (ambayo ipo nyingi tu mtaani) katika mlinganyo ndio unaweza kuona jinsi limao limekuja kuhusishwa na upungufu wa damu.

Ni kwa sababu linaishusha homa na linapambana mdogomdoogo sana na malaria hivyo matokeo yake mtu anapungukiwa damu kwa kukaa na malaria 'kiduchu' ndani ya damu kwa muda mrefu.
 
MADAI
Baadhi ya jamii huamini kuwa ulaji wa limao na ndimu husababisha upungufu wa damu mwilini.


Uvumi huu uliosambaa kwenye maeneo mengi hutoa maonyo makali hasa kwa watoto na wanawake wenye ujauzito wanaojaribu kutumia matunda haya.

Je, ni kweli kuwa matunda haya hukausha damu mwilini?
Inawezekana kuna ukweli, kuna kipindi nilipenda sana kula malimao kwa wingi nikichanganya na kahawa wakati wa jioni, baada ya muda kama mwezi hivi nilipatwa na upungufu mkubwa wa damu mwilini hali iliyopelekea kuumwa sana na kichwa pia kuishiwa nguvu hata nikitembea kidogo, nikaanza dozi ya dawa za kuongeza damu mwilini pamoja na vyakula vinavyoongeza damu mwilini.
 
Sijui kama tuna wataalamu wa afya kwa karne hii. Nasema hivi kwa sababu tuna wimbi la waitwao watalaamu wa afya tena wengine maprofesa ila ni waongo kwa kiwango cha PhD. Nina wasiwasi wanalipwa ili kupotosha umma. Juzi Janabi anasema kujifungua mtoto wa kilo 4 au 5 ni hatari na mtoto yule hana afya...sijui anataka akina mama wajifungue watoto wenye kilo mbili?

Aliwahi kusema kiuno 40 kwa wanaume na 35 kwa wanawake ni hatari na ugonjwa, sijui anataka kila mmoja awe na kiuno kama cha kwake? Kuna wakati alisema wanga haufai kwa kula, sasa watu wale nini sijui, maana karibia vyakula vyote vina wanga. Yaani ni vurugu tu. Dr mkubwa kama yule mwenye ushawishi mkubwa kwa jamii ni rahisi sana kupotosha umma kama atatumika na Mabeberu.

Hawa wanaoitwa wataalamu wa afya wanashindwa kupinga na kuzuia matumizi ya vyakula vitokanavyo na GMOs wanahangaika na Ndimu, malimao, mara unene, mara wanga, yaani hovyoo kabisa.
 
Umeeleweka.usimlaumu mtu tena kwa kutaja jina lake.fuatilia kwa kusoma vitabu na maandiko mbali mbali.Wapo watu wanatumia limao na hizo ndimu kama ulivyo fanya wewe na tunawaona wakiwa na afya njema tu
Kila wanapotaka kunywa kahawa utawasikia wanaomba ndimu na bado wanadunda
PROFESSOR hajamshikia mtu fimbo,ni haki yako kula upendacho kama unaona inafaa
Kila la heri
 
Baadhi ya jamii huamini kuwa ulaji wa limao na ndimu husababisha upungufu wa damu mwilini.


Uvumi huu uliosambaa kwenye maeneo mengi hutoa maonyo makali hasa kwa watoto na wanawake wenye ujauzito wanaojaribu kutumia matunda haya.

Je, ni kweli kuwa matunda haya hukausha damu mwilini?
Hapana, matumizi ya limao na ndimu hayasababishi upungufu wa damu mwilini. Kwa kweli, limao na ndimu ni vyanzo vizuri vya vitamini C, ambayo husaidia katika kunyonya madini ya chuma mwilini. Madini ya chuma ni muhimu kwa kutengeneza seli nyekundu za damu, hivyo matumizi ya limao na ndimu yanaweza kusaidia kupunguza hatari ya upungufu wa damu (anemia), hasa aina inayotokana na ukosefu wa madini ya chuma.

Kuna dhana potofu kwamba vyakula vya asidi kama limao vinaweza kuathiri afya ya damu, lakini hakuna ushahidi wa kisayansi unaoonyesha kuwa limao au ndimu husababisha upungufu wa damu. Badala yake, vyakula hivi vinaweza kuwa msaada kwa watu wenye hatari ya anemia kwa sababu ya uwezo wake wa kuongeza ufyonzwaji wa madini ya chuma kutoka kwenye vyakula vingine.

Ikiwa unakabiliwa na upungufu wa damu, ni muhimu kula vyakula vyenye madini ya chuma kama vile nyama, maharagwe, mboga za majani, na kushirikisha vyanzo vya vitamini C kama limao ili kusaidia katika ufyonzwaji wa madini hayo.
 
Back
Top Bottom